Hayo yalisemwa na katibu wa kikundi cha Eddy Charity cha Kibaha, Edgar Mwakalosi wakati kilipotembelea kituo cha Kisarawe Safe House na kutia misaada mnalimbali.
Mwakalosi alisema kuwa vituo hivyo vinachangamoto nyingi ikiwa ni pamoja namna ya kuwapatia elimu watoto waishio kwenye vituo hivyo hasa wanapofikia hatua ya kuelekea kufanya mitihani ya kitaifa au kwenda vyuoni.
"Jamii inapaswa kuvisaidia vituo hivyo kwenye suala la kielimu ili watoto wanaolelewa huko wapate elimu inayostahili kufikia ndoto zao kwani kila mmoja ana ndoto yake ili imfikishe pale alipodhamiria,"alisema Mwakalosi.
Alisema kuwa licha ya kutoa misaada mbalimbali lakini wametoa vifaa vya shule na fedha kwa ajili ya kukabili changamoto hizo za kielimu na mahitaji muhimu ya kila siku.
"Tumekuwa tukijitolea misaada mbalimbali kwenye vituo vya watoto wenye mahitaji lengo ni kuona wnapata tabasamu na kuondoa tofauti ya watoto hao na wale wanaoishi na familia zao,"alisema Mwakalosi.
Naye Meneja wa kituo hicho Florida Frank alisema kuwa mbali ya changamoto mbalimbali kubwa ni kwa madarasa ya mtihani ambapo huwabidi kukaa kambini hasa wale wa kidato cha pili na cha nne kwani kwa sasa wanapaswa kulipa shilingi 60,000 kwa mwanafunzi mmoja na wako wanne.
Frank alisema hata pale wanapokuwa wamechaguliwa kwenda vyuoni gharama zinakuwa ni kubwa sana hivyo kituo kuelemewa na mzigo mkubwa wa kifedha na kuomba wadau kujitolea kuunga mkono kituo chao.
Alisema kuwa jamii inapaswa kupandikiza kitu muhimu katika maisha ikiwa ni pamoja na kuwezesha kwenye suala la elimu kituo hicho kikianzishwa mwaka 2003 kikiwa na watoto watano na sasa kina watoto 48 wanaosoma elimu tofauti hadi vyuo vikuu.








