Friday, July 17, 2026

NSSF YAWATAKA WAAJIRI KUTUMIA MSAMAHA WA TOZO

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetangaza nafuu kwa waajiri wenye malimbikizo ya michango kwa kuwapatia fursa ya msamaha wa tozo zitokanazo na ucheleweshaji wa michango, huku ukiwataka kuchangamkia fursa hiyo ili kupunguza mzigo wa madeni, kuimarisha uzingatiaji wa sheria na kulinda haki za wafanyakazi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, alisema kuwa msamaha huo, ulioanza kutekelezwa tarehe 1 Juni 2026, utaendelea hadi 31 Desemba 2026. 

Bw. Mshomba alieleza kuwa tangu kuanza kwa msamaha huo, waajiri wameonyesha mwitikio chanya ambapo hadi sasa zaidi ya waajiri 6,000 wamejitokeza kutumia fursa hiyo na Mfuko umekwishakusanya zaidi ya shilingi bilioni 46 za michango tangu kuanza kwa msamaha huo tarehe 1 Juni 2026.

“Tunawasihi waajiri wote kutumia fursa hii mapema. Fedha ambazo wangezilipa kama tozo wanaweza kuzielekeza katika shughuli za uzalishaji, upanuzi wa biashara, kuongeza tija na kuboresha ustawi wa wafanyakazi,” alisema Bw. Mshomba.

Alisema msamaha huo utaendelea hadi tarehe 31 Desemba 2026, ambapo waajiri watakaolipa malimbikizo yote ya michango ya msingi ifikapo tarehe 31 Agosti 2026 watanufaika na msamaha wa asilimia 100 ya tozo.

Alifafanua kuwa waajiri watakaokamilisha malipo yao kati ya Septemba na Oktoba 2026, watanufaika na msamaha wa asilimia 75, huku wale watakaolipa kati ya Novemba na Desemba 2026 wakipata msamaha wa asilimia 50.

Aidha, alisema waajiri ambao hawakuwa na malimbikizo ya michango hadi tarehe 31 Mei 2026 lakini walikuwa na tozo pekee, watanufaika na msamaha wa asilimia 100 endapo wataendelea kuwasilisha michango yao kwa wakati hadi mwezi Desemba 2026.

Bw. Mshomba alisema fursa hiyo imetolewa ili kuwapa waajiri nafasi ya kurekebisha hali ya ulipaji wa michango na kutumia fedha ambazo zingelipwa kama tozo katika shughuli za uzalishaji, kuongeza tija na kuboresha mazingira ya kazi.

“Fedha ambazo waajiri wamekuwa wakizilipa kwa ajili ya kufidia tozo zinaweza kuelekezwa katika kuboresha maeneo yao ya kazi, kuongeza tija na kuimarisha uzalishaji.

Ndiyo maana fursa hii imetolewa ili waajiri wanufaike,” alisema.
Alisema ulipaji wa michango kwa wakati ni muhimu kwa kuwa unamwezesha mfanyakazi kupata haki zake za hifadhi ya jamii wakati anapopata majanga mbalimbali ikiwemo kustaafu.

NSSF YAENDELEA KUIMARIKA
Katika hatua nyingine, Bw. Mshomba alisema NSSF imeendelea kuimarika katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita, ambapo thamani ya Mfuko imeongezeka kutoka shilingi trilioni 4.8 mwezi Machi 2021 hadi kufikia zaidi ya shilingi trilioni 11.6 Juni 2026.

Alisema ukuaji huo umechangiwa na ongezeko la wanachama na michango, uwekezaji wenye tija, mazingira mazuri ya uwekezaji pamoja na matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma.

Alieleza kuwa kupitia mifumo ya TEHAMA, waajiri na wanachama sasa wanaweza kufuatilia na kuwasilisha michango, kufuatilia madai ya mafao na kupata huduma mbalimbali bila kulazimika kufika katika ofisi za NSSF.

Kuhusu ulipaji wa mafao, Bw. Mshomba alisema Mfuko umeendelea kuboresha mifumo yake ambapo kwa sasa mafao mengi hulipwa ndani ya siku 20, tofauti na siku 60 zinazotakiwa kisheria.

“Lengo letu ni kuhakikisha mwanachama anapata stahiki zake kwa wakati. Endapo kuna ucheleweshaji mara nyingi chanzo huwa ni mwajiri kutowasilisha michango kwa wakati,” alisema.

UWEKEZAJI WENYE TIJA, SKIMU YA HIFADHI KUONGEZA WANUFAIKA
Akizungumzia uwekezaji, alisema NSSF inaendelea kutekeleza miradi ya kimkakati inayochangia ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira, akitolea mfano Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi ambacho kimeendelea kuongeza uzalishaji, kutoa ajira na kuwawezesha wakulima wanaokizunguka.

Kuhusu Skimu ya Hifadhi, Bw. Mshomba alisema mpango huo umewezesha wananchi waliojiajiri kujiunga na mfumo wa hifadhi ya jamii na kunufaika na mafao mbalimbali ikiwemo pensheni ya uzee, pensheni ya ulemavu, pensheni ya urithi, mafao ya uzazi, msaada wa mazishi pamoja na huduma za matibabu.

“Tunawahimiza waliojiajiri kujiunga kupitia Skimu ya Hifadhi kwa sababu mpango huu unabadilisha maisha yao na kuwapa uhakika wa kunufaika na mafao mbalimbali. Lengo letu ni kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa Staa wa Mchezo katika kujilinda dhidi ya changamoto za maisha,” alisema Bw. Mshomba.

Alisema NSSF itaendelea kushirikiana na waajiri, wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kuimarisha mfumo wa hifadhi ya jamii nchini na kuhakikisha unaleta manufaa kwa Watanzania wengi zaidi.

Wednesday, July 8, 2026

DKT. NICAS MAWAZO AKUTANA NA BALOZI KAIRUKI NCHINI UINGEREZA, WAJADILI FURSA ZA UWEKEZAJI KIBAHA

London, Uingereza | Julai 8, 2026
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Nicas Mawazo ambaye yupo nchini Uingereza katika ziara nchini humo, leo Julai 8, 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uingereza, Mheshimiwa Balozi Kairuki.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Kairuki amepongeza juhudi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuimarisha diplomasia ya uchumi, kuvutia uwekezaji na kusukuma mbele agenda ya maendeleo ya taifa.

Aidha, Balozi Kairuki ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa mafanikio yake katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo na ukusanyaji wa mapato ya ndani, akieleza kuwa halmashauri hiyo imeendelea kuwa miongoni mwa halmashauri zinazofanya vizuri nchini.

Mazungumzo kati ya viongozi hao yamejikita katika kutafuta fursa za ushirikiano wa kiuchumi kwa Manispaa ya Kibaha, ikiwemo namna ya kuvutia wahisani, wawekezaji na wadau wa maendeleo kutoka Uingereza ili kuwekeza katika sekta mbalimbali zenye mchango mkubwa kwa maendeleo ya manispaa hiyo.

Dkt. Mawazo amesema kuwa mazungumzo hayo ni sehemu ya jitihada za kuitangaza Manispaa ya Kibaha kimataifa na kufungua milango ya ushirikiano itakayochochea uwekezaji, ukuaji wa uchumi na uboreshaji wa huduma kwa wananchi.

Friday, July 3, 2026

KUNENGE AMSHUKURU RAIS DK SAMIA KUKUZA VIPAJI VYA MICHEZO KWA VIJANA

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.



Mpya







MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.

mwisho.

KUNENGE AMSHUKURU RAIS DK SAMIA KUKUZA VIPAJI VYA VIJANA

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.

mwisho.

Thursday, July 2, 2026

PWANI KUMUUNGA MKONO RAIS DK SAMIA UKUSANYAJI MAPATO

MKOA wa Pwani umesema utashirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha inakusanya mapato ili kuinua uchumi kupitia uwekezaji wa viwanda kumuunga Mkono Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Hayo yelisemwa na Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Pili Mnyema wakati wa sherehe za kutimiza miaka 30 ya TRA kimkoa ambapo walushuhudia moja kwa moja maadhimisho hayo Kitaifa ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais Dk Samia.

Mnyema alisema kuwa kama Rais alivyotaka TRA kufanya vizuri ili akistaafu Mamlaka hiyo iwe kwenye hali nzuri ndiyo itakuwa furaha yake.

"Tutamuunga mkono Rais kwa kushirikiana na TRA kuhakikisha walipa kodi wanalipa kodi pasipo kukwepa kodi ili kuinua uchumi hasa ikizingatiwa Pwani ni mkoa wa kimkakati kwa kuwa na viwanda vingi,"alisema Mnyema.

Alisema kuwa ukusanyaji mzuri unaofanyika unatokana ushirikiano uliopo baina ya mamlaka na walipa kodi ambapo hicho ni kiashiria cha ukuaji wa uchumi.

"Pia ukusanyaji utaendana na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050 ambayo ndo inaanza kazi kuanzia sasa na hapa tunashirikiana na sekta binafsi katika kuchangia uchumi,"alisema Mnyema.

Aidha alisema kuwa Mkoa utasimamia kuhakikisha malengo ya nchi yanatimia kwa kuwa na uwezo wa kukusanya mapato kwa walipa kodi kulipa kwa hiyari ikiwa ni maono ya Rais.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani Salim Makame alisema kuwa Mamlaka imejipanga kuhakikisha wale wote wanastahiki kulipa wanalipa kwa hiyari.

Makame alisema kuwa wameyapokea maagizo yote yaliyotolewa na Rais ya namna ya kuboresha ukusanyaji wa Mapato pia kutumia mifumo ya teknolojia.

Wednesday, July 1, 2026

NASHUKURU SANA MTANDAO NAJUKWAA KUBWA BELLE NAIJA

ALHAMDULILAH ALLAH NDIYO SHAHIDI WA KILA JAMBO 

Jukwaa kubwa la kidijitali nchini Nigeria linalojihusisha na masuala ya burudani, mitindo, mitindo ya maisha (lifestyle), na harusi za Kiafrika. Ilianzishwa mnamo mwezi Julai mwaka 2006 na mjasiriamali wa Nigeria anayeitwa Uche Pedro (jina la kuzaliwa Uche Eze).

NASHUKURU KUPOSTI PICHA YANGU NA STAA MKUBWA NCHINI NIGERIA NI HESHIMA KUBWA KUTAMBUA MCHANGO WANGU KATIKA AFRIKA 

Layi Wasabi (jina lake halisi ni Isaac Ayomide Olayiwola) ni mchekeshaji, mwigizaji, na mtengeneza maudhui maarufu wa mtandaoni kutoka nchini Nigeria. 

Anajulikana sana kwa uchekeshaji wake wa kipekee na wa akili (philo-comedy) kupitia video fupi (skits) kwenye mitandao ya kijamii