Wednesday, February 4, 2026

JUMUIYA YA WAZAZI PWANI YAADHIMISHA MIAKA 49 YA CCM KWENYE KATA YA TANGINI

JUMUIYA ya Wazazi Mkoa wa Pwani imeadhimisha miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa  kupanda miti kwenye eneo la Shule mpya ya Msingi Tangini.

Aidha Jumuiya hiyo pia ilikabidhi vifaa kwa wagonjwa kwenye Zahanati mpya ya Tangini pamoja na kutoa fedha kiasi cha shilingi 180,000 kwa familia mbili zenye watu wenye ulemavu.

Akizungumza wakati wa kupokea ugeni kutoka Jumuiya hiyo ambapo sherehe hizo zimefanyika kimkoa kwenye Kata ya Tangini Mwenyekiti wa CCM na Diwani wa Kata ya Tangini Antony Mlao amesema kuwa anashukuru kwa kupewa heshima hiyo.

Milao amesema kuwa anaishukuru serikali kwa kuwapatia miradi hiyo ambayo ni muhimu ndani ya jamii kwani imewapunguzia wanafunzi na wananchi kwenda kupata huduma mbali.

"Tunamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia miradi hii na tunaahidi kuitunza ili iendelee kuhudumia wananchi na wanafunzi kwenye Kata yetu na Halmashauri ya Manispaa nzima ya Kibaha,"amesema Milao.

Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo kimkoa Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani Yusufu Masombola amesema kuwa lengo ni kuwaweka wananchi wote karibu na chama kwa kutembelea sekta mbalimbali.

Masombola amesema kuwa viongozi waweke taratibu za kusikiliza kero za wananchi ili kujenga imani kwao na kila mmoja afanye kazi kulingana na eneo lake.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Kibaha Mjini Yahaya Mtonda amesema kuwa viongozi kwa kushirikiana na wananchi wanapaswa kuendelea kuleta maendeleo ili kumuunga mkono Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Mtonda amesema kuwa viongozi na waccm wanapaswa kuendelea na shughuli za chama kama ilivyokuwa zamani kwani huu ni wakati wa kufanya kazi za chama kujiandaa na chaguzi za jumuiya za chama mwaka 2027.

Kwa upande wake Juma Nziajose mratibu wa chakula na lishe kutoka ofisi ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha alishukuru kwa msaada uliotolewa na jumuiya hiyo.

Nziajose alisema kuwa vifaa hivyo vitafikishwa kwa walengwa kama ilivyodhamiriwa na jumuiya licha ya kuwa Zahanati hiyo bado haijaanza kufanya kazi lakini watapeleka kwenye Hospitali mbalimbali za Manispaa.

MAADHIMISHO MIAKA 49 YA CCM YAFANYIKA WAZAZI KIMKOA KATA YA TANGINI

JUMUIYA ya Wazazi Wilaya ya Kibaha Mjini imeadhimisha miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa  kupanda miti kwenye eneo la Shule mpya ya Msingi Tangini.

Aidha Jumuiya hiyo pia ilikabidhi vifaa kwa wagonjwa kwenye Zahanati mpya ya Tangini pamoja na kutoa fedha kiasi cha shilingi 180,000 kwa familia mbili zenye watu wenye ulemavu.

Akizungumza wakati wa kupokea ugeni kutoka Jumuiya hiyo ambapo sherehe hizo zimefanyika kimkoa kwenye Kata ya Tangini Mwenyekiti wa CCM na Diwani wa Kata ya Tangini Antony Mlao amesema kuwa anashukuru kwa kupewa heshima hiyo.

Milao amesema kuwa anaishukuru serikali kwa kuwapatia miradi hiyo ambayo ni muhimu ndani ya jamii kwani imewapunguzia wanafunzi na wananchi kwenda kupata huduma mbali.

"Tunamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia miradi hii na tunaahidi kuitunza ili iendelee kuhudumia wananchi na wanafunzi kwenye Kata yetu na Halmashauri ya Manispaa nzima ya Kibaha,"amesema Milao.

Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo kimkoa Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani Yusufu Masombola amesema kuwa lengo ni kuwaweka wananchi wote karibu na chama kwa kutembelea sekta mbalimbali.

Masombola amesema kuwa viongozi waweke taratibu za kusikiliza kero za wananchi ili kujenga imani kwao na kila mmoja afanye kazi kulingana na eneo lake.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Kibaha Mjini Yahaya Mtonda amesema kuwa viongozi kwa kushirikiana na wananchi wanapaswa kuendelea kuleta maendeleo ili kumuunga mkono Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Mtonda amesema kuwa viongozi na waccm wanapaswa kuendelea na shughuli za chama kama ilivyokuwa zamani kwani huu ni wakati wa kufanya kazi za chama kujiandaa na chaguzi za jumuiya za chama mwaka 2027.

Kwa upande wake Juma Nziajose mratibu wa chakula na lishe kutoka ofisi ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha alishukuru kwa msaada uliotolewa na jumuiya hiyo.

Nziajose alisema kuwa vifaa hivyo vitafikishwa kwa walengwa kama ilivyodhamiriwa na jumuiya licha ya kuwa Zahanati hiyo bado haijaanza kufanya kazi lakini watapeleka kwenye Hospitali mbalimbali za Manispaa.

JUMUIYA YA WAZAZI MKOA WA PWANI WAFANYA MATENDO YA HURUMA MIAKA 49 YA CCM KATA TANGINI

JUMUIYA ya Wazazi Mkoa wa Pwani imeadhimisha miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kufanya matendo ya huruma kwa jamii kwa kutoa misaada mbalimbali.

Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Yahaya Mtonda amesema kuwa wameamua kufanya hivyo ili kuisaidia jamii kwani ni moja ya majukumu ya Jumuiya hiyo wakati wa maadhimisho hayo Kimkoa ambayo yamefanyika kwenye Kata ya Tangini.

Kwenye tukio la kwanza Jumuiya hiyo imetoa vifaa mbalimbali kwa wagonjwa kwenye ya Tangini ambayo hata hivyo iko kwenye hatua za mwisho kukamilika ambapo vifaa hivyo vitapelekwa kwenye Hospitali zilizopo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha.

Tukio la pili ni la upandaji wa Miti kwenye Shule mpya ya Msingi Tangini ambapo shule hiyo ni mpya ambayo imeanzishwa mwaka huu ikiwa na wanafunzi 650.

Katika tukio la tatu ilitoa fedha kiasi cha shilingi 80,000 kwa familia ya Catherine Januari ina mtoto mwenye ulemavu Catherine John (12) ambaye hawezi kukaa wala kutembea au kufanya chochote zaidi ya kulala tu.

Tukio la tatu ilitoa fedha kiasi cha shilingi 80,000 kwa Mzee Burhan Rehani ambaye ni mlemavu wa miguu wote ni wa kwenye Mtaa wa Tangini Kata ya Tangini.

Mtonda amesema kuwa aliguswa alipotembelea Kata hiyo na kuahidi kusaidia pale atakapoguswa ambapo alitoa 150,000 na mdau mwingine akaongezea 30,000 ili kusaidia familia hizo zenye uhitaji.

"Tumeamua kufanya hivi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya CCM ambapo Kimkoa yamefanyika kwenye Kata ya Tangini ambapo ni sehemu ya maadhinisho hayo,"amesema Mtonda.

Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo Yusufu Masombola amesema kuwa matukio hayo yanaonyesha jinsi gani chama kinavyoshirikiana na jamii.

Masombola amesema kuwa matukio hayo ni sehemu ya maadhimisho ya chama kutimiza miaka 49 tangu kuanzishwa kwake ambapo matukio mbalimbali yamefanyika.

Amesema kuwa Jumuiya hiyo ihakikishe inafundisha maadili mema kwa watoto na vijana ili wawe na maadili mazuri na kuachana na tabia mbaya zisizofaa.

Naye Mwenyekiti wa CCM na Diwani wa Kata ya Tangini Antony Milao amesema kuwa anaishukuru serikali ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia miradi ya maendeleo ndani ya Kata hiyo.

Milao amesema kuwa miradi hiyo muhimu ikiwa ni pamoja na Zahanati Shule ya Msingi na Sekondari itakabili changamoto ya wakazi wa Kata hiyo kupata huduma mbali.

Friday, January 30, 2026

KATA YA VISIGA YAMSHUKURU RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN SIKU 100 KUMWAGA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO

KATA ya Visiga Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha inaendelea na mchakato wa kuibadilisha Zahanati ya Visiga kuwa kituo cha afya ambapo imepokea kiasi cha shilingi milioni 57 kwa ajili hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao cha kawaida cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Visiga pia kuelezea yaliyofanyika kipindi cha siku 100 za Rais Dk Samia Suluhu Hassan Diwani wa Kata hiyo Mohamed Mpaki alisema kuwa baadhi ya kero za wananchi wa Kata hiyo zimetatuliwa.

Mpaki alisema kuwa fedha hizo zilizotolewa kwenye Zahanati hiyo ya Visiga zinatokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ambayo yamekuwa na mchango mkubwa wa kuleta maendeleo kwenye Kata hiyo ambayo ina wakazi zaidi ya 17,000.

Alisema kuwa mbali ya Zahanati hiyo kupokea fedha hizo pia na ile ya Miwaleni zimepatiwa Ultra Sound ili kwa ajili ya kuboresha huduma za afya kwa kukabili changamoto za vifaa hivyo kwenye Zahanati hizo.

"Tunaishukuru Serikali kwa kutupatia fedha kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo hasa katika kipindi cha siku 100 za Rais hakika Kata yetu inaenda kupiga hatua za kimaendeleo,"alisema Mpaki.

Aidha alisema kuwa pia zimetolewa kiasi cha shilingi milioni 110 kwa ajili ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ambapo fedha hizo zitatumika kwa ajili ya vyumba vitano vya madarasa.

"Katika siku 100 za Rais pia tumeweza kuchonga barabara zote za mitaa ya Kata yetu ambapo fedha zilizotengwa ni kiasi cha shilingi milioni 30 na tumepokea makalavati 15 ambapo nane yatatumika kwenye eneo la Gaza ambako kuna changamoto kubwa,"alisema Mpaki.

Aliongeza kuwa pia wameweza kukusanya kiasi cha shilingi milioni 128 kutoka vyanzo mbalimbali kwenye Kata hiyo na inatokana na ufuatiliaji mzuri wa vyanzo hivyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kata ya Visiga Rashid Kibiriti alisema kuwa itekelezaji wa ilani unafanyika vizuri ikiwa ni pamoja na kupokea madawati 20 kwenye Shule ya Msingi Juhudi awamu ya kwanza.

Kibiriti alisema kuwa changamoto ya maji imeanza kutatuliwa kwenye Mitaa ya Saeni na Visiga Kati mabomba yamepelekwa hivyo baada ya muda maji yataanza kupatikana na wananchi kufurahia huduma hiyo.

Thursday, January 29, 2026


 

SIKU 100 ZA RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN MIRADI YA MAENDELEO


KATA ya Visiga Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha inaendelea na mchakato wa kuibadilisha Zahanati ya Visiga kuwa kituo cha afya ambapo imepokea kiasi cha shilingi milioni 57 kwa ajili hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kikao cha kawaida cha Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Visiga pia kuelezea yaliyofanyika kipindi cha siku 100 za Rais Dk Samia Suluhu Hassan Diwani wa Kata hiyo Mohamed Mpaki alisema kuwa baadhi ya kero za wananchi wa Kata hiyo zimetatuliwa.

Mpaki alisema kuwa fedha hizo zilizotolewa kwenye Zahanati hiyo ya Visiga zinatokana na mapato ya ndani ya Halmashauri ambayo yamekuwa na mchango mkubwa wa kuleta maendeleo kwenye Kata hiyo ambayo ina wakazi zaidi ya 17,000.

Alisema kuwa mbali ya Zahanati hiyo kupokea fedha hizo pia na ile ya Miwaleni zimepatiwa Ultra Sound ili kwa ajili ya kuboresha huduma za afya kwa kukabili changamoto za vifaa hivyo kwenye Zahanati hizo.

"Tunaishukuru Serikali kwa kutupatia fedha kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo hasa katika kipindi cha siku 100 za Rais hakika Kata yetu inaenda kupiga hatua za kimaendeleo,"alisema Mpaki.

Aidha alisema kuwa pia zimetolewa kiasi cha shilingi milioni 110 kwa ajili ya ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ambapo fedha hizo zitatumika kwa ajili ya vyumba vitano vya madarasa.

"Katika siku 100 za Rais pia tumeweza kuchonga barabara zote za mitaa ya Kata yetu ambapo fedha zilizotengwa ni kiasi cha shilingi milioni 30 na tumepokea makalavati 15 ambapo nane yatatumika kwenye eneo la Gaza ambako kuna changamoto kubwa,"alisema Mpaki.

Aliongeza kuwa pia wameweza kukusanya kiasi cha shilingi milioni 128 kutoka vyanzo mbalimbali kwenye Kata hiyo na inatokana na ufuatiliaji mzuri wa vyanzo hivyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Kata ya Visiga Rashid Kibiriti alisema kuwa itekelezaji wa ilani unafanyika vizuri ikiwa ni pamoja na kupokea madawati 20 kwenye Shule ya Msingi Juhudi awamu ya kwanza.

Kibiriti alisema kuwa changamoto ya maji imeanza kutatuliwa kwenye Mitaa ya Saeni na Visiga Kati mabomba yamepelekwa hivyo baada ya muda maji yataanza kupatikana na wananchi kufurahia huduma hiyo.

Tuesday, January 27, 2026

WANASIASA WANAWAKE WATAKIWA KUJIKITA KWENYE UCHUMI

WANAWAKE wanasiasa Wilayani Kibaha wametakiwa kupambana kukuza uchumi wao ili kukabiliana na changamoto ukatili wa kijinsia wanazozipata kipindi cha kuwania uongozi.

Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Kibaha mgombea Udiwani Kata ya Kibaha kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Hamo Machapula amesema kuwa wanawake wengi wamekuwa wakikumbana na changamoto hiyo kutokana na kuwa na uchumi duni.

Machapula amesema kuwa ili kupata uongozi kwa mwanamke ni changamoto kubwa sana kutokana na baadhi ya viongozi wanaume kuwakwamisha kutokana na kuwawekea vikwazo.

"Ili tuweze kufanikiwa kupata uongozi lazima tuwe na uchumi imara ili tuweze kufanikiwa lakini uchumi wetu ukiwa chini ni changamoto kuwa viongozi,"amesema Machapula.

Alisema kuwa wanawake wanauwezo mzuri wa kuwa viongozi lakini wanakumbana na vitendo vya ukatili wa kijinsia kutoka kwa viongozi wanaume pale wanapotaka kuwania nafasi za uongozi.

"Ninachowasihi wanawake wenye ndoto za kuwa viongozi ili kukabiliana na vitendo vya ukatili pale wanapowania nafasi za uongozi ni kuwa na uchumi imara ili kukabili vitendo hivyo,"amesema Machapula.

Aidha amesema kuwa uongozi wa vyama unapaswa kuchukua hatua kwa viongozi wanaojihusisha na vitendo hivyo ili wachukuliwe hatua za kinidhamu.

"Kwanza tunapaswa kutoa taarifa pale tunapokumbana na kadhia hizo badala ya kukaa kimya kwani ukimya wetu utatusababishia madhara makubwa na kufifisha ndoto zetu,"amesema Machapula.

Alibainisha kuwa wanawake ndani ya vyama wajishughulishe na shughuli mbalimbali ili kujiongezea kipato kwani siasa inaendana na uchumi.