Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ( TFS ) imesema kuwa uhifadhi wa rasilimali za Misitu ni manufaa ya kizazi cha Sasa na vizazi vya baadae hivyo jamii inapaswa kujiepusha kuchoma moto Misitu pamoja na uvunaji haramu.
Hayo yamesemwa Leo Agosti 16,2023 na Kamishna wa uhifadhi wakala wa huduma za Misitu Tanzania Prof. Dos Silayo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa majukumu ya hifadhi hiyo ndani ya Miaka ya miwili ya serikali ya awamu ya sita .
Amesema kuwa sekta ya Misitu na nyiki nchini ni muhimu kutokana na mchango wake Katika ukuaji wa sekta ya Utalii, Maji , kilimo, mifugo, nishati pamoja na viwanda hivyo kutokana na umuhimu huo Wadau wote wanapaswa kulinda rasilimali za Misitu.
Aidha amesema kuwa wakala umeendelea kutatua migogoro kati ya hifadhi za Misitu na jamii inayoizunguka ambapo jumla ya hekta 296,881 za maeneo zimetolewa kwa wananchi kwa ajili ya makazi , kilimo na ufugaji.
Pia wakala unaendea kutoa Elimu ya uhifadhi na usimamizi wa Misitu kwa jamii sambamba na kuimarisha mipaka kwa kuisafisha , kuweka vigingi na mabango Ili kuzuia uvamizi Katika maeneo ya hifadhi.
No comments:
Post a Comment