Saturday, February 21, 2026

MATUMLA AWATAKA WANANCHI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI ILI KUTATUA CHANGAMOTO


MWENYEKITI wa Mtaa wa Mwendapole B Manispaa ya Kibaha Abubakar Matumla ameendelea na ziara ya kutafutia majawabu changamoto zinazowakabili wananchi wa Mtaa huo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Matumla amesema ziara hiyo inaifanya kwa kutembelea Balozi zote zilizopo kwenye Mtaa huo ili kubaini changamoto ili kupeleka sehemu husika kwa utatuzi.

Changamoto ambazo zimekuwa zikijirudia ni pamoja na miundombinu ya barabara, uhalifu, uvutaji wa bhangi, maji, elimu ya msingi.

Matumla amesema kuwa kutokana na changamoto hizo watawasiliana na mamlaka husika ili wazifanyie kazi changamoto hizo ili ziweze kupatiwa majawabu.

Akizingumzia uhalifu amesema kuwa tayari baadhi ya maeneo yameainishwa kuwa ni kitovu cha uhalifu pamoja na matumizi ya dawa za kulevya aina ya bhangi.

"Tayari tumeshaweka mikakati ya kudhibiti uhalifu kwa kushirikiana na Polisi Kata ili kuwakama wahalifu hao pia ni kufanya doria za kushtukiza ambapo baadhi ya wahalifu wanajificha kwenye Bodaboda ambapo tayari mipango ya kuwatambua inafanyika,"amesema Matumla.

Amesema baadhi ya maeneo kuna changamoto ya upatikanaji wa maji, miundombinu ya barabara imeharibika lakini hata hivyo Mtaa huo umepata barabara moja ambayo itajengwa lami.

"Kwa upande wa elimu ya Msingi changamoto kubwa ni uhaba wa madawati na vyumba vya madarasa ambapo Manispaa ya Kibaha imetoa madawati 20 ambayo yatasaidia kukabiliana na changamoto ya upungufu wa madawati,"amesema Matumla.




DIWANI TANGINI ATOA POLE MTOTO ALIYENUSURIKA KIFO KWA KUSOMBWA NA MAJI NA WALIOEZULIWA PAA ZA NYUMBA ZAO

DIWANI wa Kata ya Tangini Antony Milao ametoa pole kwa wananchi waliokumbwa na kadhia ya mvua ikiwemo ya mwanafunzi Morhat Abdala (9) kunusurika kifo baada ya kusombwa na maji akitoka shuleni.

Mvua hiyo iliyonyesha jana jioni ilileta athari kwa baadhi ya wakazi wa Mtaa wa Machinjioni Kata ya Tangini ambapo nyumba mbili na Machinjio ya mbuzi ambapo mapaa yaliezuliwa baada mvua kubwa kunyesha ikiambatana na upepo mkali kwenye Mtaa huo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutokea matukio hayo Milao amesema kuwa mwanafunzi huyo ambaye amepumzishwa kwenye Kituo cha Afya Mkoani akipatiwa matibabu anaendelea vizuri.

Milao amesema anamshukuru Mungu kumnusuru mtoto huyo ambaye anasoma darasa la nne Shule ya Msingi Maendeleo akiwa anatoka shule akiwa na mwenzake waliteleza wakati wakivuka kalavati na kusombwa na maji kabla ya wasamaria wema kuwaokoa.

"Pia nilimtembelea Mzee Boniface Mpanda ambaye nyumba yake imeezuliwa paa na nyumba ya Jackson Sellu ambaye hakuwepo nitawasiliana naye pamoja na sehemu ya paa la Machinjio jambo la kushukuru hakuna madhara kwa binadamu zaidi ya mapaa kungoka nimewashika mkono wale waliopata athari hizo ili waweze kutengeneza nyumba zao ili waendelee na maisha yao,"amesema Milao.

Mama wa mwanafunzi aliyesombwa na maji Fatuma Juma amesema kuwa alipata taarifa toka kwa wasamaria wema kuwa mwanae yuko Hospitali baada ya kusombwa na maji baada ya mvua kubwa kunyesha.

Juma amesema anamshukuru Mungu kwani mwanae kwa sasa anaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu na anawashukuru wasamaria wema kumuokoa mwanae na kumuwaisha hospitali.

Naye Mzee Boniface Mpanda ambaye nyumba yake imeezuliwa paa amesema kuwa alikuwa ndani wakati mvua inanyesha mara akashtukia paa linarushwa na upepo mkali na vitu vyake vyote kulowa.

Mpanda anasema majirani walimsaidia kutoa vitu vyake na kuviweka kwenye mazingira salama wanatoa shukrani zao kwa majirani kwa kutoa msaada na diwani jinsi alivyojitoa kuwasaidia.

Kwa upande wake jirani ambapo nyumba hizo mbili zilizoezuliwa paa Remminister Komanga amesema kuwa mvua hiyo ilinyesha na ilikuwa na upepo mkali na kuezua mapaa hayo pamoja na kuangusha sehemu ya ukuta wake uliozungushiwa kwenye nyumba yake.

Komanga amesema upepo huo ulikuwa ni kama kimbunga na ulikuwa ni sehemu hiyo tu kwani maeneo mengine hakukuwa na upepo zaidi ya mvua kuwa tu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Machinjioni Aidan Saimon amesema kuwa baada ya kutokea madhara hayo waliwasiliana na diwani ili waangalie namna ya kuwasaidia wananchi hao.

Simon amesema kuwa alipewa maagizo na diwani kuhakikisha vifaa vyote vya upauaji atakavyovitoa vinatumika kwa haraka ili nyumba ya Mzee Mpanda ipauliwe upya na atawasiliana na Sellu kuona atamsaidiaje ambapo vyumba vyake viwili vimeezuliwa na upepo.


 

Thursday, February 19, 2026

ATAKA MASLAHI KWA WAFANYAKAZI WA MAJUMBANI

JAMII imetakiwa kuheshimu ajira ya wafanyakazi wa majumbani kwani nitaaluma kama zilivyo taaluma zingine kwa kuifanya kuwa yenye staha kwani ni sehemu ya ustawi wa jamii na ukuzaji wa uchumi.

Hayo yalisemwa Jijini Dar es Salaam kwenye ukumbi wa Confucius wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Rashid Ally Salim Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kazi na Uwekezaji Zanzibar wakati akifungua mkutano wa mradi wa Urasimishaji wa kitaaluma kwa wafanyakazi wa majumbani Tanzania.

Salim alisema kuwa jamii inapaswa kuona kazi za nyumbani ni taaluma kwa kuzingatia maslahi na haki za msingi za mfanyakazi kwani anaiendeleza jamii.

"Hawa ni watu muhimu sana kwani wanatunza familia zetu pale tunapokuwa kazini au kwenye majukumu mengine ya kimaendeleo hivyo tuwape heshima yao,"alisema Salim.

Alisema kupatiwa mafunzo ya ujuzi kupitia vituo vya VETA ni moja ya vitu vitavyoweza kuwasaidia katika maisha yao kwani ujuzi huo utakuwa ni mkombozi kwao na utawasaidia kujitambua na kujiamini.

Naye mwakilishi kutoka Veta Abdala Ulomi alisema kuwa tayari wametoa mafunzo ya ujuzi kwa wafanyakazi wa majumbani 1,280 kwenye vyuo sita vya Bara na vitatu vya Zanzibar na mtaala wao tayari umeshaandaliwa.

Ulomi alisema kuwa wanarasimisha mafunzo kwa wafanyakazi wa majumbani kwani mahitaji yao ni makubwa ndani na nje ya nchi na hiyo itakuwa taaluma kama taaluma zingine.

Kwa upande wake Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Profesa Rose Upor alisema kuwa asilimia 95 ya wafanyakazi wa majumbani ni wanawake ambapo kuna umuhimu wa kuboresha mazingira ya hali za kijinsia.

Upor alisema kuwa suluhisho ni kukuza utu na mazingira bora ya kazi ambapo kuna haja ya kushughulikia tafiti zinazofanywa ili kuleta usawa na kuepukana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Mkurugenzi wa Shirika la CVM Tanzania Magesa Nathaniel alisema kuwa wamekuwa wakitekeleza mradi wa miaka mitatu ambao umefika mwisho wa kukuza kazi za staha na haki kwa wafanyakazi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na wadau mbalimbali wa ndani na nje.

Nathaniel alisema kuwa baadhi ya kazi walizokuwa wakifanya ni kuwajengea uelewa na kuwajengea uwezo kuwaunganisha na chama cha wafanyakazi wa majumbani CHODAWU katika utetezi wa haki zao.

Asteria Gerald mwakilishi wa CHODAWU alisema kuwa kutambuliwa kwa kazi zao kutasababisha kupata heshima ulinzi na stahiki nyingine kwani bado wananyanyaswa wanafanyiwa ukatili na wanafanya kazi kwa muda mrefu.

Gerald alisema kuwa wanaomba kuridhiwa kwa mkataba namba 189 wa Shirika la Kazi Duniani (ILO) ambayo inalinda haki hadhi usalama wa wafanyakazi wa majumbani.

Mkurugenzi wa Taasisi za Taaluma za Kijinsia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk Sara Kisanga alisema kuwa wafanyakazi wa nyumbani wanapaswa kutambuliwa na kulindwa na kuendelezwa kiujuzi.

Kisanga alisema kuwa wataalamu wanaotoka chuoni hapo wanawezesha jamii ili kuleta mabadiliko chanya ili kuwa kazi ambazo zina staha na kuzingatia haki za binadamu.

MADIWANI MANISPAA YA KIBAHA WAPITISHA BAJETI YA 2026/2027 YA TSH BILIONI 68.7 KWA KISHINDO

Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha mkoani Pwani wamepitisha kwa kishindo bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 yenye jumla ya Shilingi Bilioni 68.7 katika Baraza Maalum la Madiwani lililofanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Kibaha.

Akizungumza wakati wa kupitisha bajeti hiyo, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Mawazo Nicas, amesema bajeti hiyo ni chachu ya maendeleo kwa wananchi na imezingatia mahitaji halisi ya Halmashauri.

“Bajeti hii imepitia kamati zote, imejadiliwa na kuboreshwa. Ni wajibu wetu kuipitisha ili ikalete maendeleo kwa wananchi wetu,” amesema Dkt. Nicas.

Diwani wa Kata ya Kibaha, Omary Bula, amesema bajeti hiyo imeandaliwa kwa ushirikishwaji wa madiwani wote na kuwataka wajumbe kuipitisha kwa maslahi ya wananchi.

Awali akiwasilisha rasimu ya bajeti hiyo, Naibu Meya wa Manispaa ya Kibaha, Aziza Mruma, amesema Halmashauri imekisia kutumia kiasi hicho cha Shilingi Bilioni 68.7, ikiwa ni ongezeko la asilimia sita ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2025/2026.

Kwa mujibu wa Mruma, katika mchanganuo wa bajeti hiyo, mapato ya ndani yanatarajiwa kuwa Shilingi Bilioni 17.8, miradi ya maendeleo Shilingi Bilioni 8.7, huku asilimia 60 ya mapato ya ndani ikielekezwa kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 40 kwenye matumizi ya kawaida.

Aidha, Shilingi Bilioni 1.4 zimetengwa kwa ajili ya mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.

Katika mwaka huo wa fedha, Halmashauri inatarajia kujenga kituo kimoja cha afya na zahanati mbili, pamoja na kutekeleza miradi ya kimkakati yenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.3. Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa maegesho ya malori yenye thamani ya Shilingi Milioni 242.3, kituo cha kibiashara Mbonde, na ujenzi wa kiwanda cha kusindika nyama chenye thamani ya Shilingi Milioni 524.7.

Baada ya majadiliano, madiwani kwa pamoja waliipitisha bajeti hiyo kwa kauli moja, wakiahidi kusimamia utekelezaji wake ili kuhakikisha inaleta tija na maendeleo kwa wananchi wa Manispaa ya Kibaha.

Monday, February 16, 2026

NMB WATOA MILIONI 300 MAONYESHO YA MIFUGO

BENKI ya NMB imeingia mkataba wa udhamini wa maonyesho ya mifugo ya (Tri-Nations Livestock Expo) kwa kiasi cha shilingi milioni 300 kwa kipindi cha miaka mitatu.

Mkataba huo umeshuhudiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dk Fabian Madele kwenye Shamba la Mifugo la Mbogo lililopo Ubena Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo ambapo maonyesho hayo mwaka huu yatafanyika Juni 19 hadi 21.

Madele alisema kuwa maonyesho hayo ni muhimu kwani kwani yanaleta tija kwenye ufugaji kuimarisha ushirikiano kukuza teknolojia kwenye sekta ya ufugaji kukuza masoko ya ndani na nje kwani soko la nje ni kubwa sana.

"Malengo ifikapo 2030 kufikia uuzaji wa tani 50 kwa soko la nje ambalo ni kubwa sana hasa la Mshariki ya Kati na China hivyo lazima tutumie fursa kama hizi kuboresha ufugaji wetu ili uakisi uwingi wa mifugo yetu,"alisema Madele.

Alisema kuwa Tanzania ni ya pili kwa kuwa na mifugo mingi ikiwa na ngombe zaidi ya milioni 35 ma mbuzi milioni 28 hivyo lazima tafsiri ya idadi iendane na mapato.

"Tuwavutie vijana ili wajikite kwenye ufugaji kwani endapo nguvu itawekezwa itainua uchumi wa nchi na ili kufika huko ni kufuga kwa utaalamu kwani maofisa mifugo wamesambazwa kila mahali kikubwa ni kujenga mahusiano mazuri,"alisema Madele.

Kwa upande wake mwakilishi wa benki hiyo kupitia Mkuu wa Idara ya Kilimo Biashara wa Benki ya NMB Nsolo Mlozi alisema kuwa mwaka jana walidhamini maonyesho hayo kwa kiasi cha milioni 30 ambayo hufanyika kila mwaka.

Mlozi alisema kuwa udhamini huo ni wa miaka mitatu na ni sehemu ya kuboresha sekta hiyo ya ufugaji ambapo pia hutoa fursa za mikopo kwa wafugaji ambapo hadi sasa imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 130.

Alisema kuwa mbali ya kutoa mikopo pia inatoa elimu ya fedha, ushauri na masoko kwa wafugaji ili kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali ambapo imeweka mameneja mahusiano wanaoshughulikia wafugaji.

Naye Mkurugenzi wa Shamba la Mifugo la Mbogo Naweed Mulla alisema kuwa maonyesho hayo yamekuwa na mafanikio makubwa ambapo wafugaji wengi walijitokeza kushiriki na mwaka huu wataongezeka zaidi wakiwemo wafugaji toka nchi mbili jirani.

Mulla alisema kuwa mwaka huu wameongeza kipengele cha ufugaji wa kuku kwa upande wa wanawake ambapo kutakuwa na mshindi ambaye atatambulika kama Malkia wa ufugaji.

Mwenyekiti wa Chama Cha Wafugaji Mrida Maroche alisema kuwa wanapongeza uwekezaji unaofanyika kwenye mifugo kwani unapandisha thamani ya mifugo yao na watatumia fursa mbalimbali ili kuongeza uzalishaji kwa kuzingatia viwango ili kukabili soko la nje.

Maroche alisema kuwa mfano mzuri ni baadhi ya ngombe waliopo kwenye Shamba la Mbogo ngombe wa miaka miwili ana uzito wa kilogramu 350 na ndama wa miezi mitano ana uzito wa kilogramu 180 ambapo hayo ni mabadiliko makubwa.


GOOD NEWS FOR TANZANIA DIGITAL CONTENT CREATORS AS NEW LICENCE FEES ANNOUNCED

The Government has announced a historic measure that could significantly transform the landscape of Tanzania’s digital content industry.

Speaking at the Annual Broadcasting Service Providers Conference (ABC 2026) in Dodoma, the Deputy Minister for Information, Culture, Arts and Sports, Hamisi Mwinjuma, revealed that the licence fee for online content creators has been reduced from TSh 500,000 to just TSh 50,000, with an application fee of only TSh 10,000.

This represents a reduction of more than 90 per cent — a move widely interpreted as opening a new door for young innovators, bloggers, and digital creators who had previously struggled with the high cost of compliance.

The decision follows nearly a year of strategic consultations between the Tanzania Bloggers Network (TBN) and the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), aimed at addressing financial barriers that had constrained the growth of digital journalism and online content production in the country.

In addition, licence fees for Online Content Aggregators have been reduced from TSh 1,000,000 to TSh 100,000.

A new “Amateur” category has also been introduced specifically for emerging young creators, enabling them to formalise their activities and nurture their talents without heavy financial burdens.

Within the broader context of a rapidly expanding digital economy, this decision is expected to stimulate employment, creativity, and tax revenue generation — in line with the development vision championed by President Samia Suluhu Hassan.

If effectively implemented, these reforms may well mark the beginning of a new chapter for Tanzania’s digital creative sector.

NEEMA KWA WATENGENEZA MAUDHUI YA KIDIJITALI ADA MPYA ZA LESENI ZIKITANGAZWA

 

Serikali imetangaza hatua ya kihistoria inayoweza kubadili sura ya tasnia ya maudhui ya kidijitali nchini. Kupitia tamko lililotolewa katika Mkutano wa Mwaka wa Watoa Huduma za Utangazaji (ABC 2026) jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma, amesema ada ya leseni kwa watoa maudhui mtandaoni imeshushwa kutoka Sh500,000 hadi Sh50,000, huku ada ya maombi ikiwa Sh10,000 pekee.

Ni punguzo la zaidi ya asilimia 90, hatua ambayo wengi wameitafsiri kama mlango mpya kwa vijana wabunifu, wanablogu na watengeneza maudhui waliokuwa wakikwama kwa gharama.

Hatua hiyo imekuja baada ya mazungumzo ya karibu mwaka mzima kati ya Tanzania Bloggers Network (TBN) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), yakilenga kuondoa vikwazo vilivyokuwa vikizuia ukuaji wa sekta hii.

Zaidi ya hayo, ada ya wakusanyaji wa maudhui (Online Content Aggregators) imeshuka kutoka Sh1,000,000 hadi Sh100,000. 

Aidha, kundi jipya la “Amateur” limeanzishwa mahsusi kwa vijana wanaochipukia, likiwawezesha kujisajili rasmi bila mzigo wa kifedha.

Kwa muktadha wa uchumi wa kidijitali unaokua kwa kasi, uamuzi huu unaweza kuwa kichocheo kikubwa cha ajira, ubunifu na mapato ya kodi kwa taifa, kama yalivyo maono ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.