Wednesday, August 9, 2023

DC ATAKA MADIWANI WATUNGE SHERIA RAFIKI KWA WAWEKEZAJI

MKUU wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amewataka madiwani kutunga sheria ndogo ambazo zitaboresha mazingira mazuri kwa wafanyabiashara na wawekezaji badala ya kuweka mazingira ambayo yatakuwa kikwazo katika ukusanyaji wa mapato.

John aliyasema hayo mjini Kibaha kwenye kikao cha baraza la madiwani wa Hmashauri ya Mji Kibaha na kuwa wanapaswa kuweka mazingira rafiki badala ya kuwa kero.

Alisema kuwa sheria ndogo ndogo wanazotunga ziwavutie wafanyabiashara na wawekezaji siyo ziwe kero na kusababisha kuwakatisha tamaa badala yake ziwe vichocheo vya watu kufanya uwekezaji.

"Zisiwe kikwazo kuwakwamisha wafanyabiashara na wawekezaji na zisiwaongezee gharama bali ziwe zinzoendana na mpango wa taifa wa wa uboreshaji biashara,"alisema John.

Aidha alisema kuwa gharama za tozo mbalimbali za Halmashauri ziendane na mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuhakikisha mapato yanapatikana. 

"Mmapaswa kuwa wabunifu katika utendaji kwa kubuni mambo mbalimbali ambayo yataweka mazingira mazuri kwa wafanyabiashara na wawekezaji kwani mazingira yakiwa mazuri yatawavutia na watashiriki katika kukuza uchumi wa nchi,"alisema John.

Aliongeza kuwa wanapaswa kuhasaisha wananchi kushiriki shughuli za maendeleo ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati ili itoe matokeo kwani ucheleweshaji hauwezi kuonyesha matokeo ya haraka kwa walengwa.

No comments:

Post a Comment