TAASISI ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na Chuo cha Afya cha St David cha Jijini Dar es Salaam wametoa misaada ya kadi za bima ya afya ya jamii (CHF) vifaa vya shule na vyakula kwa wanafunzi wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi fedha kwa ajili ya bima za afya kwa baadhi ya wagonjwa waliolazwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi, vifaa kwa wanafunzi wa shule ya msingi Muungano Wilayani Kibaha na vyakula kwa wanafunzi wa shule ya Msingi Mkokozi Wilaya ya Mkuranga, katibu wa taasisi hiyo Omary Punzi alisema kuwa moja ya jukumu lao ni kuisaidia jamii.
Naye Josephine Kiondo muuguzi wa wodi ya watoto ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Tumbi alisema kuwa wanaishukuru taasisi hiyo kwa kuwasaidia familia hizo kupata kadi za bima zitawasaidia kukabiliana na gharama za matibabu na kuomba kuendelea kuwasaidia wanajamii.
Kwa upande wake Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Muungano Faith Tawe alisema kuwa wanashukuru kuwasaidia wanafunzi hao kwani itawapa ari ya kusoma ambapo baadhi ya wazazi wanalea watoto kwenye hali ngumu na kusababisha wanafunzi hao kukosa baadhi ya mahitaji ya shule hivyo kutofanya vizuri kwenye masomo yao.
Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Mkokozi Richard Tiyara alisema kuwa wanashukuru kwa misaada ya vyakula kwani wana changamoto kubwa ya chakula na shule hiyo ina wanafunzi wenye ulemavu 79 ambapo wanaoishi bweni ni 23 ambapo bweni hilo ni kwa wasichana tu limejengwa kwa thamani ya shilingi milioni 140
No comments:
Post a Comment