Tuesday, May 5, 2026

VIJANA WATAKA MFUMO UKOPAJI UBORESHWE KUVUTIA VIJANA

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kibaha Mjini umeishauri Wizara ya Maendeleo ya Vijana kuangalia upya mfumo wanamna ya kuwapata vijana kukopa ili wengi waweze kunufaika.

Akizungumza ofisini kwake Katibu wa (UVCCM) Kata ya Tangini Lazaro Benjamin alisema kuwa Wizara inapaswa kuweka mfumo rafiki na kuweka masharti nafuu.

Benjamin alisema kuwa kuweka masharti magumu kunakwamisha vijana wengi kupata fursa ya kufikia mikopo hiyo inayowalenga vijana.

"Vijana ndio nguvu kazi ya Taifa wanapokosa mitaji wanakosa fursa ya kujiajiri na matokeo yake ni kuongezeka kwa ukosefu wa ajira umasikini na hata kukata tamaa,"alisema Benjamin.

Alisema kuwa kuna umuhimu sasa wa kuongeza bajeti ya mikopo ya vijana ili iwafikie wengi zaidi pia kutoa elimu ya ujasiriamali na usimamizi wa fedha ili mikopo itumike kwa ufanisi.

"Lengo liwe ni kuwafikia vijana wengi zaidi iwezekanavyo kwani maendeleo ya Taifa letu yanategemea uwezeshaji wa vijana wake na wafanye maboresho ili kuhakikisha uwiano unazingatiwa,"alisema Benjamin.

Aidha alisema kuwa wanamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kutenga kiasi cha shilingi bilioni 200 kwa ajili ya kuwawezesha vijana kiuchumi kwani hiyo ni hatua kubwa na ya kupongezwa na inaonesha dhamira ya kweli ya serikali katika kuinua vijana wa Taifa la Tanzania.

"Wizara ifanye utafiti kwani takwimu zinaonyesha kuwa jumla ya vijana 30,384 waliomba mikopo hii lakini vijana waliokidhi vigezo vya kukopeshwa ni 1,961tu,"alisema Benjamin.

Aliongeza kuwa idadi kubwa sana ya vijana zaidi ya asilimia 90 hawakupata fursa hiyo utafiti ufanyike ili kujua ni kwa nini idadi hiyo kutokidhi vigezo na kama bajeti ni ndogo basi iongezwe ili asilimia ya vijana wanaoomba mikopo waweze kuongezeka na kupanua wigo wa ajira kwani wakipata watajiajiri.

Sunday, April 26, 2026

Shule

 


INTRNATIONAL

 


SHULE KIMATAIFA

 


ZINGATIENI DIRA YA MAENDELEO

WIZARA ya Elimu Sayansi na Teknolojia imezitaka Shule za Kimataifa nchini kujisajili kwenye mifumo na miongozo ya elimu na kiserikal ili kukidhi matakwa ya kisheria.

Hayo yalisemwa na Dk Maulid Maulid aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara Caroline Nombo wakati wa kufunga mafunzo ya siku nne kwa wamiliki wa shule hizo juu ya namna ya uendeshaji wa shule hizo mafunzo yaliyofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha.

Maulid alisema kuwa ili elimu inayotolewa na shule hizo za kimataifa lazima zihakikishe zinafanya usajili wao kupitia mifumo iliyowekwa ili kuendana na mfumo wa elimu wa nchi.

"Wamiliki wa shule hizi wanapaswa kufanya usajili kwenye mifumo ya elimu ili elimu inayotolewa itambulike na iwe na ubora unaotambulika na ushindani kimataifa kwa kuzingatia mitaala ya nchi yetu,"alisema Maulid.

Alisema kuwa shule hizo zinapaswa kujisajili kwenye mamlaka mbalimbali za taasisi za elimu ili ziweze kuendana na mifumo iliyopo ikiwemo kwenye Baraza la Mitihani NACTE na mamlaka za serikali.

"Lazima wafuate mifumo yote ya kiithibati na ubora bila kusahau kuzingatia sera ya elimu ambayo ndiyo inayotoa mwongozo wa elimu kwa taasisi za kielimu,"alisema Maulid.

Aidha alisema kuwa pia mitaala yao iendane na Dira ya Taifa ya Maendeleo ili wanafunzi wawe na uelewa wa juu ya Dira hiyo ambapo kwa sasa ni ya 2050.

"Mitaala yao iendane na Dira ya Maendeleo kwani inazingatia utoaji elimu bora ambayo inaangalia viaumbele vya nchi katika kuleta maendeleo kwa wananchi,,'alisema Maulid.

Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo ambaye ni mhasibu wa shule ya kimataifa ya Renie Joshua John alisema kuwa mafunzo hayo yatakuwa chachu kwa shule yake kwani amepata elimu ya namna ya kuweka vizuri masuala ya fedha.

John alisema kuwa wamepata uelewa mzuri wa namna ya kuendesha shule zao na kwa kuzingatia taratibu na miongozo ya kisheria ambayo wanapaswa kuifuata.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Tanzania School Leadership Institute (TSLI) na kusimamiwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia waliwahusisha wamiliki, walimu wakuu, wahasibu na viongozi wa shule za kimataifa hapa nchini

SHULE ZA KIMATAIFA ZATAKIWA KUJISAJILI KIKIDHI MATAKWA YA KISHERIA

WIZARA ya Elimu Sayansi na Teknolojia imezitaka Shule za Kimataifa nchini kujisajili kwenye mifumo na miongozo ya elimu na kiserikal ili kukidhi matakwa ya kisheria.

Hayo yalisemwa na Dk Maulid Maulid aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara Caroline Nombo wakati wa kufunga mafunzo ya siku nne kwa wamiliki wa shule hizo juu ya namna ya uendeshaji wa shule hizo mafunzo yaliyofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha.

Maulid alisema kuwa ili elimu inayotolewa na shule hizo za kimataifa lazima zihakikishe zinafanya usajili wao kupitia mifumo iliyowekwa ili kuendana na mfumo wa elimu wa nchi.

"Wamiliki wa shule hizi wanapaswa kufanya usajili kwenye mifumo ya elimu ili elimu inayotolewa itambulike na iwe na ubora unaotambulika na ushindani kimataifa kwa kuzingatia mitaala ya nchi yetu,"alisema Maulid.

Alisema kuwa shule hizo zinapaswa kujisajili kwenye mamlaka mbalimbali za taasisi za elimu ili ziweze kuendana na mifumo iliyopo ikiwemo kwenye Baraza la Mitihani NACTE na mamlaka za serikali.

"Lazima wafuate mifumo yote ya kiithibati na ubora bila kusahau kuzingatia sera ya elimu ambayo ndiyo inayotoa mwongozo wa elimu kwa taasisi za kielimu,"alisema Maulid.

Aidha alisema kuwa pia mitaala yao iendane na Dira ya Taifa ya Maendeleo ili wanafunzi wawe na uelewa wa juu ya Dira hiyo ambapo kwa sasa ni ya 2050.

"Mitaala yao iendane na Dira ya Maendeleo kwani inazingatia utoaji elimu bora ambayo inaangalia viaumbele vya nchi katika kuleta maendeleo kwa wananchi,,'alisema Maulid.

Kwa upande wake moja ya washiriki wa mafunzo hayo ambaye ni mhasibu wa shule ya kimataifa ya Renie Joshua John alisema kuwa mafunzo hayo yatakuwa chachu kwa shule yake kwani amepata elimu ya namna ya kuweka vizuri masuala ya fedha.

John alisema kuwa wamepata uelewa mzuri wa namna ya kuendesha shule zao na kwa kuzingatia taratibu na miongozo ya kisheria ambayo wanapaswa kuifuata.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Tanzania School Leadership Institute (TSLI) na kusimamiwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia waliwahusisha wamiliki, walimu wakuu, wahasibu na viongozi wa shule za kimataifa hapa nchini


Thursday, April 23, 2026

MITAALA YA SHULE ZA KIMATAIFA YAVUTIA WANAFUNZI KUTOKIMBILIA KUSOMA NJE YA NCHI


KWA kipindi cha miaka ya nyuma baadhi ya wazazi walikuwa na kasumba ya kupeleka watoto wao kusoma nje ya nchi kwa imani huko ndiko kuna elimu bora tofauti na hapa nchini.

Aidha baada ya maboresho mbalimbali kwenye shule za kimataifa hapa nchini kwa sasa wazazi wanawapeleka watoto wao kwenye shule za hapa nchini ambazo zinatoa elimu bora.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Elimu ya Ualimu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Mathias Mvula akimwakilisha Naibu Waziri wa Elimu Wanu Ameir wakati akifungua mafunzo ya wadau wa Shule za Kimataifa nchini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kibaha.

Mvula amesema kuwa Shule hizo zinafundisha kwa kuzingatia mitaala ya nchi na ile ya kimataifa ili elimu inayotolewa kuwa na ushindani na ile inayotolewa nje.

Naye Hassan Masawe kutoka Tanzania School Leadership Institute (TSLI) amesema kuwa mafunzo hayo yana lengo la kuboresha elimu inayotolewa na shule hizo kuwa na ubora baina ya elimu ya nchini na ile ya nje ya nchi.

Kwa upande wake Calista Mungwe Mkurugenzi wa shule ya Renie International ya Jijini Dar es Salaam amesema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kuboresha uendeshaji wa Shule zao.