Tuesday, July 28, 2026

MAGANYA ATAKA WANACHAMA WASICHAFUANE.

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Fadhili Maganya amewataka wanachama waache kuchafuana kuelekea uchaguzi wa ndani mwakani.

Maganya aliyasema hayo Mjini Kibaha alipokuwa  akizungumza na viongozi wa Jumuiya hiyo pamoja na wanachama wa CCM Kibaha Mjini wakati wa ziara yake kutembelea Mkoa wa Pwani kukagua uhai wa chama na miradi ya maendeleo.

Alisema kuwa chama hakina shida nao bali wafuate miongozo na utaratibu wa chama kama unavyoelekeza.

"Mwakani tunaingia kwenye uchaguzi wa ndani baadhi wameanza kuchafuana tusikubali hali hiyo asitokee mtu wa kutoa maelekezo bali chama ndiyo kinatoa maelekezo,"alisema Maganya.

Aidha alisema kuwa watu wanaanza kukinzana na uchaguzi wa mwakani na unabeba taswira ya uchaguzi wa 2030 hivyo chama kitangulizwe mbele na siyo mtu.

"Tuwaacheni walioko madarakani wafanye kazi kwani muda wa uchaguzi bado watu wasubiri hadi muda utakapofika,"alisema Maganya.

Alibainisha kuwa kuna baadhi ya watu wanasiasa wa upinzani na wanaharakati wamekuwa wakibeza na kutoa lugha za maudhi na kudhalilisha wasipewe nafasi kwani wakidai eti serilali iliyopo ni haramu.

"Tusiruhusu tabia hiyo kwani Rais Dk Samia Suluhu anafanya kazi kubwa kwa kushirikiana na chama chake kwani Tume ya Uchaguzi iliita vyama vyote na kutaka visaini sheria za uchaguzi lakini baadhi vilikataa,"alisema Maganya.

Aliongeza kuwa uchaguzi ulikuwa wazi kwa kila chama na viongozi walichaguliwa kwa utaratibu uliowekwa na Tume ya Uchaguzi hivyo havina haja ya kulalamika.

"Kamati za siasa za chama zinapaswa kutatua migogoro ya ardhi kwa kushirikiana na serikali ambayo inafanya kazi kubwa kutatua migogoro hiyo,"alisema Maganya.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya (CCM-NEC) kupitia Jumuiya ya Wazazi na Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa alisema kuwa Jumuiya imekuwa mstari wa mbele kuimarisha chama.

Jumaa alisema kuwa kwa sasa Jumuiya hiyo imeimarika sana na kuwa mhimili mkubwa wa chama katika utekelezaji wa ilani.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa Jumuiya ya Wazazi imefanya kazi kubwa katika utekelezaji wa ilani.

Koka alisema kuwa kwenye uchaguzi Mkuu Jumuiya hiyo iliongoza kwa kupiga kura na kuufanya Mkoa wa Pwani kuongoza kwenye suala la kura.

Awali akitoa taarifa ya Wilaya Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Moses Magogwa alisema kuwa uptikanaji wa huduma kwa sasa kwa wananchi ni asilimia 98.

Magogwa alisema kuwa Hslmashauri ya Manispaa imekuwa ikifanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato ambapo asilimia 60 yanatokana kodi na ushuru mbalimbali wa huduma.

Alisema kuwa ujenzi wa barabara ya njia sita kutoka Maili Moja hadi Picha ya Ndege unatarajia kuanza na barabara kwa ajili ya magari ya mizigo nao utaanzia Picha ya Ndege.

ZAHANATI YA KILIMAHEWA YAWAPUNGUZIA UMBALI WANANCHI KUPATA HUDUMA

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Fadhili Maganya amepongeza ujenzi wa Zahanati ya Kilimahewa Kata ya Tangini Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha na kuitaka kuweka dirisha la Wazee ili waweze kupata huduma kwa urahisi wakati wa kupata matibabu.

Maganya ameysema hayo Mjini Kibaha alipotembelea Zahanati hiyo wakati wa ziara yake ya kutembelea Mkoa wa Pwani kuimarisha uhai wa chama na kutembelea miradi ya maendeleo na kusema kuwa ujenzi huo ni wa mapato ya ndani.

Amesema kuwa wazee waliambiwa kuwa watatengewa dirisha kwa ajili ya kuwapatia huduma hivyo ni vema dirisha hilo likawepo kwa ajili ya kuwahudumia na siyo kusema kuwa wapishwe ili wahudumiwa bali wawe na dirisha lao maalum.

"Tuliahidi kuwa tutawawekea dirisha lao maalum kwa ajili ya kupata huduma hivyo Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha lazima ihakikishe inawawekea dirisha lao ili wapate huduma za afya kwani wao lazima wahudumiwe vizuri pasipokuwa na changamoto,"amesema Maganya. 

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Catherine Saguti alisema kuwa lengo ni kurahisha upatikanaji wa huduma za afya kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha na ulianzishwa kutokana ongezeko la mahitaji ya huduma za afya kwenye eneo hilo.

Saguti amesema kuwa ujenzi ulianza Juni 2024 Halamshauri ilipokea kiasi cha shilingi milioni 233.5 na wananchi walichangia kiasi cha shilingi milioni 1 na shilingi milioni 50 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba hivyo kufanya gharama za mradi kuwa shilingi milioni 284.6.

Amesema kuwa serikali imeajiri wauguzi 32 ambapo Zahanati hiyo ina watumishi saba wanaotoa huduma na Zahanati hiyo imepatiwa watumishi wawili hivyo hakuna upungufu wa watumishi.

Zahanati ilianza kutoa huduma Aprili 2026 na hadi sasa imeshatoa huduma kwa watu 1,103 na inatoa huduma mbalimbali.


Monday, July 27, 2026

HALMASHAURI MANISPAA YA KIBAHA YAPONGEZWA UKUSANYAJI MAPATO NA UTOAJI MIKOPO KWA VIKUNDI

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Fadhili Maganya ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa kuweza kufanikisha ukusanyaji wa mapato.

Maganya ameyasema hayo kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere wakati akizungumza na viongozi wa Jumuiya hiyo wanaccm na uongozi wa Halmashauri wakati wa ziara yake Mkoani Pwani.

Amesema kuwa Halmashauri hiyo imeonyesha jinsi gani inavyopambana katika ukusanyaji wa mapato ambayo yanasaidia katika kuleta maendeleo kwa wananchi.

"Tunaipongeza Halmashauri kwa jitihada zake za ukusanyaji wa mapato na kuifanya kuwa moja ya Halmashauri zinazofanya vizuri nchini kwenye siala la ukusanyaji wa mapato,"amesema Maganya.

Aidha ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa kuvipatia mikopo ya asilimia 10 vikundi vya wajasiriamali kwa ajili ya kuendesha shughuli zao.

"Kama mmeweza kutoa mikopo na kutoa elimu kwa wananchi juu ya kukopa fedha hizo mnafanya jambo zuri ndivyo serikali inavyotaka wananchi wakopeshwe ili wafanye shughuli zao za kiuchumi,"amesema Maganya.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa amesema kuwa mwaka 2024/2025 walitoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 2.1 kwa vikundi 400 vyenye watu zaidi ya 3,000.

Shemwelekwa amesema kuwa changamoto iliyopo ni baadhi ya vikundi kutokuwa na sifa za kukopa lakini fedha zipo kwa vile vinavyokidhi vigezo vinakopeshwa.

Alisema kuwa baada ya mikopo kurejeshwa kulikuwa na madeni yaliyofikia kiasi cha shilingi bilioni 1.2 lakini wamefanya jitihada ya kufanikisha kurejesha na madeni yaliyobakia ni milioni 300.

Tuesday, July 21, 2026

WANANCHI WAJITOLEA KUFUFUA BARABARA

MTAA wa Machinjioni umefungua barabara ya kuelekea Shule ya Msingi Mamlaka na kurahisisha watumiaji kupita kwa urahisi wakiwemo wanafunzi kwenda Shuleni na magari ya kutoa huduma inapotokea dharura kama vile moto.

Barabara  hiyo ilijifunga wakati wa ujenzi wa barabara ya lami ya kutoka Tamco-Mapinga kuelekea Bagamoyo hivyo kusababisha watumiaji wakiwemo  wanafunzi kuzunguka umbali mrefu ili kwenda shule na kwenye makazi hasa wanaotumia usafiri wa magari na pikipiki.

Akizungumza wakati wa zoezi la kujitolea kufungua barabara hiyo ambayo miaka ya nyuma ilikuwa ikipitika Mwenyekiti wa Mtaa wa Machinjioni Kata ya Tangini Wilaya ya Kibaha Aidan Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa wananchi wa eneo hilo.

Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu hasa pale endapo ikitokea dharura kama vile moto au wagonjwa ilikuwa ikiwalazimu kuzunguka mbali hasa kwa matumizi ya vyombo vya moto ikiwemo magari na pikipiki.

"Tulikaa na wananchi na kukubaliana kuchanga kiasi cha shilingi 16,000 kila Kaya ili kufanikisha ufunguaji wa barabara hiyo na wananchi waliridhia na zoezi kuanza ambapo pia tuliwasiliana na Dawasa kwani kuna bomba linapita hapo hivyo walitoa wataalamu wao na kutuelekeza namna na kuchimba ili tusiharibu bomba hilo la maji,"alisema Mchiwa.

Emanuel Sabath alisema kuwa wanaushukuru uongozi wa Mtaa kwa kuwafungulia barabara hiyo hivyo kuwarahisishia na kuwaondolea usumbufu kuzungukia mbali na kupita kwenye eneo la mtu.

Sabath alisema kufunguka barabara hiyo kutarahisisha wananchi kupata huduma ikiwa ni pamoja na inapotokea mgonjwa anataka kupelekwa Hospitali wakiwemo wanawake wajawazito na hata gari la zimamoto kupita kwani kulishawahi kutokea moto lakini gari hilo likashindwa kupita.

Alisema kuwa hata wanafunzi wanaosoma Shule ya Msingi Mamlaka hasa wanaotoka maeneo ya Kilimahewa ambapo iliwabidi wazunguke kupita sehemu nyingine ambapo huwabidi kuzunguka hivyo kuchelewa kufika shuleni.

MASAUNI AWATAKA WANANCHI KUTUMIA FURSA YA HEWA UKAA




Na Mwandishi Wetu, Rufiji

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhandisi Hamad Masauni amewataka wananchi kutumia miradi ya utunzaji wa mazingira ili kupata hewa ukaa na kujiongezea kipato.

Masauni aliyasema hayo Wilayani Rufiji alipokuwa akizungumza na wananchi wakati wa ziara yake Mkoani Pwani kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo.

Alisema kuwa hewa ukaaa ni jambo kubwa la kiuchumi hivyo wananchi watumie kila fursa inayogusa hewa ukaa watumie rasilimali vizuri kupitia misitu. 

"Rufiji ina fursa nyingi za uzalishaji hewa ukaa kupitia, misitu migomba mikorosho kwani hii ni biashara nzuri watumieni wataalam ili wawape moingozo ili kuongeza kipato kwa kutumia fursa hii,"alisema Masauni.

Aidha alisema kuwa mabadiliko ya tabia nchi ni chanzo cha biashara kupitia mkataba wa Paris baada ya kukubaliana nchi zenye rasilimali za kupunguza hewa ukaa zilipwe.

"Kupitia kilimo madini na faida ya kuhifadhi miti tutalipwa hiyo ni changamoto muifanyie kazi kwani mna rasilimali za kutosha za kuwa miradi ya hewa ukaa,"alisema Masauni

Aliongeza kuwa Watanzania wanapaswa kutunza amani iliyopo na kuachana na yale yanayoweza kuharibu amani ya nchi kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

"Kipindi cha nyuma kulitokea changamoto hata wanaccm walikuwa hawavai sare za chama lakini sasa watu wana amani hivyo tunzeni amani kwani  umuhimu wa amani unajulikana na vijana wanasababu ya kuenzi umoja na kurithisha watoto wetu na Muungano ndiyo kiungo cha amani kupitia  waasisi wa taifa letu wametuachia msingi wa amani,"alisema Masauni.

Aliipongeza Wilaya ya Rufiji kwa kutekeleza kikamilifu kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye miradi mbali mbali ya maendeleo ya elimu afya miundombinu kilimo maji.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani Mwinshehe Mlao alisema kuwa Wilaya hiyo imepiga hatua kubwa ya kimaendeleo ukilinganisha na zamani kupitia uongozi wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Mlao alisema kuwa kwa ujumla Mkoa umepiga hatua kubwa ya maendeleo hivyo watu wanapaswa kuona jinsi gani maendeleo yaliyopatikana chini ya CCM.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge 
alisema kuwa mwaka wa fedha Mkoa ulipangiwa kukusanya bilioni 88 lakini hadi Juni 30 mwaka huu tayari zimekusanywa bilioni 135 na kuwa mkoa wa pili baada ya Dar es Salaam. 

Kunenge alisema kuwa Mkoa unajivunia Rais kwa kuwatumikia Watanzania na Rufiji ina miradi mikubwa ya uwekezaji na moja mradi alionyesha Urusi ni kilimo cha ndizi kupitia moja ya kampuni kubwa afrika.

Alisema kuwa kwa sasa kuna mifugo mingi na kuna ranchi ndogo na uchumi usitegemee chanzo kimoja ili kuwa salama kwa kutumia bahari na utalii kwani huwezi kushindana na mabadiliko ya dunia ni kijini na dira 2050 inataka kuwa na ajira milioni nane pato la Taifa trilioni moja pato la mwnanchi milioni 18 kwa mwaka.

Akikaribisha ugeni wa Waziri Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Luteni Kanali Fredrick Komba alisema kuwa Wilaya hiyo imefanikiwa kupanda miti ya mikorosho ipatayo milioni 1.5.

POLISI KATA MAILIMOJA AMTEMBELEA MZEE NA KUTOA MSAADA.





Na Mwandishi Wetu, Kibaha

Polisi Kata wa Mailimoja, Mkaguzi wa Polisi, Tupilike Mwabulambo ameambatana na Stesheni Sajenti Lusekelo Mwakalinga wa Wilaya ya Kibaha kumtembelea mzee Hamisi Nampatima wa mtaa wa Uyaoni ikiwa ni sehemu ya mpango wa kuwafikia wahitaji waliopo kwenye kata yake na kutoa msaada.

Akikabidhi baadhi ya mahitaji kwa mzee huyo Julai 20, 2026 INSP Tupilike alieleza kuwa kuna makundi mbalimbali katika jamii ambao wana changamoto ikiwemo za kiusalama na mahitaji muhimu hivyo anatembelea kaya hizo kuwasikiliza na kutoa kile alichojaliwa kwa wakati huo.

Kwa upande wake Mzee Hamis Nampatima, alilishukuru Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kwa msaada wanaompatia kwani sio mara ya kwanza kufika kwake, Mara kadhaa Sajenti wa Polisi Salum Ally wa Polisi Wilaya ya Kibaha amekua akimsaidia kwa kumpatia pesa na mahitaji mbalimbali ya nyumbani.

Naye, Mwenyekiti wa Mtaa wa Uyaoni, Katani humo, Bw. Fadhili Kindamba alipongeza Jeshi la Polisi kwa namna wanavyoshirikiana na wananchi kuimarisha ulinzi na usalama na kutatua changamoto zao zingine za kijamii.

Sunday, July 19, 2026

WANANCHI MTAA WA MACHINJIONI WAJITOLEA KUFUNGUA BARABARA

MTAA wa Machinjioni umefungua barabara ya kuelekea Shule ya Msingi Mamlaka na kurahisisha watumiaji kupita kwa urahisi wakiwemo wanafunzi kwenda Shuleni na magari ya kutoa huduma inapotokea dharura kama vile moto.

Barabara  hiyo ilijifunga wakati wa ujenzi wa barabara ya lami ya kutoka Tamco-Mapinga kuelekea Bagamoyo hivyo kusababisha watumiaji wakiwemo  wanafunzi kuzunguka umbali mrefu ili kwenda shule na kwenye makazi hasa wanaotumia usafiri wa magari na pikipiki.

Akizungumza wakati wa zoezi la kujitolea kufungua barabara hiyo ambayo miaka ya nyuma ilikuwa ikipitika Mwenyekiti wa Mtaa wa Machinjioni Kata ya Tangini Wilaya ya Kibaha Aidan Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa wananchi wa eneo hilo.

Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu hasa pale endapo ikitokea dharura kama vile moto au wagonjwa ilikuwa ikiwalazimu kuzunguka mbali hasa kwa matumizi ya vyombo vya moto ikiwemo magari na pikipiki.

"Tulikaa na wananchi na kukubaliana kuchanga kiasi cha shilingi 16,000 kila Kaya ili kufanikisha ufunguaji wa barabara hiyo na wananchi waliridhia na zoezi kuanza ambapo pia tuliwasiliana na Dawasa kwani kuna bomba linapita hapo hivyo walitoa wataalamu wao na kutuelekeza namna na kuchimba ili tusiharibu bomba hilo la maji,"alisema Mchiwa.

Emanuel Sabath alisema kuwa wanaushukuru uongozi wa Mtaa kwa kuwafungulia barabara hiyo hivyo kuwarahisishia na kuwaondolea usumbufu kuzungukia mbali na kupita kwenye eneo la mtu.

Sabath alisema kufunguka barabara hiyo kutarahisisha wananchi kupata huduma ikiwa ni pamoja na inapotokea mgonjwa anataka kupelekwa Hospitali wakiwemo wanawake wajawazito na hata gari la zimamoto kupita kwani kulishawahi kutokea moto lakini gari hilo likashindwa kupita.

Alisema kuwa hata wanafunzi wanaosoma Shule ya Msingi Mamlaka hasa wanaotoka maeneo ya Kilimahewa ambapo iliwabidi wazunguke kupita sehemu nyingine ambapo huwabidi kuzunguka hivyo kuchelewa kufika shuleni.