Hayo yalisemwa na Ustaadh Mahamudu Lipambila ambaye ni katibu wa Msikiti wa Masjid Hadharaj Mzimuni Maili Kibaha Mkoani Pwani wakati wa Maadhimisho ya Sikukuu ya Kuchinja (EIDY L ADHUHAA) inayoadhimishwa ulimwenguni kote.
Lipambila alisema kuwa hadhithi ya Ibrahim ambayo ilimtaka amchinjie mwanae ili awe sadaka ambapo ndiyo chimbuko la sikukuu hiyo kubwa kwa imani ya Kiislamu.
"Ibrahim alionyesha utii kwa Mungu kwa kutaka kumtoa mwanae wa pekee ili awe sadaka ya kuchinjwa na alipokubali Mungu kwa kupitia Malaika alimletea kondoo na ndiyo akachinjwa kuwa sadaka,"alisema Lipambila.
Alisema kuwa hadithi hiyo inafundisha jinsi gani watu wanapaswa kuwa na utii juu ya imani zao na kufuata mafundisho ya Mwenyezi Mungu ambayo yatafanya watu waishi kwa kuthaminiana.
"Pia hadithi inafundisha wazazi kuwa na kiasi katika upendo juu ya watoto wao ambapo wengine wamekuwa chanzo cha mmomonyoko wa maadili kwa kutaka kuwafurahisha badala ya kumpenda zaidi Mungu kwa kufuata mafundisho yake,"alisema Lipambila.
Aidha alisema kuwa sikukuu hiyo ni ya furaha kwa kuhakikisha jamii yote inakuwa na furaha kwa kuwa na utii juu ya Mwenyezi Mungu na wanapaswa kumpenda Mungu zaidi.
"Watu waishi kama ilivyokuwa makusudio ya Mungu kutuumba na wakizingatia hayo wataishi kwa amani na upendo na hakutakuwa na tofauti za kimitazamo hasi ya kimaendeleo,"alisema Lipambila.
Aliongeza kuwa viongozi wanapaswa kuwa na hekima na utii kama aliokuwa nao Ibrahim ambaye dini zote zinamuona kama kielelezo cha imani zao kwa Mwenyezi Mungu.






