Friday, August 11, 2023

HOSPITALI YA MUHIMBILI KUPANDIKIZA MIMBA

Katika kutoa huduma za kibingwa na ubingwa bobezi hospital ya Taifa Muhimbili inampango wa kuanzisha huduma za kupandikiza mimba na upandikizaji Figo, uloto na vifaa vya usikivu ambapo  wakati wowote  kwa Wanawake ambao wana matatizo ya kutopata ujauzito watapata huduma hiyo.

Hayo amesemwa Agosti 10, 2023 Mkurugezi Mtendaji wa hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed Janabi wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu utekelezaji wa  shughuli mbalimbali na mwelekeo wa mwaka wa fedha 2023/2024.

Amesema kuwa hospital ihiyo imeona iazishe huduma hizo ili kupunguza wingi wa watu wanaokwenda nje ya inchi kwa ajili ya kupata huduma hiyo.

Pia amesema kuwa hospitali hiyo imeanzisha utaratibu wa kulipia huduma ya maegesho ilii isaidie kupunguza msongamano wa magari ndani ya hospitali kutokana na watu kuegesha magari katika maeneo hayo 

Katika hatua nyingine amesema kuwa wanatarajia kubomoa Hospitali hiyo na kujenga kubwa zaidi kwaajili ya kuboresha utoaji wa huduma bora za Afya na kuendana na wakati.

Mbali na hayo Hospitali hiyo,katika Mwaka wa Fedha 2023/2024 imeidhinishiwa na Serikali jumla ya Shilingi Bilioni170.6 ili kutekeleza vipaumbele vyake.


No comments:

Post a Comment