Tuesday, August 11, 2026

EDDY CHARITY YAWAPA TABASAMU KISARAWE SAFE HOUSE

JAMII imeaswa kugharamia suala la elimu kwenye vituo vya watoto wenye uhitaji ili kwa kutatua changamoto za kielimu kwa watoto hao waweze  kutimiza ndoto zao.

Hayo yalisemwa na katibu wa kikundi cha Eddy Charity cha Kibaha, Edgar Mwakalosi wakati kilipotembelea kituo cha Kisarawe Safe House na kutia misaada mnalimbali.

Mwakalosi alisema kuwa vituo hivyo vinachangamoto nyingi ikiwa ni pamoja namna ya kuwapatia elimu watoto waishio kwenye vituo hivyo hasa wanapofikia hatua ya kuelekea kufanya mitihani ya kitaifa au kwenda vyuoni.

"Jamii inapaswa kuvisaidia vituo hivyo kwenye suala la kielimu ili watoto wanaolelewa huko wapate elimu inayostahili kufikia ndoto zao kwani kila mmoja ana ndoto yake ili imfikishe pale alipodhamiria,"alisema Mwakalosi.

Alisema kuwa licha ya kutoa misaada mbalimbali lakini wametoa vifaa vya shule na fedha kwa ajili ya kukabili changamoto hizo za kielimu na mahitaji muhimu ya kila siku.

"Tumekuwa tukijitolea misaada mbalimbali kwenye vituo vya watoto wenye mahitaji lengo ni kuona wnapata tabasamu na kuondoa tofauti ya watoto hao na wale wanaoishi na familia zao,"alisema Mwakalosi.

Naye Meneja wa kituo hicho Florida Frank alisema kuwa mbali ya changamoto mbalimbali kubwa ni kwa madarasa ya mtihani ambapo huwabidi kukaa kambini hasa wale wa kidato cha pili na cha nne kwani kwa sasa wanapaswa kulipa shilingi 60,000 kwa mwanafunzi mmoja na wako wanne.

Frank alisema hata pale wanapokuwa wamechaguliwa kwenda vyuoni gharama zinakuwa ni kubwa sana hivyo kituo kuelemewa na mzigo mkubwa wa kifedha na kuomba wadau kujitolea kuunga mkono kituo chao.

Alisema kuwa jamii inapaswa kupandikiza kitu muhimu katika maisha ikiwa ni pamoja na kuwezesha kwenye suala la elimu kituo hicho kikianzishwa mwaka 2003 kikiwa na watoto watano na sasa kina watoto 48 wanaosoma elimu tofauti hadi vyuo vikuu.

Monday, August 10, 2026

WANNE WAFA 46 WAJERUHIWA AJALINI

WATU wanne wamefariki dunia na wengine 46 kujeruhiwa baada ya basi dogo walilokuwa wakisafiria kutoka Vikumburu Kisarawe kwenda Dar es Salaam kupinduka.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Salim Morcase ilisema kuwa basi hilo liliacha njia na kupinduka na kusababisha vifo na majeruhi.

Morcase alisema kuwa ajali hiyo ilitokea Agosti  9 mwaka huu majira ya saa 11:00 jioni huko eneo la kona ya Kinyanyiko katika barabara ya Pugu Kisarawe Wilaya ya Kisarawe.

"Gari lenye namba za usajili T 177 DBV aina ya Fuso likitokea Vikumburu kwenda Dar es Salaam likiendeshwa na Salehe Mtumwa (35) na Mkazi wa Chanika Dar es Salaam liliacha barabara na kupinduka kisha kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi kwa watu 46,"alisema Morcase.

Alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi ambapo dereva alishindwa kulimudu gari kwenye mteremko mkali hivyo kupelekea gari hilo kupinduka.

Aliwataja waliofariki kuwa ni dereva wa gari hilo Salehe Mtumwa (35) na Mkazi wa Chanika Dar es Salaam,  Mwika Gwesele (38) Mkazi wa Dar es Salaam, Fatuma Momba Mkazi wa Buguruni Dar es Salaam na Sivijui Samatha (40) Mkazi wa Dar es Salaam.

Aliwataja majeruhi wanaopatiwa matibabu Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ni Hamis Mtitu (55) Mkazi wa Mbagala, Dar es Salaam, Farida Hassan (28) Mkazi wa Vingunguti Dar es Salaam, Husna Bakari (26) Mkazi wa Buza Dar es Salaam, Radhia Sultan (36)Mkazi wa Tabata Dar es Salaam, Neema Hassan (42) Mkazi wa Temeke, Dar es Salaam.

Majeruhi wengine ni Pilli Kondo (40) Mkazi wa Tabata Dar es Salaam, Salama Ramadhan (40)Mkazi wa Kigogo Dar es Salaam, Salumu Rajabu (56) Mkazi wa Mbande Dar es Salaam, Pilli Habibu (28) Mkazi wa Majohe Dar es Salaam, Amina Ramadhan (64) Mkazi wa Boga Wilaya ya Kisarawe.

"Majeruhi wengine saba wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe ambapo kati yao wanaume ni watatu na wanawake ni wanne huku majeruhi wengine 29 wamepatiwa matibabu katika Hospitali hiyo ya Kisarawe na kuruhusiwa," alisema Morcase.

Aidha alisema kuwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linawataka madereva wote wa vyombo vya moto kuzingatia sheria ya usalama barabarani pamoja na kanuni zake ili kuepusha ajali zinazosababishwa na uzembe. 

"Hatua kali zitaendelea kuchukuliwa kwa madereva watakaosababisha ajali kwa uzembe au kutokuzingatia sheria za usalama barabarani na kanuni zake,"alisema Morcase.

Sunday, August 9, 2026

WATANZANIA WAASWA KUSAIDIA ELIMU WATOTO WA VITUO WENYE UHITAJI





JAMII imeaswa kugharamia suala la elimu kwenye vituo vya watoto wenye uhitaji ili kwa kutatua changamoto za kielimu kwa watoto hao waweze  kutimiza ndoto zao.

Hayo yalisemwa na katibu wa kikundi cha Eddy Charity cha Kibaha, Edgar Mwakalosi wakati kilipotembelea kituo cha Kisarawe Safe House na kutia misaada mnalimbali.

Mwakalosi alisema kuwa vituo hivyo vinachangamoto nyingi ikiwa ni pamoja namna ya kuwapatia elimu watoto waishio kwenye vituo hivyo hasa wanapofikia hatua ya kuelekea kufanya mitihani ya kitaifa au kwenda vyuoni.

"Jamii inapaswa kuvisaidia vituo hivyo kwenye suala la kielimu ili watoto wanaolelewa huko wapate elimu inayostahili kufikia ndoto zao kwani kila mmoja ana ndoto yake ili imfikishe pale alipodhamiria,"alisema Mwakalosi.

Alisema kuwa licha ya kutoa misaada mbalimbali lakini wametoa vifaa vya shule na fedha kwa ajili ya kukabili changamoto hizo za kielimu na mahitaji muhimu ya kila siku.

"Tumekuwa tukijitolea misaada mbalimbali kwenye vituo vya watoto wenye mahitaji lengo ni kuona wnapata tabasamu na kuondoa tofauti ya watoto hao na wale wanaoishi na familia zao,"alisema Mwakalosi.

Naye Meneja wa kituo hicho Florida Frank alisema kuwa mbali ya changamoto mbalimbali kubwa ni kwa madarasa ya mtihani ambapo huwabidi kukaa kambini hasa wale wa kidato cha pili na cha nne kwani kwa sasa wanapaswa kulipa shilingi 60,000 kwa mwanafunzi mmoja na wako wanne.

Frank alisema hata pale wanapokuwa wamechaguliwa kwenda vyuoni gharama zinakuwa ni kubwa sana hivyo kituo kuelemewa na mzigo mkubwa wa kifedha na kuomba wadau kujitolea kuunga mkono kituo chao.

Alisema kuwa jamii inapaswa kupandikiza kitu muhimu katika maisha ikiwa ni pamoja na kuwezesha kwenye suala la elimu kituo hicho kikianzishwa mwaka 2003 kikiwa na watoto watano na sasa kina watoto 48 wanaosoma elimu tofauti hadi vyuo vikuu.

Thursday, August 6, 2026

AHUKUMIWA MAISHA JELA KWA ULAWITI MWINGINE MIAKA 20 NA FAINI M 1 KWA KUDHALILISHA MTOTO

SALIM Mang'ombe (29) mkazi wa Wilaya ya Bagamoyo amehukumiwa kifungo cha maisha jela kwa kosa la kulawiti mtoto mwenye umri wa miaka (10) ambaye alikuwa ni jirani yake.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Salim Morcase alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwezi Julai.

Kwenye tukio lingine Salim Masanja (33) Mkazi wa Wilayani Kibaha amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela na kulipa fidia ya shilingi milioni moja kwa tuhuma za kumdhalilisha mtoto wa kike (6).

Morcase amesema kuwa mshtakiwa huyo ni baba mdogo wa mhanga ambaye alikuwa akiishi naye nyumbani kwake na kesi hizo ni za ukatili wa kijinsia.

Amesema kuwa kesi zilizofikishwa mahakamani kwa kipindi hicho zilikuwa 117 huku kesi 63 zilisikilizwa na kumalizika ambapo kesi 48 zimepata mafanikio.

Amesema kuwa jamii kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanapaswa kushirikiana ili kukabiliana na vitendo vya ukatili kwa watoto.

Wednesday, August 5, 2026

POLISI YAWAREJESHA SHULENI WANAFUNZI 114

JESHI la Polisi Mkoani Pwani limefanikisha kuwarejesha Shuleni wanafunzi 114 ambao walishindwa kuripoti shule kutokana na sababu mbalimbali.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Salim Morcase amesema kuwa jumla ya wanafunzi 573 walikuwa hawajaripoti shuleni.

Morcase amesema kuwa kati ya wanafunzi hao ambao hawakuripoti Shule za Msingi walikuwa 251 na wa Sekondari walikuwa ni 322 ambao walibainika katika kipindi hicho licha ya kuwa wanafunzi hao kuwa na wa miaka tofauti tofauti.

Amesema kuwa changamoto nyingine ni mimba za utotoni ukosefu wa mahitaji ya msingi kama vile sare za Shule na madaftari  na changamoto za kiafya na kiuchumi.

Amewataka wazazi na walezi kushirikina na viongozi wa dini na wa kiserikali katika kupambana na viashiria vya vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watoto ndani ya jamii.


Saturday, August 1, 2026

HALMASHAURI YA MANISPAA KIBAHA YAZINDUA MAGARI MRADI WA (TACTIC)

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imezindua magari mawili yatakayotumika kwenye mradi wa ujenzi wa barabara za lami kwenye kupitia mradi wa uboreshaji miundombinu ya Miji na Vijiji (TACTIC) wenye thamani ya shilingi bilioni 19.8

Akindua magari hayo ambayo yatatumika kwenye mradi huo Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo alisema magari hayo yatawezesha utekelezaji mradi kuwa rahisi.

Mawazo alisema kuwa magari hayo ni moja ya makubaliano mkataba wa mradi huo na yakimaliza kutumika yanarudi Halmashauri kwa ajili ya shughuli zingine za kutoa huduma kwa wananchi kupitia wataalamu.

"Mradi huu unaenda kuleta mabadiliko chanya na uboreshaji wa miundo mbinu mbalimbali ya Manispaa ya Kibaha na kuwa na mwonekano mzuri na kuleta urahisi wa usafiri na usafirishaji,"alisema Mawazo.

Alisema kuwa katika miradi hiyo ya Tactic wanakwenda kuitekeleza kwa ubora zaidi na Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha inaenda kuwa ya kwanza na mfano kwa Halmashauri zingine katika utekelezaji na usimamizi wa miradi hii nchini.

"Wananchi wa Kibaha wanapaswa kujivunia na kutangaza maendeleo yanayofanywa na serikali hii kwani Manispaa ya Kibaha ina neemeka na dira ya Rais na mmeona maendeleo yanavyokuja kwa kasi na tutakuwa Halmashauri ya mfano kwa kila kitu,"alisema Mawazo.

Akisoma taarifa ya mradi huo Ofisa Utumishi  Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mrisho Mlela alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuleta miradi yenye fedha nyingi na usimamizi mzuri wa viongozi wa Wilaya na Mkoa kwa utekelezaji wa Ilani kwa maslahi ya Manispaa ya Kibaha.

Mlela alimpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa kwa usimamizi mzuri wa masuala mbalimbali ya mapato usimamizi wa miradi pamoja na tija katika utendaji wa Halmashauri.

Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha imepokea magari hayo mawili kutoka kwenye Mkataba wa mradi wa Tactic ambapo yatatumika katika mradi wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 4.8 Tughe-Anglikana barabara ya Picha ya Ndege - Lulanzi na soko la Loliondo Mnarani.

MADARASA JANJA KUPUNGUZA CHANGAMOTO UPUNGUFU WA WALIMU NCHINI

MEYA wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo amezindua Darasa Janja (Live Teaching) Shule ya Sekondari Bundikani na kuiomba Serikali kuanzisha madarasa hayo kote nchini ili kukabiliana na upungufu wa walimu

Mawazo alitoa ombi hilo wakati akizindua darasa hilo shuleni hapo ambapo shule hiyo ni Sekondari ya Kata ya Maili Moja Wilayani Kibaha na kuwa darasa janja yatasaidia kuwafanya wanafunzi kuwa na ari ya kusoma.

Amesema kuwa mwalimu mmoja anayefundisha kupitia darasa janja moja anaweza kufundisha shule zote ambazo zitakuwa zimeunganishwa kwenye mfumo huo wa darasa la aina hiyo kote nchini kwa wakati mmoja.

"Mfumo huu wa darasa janja ni mzuri kwa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa walimu kwani mwalimu mmoja anauwezo kufundisha shule zote ambazo zimeunganishwa kwenye mfumo huo,"amesema Nicas.

Aidha amesema kuwa pia mbali ya kufundisha wakati mmoja pia yale aliyofundisha mwalimu huyo yanaweza kurekodiwa na kuwafundisha wanafunzi wengine kwa ubora ule ule.

"Jambo zuri ni kuwa walimu wote wanaofundisha kupitia madarasa janja wote ni wale wenye umahiri wa kufundisha hivyo watawajengea wanafunzi uwezo mkubwa wa kujifunza na kupata ujuzi,"amesema Mawazo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mrisho Mlela amesema kuwa wataendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa janja kwenye shule za sekondari.

Mlela amesema kuwa wameendelea kuboresha sekta ya elimu kwa kujenga shule tatu za mfumo wa Kiingereza na shule hizo zote zimejengwa kutokana na fedha za mapato ya ndani na kutengeneza madawati viti na meza 4,000 kwa shule za msingi na sekondari.

Naye Mkuu wa Shule ya Bundikani Bernard Muyenjwa amesema kuwa wanaishukuru Serikali kwa kuwapatia darasa hilo janja kwani litarahisisha katika ufundishaji na kupunguza changamoto ya upungufu wa walimu.

Muyenjwa amesema kuwa kuanzishwa kwa darasa janja hilo shuleni kwao kutasaidia walimu kufundisha bila ya kuchoka wala kutumia nguvu kubwa na kuwapa wanafunzi umahiri na kujua namna ya kutumia teknolojia.

mwisho

Thursday, July 30, 2026

BINTI ATUHUMIWA KUMUUA MAMA YAKE MZAZI KWA KUMKATAZA KWENDA KWENYE SHEREHE YA KUMBUKIZI YA KUZALIWA RAFIKI YAKE.

BINTI mwenye umri wa miaka (16) Mkulima na Mkazi wa Kijiji cha Msoga Chalinze Wilayani Bagamoyo anashikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya mama yake mzazi baada ya kumzuia kuhudhuria sherehe ya kumbukumbu ya kuzaliwa rafiki yake.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Salim Morcase kuwa Mama yake Hadija Shaha ambaye ni mlemavu wa miguu.

Morcase amesema kuwa tukio hilo lilitokea Julai 28 mwaka huu majira ya saa 5:00 usiku huko katika Kijiji cha Msoga Chalinze ambapo mtuhumiwa alimuua mama yake kwa kumchoma kwa kitu chenye ncha kali.

"Chanzo cha tukio hilo ni kuwa marehemu alimkataza binti yake Rahma Tito kwenda kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa ya rafiki yake (birthday party) iliyokuwa inafanyika maeneo ya jirani na Hospitali ya Msoga,"amesema Morcase. 

Amesema kuwa baada ya binti huyo kuzuiwa kwenda kwenye sherehe alianza kumshambulia mama yake kisha kumchoma na kitu chenye ncha kali kichwani.

"Julai 29 mwaka huu  majira ya saa 1:00 asubuhi fundi ujenzi alifika nyumbani kwa Shaha kufuata mfuko wa saruji na fedha yake ya ujenzi ndipo alipogonga mlango na kufunguliwa na binti  wa marehemu jirani huyo aligundua kuna mwili wa marehemu ukiwa umelala sakafuni ukiwa na majeraha kichwani yanayotiririsha damu,"amesema Morcase.

Amesema kuwa mwili wa marehemu ulipelekwa Hospitali ya Msoga ambapo ulifanyiwa uchunguzi wa daktari kisha ulikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi. 

"Mara baada ya upelelezi kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo na Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linatoa rai kwa wazazi walezi viongozi wa dini na jamii kwa ujumla kushirikiana katika malezi ya watoto,"amesema Morcase.

Aidha amesema kuwa ushirikiano huo utasaidia kubaini tabia na changamoto za watoto wao kwenye makuzi ili hatua zichukuliwe mapema kabla hayajatokea madhara yoyote.

Tuesday, July 28, 2026

MAGANYA ATAKA WANACHAMA WASICHAFUANE.

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Fadhili Maganya amewataka wanachama waache kuchafuana kuelekea uchaguzi wa ndani mwakani.

Maganya aliyasema hayo Mjini Kibaha alipokuwa  akizungumza na viongozi wa Jumuiya hiyo pamoja na wanachama wa CCM Kibaha Mjini wakati wa ziara yake kutembelea Mkoa wa Pwani kukagua uhai wa chama na miradi ya maendeleo.

Alisema kuwa chama hakina shida nao bali wafuate miongozo na utaratibu wa chama kama unavyoelekeza.

"Mwakani tunaingia kwenye uchaguzi wa ndani baadhi wameanza kuchafuana tusikubali hali hiyo asitokee mtu wa kutoa maelekezo bali chama ndiyo kinatoa maelekezo,"alisema Maganya.

Aidha alisema kuwa watu wanaanza kukinzana na uchaguzi wa mwakani na unabeba taswira ya uchaguzi wa 2030 hivyo chama kitangulizwe mbele na siyo mtu.

"Tuwaacheni walioko madarakani wafanye kazi kwani muda wa uchaguzi bado watu wasubiri hadi muda utakapofika,"alisema Maganya.

Alibainisha kuwa kuna baadhi ya watu wanasiasa wa upinzani na wanaharakati wamekuwa wakibeza na kutoa lugha za maudhi na kudhalilisha wasipewe nafasi kwani wakidai eti serilali iliyopo ni haramu.

"Tusiruhusu tabia hiyo kwani Rais Dk Samia Suluhu anafanya kazi kubwa kwa kushirikiana na chama chake kwani Tume ya Uchaguzi iliita vyama vyote na kutaka visaini sheria za uchaguzi lakini baadhi vilikataa,"alisema Maganya.

Aliongeza kuwa uchaguzi ulikuwa wazi kwa kila chama na viongozi walichaguliwa kwa utaratibu uliowekwa na Tume ya Uchaguzi hivyo havina haja ya kulalamika.

"Kamati za siasa za chama zinapaswa kutatua migogoro ya ardhi kwa kushirikiana na serikali ambayo inafanya kazi kubwa kutatua migogoro hiyo,"alisema Maganya.

Naye Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya (CCM-NEC) kupitia Jumuiya ya Wazazi na Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa alisema kuwa Jumuiya imekuwa mstari wa mbele kuimarisha chama.

Jumaa alisema kuwa kwa sasa Jumuiya hiyo imeimarika sana na kuwa mhimili mkubwa wa chama katika utekelezaji wa ilani.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa Jumuiya ya Wazazi imefanya kazi kubwa katika utekelezaji wa ilani.

Koka alisema kuwa kwenye uchaguzi Mkuu Jumuiya hiyo iliongoza kwa kupiga kura na kuufanya Mkoa wa Pwani kuongoza kwenye suala la kura.

Awali akitoa taarifa ya Wilaya Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Moses Magogwa alisema kuwa uptikanaji wa huduma kwa sasa kwa wananchi ni asilimia 98.

Magogwa alisema kuwa Hslmashauri ya Manispaa imekuwa ikifanya vizuri katika ukusanyaji wa mapato ambapo asilimia 60 yanatokana kodi na ushuru mbalimbali wa huduma.

Alisema kuwa ujenzi wa barabara ya njia sita kutoka Maili Moja hadi Picha ya Ndege unatarajia kuanza na barabara kwa ajili ya magari ya mizigo nao utaanzia Picha ya Ndege.

ZAHANATI YA KILIMAHEWA YAWAPUNGUZIA UMBALI WANANCHI KUPATA HUDUMA

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Fadhili Maganya amepongeza ujenzi wa Zahanati ya Kilimahewa Kata ya Tangini Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha na kuitaka kuweka dirisha la Wazee ili waweze kupata huduma kwa urahisi wakati wa kupata matibabu.

Maganya ameysema hayo Mjini Kibaha alipotembelea Zahanati hiyo wakati wa ziara yake ya kutembelea Mkoa wa Pwani kuimarisha uhai wa chama na kutembelea miradi ya maendeleo na kusema kuwa ujenzi huo ni wa mapato ya ndani.

Amesema kuwa wazee waliambiwa kuwa watatengewa dirisha kwa ajili ya kuwapatia huduma hivyo ni vema dirisha hilo likawepo kwa ajili ya kuwahudumia na siyo kusema kuwa wapishwe ili wahudumiwa bali wawe na dirisha lao maalum.

"Tuliahidi kuwa tutawawekea dirisha lao maalum kwa ajili ya kupata huduma hivyo Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha lazima ihakikishe inawawekea dirisha lao ili wapate huduma za afya kwani wao lazima wahudumiwe vizuri pasipokuwa na changamoto,"amesema Maganya. 

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Catherine Saguti alisema kuwa lengo ni kurahisha upatikanaji wa huduma za afya kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha na ulianzishwa kutokana ongezeko la mahitaji ya huduma za afya kwenye eneo hilo.

Saguti amesema kuwa ujenzi ulianza Juni 2024 Halamshauri ilipokea kiasi cha shilingi milioni 233.5 na wananchi walichangia kiasi cha shilingi milioni 1 na shilingi milioni 50 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba hivyo kufanya gharama za mradi kuwa shilingi milioni 284.6.

Amesema kuwa serikali imeajiri wauguzi 32 ambapo Zahanati hiyo ina watumishi saba wanaotoa huduma na Zahanati hiyo imepatiwa watumishi wawili hivyo hakuna upungufu wa watumishi.

Zahanati ilianza kutoa huduma Aprili 2026 na hadi sasa imeshatoa huduma kwa watu 1,103 na inatoa huduma mbalimbali.


Monday, July 27, 2026

HALMASHAURI MANISPAA YA KIBAHA YAPONGEZWA UKUSANYAJI MAPATO NA UTOAJI MIKOPO KWA VIKUNDI

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Fadhili Maganya ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa kuweza kufanikisha ukusanyaji wa mapato.

Maganya ameyasema hayo kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere wakati akizungumza na viongozi wa Jumuiya hiyo wanaccm na uongozi wa Halmashauri wakati wa ziara yake Mkoani Pwani.

Amesema kuwa Halmashauri hiyo imeonyesha jinsi gani inavyopambana katika ukusanyaji wa mapato ambayo yanasaidia katika kuleta maendeleo kwa wananchi.

"Tunaipongeza Halmashauri kwa jitihada zake za ukusanyaji wa mapato na kuifanya kuwa moja ya Halmashauri zinazofanya vizuri nchini kwenye siala la ukusanyaji wa mapato,"amesema Maganya.

Aidha ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa kuvipatia mikopo ya asilimia 10 vikundi vya wajasiriamali kwa ajili ya kuendesha shughuli zao.

"Kama mmeweza kutoa mikopo na kutoa elimu kwa wananchi juu ya kukopa fedha hizo mnafanya jambo zuri ndivyo serikali inavyotaka wananchi wakopeshwe ili wafanye shughuli zao za kiuchumi,"amesema Maganya.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa amesema kuwa mwaka 2024/2025 walitoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 2.1 kwa vikundi 400 vyenye watu zaidi ya 3,000.

Shemwelekwa amesema kuwa changamoto iliyopo ni baadhi ya vikundi kutokuwa na sifa za kukopa lakini fedha zipo kwa vile vinavyokidhi vigezo vinakopeshwa.

Alisema kuwa baada ya mikopo kurejeshwa kulikuwa na madeni yaliyofikia kiasi cha shilingi bilioni 1.2 lakini wamefanya jitihada ya kufanikisha kurejesha na madeni yaliyobakia ni milioni 300.

Tuesday, July 21, 2026

WANANCHI WAJITOLEA KUFUFUA BARABARA

MTAA wa Machinjioni umefungua barabara ya kuelekea Shule ya Msingi Mamlaka na kurahisisha watumiaji kupita kwa urahisi wakiwemo wanafunzi kwenda Shuleni na magari ya kutoa huduma inapotokea dharura kama vile moto.

Barabara  hiyo ilijifunga wakati wa ujenzi wa barabara ya lami ya kutoka Tamco-Mapinga kuelekea Bagamoyo hivyo kusababisha watumiaji wakiwemo  wanafunzi kuzunguka umbali mrefu ili kwenda shule na kwenye makazi hasa wanaotumia usafiri wa magari na pikipiki.

Akizungumza wakati wa zoezi la kujitolea kufungua barabara hiyo ambayo miaka ya nyuma ilikuwa ikipitika Mwenyekiti wa Mtaa wa Machinjioni Kata ya Tangini Wilaya ya Kibaha Aidan Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa wananchi wa eneo hilo.

Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu hasa pale endapo ikitokea dharura kama vile moto au wagonjwa ilikuwa ikiwalazimu kuzunguka mbali hasa kwa matumizi ya vyombo vya moto ikiwemo magari na pikipiki.

"Tulikaa na wananchi na kukubaliana kuchanga kiasi cha shilingi 16,000 kila Kaya ili kufanikisha ufunguaji wa barabara hiyo na wananchi waliridhia na zoezi kuanza ambapo pia tuliwasiliana na Dawasa kwani kuna bomba linapita hapo hivyo walitoa wataalamu wao na kutuelekeza namna na kuchimba ili tusiharibu bomba hilo la maji,"alisema Mchiwa.

Emanuel Sabath alisema kuwa wanaushukuru uongozi wa Mtaa kwa kuwafungulia barabara hiyo hivyo kuwarahisishia na kuwaondolea usumbufu kuzungukia mbali na kupita kwenye eneo la mtu.

Sabath alisema kufunguka barabara hiyo kutarahisisha wananchi kupata huduma ikiwa ni pamoja na inapotokea mgonjwa anataka kupelekwa Hospitali wakiwemo wanawake wajawazito na hata gari la zimamoto kupita kwani kulishawahi kutokea moto lakini gari hilo likashindwa kupita.

Alisema kuwa hata wanafunzi wanaosoma Shule ya Msingi Mamlaka hasa wanaotoka maeneo ya Kilimahewa ambapo iliwabidi wazunguke kupita sehemu nyingine ambapo huwabidi kuzunguka hivyo kuchelewa kufika shuleni.

MASAUNI AWATAKA WANANCHI KUTUMIA FURSA YA HEWA UKAA




Na Mwandishi Wetu, Rufiji

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhandisi Hamad Masauni amewataka wananchi kutumia miradi ya utunzaji wa mazingira ili kupata hewa ukaa na kujiongezea kipato.

Masauni aliyasema hayo Wilayani Rufiji alipokuwa akizungumza na wananchi wakati wa ziara yake Mkoani Pwani kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo.

Alisema kuwa hewa ukaaa ni jambo kubwa la kiuchumi hivyo wananchi watumie kila fursa inayogusa hewa ukaa watumie rasilimali vizuri kupitia misitu. 

"Rufiji ina fursa nyingi za uzalishaji hewa ukaa kupitia, misitu migomba mikorosho kwani hii ni biashara nzuri watumieni wataalam ili wawape moingozo ili kuongeza kipato kwa kutumia fursa hii,"alisema Masauni.

Aidha alisema kuwa mabadiliko ya tabia nchi ni chanzo cha biashara kupitia mkataba wa Paris baada ya kukubaliana nchi zenye rasilimali za kupunguza hewa ukaa zilipwe.

"Kupitia kilimo madini na faida ya kuhifadhi miti tutalipwa hiyo ni changamoto muifanyie kazi kwani mna rasilimali za kutosha za kuwa miradi ya hewa ukaa,"alisema Masauni

Aliongeza kuwa Watanzania wanapaswa kutunza amani iliyopo na kuachana na yale yanayoweza kuharibu amani ya nchi kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma.

"Kipindi cha nyuma kulitokea changamoto hata wanaccm walikuwa hawavai sare za chama lakini sasa watu wana amani hivyo tunzeni amani kwani  umuhimu wa amani unajulikana na vijana wanasababu ya kuenzi umoja na kurithisha watoto wetu na Muungano ndiyo kiungo cha amani kupitia  waasisi wa taifa letu wametuachia msingi wa amani,"alisema Masauni.

Aliipongeza Wilaya ya Rufiji kwa kutekeleza kikamilifu kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye miradi mbali mbali ya maendeleo ya elimu afya miundombinu kilimo maji.

Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani Mwinshehe Mlao alisema kuwa Wilaya hiyo imepiga hatua kubwa ya kimaendeleo ukilinganisha na zamani kupitia uongozi wa Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Mlao alisema kuwa kwa ujumla Mkoa umepiga hatua kubwa ya maendeleo hivyo watu wanapaswa kuona jinsi gani maendeleo yaliyopatikana chini ya CCM.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge 
alisema kuwa mwaka wa fedha Mkoa ulipangiwa kukusanya bilioni 88 lakini hadi Juni 30 mwaka huu tayari zimekusanywa bilioni 135 na kuwa mkoa wa pili baada ya Dar es Salaam. 

Kunenge alisema kuwa Mkoa unajivunia Rais kwa kuwatumikia Watanzania na Rufiji ina miradi mikubwa ya uwekezaji na moja mradi alionyesha Urusi ni kilimo cha ndizi kupitia moja ya kampuni kubwa afrika.

Alisema kuwa kwa sasa kuna mifugo mingi na kuna ranchi ndogo na uchumi usitegemee chanzo kimoja ili kuwa salama kwa kutumia bahari na utalii kwani huwezi kushindana na mabadiliko ya dunia ni kijini na dira 2050 inataka kuwa na ajira milioni nane pato la Taifa trilioni moja pato la mwnanchi milioni 18 kwa mwaka.

Akikaribisha ugeni wa Waziri Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Luteni Kanali Fredrick Komba alisema kuwa Wilaya hiyo imefanikiwa kupanda miti ya mikorosho ipatayo milioni 1.5.

POLISI KATA MAILIMOJA AMTEMBELEA MZEE NA KUTOA MSAADA.





Na Mwandishi Wetu, Kibaha

Polisi Kata wa Mailimoja, Mkaguzi wa Polisi, Tupilike Mwabulambo ameambatana na Stesheni Sajenti Lusekelo Mwakalinga wa Wilaya ya Kibaha kumtembelea mzee Hamisi Nampatima wa mtaa wa Uyaoni ikiwa ni sehemu ya mpango wa kuwafikia wahitaji waliopo kwenye kata yake na kutoa msaada.

Akikabidhi baadhi ya mahitaji kwa mzee huyo Julai 20, 2026 INSP Tupilike alieleza kuwa kuna makundi mbalimbali katika jamii ambao wana changamoto ikiwemo za kiusalama na mahitaji muhimu hivyo anatembelea kaya hizo kuwasikiliza na kutoa kile alichojaliwa kwa wakati huo.

Kwa upande wake Mzee Hamis Nampatima, alilishukuru Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kwa msaada wanaompatia kwani sio mara ya kwanza kufika kwake, Mara kadhaa Sajenti wa Polisi Salum Ally wa Polisi Wilaya ya Kibaha amekua akimsaidia kwa kumpatia pesa na mahitaji mbalimbali ya nyumbani.

Naye, Mwenyekiti wa Mtaa wa Uyaoni, Katani humo, Bw. Fadhili Kindamba alipongeza Jeshi la Polisi kwa namna wanavyoshirikiana na wananchi kuimarisha ulinzi na usalama na kutatua changamoto zao zingine za kijamii.

Sunday, July 19, 2026

WANANCHI MTAA WA MACHINJIONI WAJITOLEA KUFUNGUA BARABARA

MTAA wa Machinjioni umefungua barabara ya kuelekea Shule ya Msingi Mamlaka na kurahisisha watumiaji kupita kwa urahisi wakiwemo wanafunzi kwenda Shuleni na magari ya kutoa huduma inapotokea dharura kama vile moto.

Barabara  hiyo ilijifunga wakati wa ujenzi wa barabara ya lami ya kutoka Tamco-Mapinga kuelekea Bagamoyo hivyo kusababisha watumiaji wakiwemo  wanafunzi kuzunguka umbali mrefu ili kwenda shule na kwenye makazi hasa wanaotumia usafiri wa magari na pikipiki.

Akizungumza wakati wa zoezi la kujitolea kufungua barabara hiyo ambayo miaka ya nyuma ilikuwa ikipitika Mwenyekiti wa Mtaa wa Machinjioni Kata ya Tangini Wilaya ya Kibaha Aidan Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu kwa wananchi wa eneo hilo.

Mchiwa alisema kuwa barabara hiyo ni muhimu hasa pale endapo ikitokea dharura kama vile moto au wagonjwa ilikuwa ikiwalazimu kuzunguka mbali hasa kwa matumizi ya vyombo vya moto ikiwemo magari na pikipiki.

"Tulikaa na wananchi na kukubaliana kuchanga kiasi cha shilingi 16,000 kila Kaya ili kufanikisha ufunguaji wa barabara hiyo na wananchi waliridhia na zoezi kuanza ambapo pia tuliwasiliana na Dawasa kwani kuna bomba linapita hapo hivyo walitoa wataalamu wao na kutuelekeza namna na kuchimba ili tusiharibu bomba hilo la maji,"alisema Mchiwa.

Emanuel Sabath alisema kuwa wanaushukuru uongozi wa Mtaa kwa kuwafungulia barabara hiyo hivyo kuwarahisishia na kuwaondolea usumbufu kuzungukia mbali na kupita kwenye eneo la mtu.

Sabath alisema kufunguka barabara hiyo kutarahisisha wananchi kupata huduma ikiwa ni pamoja na inapotokea mgonjwa anataka kupelekwa Hospitali wakiwemo wanawake wajawazito na hata gari la zimamoto kupita kwani kulishawahi kutokea moto lakini gari hilo likashindwa kupita.

Alisema kuwa hata wanafunzi wanaosoma Shule ya Msingi Mamlaka hasa wanaotoka maeneo ya Kilimahewa ambapo iliwabidi wazunguke kupita sehemu nyingine ambapo huwabidi kuzunguka hivyo kuchelewa kufika shuleni.

Friday, July 17, 2026

NSSF YAWATAKA WAAJIRI KUTUMIA MSAMAHA WA TOZO

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umetangaza nafuu kwa waajiri wenye malimbikizo ya michango kwa kuwapatia fursa ya msamaha wa tozo zitokanazo na ucheleweshaji wa michango, huku ukiwataka kuchangamkia fursa hiyo ili kupunguza mzigo wa madeni, kuimarisha uzingatiaji wa sheria na kulinda haki za wafanyakazi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba, alisema kuwa msamaha huo, ulioanza kutekelezwa tarehe 1 Juni 2026, utaendelea hadi 31 Desemba 2026. 

Bw. Mshomba alieleza kuwa tangu kuanza kwa msamaha huo, waajiri wameonyesha mwitikio chanya ambapo hadi sasa zaidi ya waajiri 6,000 wamejitokeza kutumia fursa hiyo na Mfuko umekwishakusanya zaidi ya shilingi bilioni 46 za michango tangu kuanza kwa msamaha huo tarehe 1 Juni 2026.

“Tunawasihi waajiri wote kutumia fursa hii mapema. Fedha ambazo wangezilipa kama tozo wanaweza kuzielekeza katika shughuli za uzalishaji, upanuzi wa biashara, kuongeza tija na kuboresha ustawi wa wafanyakazi,” alisema Bw. Mshomba.

Alisema msamaha huo utaendelea hadi tarehe 31 Desemba 2026, ambapo waajiri watakaolipa malimbikizo yote ya michango ya msingi ifikapo tarehe 31 Agosti 2026 watanufaika na msamaha wa asilimia 100 ya tozo.

Alifafanua kuwa waajiri watakaokamilisha malipo yao kati ya Septemba na Oktoba 2026, watanufaika na msamaha wa asilimia 75, huku wale watakaolipa kati ya Novemba na Desemba 2026 wakipata msamaha wa asilimia 50.

Aidha, alisema waajiri ambao hawakuwa na malimbikizo ya michango hadi tarehe 31 Mei 2026 lakini walikuwa na tozo pekee, watanufaika na msamaha wa asilimia 100 endapo wataendelea kuwasilisha michango yao kwa wakati hadi mwezi Desemba 2026.

Bw. Mshomba alisema fursa hiyo imetolewa ili kuwapa waajiri nafasi ya kurekebisha hali ya ulipaji wa michango na kutumia fedha ambazo zingelipwa kama tozo katika shughuli za uzalishaji, kuongeza tija na kuboresha mazingira ya kazi.

“Fedha ambazo waajiri wamekuwa wakizilipa kwa ajili ya kufidia tozo zinaweza kuelekezwa katika kuboresha maeneo yao ya kazi, kuongeza tija na kuimarisha uzalishaji.

Ndiyo maana fursa hii imetolewa ili waajiri wanufaike,” alisema.
Alisema ulipaji wa michango kwa wakati ni muhimu kwa kuwa unamwezesha mfanyakazi kupata haki zake za hifadhi ya jamii wakati anapopata majanga mbalimbali ikiwemo kustaafu.

NSSF YAENDELEA KUIMARIKA
Katika hatua nyingine, Bw. Mshomba alisema NSSF imeendelea kuimarika katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita, ambapo thamani ya Mfuko imeongezeka kutoka shilingi trilioni 4.8 mwezi Machi 2021 hadi kufikia zaidi ya shilingi trilioni 11.6 Juni 2026.

Alisema ukuaji huo umechangiwa na ongezeko la wanachama na michango, uwekezaji wenye tija, mazingira mazuri ya uwekezaji pamoja na matumizi ya teknolojia katika kuboresha huduma.

Alieleza kuwa kupitia mifumo ya TEHAMA, waajiri na wanachama sasa wanaweza kufuatilia na kuwasilisha michango, kufuatilia madai ya mafao na kupata huduma mbalimbali bila kulazimika kufika katika ofisi za NSSF.

Kuhusu ulipaji wa mafao, Bw. Mshomba alisema Mfuko umeendelea kuboresha mifumo yake ambapo kwa sasa mafao mengi hulipwa ndani ya siku 20, tofauti na siku 60 zinazotakiwa kisheria.

“Lengo letu ni kuhakikisha mwanachama anapata stahiki zake kwa wakati. Endapo kuna ucheleweshaji mara nyingi chanzo huwa ni mwajiri kutowasilisha michango kwa wakati,” alisema.

UWEKEZAJI WENYE TIJA, SKIMU YA HIFADHI KUONGEZA WANUFAIKA
Akizungumzia uwekezaji, alisema NSSF inaendelea kutekeleza miradi ya kimkakati inayochangia ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira, akitolea mfano Kiwanda cha Sukari cha Mkulazi ambacho kimeendelea kuongeza uzalishaji, kutoa ajira na kuwawezesha wakulima wanaokizunguka.

Kuhusu Skimu ya Hifadhi, Bw. Mshomba alisema mpango huo umewezesha wananchi waliojiajiri kujiunga na mfumo wa hifadhi ya jamii na kunufaika na mafao mbalimbali ikiwemo pensheni ya uzee, pensheni ya ulemavu, pensheni ya urithi, mafao ya uzazi, msaada wa mazishi pamoja na huduma za matibabu.

“Tunawahimiza waliojiajiri kujiunga kupitia Skimu ya Hifadhi kwa sababu mpango huu unabadilisha maisha yao na kuwapa uhakika wa kunufaika na mafao mbalimbali. Lengo letu ni kuhakikisha kila Mtanzania anakuwa Staa wa Mchezo katika kujilinda dhidi ya changamoto za maisha,” alisema Bw. Mshomba.

Alisema NSSF itaendelea kushirikiana na waajiri, wafanyakazi na wadau mbalimbali katika kuimarisha mfumo wa hifadhi ya jamii nchini na kuhakikisha unaleta manufaa kwa Watanzania wengi zaidi.

Wednesday, July 8, 2026

DKT. NICAS MAWAZO AKUTANA NA BALOZI KAIRUKI NCHINI UINGEREZA, WAJADILI FURSA ZA UWEKEZAJI KIBAHA

London, Uingereza | Julai 8, 2026
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Nicas Mawazo ambaye yupo nchini Uingereza katika ziara nchini humo, leo Julai 8, 2026 amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uingereza, Mheshimiwa Balozi Kairuki.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Kairuki amepongeza juhudi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuimarisha diplomasia ya uchumi, kuvutia uwekezaji na kusukuma mbele agenda ya maendeleo ya taifa.

Aidha, Balozi Kairuki ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha kwa mafanikio yake katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo na ukusanyaji wa mapato ya ndani, akieleza kuwa halmashauri hiyo imeendelea kuwa miongoni mwa halmashauri zinazofanya vizuri nchini.

Mazungumzo kati ya viongozi hao yamejikita katika kutafuta fursa za ushirikiano wa kiuchumi kwa Manispaa ya Kibaha, ikiwemo namna ya kuvutia wahisani, wawekezaji na wadau wa maendeleo kutoka Uingereza ili kuwekeza katika sekta mbalimbali zenye mchango mkubwa kwa maendeleo ya manispaa hiyo.

Dkt. Mawazo amesema kuwa mazungumzo hayo ni sehemu ya jitihada za kuitangaza Manispaa ya Kibaha kimataifa na kufungua milango ya ushirikiano itakayochochea uwekezaji, ukuaji wa uchumi na uboreshaji wa huduma kwa wananchi.

Friday, July 3, 2026

KUNENGE AMSHUKURU RAIS DK SAMIA KUKUZA VIPAJI VYA MICHEZO KWA VIJANA

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.



Mpya







MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.

mwisho.

KUNENGE AMSHUKURU RAIS DK SAMIA KUKUZA VIPAJI VYA VIJANA

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuinua vipaji vya wanamichezo vijana ili kuwa tegemeo kwa Taifa.

Kunenge ameyasema hayo wakati akizindua michezo ya riadha Kitaifa kwenye uwanja wa Filbert Bayi Mkuza Wilayani Kibaha.

Amesema kuwa Rais ameweka mazingira mazuri kwa wanamichezo nchini ambapo kwa sasa nchi inafanya vizuri kwenye michezo mbalimbali ikiwemo riadha.

"Nawapongeza Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuweka misingi mizuri kwa vijana wadogo ambao wameonyesha umahiri wa kukimbia licha ya kuwa na umri mdogo huu ndiyo uwekezaji mzuri kwenye vipaji,"amesema Kunenge.

Aidha amesema kuwa riadha ni mchezo ambao hupambani na mpinzani wako bali unapambana na rekodi hata ukishinda kama hujafikia rekodi nzuri bado hujapata mafanikio.

"Nimefurahi nimewaona manguli wa riadha nchi kama vile Steven Akwari, Juma Ikangaa, Filbert Bayi, Seleman Nyambui hawa waliiletea nchi sifa kubwa huko duniani vijana wanapaswa kuwaiga ili nao wafanye vyema,"alisema Kunenge.

Amebainisha kuwa Mkoa wa Pwani uko kwenye mipango mbalimbali ya kujenga viwanja ambavyo vitakuwa na ubora ili kupata wanamichezo wazuri wa baadaye.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya ufundi wa Shirikisho la Riadha Tanzania Alfredo Shahanga amesema kuwa wanajivunia kwa wanariadha wake kufanya vizuri akiwemo Alfonce Simbu kwa kushinda medali ya dhahabu kwenye mbio za marathoni za Dunia za Tokyo.

Shahanga amesema kuwa changamoto kubwa ni upungufu wa fedha viwanja vizuri vyenye vifaa vya kisasa na uwekezaji kwa vijana hata hivyo wanashirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha changamoto hizo zinapungua na mchezo unachezwa.

Naye katibu wa Chama cha Riadha Mkoa wa Pwani Elisha Daniel amesema kuwa mashindano hayo yameanza vyema kwani walifanya maandalizi vizuri na matarajio mwaka huu mafanikio yatakuwa makubwa.

Daniel akizungumzia juu ya timu ya mkoa huo amesema kuwa maandalizi ya timu yako vizuri na wanategemea kufanya vizuri kwani vijana wameandaliwa vizuri na walimu wao lengo ni kuupambania mkoa.

mwisho.

Thursday, July 2, 2026

PWANI KUMUUNGA MKONO RAIS DK SAMIA UKUSANYAJI MAPATO

MKOA wa Pwani umesema utashirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha inakusanya mapato ili kuinua uchumi kupitia uwekezaji wa viwanda kumuunga Mkono Rais Dk Samia Suluhu Hassan.

Hayo yelisemwa na Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Pili Mnyema wakati wa sherehe za kutimiza miaka 30 ya TRA kimkoa ambapo walushuhudia moja kwa moja maadhimisho hayo Kitaifa ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais Dk Samia.

Mnyema alisema kuwa kama Rais alivyotaka TRA kufanya vizuri ili akistaafu Mamlaka hiyo iwe kwenye hali nzuri ndiyo itakuwa furaha yake.

"Tutamuunga mkono Rais kwa kushirikiana na TRA kuhakikisha walipa kodi wanalipa kodi pasipo kukwepa kodi ili kuinua uchumi hasa ikizingatiwa Pwani ni mkoa wa kimkakati kwa kuwa na viwanda vingi,"alisema Mnyema.

Alisema kuwa ukusanyaji mzuri unaofanyika unatokana ushirikiano uliopo baina ya mamlaka na walipa kodi ambapo hicho ni kiashiria cha ukuaji wa uchumi.

"Pia ukusanyaji utaendana na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya mwaka 2050 ambayo ndo inaanza kazi kuanzia sasa na hapa tunashirikiana na sekta binafsi katika kuchangia uchumi,"alisema Mnyema.

Aidha alisema kuwa Mkoa utasimamia kuhakikisha malengo ya nchi yanatimia kwa kuwa na uwezo wa kukusanya mapato kwa walipa kodi kulipa kwa hiyari ikiwa ni maono ya Rais.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani Salim Makame alisema kuwa Mamlaka imejipanga kuhakikisha wale wote wanastahiki kulipa wanalipa kwa hiyari.

Makame alisema kuwa wameyapokea maagizo yote yaliyotolewa na Rais ya namna ya kuboresha ukusanyaji wa Mapato pia kutumia mifumo ya teknolojia.

Wednesday, July 1, 2026

NASHUKURU SANA MTANDAO NAJUKWAA KUBWA BELLE NAIJA

ALHAMDULILAH ALLAH NDIYO SHAHIDI WA KILA JAMBO 

Jukwaa kubwa la kidijitali nchini Nigeria linalojihusisha na masuala ya burudani, mitindo, mitindo ya maisha (lifestyle), na harusi za Kiafrika. Ilianzishwa mnamo mwezi Julai mwaka 2006 na mjasiriamali wa Nigeria anayeitwa Uche Pedro (jina la kuzaliwa Uche Eze).

NASHUKURU KUPOSTI PICHA YANGU NA STAA MKUBWA NCHINI NIGERIA NI HESHIMA KUBWA KUTAMBUA MCHANGO WANGU KATIKA AFRIKA 

Layi Wasabi (jina lake halisi ni Isaac Ayomide Olayiwola) ni mchekeshaji, mwigizaji, na mtengeneza maudhui maarufu wa mtandaoni kutoka nchini Nigeria. 

Anajulikana sana kwa uchekeshaji wake wa kipekee na wa akili (philo-comedy) kupitia video fupi (skits) kwenye mitandao ya kijamii

MKUTANO (AFRICA'S CREATIVE FUTURE TAKES CENTRE STAGE IN LUSAKA- (MUSTAKABALI WA UBUNIFU WA AFRIKA WACHUKUA KITUO KIKUU LUSAKA)

ALHAMDULILAH ALLAH NDIYO SHAHIDI WA KILA JAMBO 
LEO TAREHE 29 JUNE 

NIMESHIRIKI  MKUTANO (AFRICA'S CREATIVE FUTURE TAKES CENTRE STAGE IN LUSAKA- (MUSTAKABALI WA UBUNIFU WA AFRIKA WACHUKUA KITUO KIKUU LUSAKA)

Mkutano huu utachukua siku 7 kuanzia tarehe 29 Juni  hadi 5 Julai 

Mkutano huo ulioandaliwa na Wizara ya Vijana, Michezo na Sanaa nchini Zambia Kwa siku tano takribani vijana 3000 kushikiriki 
Kuanzia watengenezaji filamu na wanamuziki hadi wabunifu wa mitindo, wawekezaji na watunga sera, mamia ya wajumbe kutoka kote barani wamekusanyika katika 

Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mulungushi kwa ajili ya Mkutano wa Biashara wa Viwanda vya Ubunifu wa 2026, Soko la Ubunifu la Afrika (ACM) na Tamasha la Sanaa la Kitaifa la Kwimbo, wakiwa wameunganishwa na lengo moja la kugeuza ubunifu wa Afrika kuwa biashara, ajira na fursa za kimataifa.

Akifungua rasmi mkutano huo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Vijana, Michezo na Sanaa, Bw. Kangwa Chileshe, 

Alisema Zambia imepiga hatua kubwa katika kuiweka sekta ya ubunifu katika nafasi nzuri ya kuchangia uchumi wa nchi.

Alitaja mfululizo wa mageuzi yaliyotekelezwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa Sanaa kama idara ndani ya Wizara, uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Sanaa ya kwanza ya nchi, mapitio ya Sera ya Taifa ya Filamu, marekebisho ya sheria iliyopitwa na wakati, kuondolewa kwa ushuru wa uagizaji wa vifaa vya filamu na muziki, na Zambia kujiunga na mfumo wa ATA Carnet ili kurahisisha usafirishaji wa vifaa vya ubunifu kuvuka mipaka.

Bw. Chileshe alisema serikali pia imewekeza kwa wasanii wenyewe, ambapo zaidi ya wabunifu 3,000 wamepatiwa mafunzo ya kusoma na kuandika kuhusu fedha na maendeleo ya biashara, huku zaidi ya 2,000 wameandikishwa kwenye mfuko wa hifadhi ya jamii ambao hutoa pensheni, mafao ya uzazi, msaada wa mazishi na upatikanaji wa mikopo.

Monday, June 29, 2026

POLISI MKOANI PWANI LINACHUNGUZA VIFO VYA MWANAMKE NA MTOTO

JESHI la Polisi Mkoani Pwani linafanya uchunguzi wa tukio la mauaji ya mwanamke mmoja na mtoto ambao hawakufahamika yaliyotokea Mbwewe Wilaya ya Kipolisi Chalinze Mkoa wa Pwani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani Salim Morcase kwa vyombo vya habari zilisema kuwa tukio hilo la mauaji ya watu wawili lililotokea Juni 2 mwaka huu  majira ya saa 9:00 alasiri huko Kitongoji cha Nung'uli Kijiji cha Kwang'andu Kata ya Mbwewe Halmashauri ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo.

Taarifa hiyo ilibainika kuwa watu hao ni mwanamke
mmoja anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka (20-25) na mtoto ambaye hakufahamika jinsia yake kutokana na kuungua sana na moto mwenye
umri unaokadiriwa kuwa miaka (3-6) ambao mpaka sasa bado hawajafahamika wala watu waliosababisha mauaji hayo.

"Ikumbukwe katika eneo la tukio hilo zilikutwa tiketi mbili za basi la Passion Video Coach linalofanya safari zake kati ya Dar es Salaam kwenda Miono kupitia Chalinze zilizokatwa tarehe Mei 31 mwaka huu,"alisema taarifa hiyo.

Taarifa zilisema kuwa tiketi hizo zilikiwa na majina ya Adela na Modest ambapo Jeshi bado linachunguza chanzo cha mauaji hayo wakati miili ya wahanga imehifadhiwa katika Hospitali ya Msoga Halmashauri ya Chalinze.

Kutokana na mauaji hayo Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani linaendelea kutoa wito kwa mtu yeyote anayewafahamu watu hao au mwenye taarifa zozote zinazoweza kusaidia kuwatambua wafike Ofisi ya kamanda wa Polisi Mkoa
wa Pwani.

 "Au wapige simu namba 073900995, 065837601 0 na 0753855570 ili kuendelea kusaidia uchunguzi na kuwapata ndugu wa marehemu kwa wakati,"iliongeza taarifa hiyo.

AKINAMAMA WATAKIWA KUWAKUMBUKA VIJANA WAKIUME

MWANASIASA mkongwe na aliyewahi kuwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto Sophia Simba ameitaka jamii kuwawezesha kiuchumi vijana wa kiume ambao wamesahaulika.

Simba ameyasema hayo Mjini Kibaha wakati wa kuadhimisha miaka 10 ya Kikundi cha Super Women 2017 na kuwa baada ya wanawake kufanikiwa vijana wakiume nao waangaliwe.

Amesema kuwa kwa muda mrefu jamii iliwekeza kudai haki za wanawake ambapo kwa sasa wamepiga hatua ya kimaendekeo baada ya nguvu kubwa kutumika huku wale wa kiume wakiwa wamesahaulika.

Simba ambaye pia aliwahi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora alisema kuwa kwa sasa vijana wa kiume wana hali mbaya kiuchumi.

"Tumshukuru Mungu kwani kwa sasa wanawake angalau wamepiga hatua kiuchumi tuwaangalie na vijana wakiume ili nao kwa kuwajengea uwezo wa kiuchumi,"amesema Simba.

Aidha alikipongeza kikundi hicho kwa mafanikio waliyoyapata kwa muda huo tangu kuanzishwa kwake kwani baadhi ya vikundi vinaanzishwa na havichukui muda mrefu vinakufa.

Naye mwanzilishi wa kikundi hicho Beth Msimbe amesema kuwa wamepata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kukopeshana fedha kwa riba nafuu kupitia mfuko wa kikundi kwa fedha wanazoweka ambapo mkopo ni mara tatu ya fedha waliojiwekea.

Msimbe amesema kuwa wameweza kukuza biashara zao na kuwa wafanyabiashara wakubwa pia wamekuwa wakifanya matendo ya huruma kwa watu wenye uhitaji na kuwataka wanawake wawe na wavumilivu kwa kufuata sheria na taratibu.

Kwa upande wake mwenyekiti kikundi hicho Betha Kimambo amesema kuwa wanatarajia kuanzisha mradi wa kukodisha vyombo ili kuongeza kipato ndani ya kikundi.

Kimambo amesema kuwa mbali ya kupata mafanikio kuna baadhi ya changamoto ikiwa ni pamoja na baadhi ya wanachama kujitoa.





Sunday, June 28, 2026

VIJANA WENYE VIPAJI VYA MICHEZO WATAKIWA KUWA NA NIDHAMU

VIJANA wenye vipaji vya michezo nchini wametakiwa kusoma kwabidii na kuwa na nidhamu ili waweze kufikia viwango vya juu na kuwa tegemeo kwa Taifa.

Hayo yamesemwa na Gilbert Maregesi ambaye alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kibaha wakati wa kufunga tamasha la michezo lililoandaliwa na Compassion Kanda ya Mashariki lililofanyika kwenye Viwanja vya Shirika la Elimu Kibaha Tumbi.

Maregesi amesema kuwa serikali imekuwa ikiwekeza kwenye sekta ya michezo kwa vijana ili kuendeleza vipaji vyao na kuwa tegemeo kwa Taifa kwenye sekta hiyo ambayo pia ni ajira kwa vijana.

"Ili kulinda vipaji vyenu mnapaswa kuwa na nidhamu ili muweze kufika mbali kwani mbali ya kunufaika binafsi pia mtaliwezesha Taifa kuwa na wachezaji wazuri watakaoliwakilisha Taifa kwenye michezo mbalimbali,"amesema Maregesi. 

Naye mwakilishi wa meneja wa Compassion Kanda ya Mashariki Daudi Lawi inayoundwa na mikoa ya Pwani Morogoro na Dar es Salaam amesema tamasha hilo la awamu ya nne limeshirikisha wanamichezo 430 kutoka mikoa hiyo.

Lawi amesema kuwa baada ya kukamilisha tamasha hilo lilobeba ujumbe wa Kipaji changu Mtaji wangu watachaguliwa wachezaji bora ambao watawakilisha Kanda hiyo kwenye mashindano ya Taifa.

Kwa upande wake James Mhina Kanda ya Mlandizi ambao walikuwa wenyeji wa mashindano hayo amesema kuwa michezo hiyo inajenga mahusiano na kipaji ni msaada katika maisha.

Mwenyekiti wa Mashindano hayo Lucas Kiluwasha amesema kuwa vipaji vyao ndiyo mtaji wao hivyo wavitumie vizuri na kuwataka wadau wa michezo kushuhudia michezo ili wachukue vipaji na kuviendeleza.

Rais wa Vijana Kanda ya Mashariki amesema kuwa michezo hiyo imewasaidia kuwaongezea ujuzi na kukuza vipaji vyao na kujumuika na kufahamiana kwani hiyo ndiyo njia ya mafanikio.

Mgeni rasmi ametoa fursa ya vijana Milovan Kilingo kutoka Gairo na Joshua Joakim wa Mkuza Kibaha kujiunga na bendi ya Jkt Ruvu ili waendeleze vipaji vyao.

Baadhi ya michezo iliyochezwa ni pamoja na mpira wa miguu, pete, riadha na michezo ya ndani ikiwemo sanaa ya uimbaji, upigaji wa vyombo vya muziki, maonyesho ya mavazi na sarakasi na yalishirikisha vijana wenye umri chini ya mi 17 na 22.

MWANADIPLOMASIA OMARY PUNZI ATEULIWA KUSHIRIKI MKUTANO WA CREATIVE

Mwanadiplomasia na Mchambuzi wa Masuala ya Kidiplomasia Siasa , Itifaki na Maadili Omary Punzi ateuliwa kushiriki katika mkutano wa Creative Convergence 2026 . 

Mkutano huu unaojumuisha Africa Creative Market (ACM), Creative Industry Business Summit (CIBS), na Kwimbo National Arts Festival, unafanyika kuanzia Juni 29 hadi Julai 4, 2026 jijini Lusaka, Zambia.

Mkutano huo unaisimamiwa na Wizara ya Vijana, Michezo na Sanaa nchini Zambia 

Utafanyika katika  kumbi za mikutano zilizopo Mulungushi International Conference Centre kuanzia Juni 29 hadi Julai 2, 2026 na kuanzia tarehe 3 hadi 4 Julai 

Tamasha la Sanaa,  tamasha la Kwimbo  huko Polo B, Lusaka Showgrounds. 

Mkutano huo utakutanisha Vijana zaidi 10000  kutoka Bara la Afrika.

kushiriki  Programu na Warsha (Sessions & Masterclasses)

Mijadala ya Biashara, Mijadala inayohusu biashara ya sanaa, filamu, muziki, teknolojia (kama AI), na mitindo.

Mafunzo ya Kitaalamu, Ufikiaji wa masterclasses zinazoendeshwa na washirika wa sekta, mfano mafunzo ya upigaji picha au uigizaji.

Kuunganisha Mtandao wa Biashara (Networking & Deal Rooms)

Ushirikiano wa Kibiashara, mikutano ya kibiashara (kama vile Deal Rooms au Creative Pitch Zone) ambapo wabunifu wanakutana na wawekezaji, wafadhili, na watengeneza sera ili kugeuza mawazo kuwa mikataba ya kazi.

MAWAZO YA VIJANA




SERIKALI imesema kuwa itatumia mawazo ya vijana walioshiriki shindano la Vijana Uchumi Challenge kuwa mpango ambao utaleta suluhisho la namna ya kutatua baadhi ya changamoto ndani ya jamii.

Hayo yalisemwa Kibaha na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Jenifa Omollo wakati wa kufunfa mafunzo ya siku nne kwa vijana 100 walioandika mawazo juu ya masuala ya uchumi kupitia jukwaa la Vijana Uchumi Challenge.

Omollo alisema kuwa mawazo yaliyoandikwa na vijana yameonyesha kuwa yakiboreshwa yanaweza kuwa mpango mzuri ambao unaweza kukabili changamoto mbalimbali ndani ya jamii na Taifa kwa ujumla.

"Mawazo yote yaliyowasilishwa hayataachwa badala yake yataboreshwa na kupatiwa fursa ili yawe mpango ambao utakuwa suluhu kwa baadhi ya changamoto ili kuleta tija na kusaidia Taifa mojawapo likatoa ajira kwa vijana,"alisema Omollo.

Alisema kuwa mawqzo hayo ni bunifu ambazo zimeonyesha jinsi gani vijana walivyokuwa na vipaji ambavyo vitatoa ajira na kuwa na manufaa kwa watu wengi hivyo kulisaidia Taifa.

"Vijana wana fursa nyingi kiuchumi lakini wanakosa taarifa sahihi kwani mawazo kama haya wanaweza kuyapatia fedha za Halmashauri nchini kupitia manunuzi ya umma kwenye mfumo wa Nest au mpango wa yendelezaji vipaji,"alisema Omollo.

Aidha alisema moja ya sekta yenye fursa nyingi ni kilimo ambayo imeajiri asilimia 75 ya Watanzania vijana wanaweza kunufaika kiuchumi kupitia mnyororo wa thamani na fursa kupitia dijitali.

Naye mwenyekiti wa kamati ya Vijana Uchumi Challenge Joseph Malecela alisema kuwa jumla ya mawazo zaidi ya 7,000 ya vijana kote nchini wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35 yaliwasilishwa na kuchujwa na kubaki 100 ambayo yatashindanishwa kupata mshindi.

 

Malecela alisema kuwa washiriki hao 100 ambao waliiingia kambini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere wamechujwa na majaji wabobezi wa masuala ya uchumi na fedha na kubaki 10 watashindana ili kumpata mshindi wa shindano hilo.


Rais Dk Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha kumpata kijana mwenye wazo zuri Julai 6 mwaka huu Jjiini Dar es Salaam  kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere Internation Convention Centre (JNICC) Jijuni Dar es Salaam.



mwisho

WALIPA KODI WATAKIWA KUONYESHA UZALENDO KWA KULIPA KWA WAKATI

WALIPA kodi wa Mkoa wa Pwani wametakiwa kulipa kwa wakati ili kuonesha uzalendo kwa nchi na mapato yanayokusanywa yaweze kutumika kwenye miradi mikubwa ya kimkakati ya maendeleo.

Hayo yalisemwa na Lilian Shirima aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Kibaha wakati wa mazoezi ya wadau na walipakodi ikiwa ni kuelekea miaka 30 ya mamlaka hiyo.

Shirima alisema kuwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ya maendeleo inatokana na kodi zinazolipwa hivyo wanapaswa kulipa kodi kwa wakati ili zifanikishe malengo ya utekelezaji wa miradi hiyo.

"Wafanyabiashara wanapaswa kutoa risiti pale wanapofanya mauzo na wananchi nao wanapaswa kudai risiti pale wanaponunua bidhaa kwani huo ndiyo uzalendo wa nchi,"alisema Shirima.

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani Peter Eliona    alisema kuwa wafanyabiashara wanapaswa kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwani kukwepa kulipa kodi ni kurudisha nyuma maendeleo ya nchi ambapo mapato hayo yanaleta maendeleo.

Eliona alisema kuwa kulipaji kodi ni uzalendo hivyo wanapaswa kulipa kodi kwani fedha zinazokusanywa kazi yake kubwa ni kuleta maendeleo kupitia miradi mbalimbali hasa ile mikubwa kama vile miradi ya elimu afya miundombinu ya barabara na reli.

Alisema kuwa fedha hizo matumizi yake ni kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya wananchi hivyo kutolipa kodi na kurudisha nyuma jitihada za serikali za kuleta maendeleo kwa wananchi.

Aidha alisema kuwa katika kuelekea miaka 30 ya TRA wamefanya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuimarisha afya kwa kufanya mazoezi kufanya usafi kwenye eneo la wafanyabiashara Chalinze.

"Ulipaji wa kodi unasaidia serikali katika utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi zikiwemo za kiafya na huduma zote ambazo wananchi wanapaswa kuzipata kwenye maeneo yao,"alisema Eliona.

Naye Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara (JWT) Mkoa wa Pwani Abdala Ndauka alisema kuwa ulipaji kodi umekuwa rahisi kwa sasa kutokana na mahusiano mazuri yaliyopo baiba ya wafanyabiashara na mamlaka.

Ndauka alisema mtaji mkubwa wa mfanyabiashara ni afya njema hivyo mazoezi hayo yanasaidia kuimarisha afya na kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

MAWAZO VIJANA CHALLENGE KUTUMIKA KIMAENDELEO



SERIKALI imesema kuwa itatumia mawazo ya vijana walioshiriki shindano la Vijana Uchumi Challenge kuwa mpango ambao utaleta suluhisho la namna ya kutatua baadhi ya changamoto ndani ya jamii.

Hayo yalisemwa Kibaha na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Jenifa Omollo wakati wa kufunfa mafunzo ya siku nne kwa vijana 100 walioandika mawazo juu ya masuala ya uchumi kupitia jukwaa la Vijana Uchumi Challenge.

Omollo alisema kuwa mawazo yaliyoandikwa na vijana yameonyesha kuwa yakiboreshwa yanaweza kuwa mpango mzuri ambao unaweza kukabili changamoto mbalimbali ndani ya jamii na Taifa kwa ujumla.

"Mawazo yote yaliyowasilishwa hayataachwa badala yake yataboreshwa na kupatiwa fursa ili yawe mpango ambao utakuwa suluhu kwa baadhi ya changamoto ili kuleta tija na kusaidia Taifa mojawapo likatoa ajira kwa vijana,"alisema Omollo.

Alisema kuwa mawqzo hayo ni bunifu ambazo zimeonyesha jinsi gani vijana walivyokuwa na vipaji ambavyo vitatoa ajira na kuwa na manufaa kwa watu wengi hivyo kulisaidia Taifa.

Naye mwenyekiti wa kamati ya Vijana Uchumi Challenge Joseph Malecela alisema kuwa jumla ya mawazo zaidi ya 7,000 ya vijana kote nchini wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35 yaliwasilishwa na kuchujwa na kubaki 100 ambayo yatashindanishwa kupata mshindi.

Malecela alisema kuwa washiriki hao 100 ambao waliiingia kambini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere wamechujwa na majaji wabobezi wa masuala ya uchumi na fedha na kubaki 10 watashindana ili kumpata mshindi wa shindano hilo.

Rais Dk Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha kumpata kijana mwenye wazo zuri Julai 6 mwaka huu Jjiini Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere Internation Convention Centre (JNICC) Jijuni Dar es Salaam.







mwisho