Tuesday, August 11, 2026

EDDY CHARITY YAWAPA TABASAMU KISARAWE SAFE HOUSE

JAMII imeaswa kugharamia suala la elimu kwenye vituo vya watoto wenye uhitaji ili kwa kutatua changamoto za kielimu kwa watoto hao waweze  kutimiza ndoto zao.

Hayo yalisemwa na katibu wa kikundi cha Eddy Charity cha Kibaha, Edgar Mwakalosi wakati kilipotembelea kituo cha Kisarawe Safe House na kutia misaada mnalimbali.

Mwakalosi alisema kuwa vituo hivyo vinachangamoto nyingi ikiwa ni pamoja namna ya kuwapatia elimu watoto waishio kwenye vituo hivyo hasa wanapofikia hatua ya kuelekea kufanya mitihani ya kitaifa au kwenda vyuoni.

"Jamii inapaswa kuvisaidia vituo hivyo kwenye suala la kielimu ili watoto wanaolelewa huko wapate elimu inayostahili kufikia ndoto zao kwani kila mmoja ana ndoto yake ili imfikishe pale alipodhamiria,"alisema Mwakalosi.

Alisema kuwa licha ya kutoa misaada mbalimbali lakini wametoa vifaa vya shule na fedha kwa ajili ya kukabili changamoto hizo za kielimu na mahitaji muhimu ya kila siku.

"Tumekuwa tukijitolea misaada mbalimbali kwenye vituo vya watoto wenye mahitaji lengo ni kuona wnapata tabasamu na kuondoa tofauti ya watoto hao na wale wanaoishi na familia zao,"alisema Mwakalosi.

Naye Meneja wa kituo hicho Florida Frank alisema kuwa mbali ya changamoto mbalimbali kubwa ni kwa madarasa ya mtihani ambapo huwabidi kukaa kambini hasa wale wa kidato cha pili na cha nne kwani kwa sasa wanapaswa kulipa shilingi 60,000 kwa mwanafunzi mmoja na wako wanne.

Frank alisema hata pale wanapokuwa wamechaguliwa kwenda vyuoni gharama zinakuwa ni kubwa sana hivyo kituo kuelemewa na mzigo mkubwa wa kifedha na kuomba wadau kujitolea kuunga mkono kituo chao.

Alisema kuwa jamii inapaswa kupandikiza kitu muhimu katika maisha ikiwa ni pamoja na kuwezesha kwenye suala la elimu kituo hicho kikianzishwa mwaka 2003 kikiwa na watoto watano na sasa kina watoto 48 wanaosoma elimu tofauti hadi vyuo vikuu.

Monday, August 10, 2026

WANNE WAFA 46 WAJERUHIWA AJALINI

WATU wanne wamefariki dunia na wengine 46 kujeruhiwa baada ya basi dogo walilokuwa wakisafiria kutoka Vikumburu Kisarawe kwenda Dar es Salaam kupinduka.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Salim Morcase ilisema kuwa basi hilo liliacha njia na kupinduka na kusababisha vifo na majeruhi.

Morcase alisema kuwa ajali hiyo ilitokea Agosti  9 mwaka huu majira ya saa 11:00 jioni huko eneo la kona ya Kinyanyiko katika barabara ya Pugu Kisarawe Wilaya ya Kisarawe.

"Gari lenye namba za usajili T 177 DBV aina ya Fuso likitokea Vikumburu kwenda Dar es Salaam likiendeshwa na Salehe Mtumwa (35) na Mkazi wa Chanika Dar es Salaam liliacha barabara na kupinduka kisha kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi kwa watu 46,"alisema Morcase.

Alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi ambapo dereva alishindwa kulimudu gari kwenye mteremko mkali hivyo kupelekea gari hilo kupinduka.

Aliwataja waliofariki kuwa ni dereva wa gari hilo Salehe Mtumwa (35) na Mkazi wa Chanika Dar es Salaam,  Mwika Gwesele (38) Mkazi wa Dar es Salaam, Fatuma Momba Mkazi wa Buguruni Dar es Salaam na Sivijui Samatha (40) Mkazi wa Dar es Salaam.

Aliwataja majeruhi wanaopatiwa matibabu Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ni Hamis Mtitu (55) Mkazi wa Mbagala, Dar es Salaam, Farida Hassan (28) Mkazi wa Vingunguti Dar es Salaam, Husna Bakari (26) Mkazi wa Buza Dar es Salaam, Radhia Sultan (36)Mkazi wa Tabata Dar es Salaam, Neema Hassan (42) Mkazi wa Temeke, Dar es Salaam.

Majeruhi wengine ni Pilli Kondo (40) Mkazi wa Tabata Dar es Salaam, Salama Ramadhan (40)Mkazi wa Kigogo Dar es Salaam, Salumu Rajabu (56) Mkazi wa Mbande Dar es Salaam, Pilli Habibu (28) Mkazi wa Majohe Dar es Salaam, Amina Ramadhan (64) Mkazi wa Boga Wilaya ya Kisarawe.

"Majeruhi wengine saba wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe ambapo kati yao wanaume ni watatu na wanawake ni wanne huku majeruhi wengine 29 wamepatiwa matibabu katika Hospitali hiyo ya Kisarawe na kuruhusiwa," alisema Morcase.

Aidha alisema kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linawataka madereva wote wa vyombo vya moto kuzingatia sheria ya usalama barabarani pamoja na kanuni zake ili kuepusha ajali zinazosababishwa na uzembe. 

"Hatua kali zitaendelea kuchukuliwa kwa madereva watakaosababisha ajali kwa uzembe au kutokuzingatia sheria za usalama barabarani na kanuni zake,"alisema Morcase.

Sunday, August 9, 2026

WATANZANIA WAASWA KUSAIDIA ELIMU WATOTO WA VITUO WENYE UHITAJI





JAMII imeaswa kugharamia suala la elimu kwenye vituo vya watoto wenye uhitaji ili kwa kutatua changamoto za kielimu kwa watoto hao waweze  kutimiza ndoto zao.

Hayo yalisemwa na katibu wa kikundi cha Eddy Charity cha Kibaha, Edgar Mwakalosi wakati kilipotembelea kituo cha Kisarawe Safe House na kutia misaada mnalimbali.

Mwakalosi alisema kuwa vituo hivyo vinachangamoto nyingi ikiwa ni pamoja namna ya kuwapatia elimu watoto waishio kwenye vituo hivyo hasa wanapofikia hatua ya kuelekea kufanya mitihani ya kitaifa au kwenda vyuoni.

"Jamii inapaswa kuvisaidia vituo hivyo kwenye suala la kielimu ili watoto wanaolelewa huko wapate elimu inayostahili kufikia ndoto zao kwani kila mmoja ana ndoto yake ili imfikishe pale alipodhamiria,"alisema Mwakalosi.

Alisema kuwa licha ya kutoa misaada mbalimbali lakini wametoa vifaa vya shule na fedha kwa ajili ya kukabili changamoto hizo za kielimu na mahitaji muhimu ya kila siku.

"Tumekuwa tukijitolea misaada mbalimbali kwenye vituo vya watoto wenye mahitaji lengo ni kuona wnapata tabasamu na kuondoa tofauti ya watoto hao na wale wanaoishi na familia zao,"alisema Mwakalosi.

Naye Meneja wa kituo hicho Florida Frank alisema kuwa mbali ya changamoto mbalimbali kubwa ni kwa madarasa ya mtihani ambapo huwabidi kukaa kambini hasa wale wa kidato cha pili na cha nne kwani kwa sasa wanapaswa kulipa shilingi 60,000 kwa mwanafunzi mmoja na wako wanne.

Frank alisema hata pale wanapokuwa wamechaguliwa kwenda vyuoni gharama zinakuwa ni kubwa sana hivyo kituo kuelemewa na mzigo mkubwa wa kifedha na kuomba wadau kujitolea kuunga mkono kituo chao.

Alisema kuwa jamii inapaswa kupandikiza kitu muhimu katika maisha ikiwa ni pamoja na kuwezesha kwenye suala la elimu kituo hicho kikianzishwa mwaka 2003 kikiwa na watoto watano na sasa kina watoto 48 wanaosoma elimu tofauti hadi vyuo vikuu.

Thursday, August 6, 2026

AHUKUMIWA MAISHA JELA KWA ULAWITI MWINGINE MIAKA 20 NA FAINI M 1 KWA KUDHALILISHA MTOTO

SALIM Mang'ombe (29) mkazi wa Wilaya ya Bagamoyo amehukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kosa la kulawiti mtoto mwenye umri wa miaka (10) ambaye alikuwa ni jirani yake.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Salim Morcase alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwezi Julai.

Kwenye tukio lingine Salim Masanja (33) Mkazi wa Wilayani Kibaha amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela na kulipa fidia ya shilingi milioni moja kwa tuhuma za kumdhalilisha mtoto wa kike (6).

Morcase amesema kuwa mshtakiwa huyo ni baba mdogo wa mhanga ambaye alikuwa akiishi naye nyumbani kwake na kesi hizo ni za ukatili wa kijinsia.

Amesema kuwa kesi zilizofikishwa mahakamani kwa kipindi hicho zilikuwa 117 huku kesi 63 zilisikilizwa na kumalizika ambapo kesi 48 zimepata mafanikio.

Amesema kuwa jamii kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanapaswa kushirikiana ili kukabiliana na vitendo vya ukatili kwa watoto.

Wednesday, August 5, 2026

POLISI YAWAREJESHA SHULENI WANAFUNZI 114

JESHI la Polisi Mkoani Pwani limefanikisha kuwarejesha Shuleni wanafunzi 114 ambao walishindwa kuripoti shule kutokana na sababu mbalimbali.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Salim Morcase amesema kuwa jumla ya wanafunzi 573 walikuwa hawajaripoti shuleni.

Morcase amesema kuwa kati ya wanafunzi hao ambao hawakuripoti Shule za Msingi walikuwa 251 na wa Sekondari walikuwa ni 322 ambao walibainika katika kipindi hicho licha ya kuwa wanafunzi hao kuwa na wa miaka tofauti tofauti.

Amesema kuwa changamoto nyingine ni mimba za utotoni ukosefu wa mahitaji ya msingi kama vile sare za Shule na madaftari  na changamoto za kiafya na kiuchumi.

Amewataka wazazi na walezi kushirikina na viongozi wa dini na wa kiserikali katika kupambana na viashiria vya vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto ndani ya jamii.


Saturday, August 1, 2026

HALMASHAURI YA MANISPAA KIBAHA YAZINDUA MAGARI MRADI WA (TACTIC)

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imezindua magari mawili yatakayotumika kwenye mradi wa ujenzi wa barabara za lami kwenye kupitia mradi wa uboreshaji miundombinu ya Miji na Vijiji (TACTIC) wenye thamani ya shilingi bilioni 19.8

Akindua magari hayo ambayo yatatumika kwenye mradi huo Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo alisema magari hayo yatawezesha utekelezaji mradi kuwa rahisi.

Mawazo alisema kuwa magari hayo ni moja ya makubaliano mkataba wa mradi huo na yakimaliza kutumika yanarudi Halmashauri kwa ajili ya shughuli zingine za kutoa huduma kwa wananchi kupitia wataalamu.

"Mradi huu unaenda kuleta mabadiliko chanya na uboreshaji wa miundo mbinu mbalimbali ya Manispaa ya Kibaha na kuwa na mwonekano mzuri na kuleta urahisi wa usafiri na usafirishaji,"alisema Mawazo.

Alisema kuwa katika miradi hiyo ya Tactic wanakwenda kuitekeleza kwa ubora zaidi na Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha inaenda kuwa ya kwanza na mfano kwa Halmashauri zingine katika utekelezaji na usimamizi wa miradi hii nchini.

"Wananchi wa Kibaha wanapaswa kujivunia na kutangaza maendeleo yanayofanywa na serikali hii kwani Manispaa ya Kibaha ina neemeka na dira ya Rais na mmeona maendeleo yanavyokuja kwa kasi na tutakuwa Halmashauri ya mfano kwa kila kitu,"alisema Mawazo.

Akisoma taarifa ya mradi huo Ofisa Utumishi  Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mrisho Mlela alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuleta miradi yenye fedha nyingi na usimamizi mzuri wa viongozi wa Wilaya na Mkoa kwa utekelezaji wa Ilani kwa maslahi ya Manispaa ya Kibaha.

Mlela alimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa kwa usimamizi mzuri wa masuala mbalimbali ya mapato usimamizi wa miradi pamoja na tija katika utendaji wa Halmashauri.

Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha imepokea magari hayo mawili kutoka kwenye Mkataba wa mradi wa Tactic ambapo yatatumika katika mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 4.8 Tughe-Anglikana barabara ya Picha ya Ndege - Lulanzi na soko la Loliondo Mnarani.

MADARASA JANJA KUPUNGUZA CHANGAMOTO UPUNGUFU WA WALIMU NCHINI

MEYA wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo amezindua Darasa Janja (Live Teaching) Shule ya Sekondari Bundikani na kuiomba Serikali kuanzisha madarasa hayo kote nchini ili kukabiliana na upungufu wa walimu

Mawazo alitoa ombi hilo wakati akizindua darasa hilo shuleni hapo ambapo shule hiyo ni Sekondari ya Kata ya Maili Moja Wilayani Kibaha na kuwa darasa janja yatasaidia kuwafanya wanafunzi kuwa na ari ya kusoma.

Amesema kuwa mwalimu mmoja anayefundisha kupitia darasa janja moja anaweza kufundisha shule zote ambazo zitakuwa zimeunganishwa kwenye mfumo huo wa darasa la aina hiyo kote nchini kwa wakati mmoja.

"Mfumo huu wa darasa janja ni mzuri kwa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa walimu kwani mwalimu mmoja anauwezo kufundisha shule zote ambazo zimeunganishwa kwenye mfumo huo,"amesema Nicas.

Aidha amesema kuwa pia mbali ya kufundisha wakati mmoja pia yale aliyofundisha mwalimu huyo yanaweza kurekodiwa na kuwafundisha wanafunzi wengine kwa ubora ule ule.

"Jambo zuri ni kuwa walimu wote wanaofundisha kupitia madarasa janja wote ni wale wenye umahiri wa kufundisha hivyo watawajengea wanafunzi uwezo mkubwa wa kujifunza na kupata ujuzi,"amesema Mawazo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mrisho Mlela amesema kuwa wataendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa janja kwenye shule za sekondari.

Mlela amesema kuwa wameendelea kuboresha sekta ya elimu kwa kujenga shule tatu za mfumo wa Kiingereza na shule hizo zote zimejengwa kutokana na fedha za mapato ya ndani na kutengeneza madawati viti na meza 4,000 kwa shule za msingi na sekondari.

Naye Mkuu wa Shule ya Bundikani Bernard Muyenjwa amesema kuwa wanaishukuru Serikali kwa kuwapatia darasa hilo janja kwani litarahisisha katika ufundishaji na kupunguza changamoto ya upungufu wa walimu.

Muyenjwa amesema kuwa kuanzishwa kwa darasa janja hilo shuleni kwao kutasaidia walimu kufundisha bila ya kuchoka wala kutumia nguvu kubwa na kuwapa wanafunzi umahiri na kujua namna ya kutumia teknolojia.

mwisho