Friday, July 3, 2026

KUNENGE AMSHUKURU RAIS DK SAMIA KUKUZA VIPAJI VYA MICHEZO KWA VIJANA

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.



Mpya







MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.

mwisho.

KUNENGE AMSHUKURU RAIS DK SAMIA KUKUZA VIPAJI VYA VIJANA

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.

mwisho.

Thursday, July 2, 2026

PWANI KUMUUNGA MKONO RAIS DK SAMIA UKUSANYAJI MAPATO

MKOA wa Pwani umesema utashirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha inakusanya mapato ili kuinua uchumi kupitia uwekezaji wa viwanda kumuunga Mkono Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Hayo yelisemwa na Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Pili Mnyema wakati wa sherehe za kutimiza miaka 30 ya TRA kimkoa ambapo walushuhudia moja kwa moja maadhimisho hayo Kitaifa ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais Dk Samia.

Mnyema alisema kuwa kama Rais alivyotaka TRA kufanya vizuri ili akistaafu Mamlaka hiyo iwe kwenye hali nzuri ndiyo itakuwa furaha yake.

"Tutamuunga mkono Rais kwa kushirikiana na TRA kuhakikisha walipa kodi wanalipa kodi pasipo kukwepa kodi ili kuinua uchumi hasa ikizingatiwa Pwani ni mkoa wa kimkakati kwa kuwa na viwanda vingi,"alisema Mnyema.

Alisema kuwa ukusanyaji mzuri unaofanyika unatokana ushirikiano uliopo baina ya mamlaka na walipa kodi ambapo hicho ni kiashiria cha ukuaji wa uchumi.

"Pia ukusanyaji utaendana na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050 ambayo ndo inaanza kazi kuanzia sasa na hapa tunashirikiana na sekta binafsi katika kuchangia uchumi,"alisema Mnyema.

Aidha alisema kuwa Mkoa utasimamia kuhakikisha malengo ya nchi yanatimia kwa kuwa na uwezo wa kukusanya mapato kwa walipa kodi kulipa kwa hiyari ikiwa ni maono ya Rais.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani Salim Makame alisema kuwa Mamlaka imejipanga kuhakikisha wale wote wanastahiki kulipa wanalipa kwa hiyari.

Makame alisema kuwa wameyapokea maagizo yote yaliyotolewa na Rais ya namna ya kuboresha ukusanyaji wa Mapato pia kutumia mifumo ya teknolojia.

Wednesday, July 1, 2026

NASHUKURU SANA MTANDAO NAJUKWAA KUBWA BELLE NAIJA

ALHAMDULILAH ALLAH NDIYO SHAHIDI WA KILA JAMBO 

Jukwaa kubwa la kidijitali nchini Nigeria linalojihusisha na masuala ya burudani, mitindo, mitindo ya maisha (lifestyle), na harusi za Kiafrika. Ilianzishwa mnamo mwezi Julai mwaka 2006 na mjasiriamali wa Nigeria anayeitwa Uche Pedro (jina la kuzaliwa Uche Eze).

NASHUKURU KUPOSTI PICHA YANGU NA STAA MKUBWA NCHINI NIGERIA NI HESHIMA KUBWA KUTAMBUA MCHANGO WANGU KATIKA AFRIKA 

Layi Wasabi (jina lake halisi ni Isaac Ayomide Olayiwola) ni mchekeshaji, mwigizaji, na mtengeneza maudhui maarufu wa mtandaoni kutoka nchini Nigeria. 

Anajulikana sana kwa uchekeshaji wake wa kipekee na wa akili (philo-comedy) kupitia video fupi (skits) kwenye mitandao ya kijamii

MKUTANO (AFRICA'S CREATIVE FUTURE TAKES CENTRE STAGE IN LUSAKA- (MUSTAKABALI WA UBUNIFU WA AFRIKA WACHUKUA KITUO KIKUU LUSAKA)

ALHAMDULILAH ALLAH NDIYO SHAHIDI WA KILA JAMBO 
LEO TAREHE 29 JUNE 

NIMESHIRIKI  MKUTANO (AFRICA'S CREATIVE FUTURE TAKES CENTRE STAGE IN LUSAKA- (MUSTAKABALI WA UBUNIFU WA AFRIKA WACHUKUA KITUO KIKUU LUSAKA)

Mkutano huu utachukua siku 7 kuanzia tarehe 29 Juni  hadi 5 Julai 

Mkutano huo ulioandaliwa na Wizara ya Vijana, Michezo na Sanaa nchini Zambia Kwa siku tano takribani vijana 3000 kushikiriki 
Kuanzia watengenezaji filamu na wanamuziki hadi wabunifu wa mitindo, wawekezaji na watunga sera, mamia ya wajumbe kutoka kote barani wamekusanyika katika 

Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mulungushi kwa ajili ya Mkutano wa Biashara wa Viwanda vya Ubunifu wa 2026, Soko la Ubunifu la Afrika (ACM) na Tamasha la Sanaa la Kitaifa la Kwimbo, wakiwa wameunganishwa na lengo moja la kugeuza ubunifu wa Afrika kuwa biashara, ajira na fursa za kimataifa.

Akifungua rasmi mkutano huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Michezo na Sanaa, Bw. Kangwa Chileshe, 

Alisema Zambia imepiga hatua kubwa katika kuiweka sekta ya ubunifu katika nafasi nzuri ya kuchangia uchumi wa nchi.

Alitaja mfululizo wa mageuzi yaliyotekelezwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa Sanaa kama idara ndani ya Wizara, uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Sanaa ya kwanza ya nchi, mapitio ya Sera ya Taifa ya Filamu, marekebisho ya sheria iliyopitwa na wakati, kuondolewa kwa ushuru wa uagizaji wa vifaa vya filamu na muziki, na Zambia kujiunga na mfumo wa ATA Carnet ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya ubunifu kuvuka mipaka.

Bw. Chileshe alisema serikali pia imewekeza kwa wasanii wenyewe, ambapo zaidi ya wabunifu 3,000 wamepatiwa mafunzo ya kusoma na kuandika kuhusu fedha na maendeleo ya biashara, huku zaidi ya 2,000 wameandikishwa kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii ambao hutoa pensheni, mafao ya uzazi, msaada wa mazishi na upatikanaji wa mikopo.

Monday, June 29, 2026

POLISI MKOANI PWANI LINACHUNGUZA VIFO VYA MWANAMKE NA MTOTO

JESHI la Polisi Mkoani Pwani linafanya uchunguzi wa tukio la mauaji ya mwanamke mmoja na mtoto ambao hawakufahamika yaliyotokea Mbwewe Wilaya ya Kipolisi Chalinze Mkoa wa Pwani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani Salim Morcase kwa vyombo vya habari zilisema kuwa tukio hilo la mauaji ya watu wawili lililotokea Juni 2 mwaka huu  majira ya saa 9:00 alasiri huko Kitongoji cha Nung'uli Kijiji cha Kwang'andu Kata ya Mbwewe Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo.

Taarifa hiyo ilibainika kuwa watu hao ni mwanamke
mmoja anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka (20-25) na mtoto ambaye hakufahamika jinsia yake kutokana na kuungua sana na moto mwenye
umri unaokadiriwa kuwa miaka (3-6) ambao mpaka sasa bado hawajafahamika wala watu waliosababisha mauaji hayo.

"Ikumbukwe katika eneo la tukio hilo zilikutwa tiketi mbili za basi la Passion Video Coach linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam kwenda Miono kupitia Chalinze zilizokatwa tarehe Mei 31 mwaka huu,"alisema taarifa hiyo.

Taarifa zilisema kuwa tiketi hizo zilikiwa na majina ya Adela na Modest ambapo Jeshi bado linachunguza chanzo cha mauaji hayo wakati miili ya wahanga imehifadhiwa katika Hospitali ya Msoga Halmashauri ya Chalinze.

Kutokana na mauaji hayo Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linaendelea kutoa wito kwa mtu yeyote anayewafahamu watu hao au mwenye taarifa zozote zinazoweza kusaidia kuwatambua wafike Ofisi ya kamanda wa Polisi Mkoa
wa Pwani.

 "Au wapige simu namba 073900995, 065837601 0 na 0753855570 ili kuendelea kusaidia uchunguzi na kuwapata ndugu wa marehemu kwa wakati,"iliongeza taarifa hiyo.