Sunday, September 13, 2026

NYIKA NA BABERIAN KUKIPIGA FAINALI MEETING POINT SUPER CUP 2026

TIMU za soka za Nyika na Baberian zinatarajiwa kuchuana kwenye hatua ya fainali ya kinyanganyiro cha Meeting Point Super Cup baada ya kushinda michezo yao ya hatua ya nusu fainali.

Nyika ilifanikiwa kuifunga Kiduli kwa mikwaju ya penati 4-3 kwenye nusu fainali ya kwanza na Baberian waliifunga Nyumbu kwa mabao 2-0 michezo yote ilifanyika uwanja wa Mwendapole Kibaha.

Mchezo huo wa hatua ya fainali utachezwa kwenye uwanja wa Mwendapole ambapo mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu ndiyo utaanza kati ya Kiduli na Nyumbu.


NYIKA NA BABERIAN KUCHUANA FAINALI YA MEETING POINT SUPER CUP

MIAMBA ya soka Mkoa wa Pwani Nyika na Baberian zinatarajiwa kuchuana kwenye hatua ya fainali ya kinyanganyiro cha Meeting Point Super Cup baada ya kushinda michezo yao ya hatua ya nusu fainali.

Nyika ilifanikiwa kuifunga Kiduli kwa mikwaju ya penati 4-3 kwenye nusu fainali ya kwanza na Baberian waliifunga Nyumbu kwa mabao 2-0 michezo yote ilifanyika uwanja wa Mwendapole Kibaha.

Mchezo huo wa hatua ya fainali utachezwa kwenye uwanja wa Mwendapole ambapo mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu ndiyo utaanza kati ya Kiduli na Nyumbu.

MUHEZA WALILIA RUTI YA DALADALA KWENDA MAILI MOJA

WAKAZI wa Mtaa wa Muheza Kata ya Maili Moja Wilayani Kibaha Mkoani Pwani wameomba kupatiwa ruti ya Daladala kutoka Maili Moja kwenda kwenye Mtaa huo na kupunguza gharama za pikipiki ambazo ni 4,000.

Aidha wamesema usafiri wao mkubwa ni pikipiki na hutumia kiasi cha shilingi 8,000 kwenda na kurudi kufuata mahitaji au kupata huduma za msingi za kila siku.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Diwani wa Kata ya Maili Moja mwananchi Veronica Christopher alisema kuwa maombi yao ni kupatiwa ruti ili wawe na usafiri wa uhakika.

Christopher alisema kuwa suala la usafiri ni changamoto kubwa kwani hakuna usafiri wa uhakika zaidi ya pikipiki ambapo gharama zake ni kubwa sana na kipindi cha mvua gharama inaongezeka kwani barabara inaharibika sana kutokana na utelezi na tope jingi.

"Kwa sasa maisha ni magumu sana hebu fikiria ili uende kufuata mahitaji au huduma uwe na 8,000 au zaidi kwa kwenda na kurudi na kwenda huko ni lazima kwani ndiko huduma na mahitaji muhimu hupatikana hivyo tukipata ruti ya Daladala itatupunguzia gharama,"alisema Christopher.

Alisema kuwa Maili Moja ndiyo Mjini na kwa wale wanaofanya safari kwenda maeneo mbalimbali lazima wafike Maili Moja ambako ndiko wanakopata mahitaji lakini usafiri gharama ni kubwa sana za kwenda na kurudi.

Akijibu hoja hiyo Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo alisema kuwa mpango huo ni mzuri na leo atakutana na wenye viti wa Mitaa iliyoko kwenye Kata ya Maili Moja na LATRA ofisini kwake ili kupanga ruti hiyo.

Mawazo alisema kuwa hoja hiyo ni ya msingi kwani Serikali ina lengo la kuwapunguzia mzigo wananchi kwa kuwatatulia changamoto kama hizo ambazo ziko ndani ya uwezo wa serikali.

Naye Diwani wa Kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi alisema mpango wa kuboresha barabara kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini TARURA imetenga shilingi milioni 50 kwa kila Kata ambapo Mtaa huo wenye wakazi 12,000 na Mtaa wa Maili Moja wenye wakazi 4,000 watanufaika.

Lutambi alisema kuwa fedha hizo zimetengwa kwenye bajeti ya mwaka 2026/2027 kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu ya barabara ikiwemo madaraja na makalavati.

Alisema kuwa baadhi ya maeneo mvua ikinyesha kwenye vivuko hakupitiki kutokana na maji kujaa ambapo kipaumbele kitawekwa kwenye maeneo ya Mkwanda Machokodo Makanyaga na Kwakamese kutawekwa Makalavati.

Saturday, September 12, 2026

NYIKA FC YAINGIA FAINALI MICHUANO MEETING POINT SUPER CUP

TIMU ya soka ya Nyika Fc imeifunga Kiduli Fc kwa penati 4-3 kwenye michuano ya Meeting Point Super Cup kwenye uwanja wa Mwendapole Kibaha. 

Timu hizo ziliingia kwenye hatua ya penati baada ya kufungana goli 1-1 hadi dakika 90 zilipotamatika kwenye mchezo huo.

Kutokana na matukio hayo Nyika imeingia hatua ya fainali ikisubiri mchezo kati ya Nyumbu na Baberian mchezo utakaopigwa kwenye uwanja huo huo wa Mwendapole.

DIWANI LUTAMBI AWATAKA WANANCHI KURASIMISHA ARDHI WAMILIKI KISHERIA

WANANCHI wa Mtaa wa Muheza Kata ya Maili Moja wametakiwa kuchangamkia fursa ya urasimishaji ardhi baada ya serikali kupunguza gharama kutoka 150,000 hadi 130,000.

Akizungumza na wananchi wa Mtaa huo Diwani wa Kata ya hiyo Ramadhan Lutambi alisema kuwa hiyo ni fursa kwa wananchi kuelekea kupata umiliki wa ardhi kisheria.

Lutambi alisema kuwa kumiliki ardhi kisheria kuna faida nyingi ikiwa ni pamoja na kuepukana na migogoro ya ardhi ambaye imeleta changamoto kubwa kwa wananchi.

"Tunaishukuru Serikali kwa kupunguza gharama za urasimishaji ardhi hivyo kuwafanya wananchi kumiliki ardhi kisheria hivyo kuwa na umiliki halali na kupunguza migogoro,"alisema Lutambi.

Akizungumzia suala la changamoto ya maji alisema kuwa kuna mradi wa maji ambao kwa sasa uko kwenye utekelezaji ambapo mitaa yote itapitiwa ambapo kwenye mtaa huo watu zaidi ya 8,000 hawapati huduma hiyo.

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo alisema kuwa mikopo ya asilimia 10 ipo kwa makundi wakiwemo wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Mawazo alisema kuwa fedha zimetengwa jambo kubwa ni walengwa kuunda vikundi ambavyo vitatimiza masharti ikiwa ni pamoja na usajili huku kwa watu wenye ulemavu hata kwa mtu mmoja anaruhusiwa.

Akizungumza kwa njia ya simu Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John alisema kuwa mradi wa maji wa Pangani utaondoa changamoto ya maji kwenye mtaa huo hivyo wananchi wawe na subira.

John alisema kuwa Serikali imekuwa ikipambana kuhakikisha wananchi wanaondokana na changamoto hiyo ambayo imekuwa kero kubwa lakini inakwenda kupatiwa suluhu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa alisema kuwa mipango iliyopo ni ujenzi wa Shule ya Sekondari na Zahanati.

Shemwelekwa alisema kuwa kuhusu urasimishaji vifaa vimenunuliwa kwa ajili ya urasimishaji hivyo wananchi wajiandae na watazichukua changamoto zilizotolewa na wananchi ili wazipatie ufumbuzi.

Wednesday, September 9, 2026

ULEGA ATAKA MIUNDOMBINU ITOE HUDUMA KIPINDI CHA MVUA ZA ELNINO.

WAZIRI wa Ujenzi Abdala Ulega ametaka hatua za haraka kuchukuliwa ili miundombinu ya barabara iendelea kutoa huduma hata wakati wa mvua kubwa za Elnino zinazotarajiwa kuanza kunyesha hivi karibuni kote nchini.

Ulega ametoa maelekezo hayo akiwa mkoani Pwani katika ziara yake aliyoianza ya ukaguzi wa maandalizi ya kimiundombinu kufuatia maelekezo ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa watendaji wa Serikali kuhakikisha nchi inakingwa na athari za mvua zinazoweza kujitokeza wakati huo.

Amesema kuwa inapaswa kufanyika kwa ukaguzi wa barabara na madaraja kote nchini kama sehemu ya maandalizi dhidi ya mvua kubwa za Elnino zinazotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Aidha amesema kuwa ukaguzi huo ndiyo utakuwa msingi wa kufahamu ni wapi na wapi panahitaji kufanyiwa kazi ili mvua hizo zisiathiri mzunguko wa watu na biashara.

"Naagiza Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) kuhakikisha barabara na madaraja yote nchini yanakaguliwa na hatua za haraka kuchukuliwa ili miundombinu hiyo iendelea kutoa huduma hata wakati wa mvua kubwa zinazotarajiwa kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini",amesema Ulega.

Amesisitiza kuwa pamoja na uwepo wa vifaa ³na mitambo utayari wa wataalam na watendaji ndio msingi wa kuhakikisha nchi inapita salama katika kipindi cha mvua hizo.

"Wizara ya Ujenzi kwa kushirikiana na TANROADS kufanya tathmini ya kila wiki katika mikoa yote nchini ili kubaini maeneo yoyote yanayohitaji kuongezewa nguvu kwa wakati ili kuhakikisha huduma za dharura zinafika kila kona ya nchi,"amesema Ulega.

Aliingeza kuwa TANROADS mejipanga katika kanda mbalimbali na Mkoa wa Pwani ndiyo kitovu cha kanda zote kwa ajili maandalizi ya tahadhari ya mvua za Elnino.

Pia alikagua pia vifaa mbalimbali vitakavyotumika kufanya matengenezo ya dharura katika miundombinu ya barabara na madaraja nchini
kote.

Meneja wa TANROADS Mkoa waPwani Mhandisi Joel Mwambungu amesema kuwa wamejipanga kukabiliana na athari za mvua hizo kwa ununuzi na usambazaji wa vifaa vya dharura katika maeneo mbalimbali nchini.

Mwambungu amesema kuwa TANROADS tayari ina kalavati za chuma zenye jumla ya urefu wa mita 5,638 zitakazotumika katika maeneo ambayo barabara au madaraja yanaweza kupata athari kutokana na mvua hizo.

mwisho.

Tuesday, September 8, 2026

MEYA DK NICAS MAWAZO AKABIDHI PHOTOCOPY MACHINE KWA SEKONDARI YA MWAMBISI




MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo amekabidhi mashine ya kudurusu karatasi kwa Shule ya Sekondari Mwambisi na kusema kuwa itapunguza gharama za uandaaji mitihani.

Mawazo alikabidhi mashine kwa uongozi wa shule hiyo kwa kushuhudiwa na Ofisa elimu Sekondari, bodi za Shule za Sekondari za Manispaa, baadhi ya wazazi na wanafunzi wa Shule hiyo.

Amesema kuwa Serika inaendelea kuwaka mazingira mazuri ya kufundishia na kujifunzia kwa wanafunzi ili kuongeza ufaulu na kupunguza changamoto za Shule ndani ya Manispaa.

"Utoaji wa mashine hii ni kuunga mkono jitihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan ambaye ni kinara wa elimu kwani amejitahidi kujenga miundombinu ya elimu,"amesema Mawazo.

Aidha amesema kuwa miaka ya nyuma Shule zilijengwa na wananchi lakini kwa miaka ya sasa Serikali imejenga miundombinu mingi ya elimu hivyo wadau nao waunge mkono serikali.

"Kuhusu bweni wenyeviti wa bodi za Shule zielezee kwenye mipango yao juu ya mahitaji hayo na kama yapo tutaongea na wadau ili kushirikiana na serikali kuyajenga kama kuna mahitaji hayo,"amesema Mawazo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Yahaya Mtonda amesema kuwa kuna haja ya kuipandisha hadhi Shule hiyo ili iwe na kidato cha tano.

Mtonda amesema kuwa baadhi ya wanafunzi wanashindwa kwenda kusoma mbali pale wanapofaulu kutoka Shule za Msingi kwenye Manispaa ya Kibaha.