Tuesday, August 8, 2023

KATIBU WA TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYAERERE MKOA WA PWANI ATEMBELEA BANDA LA HIFADHI ZA TAIFA

 



 KATIBU wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa Pwani Ndugu Omary Punzi ametembelea Banda la Hifadhi za Taifa katika Maonyesho ya sikukuu ya wakulima nane nane 8.Agosti 2023 yaliyofanyika mkoani Morogoro Kanda ya Mashariki yakijumuisha mikoa mitatu Morogoro, Pwani na Dar es Salaam.

Punzi amesema kitu cha Kujivunia ni kuonana kuwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mwasisi wa Taifa letu la Tanzania Kutolewa katika idara ya Makumbusho na Kuwekwa katika idara ya Maliasili ya Hifadhi na hii Ndiyo heshima kubwa iliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chiini ya Uongozi wa Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hassani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 Kilio hiki Hakika kimesikika Tangu Tarehe 14.5.2022 katika kongamano la Miaka 100 ya Mwalimu Nyerere Katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete DODOMA Mgeni Rasmi alikuwa Mheshimiwa Kasimu Majaliwa Waziri Mkuu wa Tanzania akiwakilishwa na Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda Waziri Mkuu Mstaafu.

No comments:

Post a Comment