Saturday, August 19, 2023

JUKWAA LA WAZALENDO HURU TANZANIA KUUNGA MKONO ROYAL TOUR


JUKWAA la Wazalendo Huru Tanzania Mkoa wa Pwani katika kuunga jitihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kutangaza utalii inatarajia kufanya ziara Visiwani Zanzibar kutembelea vivutio vya utalii.

Akizungumza na waandishi wa Habari Mjini Kibaha mwenyekiti wa Taasisi hiyo Hadija Juma alisema kuwa hiyo ni sehemu mojawapo ya kuunga mkono jitihada za serikali kwa vitendo.

Juma alisema kuwa utalii ni moja ya vyanzo vikuu vya pato la Taifa hivyo wameona waihamasishe jamii kutembelea vivutio vilivyopo ikiwa ni utalii wa ndani.

Kwa upande wake katibu wa taasisi hiyo Hawa Cheka alisema kuwa lengo lao ni kuelezea mafanikio ya serikali kwenye nyanja mbalimbali za kiafya, kielimu, kisiasa, kijamii na kiuchumi.

Cheka alisema kuwa mbali ya malengo hayo pia ni kuwafanya Watanzania kuwa Wazalendo, kuwa waadilifu, kuheshimu mila na desturi na kujitolea kwenye shughuli za maendeleo.

No comments:

Post a Comment