Serikali imetoa billion 12 kwa ajili ya mradi wa kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kusambaza bidhaa za Petroli na Diseli vijijini Tanzania bara kwa lengo la kulinda Mazingira na Afya ya watumiaji na kuboresha upatikanaji na Usambazaji wa Mafuta vijijini.
Mkurugenzi Mkuu Wa Wakala wa Nishati Vijiini REA Mhandisi Hassan Said amesema hayo leo Jijini Dodoma katika Mkutano na waandishi wa habari akisema usambazaji wa mradi huo unahusu kuwekeza ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta katika maeneo mbalimbali Vijiini.
Said amesema kuwa moja ya changamoto inayosababisha wananchi wasitumie nishati safi na kuendelea kutumia nishati ya asili yaani mkaa na kuni ni pamoja na upatikanaji wake kwani nishati asilia zimekua zikipatikana kwa urahisi.
Aidha amesema Wakala umeanza kutekeleza Mradi wa kusambaza mitungi ya gesi ya kupikia kwa utaratibu wa utoaji ruzuku kuwezesha usambazaji wa mitungi ya gesi ya kupikia (LPG) 71,000 yenye thamani ya shilingi bilioni 3 pamoja na majiko banifu 200,000 (laki mbili) katika maeneo ya vijijini huku kwa mwaka wa fedha 2023/24 jumla ya fedha takribani bilioni 10 zimetengwa kwaajili ya kufanikisha mradi huo.
Pia ametoa rai kwa Watanzania kutumia mafundi wanaotambulika na Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO) kuondoa lawama zinazotolewa na wananchi dhidi ya Serikali zinazosababishwa vishoka wanaofanya uunganishaji wa umeme kinyume cha sheria.
Serikali imetoa jumla ya shilingi trillioni 1.7 kwa Wakala wa Nishati Vijiini (REA) kwaajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya nishati nchini.
Kadhalika Serikali kupitia REA kwa kushirikiana na Benki ya Dunia (WB) imetenga Dola za Kimarekani milioni 6 kwa ajili ya mradi wa usambazaji wa majiko banifu ya kupikia.
No comments:
Post a Comment