Friday, January 30, 2026

KATA YA VISIGA YAMSHUKURU RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN SIKU 100 KUMWAGA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO

KATA ya Visiga Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha inaendelea na mchakato wa kuibadilisha Zahanati ya Visiga kuwa kituo cha afya ambapo imepokea kiasi cha shilingi milioni 57 kwa ajili hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao cha kawaida cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Visiga pia kuelezea yaliyofanyika kipindi cha siku 100 za Rais Dk Samia Suluhu Hassan Diwani wa Kata hiyo Mohamed Mpaki alisema kuwa baadhi ya kero za wananchi wa Kata hiyo zimetatuliwa.

Mpaki alisema kuwa fedha hizo zilizotolewa kwenye Zahanati hiyo ya Visiga zinatokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ambayo yamekuwa na mchango mkubwa wa kuleta maendeleo kwenye Kata hiyo ambayo ina wakazi zaidi ya 17,000.

Alisema kuwa mbali ya Zahanati hiyo kupokea fedha hizo pia na ile ya Miwaleni zimepatiwa Ultra Sound ili kwa ajili ya kuboresha huduma za afya kwa kukabili changamoto za vifaa hivyo kwenye Zahanati hizo.

"Tunaishukuru Serikali kwa kutupatia fedha kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo hasa katika kipindi cha siku 100 za Rais hakika Kata yetu inaenda kupiga hatua za kimaendeleo,"alisema Mpaki.

Aidha alisema kuwa pia zimetolewa kiasi cha shilingi milioni 110 kwa ajili ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ambapo fedha hizo zitatumika kwa ajili ya vyumba vitano vya madarasa.

"Katika siku 100 za Rais pia tumeweza kuchonga barabara zote za mitaa ya Kata yetu ambapo fedha zilizotengwa ni kiasi cha shilingi milioni 30 na tumepokea makalavati 15 ambapo nane yatatumika kwenye eneo la Gaza ambako kuna changamoto kubwa,"alisema Mpaki.

Aliongeza kuwa pia wameweza kukusanya kiasi cha shilingi milioni 128 kutoka vyanzo mbalimbali kwenye Kata hiyo na inatokana na ufuatiliaji mzuri wa vyanzo hivyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kata ya Visiga Rashid Kibiriti alisema kuwa itekelezaji wa ilani unafanyika vizuri ikiwa ni pamoja na kupokea madawati 20 kwenye Shule ya Msingi Juhudi awamu ya kwanza.

Kibiriti alisema kuwa changamoto ya maji imeanza kutatuliwa kwenye Mitaa ya Saeni na Visiga Kati mabomba yamepelekwa hivyo baada ya muda maji yataanza kupatikana na wananchi kufurahia huduma hiyo.

Thursday, January 29, 2026


 

SIKU 100 ZA RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN MIRADI YA MAENDELEO


KATA ya Visiga Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha inaendelea na mchakato wa kuibadilisha Zahanati ya Visiga kuwa kituo cha afya ambapo imepokea kiasi cha shilingi milioni 57 kwa ajili hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao cha kawaida cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Visiga pia kuelezea yaliyofanyika kipindi cha siku 100 za Rais Dk Samia Suluhu Hassan Diwani wa Kata hiyo Mohamed Mpaki alisema kuwa baadhi ya kero za wananchi wa Kata hiyo zimetatuliwa.

Mpaki alisema kuwa fedha hizo zilizotolewa kwenye Zahanati hiyo ya Visiga zinatokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ambayo yamekuwa na mchango mkubwa wa kuleta maendeleo kwenye Kata hiyo ambayo ina wakazi zaidi ya 17,000.

Alisema kuwa mbali ya Zahanati hiyo kupokea fedha hizo pia na ile ya Miwaleni zimepatiwa Ultra Sound ili kwa ajili ya kuboresha huduma za afya kwa kukabili changamoto za vifaa hivyo kwenye Zahanati hizo.

"Tunaishukuru Serikali kwa kutupatia fedha kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo hasa katika kipindi cha siku 100 za Rais hakika Kata yetu inaenda kupiga hatua za kimaendeleo,"alisema Mpaki.

Aidha alisema kuwa pia zimetolewa kiasi cha shilingi milioni 110 kwa ajili ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ambapo fedha hizo zitatumika kwa ajili ya vyumba vitano vya madarasa.

"Katika siku 100 za Rais pia tumeweza kuchonga barabara zote za mitaa ya Kata yetu ambapo fedha zilizotengwa ni kiasi cha shilingi milioni 30 na tumepokea makalavati 15 ambapo nane yatatumika kwenye eneo la Gaza ambako kuna changamoto kubwa,"alisema Mpaki.

Aliongeza kuwa pia wameweza kukusanya kiasi cha shilingi milioni 128 kutoka vyanzo mbalimbali kwenye Kata hiyo na inatokana na ufuatiliaji mzuri wa vyanzo hivyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kata ya Visiga Rashid Kibiriti alisema kuwa itekelezaji wa ilani unafanyika vizuri ikiwa ni pamoja na kupokea madawati 20 kwenye Shule ya Msingi Juhudi awamu ya kwanza.

Kibiriti alisema kuwa changamoto ya maji imeanza kutatuliwa kwenye Mitaa ya Saeni na Visiga Kati mabomba yamepelekwa hivyo baada ya muda maji yataanza kupatikana na wananchi kufurahia huduma hiyo.

Tuesday, January 27, 2026

WANASIASA WANAWAKE WATAKIWA KUJIKITA KWENYE UCHUMI

WANAWAKE wanasiasa Wilayani Kibaha wametakiwa kupambana kukuza uchumi wao ili kukabiliana na changamoto ukatili wa kijinsia wanazozipata kipindi cha kuwania uongozi.

Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Kibaha mgombea Udiwani Kata ya Kibaha kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Hamo Machapula amesema kuwa wanawake wengi wamekuwa wakikumbana na changamoto hiyo kutokana na kuwa na uchumi duni.

Machapula amesema kuwa ili kupata uongozi kwa mwanamke ni changamoto kubwa sana kutokana na baadhi ya viongozi wanaume kuwakwamisha kutokana na kuwawekea vikwazo.

"Ili tuweze kufanikiwa kupata uongozi lazima tuwe na uchumi imara ili tuweze kufanikiwa lakini uchumi wetu ukiwa chini ni changamoto kuwa viongozi,"amesema Machapula.

Alisema kuwa wanawake wanauwezo mzuri wa kuwa viongozi lakini wanakumbana na vitendo vya ukatili wa kijinsia kutoka kwa viongozi wanaume pale wanapotaka kuwania nafasi za uongozi.

"Ninachowasihi wanawake wenye ndoto za kuwa viongozi ili kukabiliana na vitendo vya ukatili pale wanapowania nafasi za uongozi ni kuwa na uchumi imara ili kukabili vitendo hivyo,"amesema Machapula.

Aidha amesema kuwa uongozi wa vyama unapaswa kuchukua hatua kwa viongozi wanaojihusisha na vitendo hivyo ili wachukuliwe hatua za kinidhamu.

"Kwanza tunapaswa kutoa taarifa pale tunapokumbana na kadhia hizo badala ya kukaa kimya kwani ukimya wetu utatusababishia madhara makubwa na kufifisha ndoto zetu,"amesema Machapula.

Alibainisha kuwa wanawake ndani ya vyama wajishughulishe na shughuli mbalimbali ili kujiongezea kipato kwani siasa inaendana na uchumi.








Monday, January 26, 2026

MITI 6,379 KUPANDWA PWANI KUMBUKIZI KUZALIWA DK SAMIA SULUHU HASSAN


MITI 6,379 itapandwa Mkoani Pwani katika kuadhimisha siku ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu Abubakar Kunenge amesema zoezi hilo litafanyika kesho huko Wilayani Rufiji.

Kunenge amesema kuwa zoezi la upandaji wa miti hiyo ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Rais katika kulinda na kutunza mazingira hapa nchini ili kukabili mabadiliko ya Tabianchi.

"Zoezi hilo litahusisha upandaji wa miti ya matunda 671 pamoja na miti 5,708 ya mbao na vivuli, ambayo itapandwa katika maeneo ya shule ili kuwajengea wanafunzi utamaduni wa kutunza mazingira,"amesema Kunenge.

Amesema kuwa zoezi hilo ni sehemu ya mpango wa Mkoa wa Pwani wa kupanda jumla ya miti milioni 13.5 wakati wa mvua za masika pamoja na ugawaji wa miche ya mikorosho milioni 1.5 kwa wakulima wa Wilaya ya Rufiji chini ya kauli mbiu “Uzalendo ni Kutunza Mazingira – Shiriki Kupanda Miti.”

HALMASHAURI YAKABIDHI MADAWATI 4,000

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imetoa madawati viti na meza 4,000 kwa Shule za Msingi na Sekondari vikiwa na thamani ya shilingi milioni 400.

Akikabidhi madawati viti na meza Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John alisema kuwa Halmashauri imefanya jambo zuri la kukabili changamoto ya wanafunzi kukaa chini.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo alisema kuwa idadi ya wanafunzi inaongezeka kutokana na wazazi kuhamia Kibaha.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa alisema kuwa walitenga kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya kutengeneza madawati viti na meza 4,000 ikiwa kwa Shule za Msingi madawati 2,000 na Sekondari viti na meza 2,000.

Sunday, January 25, 2026

VIJANA WATUNZE AMANI

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) NEC Taifa kupitia Jumuiya ya Wazazi Hamoud Jumaa ameitaka Jumuiya hiyo kuwapa vijana malezi mazuri ili watunze amani.

Jumaa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini ameyasema hayo Mjini Kibaha wakati akifungua baraza la Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani.

Amesema kazi ya Jumuiya hiyo ni kuhakikisha jamii hususani vijana wanakuwa na malezi bora ili kutojiingiza kwenye makundi ambayo hayana maadili mema.

"Tuwape elimu na malezi mazuri vijana wetu na tuzungumze nao juu ya amani kwani amani pia huleta afya njema na amani ndiyo kila jambo hivyo tuhubiri amani,"amesema Jumaa.  

Aidha amesema vijana nchini wanapaswa kudumisha amani na kutokubali kurubuniwa ili wasivunje amani iliyopo kwani bila amani hatutaweza kufanya mambo ya maendeleo.

"Vijana wanapaswa kulinda amani kwani ndiyo msingi wa Taifa la Tanzania na wasukubali kushawishiwa na watu kuharibu amani iliyopo kwani ikipotea ni gharama kuirudisha,"amesema Jumaa.

Amewataka viongozi wa Jumuiya  hiyo kuanza maandalizi ya uchaguzi wa Jumuiya utakaofanyika mwakani kwani uchaguzi ndani ya chama ni mgumu kuliko uchaguzi wa vyama.

"Muanze maandalizi na kama kuna kiongozi anaona anauwezo ajiandae kugombea kwenye chama wakati ukifika kwani Jumuiya hii ndiyo inayobeba jumuiya zote za chama,"amesema Jumaa.

Aliongeza kuwa viongozi wanapaswa kuacha alama kwa kuwa na miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kununua ardhi pamoja na ofisi za makatibu wa jumuiya kwa kila wilaya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Pwani Josiah Jackson amesema kuwa uchaguzi umekwisha kilichobaki ni kujenga jumuiya na chama.

Jackson amesema kuwa wanachama waache makandokando kwa kuwaacha waliochaguliwa wafanye kazi zao na kuwaunga mkono ambapo kwa mkoa walipata madiwani 17 kutoka jumuiya.

Naye katibu wa CCM Mkoa wa Pwani  Kitte Mfilinge amesema kuwa anaipongeza jumuiya kwa kufanya vizuri kwenye uchaguzi mkuu kwani mkoa umeshika nafasi tatu za juu hapa nchini.

Mfilinge amesema kuwa Jumuiya hiyo iko vizuri kwani ina mshikamano na imetulia hivyo kwa sasa wajiandae na uchaguzi wa jumuiya mwakani lengo ni kujenga chama ili kiwe imara.