Mwanadiplomasia na Mchambuzi wa Masuala ya Kidiplomasia Siasa , Itifaki na Maadili Omary Punzi ateuliwa kushiriki katika mkutano wa Creative Convergence 2026 .
Mkutano huu unaojumuisha Africa Creative Market (ACM), Creative Industry Business Summit (CIBS), na Kwimbo National Arts Festival, unafanyika kuanzia Juni 29 hadi Julai 4, 2026 jijini Lusaka, Zambia.
Mkutano huo unaisimamiwa na Wizara ya Vijana, Michezo na Sanaa nchini Zambia
Utafanyika katika kumbi za mikutano zilizopo Mulungushi International Conference Centre kuanzia Juni 29 hadi Julai 2, 2026 na kuanzia tarehe 3 hadi 4 Julai
Tamasha la Sanaa, tamasha la Kwimbo huko Polo B, Lusaka Showgrounds.
Mkutano huo utakutanisha Vijana zaidi 10000 kutoka Bara la Afrika.
kushiriki Programu na Warsha (Sessions & Masterclasses)
Mijadala ya Biashara, Mijadala inayohusu biashara ya sanaa, filamu, muziki, teknolojia (kama AI), na mitindo.
Mafunzo ya Kitaalamu, Ufikiaji wa masterclasses zinazoendeshwa na washirika wa sekta, mfano mafunzo ya upigaji picha au uigizaji.
Kuunganisha Mtandao wa Biashara (Networking & Deal Rooms)
Ushirikiano wa Kibiashara, mikutano ya kibiashara (kama vile Deal Rooms au Creative Pitch Zone) ambapo wabunifu wanakutana na wawekezaji, wafadhili, na watengeneza sera ili kugeuza mawazo kuwa mikataba ya kazi.

No comments:
Post a Comment