Aidha Jumuiya hiyo pia ilikabidhi vifaa kwa wagonjwa kwenye Zahanati mpya ya Tangini pamoja na kutoa fedha kiasi cha shilingi 180,000 kwa familia mbili zenye watu wenye ulemavu.
Akizungumza wakati wa kupokea ugeni kutoka Jumuiya hiyo ambapo sherehe hizo zimefanyika kimkoa kwenye Kata ya Tangini Mwenyekiti wa CCM na Diwani wa Kata ya Tangini Antony Mlao amesema kuwa anashukuru kwa kupewa heshima hiyo.
Milao amesema kuwa anaishukuru serikali kwa kuwapatia miradi hiyo ambayo ni muhimu ndani ya jamii kwani imewapunguzia wanafunzi na wananchi kwenda kupata huduma mbali.
"Tunamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia miradi hii na tunaahidi kuitunza ili iendelee kuhudumia wananchi na wanafunzi kwenye Kata yetu na Halmashauri ya Manispaa nzima ya Kibaha,"amesema Milao.
Mgeni rasmi kwenye maadhimisho hayo kimkoa Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani Yusufu Masombola amesema kuwa lengo ni kuwaweka wananchi wote karibu na chama kwa kutembelea sekta mbalimbali.
Masombola amesema kuwa viongozi waweke taratibu za kusikiliza kero za wananchi ili kujenga imani kwao na kila mmoja afanye kazi kulingana na eneo lake.
Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Kibaha Mjini Yahaya Mtonda amesema kuwa viongozi kwa kushirikiana na wananchi wanapaswa kuendelea kuleta maendeleo ili kumuunga mkono Rais Dk Samia Suluhu Hassan.
Mtonda amesema kuwa viongozi na waccm wanapaswa kuendelea na shughuli za chama kama ilivyokuwa zamani kwani huu ni wakati wa kufanya kazi za chama kujiandaa na chaguzi za jumuiya za chama mwaka 2027.
Kwa upande wake Juma Nziajose mratibu wa chakula na lishe kutoka ofisi ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha alishukuru kwa msaada uliotolewa na jumuiya hiyo.
Nziajose alisema kuwa vifaa hivyo vitafikishwa kwa walengwa kama ilivyodhamiriwa na jumuiya licha ya kuwa Zahanati hiyo bado haijaanza kufanya kazi lakini watapeleka kwenye Hospitali mbalimbali za Manispaa.






