Sunday, June 28, 2026

VIJANA WENYE VIPAJI VYA MICHEZO WATAKIWA KUWA NA NIDHAMU

VIJANA wenye vipaji vya michezo nchini wametakiwa kusoma kwabidii na kuwa na nidhamu ili waweze kufikia viwango vya juu na kuwa tegemeo kwa Taifa.

Hayo yamesemwa na Gilbert Maregesi ambaye alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kibaha wakati wa kufunga tamasha la michezo lililoandaliwa na Compassion Kanda ya Mashariki lililofanyika kwenye Viwanja vya Shirika la Elimu Kibaha Tumbi.

Maregesi amesema kuwa serikali imekuwa ikiwekeza kwenye sekta ya michezo kwa vijana ili kuendeleza vipaji vyao na kuwa tegemeo kwa Taifa kwenye sekta hiyo ambayo pia ni ajira kwa vijana.

"Ili kulinda vipaji vyenu mnapaswa kuwa na nidhamu ili muweze kufika mbali kwani mbali ya kunufaika binafsi pia mtaliwezesha Taifa kuwa na wachezaji wazuri watakaoliwakilisha Taifa kwenye michezo mbalimbali,"amesema Maregesi. 

Naye mwakilishi wa meneja wa Compassion Kanda ya Mashariki Daudi Lawi inayoundwa na mikoa ya Pwani Morogoro na Dar es Salaam amesema tamasha hilo la awamu ya nne limeshirikisha wanamichezo 430 kutoka mikoa hiyo.

Lawi amesema kuwa baada ya kukamilisha tamasha hilo lilobeba ujumbe wa Kipaji changu Mtaji wangu watachaguliwa wachezaji bora ambao watawakilisha Kanda hiyo kwenye mashindano ya Taifa.

Kwa upande wake James Mhina Kanda ya Mlandizi ambao walikuwa wenyeji wa mashindano hayo amesema kuwa michezo hiyo inajenga mahusiano na kipaji ni msaada katika maisha.

Mwenyekiti wa Mashindano hayo Lucas Kiluwasha amesema kuwa vipaji vyao ndiyo mtaji wao hivyo wavitumie vizuri na kuwataka wadau wa michezo kushuhudia michezo ili wachukue vipaji na kuviendeleza.

Rais wa Vijana Kanda ya Mashariki amesema kuwa michezo hiyo imewasaidia kuwaongezea ujuzi na kukuza vipaji vyao na kujumuika na kufahamiana kwani hiyo ndiyo njia ya mafanikio.

Mgeni rasmi ametoa fursa ya vijana Milovan Kilingo kutoka Gairo na Joshua Joakim wa Mkuza Kibaha kujiunga na bendi ya Jkt Ruvu ili waendeleze vipaji vyao.

Baadhi ya michezo iliyochezwa ni pamoja na mpira wa miguu, pete, riadha na michezo ya ndani ikiwemo sanaa ya uimbaji, upigaji wa vyombo vya muziki, maonyesho ya mavazi na sarakasi na yalishirikisha vijana wenye umri chini ya mi 17 na 22.

MWANADIPLOMASIA OMARY PUNZI ATEULIWA KUSHIRIKI MKUTANO WA CREATIVE

Mwanadiplomasia na Mchambuzi wa Masuala ya Kidiplomasia Siasa , Itifaki na Maadili Omary Punzi ateuliwa kushiriki katika mkutano wa Creative Convergence 2026 . 

Mkutano huu unaojumuisha Africa Creative Market (ACM), Creative Industry Business Summit (CIBS), na Kwimbo National Arts Festival, unafanyika kuanzia Juni 29 hadi Julai 4, 2026 jijini Lusaka, Zambia.

Mkutano huo unaisimamiwa na Wizara ya Vijana, Michezo na Sanaa nchini Zambia 

Utafanyika katika  kumbi za mikutano zilizopo Mulungushi International Conference Centre kuanzia Juni 29 hadi Julai 2, 2026 na kuanzia tarehe 3 hadi 4 Julai 

Tamasha la Sanaa,  tamasha la Kwimbo  huko Polo B, Lusaka Showgrounds. 

Mkutano huo utakutanisha Vijana zaidi 10000  kutoka Bara la Afrika.

kushiriki  Programu na Warsha (Sessions & Masterclasses)

Mijadala ya Biashara, Mijadala inayohusu biashara ya sanaa, filamu, muziki, teknolojia (kama AI), na mitindo.

Mafunzo ya Kitaalamu, Ufikiaji wa masterclasses zinazoendeshwa na washirika wa sekta, mfano mafunzo ya upigaji picha au uigizaji.

Kuunganisha Mtandao wa Biashara (Networking & Deal Rooms)

Ushirikiano wa Kibiashara, mikutano ya kibiashara (kama vile Deal Rooms au Creative Pitch Zone) ambapo wabunifu wanakutana na wawekezaji, wafadhili, na watengeneza sera ili kugeuza mawazo kuwa mikataba ya kazi.

MAWAZO YA VIJANA




SERIKALI imesema kuwa itatumia mawazo ya vijana walioshiriki shindano la Vijana Uchumi Challenge kuwa mpango ambao utaleta suluhisho la namna ya kutatua baadhi ya changamoto ndani ya jamii.

Hayo yalisemwa Kibaha na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Jenifa Omollo wakati wa kufunfa mafunzo ya siku nne kwa vijana 100 walioandika mawazo juu ya masuala ya uchumi kupitia jukwaa la Vijana Uchumi Challenge.

Omollo alisema kuwa mawazo yaliyoandikwa na vijana yameonyesha kuwa yakiboreshwa yanaweza kuwa mpango mzuri ambao unaweza kukabili changamoto mbalimbali ndani ya jamii na Taifa kwa ujumla.

"Mawazo yote yaliyowasilishwa hayataachwa badala yake yataboreshwa na kupatiwa fursa ili yawe mpango ambao utakuwa suluhu kwa baadhi ya changamoto ili kuleta tija na kusaidia Taifa mojawapo likatoa ajira kwa vijana,"alisema Omollo.

Alisema kuwa mawqzo hayo ni bunifu ambazo zimeonyesha jinsi gani vijana walivyokuwa na vipaji ambavyo vitatoa ajira na kuwa na manufaa kwa watu wengi hivyo kulisaidia Taifa.

"Vijana wana fursa nyingi kiuchumi lakini wanakosa taarifa sahihi kwani mawazo kama haya wanaweza kuyapatia fedha za Halmashauri nchini kupitia manunuzi ya umma kwenye mfumo wa Nest au mpango wa yendelezaji vipaji,"alisema Omollo.

Aidha alisema moja ya sekta yenye fursa nyingi ni kilimo ambayo imeajiri asilimia 75 ya Watanzania vijana wanaweza kunufaika kiuchumi kupitia mnyororo wa thamani na fursa kupitia dijitali.

Naye mwenyekiti wa kamati ya Vijana Uchumi Challenge Joseph Malecela alisema kuwa jumla ya mawazo zaidi ya 7,000 ya vijana kote nchini wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35 yaliwasilishwa na kuchujwa na kubaki 100 ambayo yatashindanishwa kupata mshindi.

 

Malecela alisema kuwa washiriki hao 100 ambao waliiingia kambini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere wamechujwa na majaji wabobezi wa masuala ya uchumi na fedha na kubaki 10 watashindana ili kumpata mshindi wa shindano hilo.


Rais Dk Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha kumpata kijana mwenye wazo zuri Julai 6 mwaka huu Jjiini Dar es Salaam  kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere Internation Convention Centre (JNICC) Jijuni Dar es Salaam.



mwisho

WALIPA KODI WATAKIWA KUONYESHA UZALENDO KWA KULIPA KWA WAKATI

WALIPA kodi wa Mkoa wa Pwani wametakiwa kulipa kwa wakati ili kuonesha uzalendo kwa nchi na mapato yanayokusanywa yaweze kutumika kwenye miradi mikubwa ya kimkakati ya maendeleo.

Hayo yalisemwa na Lilian Shirima aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kibaha wakati wa mazoezi ya wadau na walipakodi ikiwa ni kuelekea miaka 30 ya mamlaka hiyo.

Shirima alisema kuwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ya maendeleo inatokana na kodi zinazolipwa hivyo wanapaswa kulipa kodi kwa wakati ili zifanikishe malengo ya utekelezaji wa miradi hiyo.

"Wafanyabiashara wanapaswa kutoa risiti pale wanapofanya mauzo na wananchi nao wanapaswa kudai risiti pale wanaponunua bidhaa kwani huo ndiyo uzalendo wa nchi,"alisema Shirima.

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani Peter Eliona    alisema kuwa wafanyabiashara wanapaswa kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwani kukwepa kulipa kodi ni kurudisha nyuma maendeleo ya nchi ambapo mapato hayo yanaleta maendeleo.

Eliona alisema kuwa kulipaji kodi ni uzalendo hivyo wanapaswa kulipa kodi kwani fedha zinazokusanywa kazi yake kubwa ni kuleta maendeleo kupitia miradi mbalimbali hasa ile mikubwa kama vile miradi ya elimu afya miundombinu ya barabara na reli.

Alisema kuwa fedha hizo matumizi yake ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya wananchi hivyo kutolipa kodi na kurudisha nyuma jitihada za serikali za kuleta maendeleo kwa wananchi.

Aidha alisema kuwa katika kuelekea miaka 30 ya TRA wamefanya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuimarisha afya kwa kufanya mazoezi kufanya usafi kwenye eneo la wafanyabiashara Chalinze.

"Ulipaji wa kodi unasaidia serikali katika utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi zikiwemo za kiafya na huduma zote ambazo wananchi wanapaswa kuzipata kwenye maeneo yao,"alisema Eliona.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara (JWT) Mkoa wa Pwani Abdala Ndauka alisema kuwa ulipaji kodi umekuwa rahisi kwa sasa kutokana na mahusiano mazuri yaliyopo baiba ya wafanyabiashara na mamlaka.

Ndauka alisema mtaji mkubwa wa mfanyabiashara ni afya njema hivyo mazoezi hayo yanasaidia kuimarisha afya na kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

MAWAZO VIJANA CHALLENGE KUTUMIKA KIMAENDELEO



SERIKALI imesema kuwa itatumia mawazo ya vijana walioshiriki shindano la Vijana Uchumi Challenge kuwa mpango ambao utaleta suluhisho la namna ya kutatua baadhi ya changamoto ndani ya jamii.

Hayo yalisemwa Kibaha na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Jenifa Omollo wakati wa kufunfa mafunzo ya siku nne kwa vijana 100 walioandika mawazo juu ya masuala ya uchumi kupitia jukwaa la Vijana Uchumi Challenge.

Omollo alisema kuwa mawazo yaliyoandikwa na vijana yameonyesha kuwa yakiboreshwa yanaweza kuwa mpango mzuri ambao unaweza kukabili changamoto mbalimbali ndani ya jamii na Taifa kwa ujumla.

"Mawazo yote yaliyowasilishwa hayataachwa badala yake yataboreshwa na kupatiwa fursa ili yawe mpango ambao utakuwa suluhu kwa baadhi ya changamoto ili kuleta tija na kusaidia Taifa mojawapo likatoa ajira kwa vijana,"alisema Omollo.

Alisema kuwa mawqzo hayo ni bunifu ambazo zimeonyesha jinsi gani vijana walivyokuwa na vipaji ambavyo vitatoa ajira na kuwa na manufaa kwa watu wengi hivyo kulisaidia Taifa.

Naye mwenyekiti wa kamati ya Vijana Uchumi Challenge Joseph Malecela alisema kuwa jumla ya mawazo zaidi ya 7,000 ya vijana kote nchini wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35 yaliwasilishwa na kuchujwa na kubaki 100 ambayo yatashindanishwa kupata mshindi.

Malecela alisema kuwa washiriki hao 100 ambao waliiingia kambini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere wamechujwa na majaji wabobezi wa masuala ya uchumi na fedha na kubaki 10 watashindana ili kumpata mshindi wa shindano hilo.

Rais Dk Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha kumpata kijana mwenye wazo zuri Julai 6 mwaka huu Jjiini Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere Internation Convention Centre (JNICC) Jijuni Dar es Salaam.







mwisho


Thursday, June 25, 2026

MAWAKALA WAITWA KUCHANGAMKIA VIPAJI TUMBI KIBAHA

MAWAKALA wa michezo ikiwemo soka wametakiwa kujitokeza kushuhudia vipaji vya wacehzaji chini ya miaka 17 na 22 kwenye mashindano ya Compassion ili kuwa na timu bora zitakazozalisha wachezaji wakulitumikia Taifa ambapo moja zao la wachezaji hao ni Dickson Job anayechezea timu ya Yanga.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Lucas Kiluwasha ambaye ni mwenyekiti wa Mashindano ya Compassion Kanda ya Mashariki kwenye Viwanja vya Shirika la Elimu Kibaha Tumbi.

Mashindano hayo ambayo ni ya nne kufanyika yameweza kuwatoa wachezaji wengi akiwemo Dickson Job wa Yanga, Paschal Msindo wa timu ya Azam na Haji Abdala kipa wa timu ya Serengeti Boys chini ya miaka 17 iliyoshika nafasi ya pili kwenye michuano ya Afcon ya vijana iliyofanyika Morocco hivi karibuni.

Mbali ya kuzalisha wachezaji hao ambao wanatambulika pia imezalisha wachezaji wengine ambao wako timu za Yanga B, Azam na Fountain Gate pamoja na msanii wa muziki wa kisasa Dogo Janja na wasanii mbalimbali hapa nchini.

Kiluwasha amesema kuwa mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka yanashirikisha jumla ya mikoa mitatu ya Pwani, Dar es Salaam na Morogoro ambapo kuna wachezaji zaidi ya 430 kauli mbiu ya mwaka huu inasema “Kipaji Changu Mtaji Wangu”.

“Michezo inayoshindaniwa ni pamoja na soka, mpira wa pete, riadha na michezo ya ndani ikiwa ni pamoja na kupiga vyombo vya muziki, ubunifu wa mavi na sanaa mbalimbali lengo ni kuinua na kuibua vipaji kwa vijana,”alisema Kiluwasha.

Alisema kuwa kwa sasa mara wanapopatikana vijana wa michezo husika huwapeleka ili wakaendeleze vipaji vyao ambapo wa soka huwapeleka kwenye timu zenye Academy ili waweze kukuza vipaji vyao na kujipatia ajira kupitia michezo.

“Changamoto kubwa ni ushiriki mdogo wa wadau kujitokeza kuhudhuria mashindano yao pia baadhi ya wachezaji kwenda kushiriki michezo ya Umisseta na Umitashumta kwani nao hufanya kipindi cha likizo hivyo kuwa na mwingiliano,”alisema Kiluwasha.

Aidha alisem akuwa malengo yao ya baadaye ni kuanzisha timu ya mipra wa miguu ili ishiriki ligi mbalimbali na hatimaye kufika ligi kuu pia wanazikaribisha timu mbalimbali kama zinahitaji wachezaji kuona nao ili kukubalina na kuwachukua ili wakaendeleze vipaji vyao.

Wachezaji hao wanatoka kwenye vituo vya huduma ya mtoto na kijana kwenye makanisa ya Kiinjili na Kipentekoste kwenye mikoa hiyo na wachezaji watakaofanya vizuri watachaguliwa kwenda kushiriki mashindano hayo kitaifa.

Tuesday, June 23, 2026

WAZO BORA LA KIJANA KUNYAKUA MILIONI 50

KIJANA mwenye wazo bora kati ya vijana 100 watakaowania kinyanganyiro cha Vijana Uchumi Challenge anatarajiwa kujinyakulia kitita cha shilingi milioni 50.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Dk Kedmon Mapana wakati akizungumza na vijana hao 100 watakaokuwa kambini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopo Kibaha Mkoani Pwani.

Mapana amesema kuwa wapili akijinyakulia shilingi milioni 20 na watatu milioni 10 ambapo vijana wanaoshiriki ni wenye umri chini ya miaka 35 kutoka nchi nzima.

"Wizara ilitoa shindano la vijana kutoa wazo la kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia mawazo ya vijana kukuza ubunifu na Ujasiriamali na kuwapa vijana fursa ya kuonyesha mawazo yao ya kibiashara na miradi ya kibunifu inayoweza kutatua changamoto za kijamii na kiuchumi,"amesema Mapana.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya Vijana Uchumi Challenge Joseph Malecela amesema kuwa jumla ya mawazo zaidi ya 7,000 ya vijana kote nchini yaliwasilishwa na kuchujwa na kubaki 100 ambayo yatashindanishwa kupata mshindi.

Malecela amesema kuwa washiriki hao 100 ambao wameingia kambini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere watachujwa na majaji wabobezi wa masuala ya uchumi na fedha na kubaki 30 na baadaye 10.

Kilele kinatarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi atakuwa Rais Dk Samia Suluhu Hassan.