MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Mussa Mansour ametoa vifaa vya ujenzi wa ofisi ya CCM Kata ya Mkuza Wilaya ya Kibaha Mjini.
Akizindua ujenzi wa ofisi hiyo na kuhudhuria Mkutano Maalum wa Kata hiyo Mansour amesema kuwa alipewa ombi na Kata hiyo ambayo inatumia ofisi za tawi kwa ajili ya shughuli zake.
Mansour amesema kuwa lengo la kutoa vifaa hivyo vya ujenzi ni kufanikisha Kata hiyo kuwa na ofisi ili kuwa na ofisi badala ya kutegemea ofisi ambazo siyo zao.
"Nimejitolea ili kuimarisha chama na ningetamani uchaguzi wa ndani ya chama mwakani ufanyike kwenye ofisi hizo kikubwa ni uongozi kufuata taratibu ili tuweze kufikia lengo la kuzikamilisha,"amesema Mansour.
Amesema kuwa aliahidi mchanga, simenti, kokoto nondo na matofali anashukuru kwani vyote amevitoa kilichobaki ni ujenzi tu kuanza na uzinduzi uliifanyika ndiyo ishara ya kazi kuanza.
Naye Mwenyekiti wa Kata ya Mkuza Matata Ngollo amesema kuwa wanamshukuru Mjumbe huyo wa Halmashauri ya Mkoa kwa kujitoa kwake kusaidia ujenzi huo.
Ngollo amesema kuwa wanamshukuru kwani vifaa hivyo vitafanya ujenzi kwa asilimia 80 na itabaki umaliziaji tu hivyo kuifanya Kata nayo kumiliki ofisi yake.
Mjumbe huyo alikuwa mgeni rasmi kwenye Mkutano Maalum wa Kata ambapo alizungumza na viongozi mbalimbali wa ngazi za matawi, alizindua tawi la CCM la waendesha bodaboda tawi la Barckyard, alitembelea kijiwe cha draft na kutoa fedha kwa makundi maalum wakiwemo wajane, wazee, bodaboda na watu wenye ulemavu na vijana na alitembelea soko la Mkuza.






