Mageuzi hayo yamefanya Tanzania kuwa Nchi ya pili Duniani kwa kuzalisha mkonge ikitanguliwa na Brazili.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Tanzania Saddy Kambona wakati akizugumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa majukumu wa bodi hiyo na mwelekeo katika mwaka huu wa fedha 2023/24.
Kambona ametaja Wilaya zilizopatiwa mbegu hizo ni Korogwe, Muheza, Tanga, Mkinga, Handeni, Kilindi, Rorya, Bunda, Butiama, bariadi, Bagamoyo, Kisarawe, Mkuranga, Manyoni, Singida Vijijini na Mkalama.
Amesema Rais Dk.Samia ametoa fedha kwa ajili ya kununua mitambo mipya ya kuchakata Mkonge na kufufua mitambo ya kuchakata mkonge ya mashamba ya Kibaranga Wilayani Muheza, Tanga na shamba la serikali la TPL lililopo Kata ya Bwawani Wilayani Arumeru, Arusha ambalo linasimamiwa na kuendeshwa na TSB.
Aidha,Kambona amesema Serikali iliongeza lengo na kuiagiza Bodi ya Mkonge Tanzania kuhakikisha kuwa uzalishaji unaongezeka hadi kufikia tani 120,000 kwa Mwaka, ifikapo Mwaka 2025/2026.
No comments:
Post a Comment