Monday, August 14, 2023

TUME YA MAENDELEO USHIRIKA TANZANIA YAONDOA BODI 55

Tume ya maendeleo ya Ushirika Tanzania imeondoa bodi za vyama  vya Ushirika 55  ambazo hazikufuata kanuni na taratibu za Ushirika,na kupeleke masuala 30 polisi na masuala 47 Takukuru kwaajili ya kuyafanyia Kazi.

Hayo yameelezwa na Mrajisi wa vyama vya Ushirika na Mtendaji Mkuu wa Tume ya maendeleo ya Ushirika Tanzania Dkt Benson Ndiege katika mkutano wake Jijini Dodoma akieleza utekelezaji wa majukumu ya tume hiyo na mwelekeo wa utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2023/24.

Aidha Dkt Ndiege amesema katika kuhakikisha Maafisa Ushirika wanaweza kubaini na kutatua changamoto mbalimbali zinazokabili vyama wameamua kutoa mafunzo kwa Maafisa hawa.

Hata hivyo tume hiyo ufanya ukaguzi wa Mara kwa Mara katika vyama vya Ushirika ikiwa lengo ni kubaini uzingatiwaji wa matakwa ya Sheria kanuni na miongozo mbalimbali inayohusiana na utendaji wa vyama vya Ushirika.

No comments:

Post a Comment