Monday, June 29, 2026
POLISI MKOANI PWANI LINACHUNGUZA VIFO VYA MWANAMKE NA MTOTO
AKINAMAMA WATAKIWA KUWAKUMBUKA VIJANA WAKIUME
Sunday, June 28, 2026
VIJANA WENYE VIPAJI VYA MICHEZO WATAKIWA KUWA NA NIDHAMU
MWANADIPLOMASIA OMARY PUNZI ATEULIWA KUSHIRIKI MKUTANO WA CREATIVE
Mwanadiplomasia na Mchambuzi wa Masuala ya Kidiplomasia Siasa , Itifaki na Maadili Omary Punzi ateuliwa kushiriki katika mkutano wa Creative Convergence 2026 .
Mkutano huu unaojumuisha Africa Creative Market (ACM), Creative Industry Business Summit (CIBS), na Kwimbo National Arts Festival, unafanyika kuanzia Juni 29 hadi Julai 4, 2026 jijini Lusaka, Zambia.
Mkutano huo unaisimamiwa na Wizara ya Vijana, Michezo na Sanaa nchini Zambia
Utafanyika katika kumbi za mikutano zilizopo Mulungushi International Conference Centre kuanzia Juni 29 hadi Julai 2, 2026 na kuanzia tarehe 3 hadi 4 Julai
Tamasha la Sanaa, tamasha la Kwimbo huko Polo B, Lusaka Showgrounds.
Mkutano huo utakutanisha Vijana zaidi 10000 kutoka Bara la Afrika.
kushiriki Programu na Warsha (Sessions & Masterclasses)
Mijadala ya Biashara, Mijadala inayohusu biashara ya sanaa, filamu, muziki, teknolojia (kama AI), na mitindo.
Mafunzo ya Kitaalamu, Ufikiaji wa masterclasses zinazoendeshwa na washirika wa sekta, mfano mafunzo ya upigaji picha au uigizaji.
Kuunganisha Mtandao wa Biashara (Networking & Deal Rooms)
Ushirikiano wa Kibiashara, mikutano ya kibiashara (kama vile Deal Rooms au Creative Pitch Zone) ambapo wabunifu wanakutana na wawekezaji, wafadhili, na watengeneza sera ili kugeuza mawazo kuwa mikataba ya kazi.
MAWAZO YA VIJANA
Malecela alisema kuwa washiriki hao 100 ambao waliiingia kambini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere wamechujwa na majaji wabobezi wa masuala ya uchumi na fedha na kubaki 10 watashindana ili kumpata mshindi wa shindano hilo.
Rais Dk Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha kumpata kijana mwenye wazo zuri Julai 6 mwaka huu Jjiini Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere Internation Convention Centre (JNICC) Jijuni Dar es Salaam.
mwisho
WALIPA KODI WATAKIWA KUONYESHA UZALENDO KWA KULIPA KWA WAKATI
MAWAZO VIJANA CHALLENGE KUTUMIKA KIMAENDELEO
Hayo yalisemwa Kibaha na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana Jenifa Omollo wakati wa kufunfa mafunzo ya siku nne kwa vijana 100 walioandika mawazo juu ya masuala ya uchumi kupitia jukwaa la Vijana Uchumi Challenge.
Omollo alisema kuwa mawazo yaliyoandikwa na vijana yameonyesha kuwa yakiboreshwa yanaweza kuwa mpango mzuri ambao unaweza kukabili changamoto mbalimbali ndani ya jamii na Taifa kwa ujumla.
"Mawazo yote yaliyowasilishwa hayataachwa badala yake yataboreshwa na kupatiwa fursa ili yawe mpango ambao utakuwa suluhu kwa baadhi ya changamoto ili kuleta tija na kusaidia Taifa mojawapo likatoa ajira kwa vijana,"alisema Omollo.
Alisema kuwa mawqzo hayo ni bunifu ambazo zimeonyesha jinsi gani vijana walivyokuwa na vipaji ambavyo vitatoa ajira na kuwa na manufaa kwa watu wengi hivyo kulisaidia Taifa.
Naye mwenyekiti wa kamati ya Vijana Uchumi Challenge Joseph Malecela alisema kuwa jumla ya mawazo zaidi ya 7,000 ya vijana kote nchini wenye umri kati ya miaka 15 hadi 35 yaliwasilishwa na kuchujwa na kubaki 100 ambayo yatashindanishwa kupata mshindi.
Malecela alisema kuwa washiriki hao 100 ambao waliiingia kambini kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere wamechujwa na majaji wabobezi wa masuala ya uchumi na fedha na kubaki 10 watashindana ili kumpata mshindi wa shindano hilo.
Rais Dk Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha kumpata kijana mwenye wazo zuri Julai 6 mwaka huu Jjiini Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Julius Nyerere Internation Convention Centre (JNICC) Jijuni Dar es Salaam.
mwisho
Thursday, June 25, 2026
MAWAKALA WAITWA KUCHANGAMKIA VIPAJI TUMBI KIBAHA
Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Lucas Kiluwasha ambaye ni mwenyekiti wa Mashindano ya Compassion Kanda ya Mashariki kwenye Viwanja vya Shirika la Elimu Kibaha Tumbi.
Mashindano hayo ambayo ni ya nne kufanyika yameweza kuwatoa wachezaji wengi akiwemo Dickson Job wa Yanga, Paschal Msindo wa timu ya Azam na Haji Abdala kipa wa timu ya Serengeti Boys chini ya miaka 17 iliyoshika nafasi ya pili kwenye michuano ya Afcon ya vijana iliyofanyika Morocco hivi karibuni.
Mbali ya kuzalisha wachezaji hao ambao wanatambulika pia imezalisha wachezaji wengine ambao wako timu za Yanga B, Azam na Fountain Gate pamoja na msanii wa muziki wa kisasa Dogo Janja na wasanii mbalimbali hapa nchini.
Kiluwasha amesema kuwa mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka yanashirikisha jumla ya mikoa mitatu ya Pwani, Dar es Salaam na Morogoro ambapo kuna wachezaji zaidi ya 430 kauli mbiu ya mwaka huu inasema “Kipaji Changu Mtaji Wangu”.
“Michezo inayoshindaniwa ni pamoja na soka, mpira wa pete, riadha na michezo ya ndani ikiwa ni pamoja na kupiga vyombo vya muziki, ubunifu wa mavi na sanaa mbalimbali lengo ni kuinua na kuibua vipaji kwa vijana,”alisema Kiluwasha.
Alisema kuwa kwa sasa mara wanapopatikana vijana wa michezo husika huwapeleka ili wakaendeleze vipaji vyao ambapo wa soka huwapeleka kwenye timu zenye Academy ili waweze kukuza vipaji vyao na kujipatia ajira kupitia michezo.
“Changamoto kubwa ni ushiriki mdogo wa wadau kujitokeza kuhudhuria mashindano yao pia baadhi ya wachezaji kwenda kushiriki michezo ya Umisseta na Umitashumta kwani nao hufanya kipindi cha likizo hivyo kuwa na mwingiliano,”alisema Kiluwasha.
Aidha alisem akuwa malengo yao ya baadaye ni kuanzisha timu ya mipra wa miguu ili ishiriki ligi mbalimbali na hatimaye kufika ligi kuu pia wanazikaribisha timu mbalimbali kama zinahitaji wachezaji kuona nao ili kukubalina na kuwachukua ili wakaendeleze vipaji vyao.
Wachezaji hao wanatoka kwenye vituo vya huduma ya mtoto na kijana kwenye makanisa ya Kiinjili na Kipentekoste kwenye mikoa hiyo na wachezaji watakaofanya vizuri watachaguliwa kwenda kushiriki mashindano hayo kitaifa.
Tuesday, June 23, 2026
WAZO BORA LA KIJANA KUNYAKUA MILIONI 50
VIJANA 100 KUWANIA MILIONI 50 VIJANA UCHUMI CHALLANGE
PWANI YAKUSANYA BILIONI 266
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi bilioni 266 katika kipindi cha miaka 10 iliyopita na kuvuka malengo yaliyowekwa ya kukusanya shilingi bilioni 235 katika kipindi hicho.
Akizungumza kwenye Kongamano la Mamlaka hiyo ya kutimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwake Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani Peter Jackson alisema kuwa mafanikio hayo ni ongezeko la asilimia 113 ya makusanyo kwa kipindi hicho.
Jackson alisema kuwa mafanikio hayo yametokana na ushirikiano ulioonyeshwa na wafanyabiashara na wadau wote wa kodi ambapo katika kipindi hicho malaengo ya makusanyo yalikuwa ni bilioni 23 lakini zilikusanywa kiasi cha shilingi bilioni 27.
“Kwa wastani makusanyo kwa kipindi cha miaka 10 ni ongezeko la asilimia 10 ambapo yamekuwa yakiongezeka hadi kufikia kiasi hicho na kuonyesha jinsi gani mamlaka hiyo inavyopiga hatua katika kuleta maendeleo ya nchi,”alisema Jackson.
Alisema kuwa makusanyo yana faida kubwa kwani yanatumika kwa ajili ya kufanya shughuli za kimaendeleo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa miundombinu ikiwemo ya barabara ujenzi wa reli ya kisasa SGR huduma za afya, huduma za elimu na masuala mbalimbali.
Aidha alisema kuwa ukusanyaji wa mapato makubwa ndiyo njia ya kukuza uchumi wa nchi ambapo walipa kodi wanapaswa kulipa kwa hiyari na kwa wakati ili kuondoa changamoto za kupewa adhabu ambayo inawarudisha nyuma.
“Kwa sasa tumeweka mifumo madhubuti ya ukusanyaji na namna ya kuwafikia kwa urahisi walipa kodi na kuwaondolea usumbufu wa kufika ofisini badala yake wanauwezo wa kulipa au kufanya shughuli zote wakiwa maeneo yao jambo ambalo limerahisisha utendaji kazi,”alisema Jackson.
Akizungumzia kuhusu changamoto alisema kuwa ukuaji wa uchumi usio rasmi umekuwa ni tatizo kwani unakuwa nje ya mfumo rasmi hivyo kusababisha kukosekana kwa mapato kutokana na kukwepa au kupunguza kodi kuongezeka kwa biashara mtandaoni biashara haramu na za magendo ambazo huathiri ushindani wa kibiashara..
Kwa upande wake mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Pwani Abdala Ndauka alisema kuwa baadhi ya wafanyabiashara hawana uelewa juu ya masuala ya ulipaji kodi hivyo kuna haja ya kutolewa elimu ya kutosha.
Ndauka alisema kuwa ulipaji kodi unapaswa kuwa rafiki na si kama adhabu bali uwe rafiki hata hivyo malalamiko kwa sasa yamepungua kwani kwa sasa kumekuwa na majadiliano juu ya changamoto zinazowakumba walipa kodi na watengeneze walipa kodi wapya.
Mwenyekiti wa Chemba ya wafanyabiashara Mkoa wa Pwani Said Mfinanga alisema kuwa matumizi ya teknolojia yamesaidia kuwapunguzia muda walipa kodi kwenda ofisini ili kufanya kufanya taratibu mbalimbali juu ya masuala ya ya biashara zao.
Mfinanga alisema kuwa mfumo wa teknolojia pia utumike kutoa elimu juu ya masuala ya ulipaji kodi na taratibu zote zihusikanazo na masula ya kodi ili kujenga uelewa wa pamoja kwa walipa kodi na mamlaka hiyo ambayo inajuhusisha na ukusanyaji wa mapato ya serikali.
Naye mwenyekiti wa Shirikisho la Umoja wa Machinga (SHIUMA) Mkoa wa Pwani Philemon Maliga alisema kuwa ili kuboresha ukusanyaji wa mapato Mamlaka inapaswa kuwa na mahusiano bora na mazuri na walipakodi kwnai kundi lao ni kubwa na lina uwezo wa kuchangia pato la serikali.
Maliga alisema kuwa TRA iatoe limu kuanzia mashuleni na sehemu mbalimbali ili kuwajengea walipa kodi utamaduni wa kulipa mapato ili kuonyesha uzalendo wa nchi yao kwani kodi ndiyo msingi mkubwa wa maendeleo.
Monday, June 15, 2026
TAARIFA KWA UMMA
Ofisi ya Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, inapinga na kukanusha vikali taarifa ya uongo na upotoshaji inayosambaa mitandaoni, ikidai kuwa Dkt. Kikwete anahusishwa na mradi unaodaiwa kuwa wa uwekezaji unaowaahidi Watanzania kipato cha uhakika kupitia jukwaa la kifedha linalotumia teknolojia ya akili mnemba
Taarifa hiyo inadai kuwa maelfu ya Watanzania tayari wamenufaika na mradi huo baada ya kuwekeza kiasi cha shilingi 653,000, huku wakiahidiwa kupata zaidi ya shilingi 9,200,000 kwa mwezi. Madai hayo si ya kweli hata kidogo.
Ofisi ya Rais Mstaafu inapenda kuweka wazi kwamba Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete hajawahi kushiriki, kuidhinisha, kutangaza, kuunga mkono, wala kuhusika kwa namna yoyote ile na mpango huo wa kifedha.
Ofisi yake haijawahi kuruhusu matumizi ya jina, picha, au heshima yake kuhusishwa na mradi huo unaodaiwa, na haitajihusisha na shughuli za aina hiyo.
Wananchi wanashauriwa kupuuza taarifa hiyo ya uongo na kuwa makini dhidi ya miradi ya kitapeli na vitendo haramu vya aina hiyo.
Mtu yeyote atakayekutana na taarifa kama hizo za upotoshaji anapaswa kuzichukulia kama habari za uongo, kuepuka kuzisambaza, kujisajili, au kutuma fedha kwa mtu au jukwaa lolote linalohusishwa nazo.
Sunday, June 14, 2026
PWANI YAENDELEA KUHAMASISHA UCHANGIAJI DAMU KUOKOA MAISHA YA WATU
MKOA wa Pwani umekusanya jumla ya chupa za damu 1,129 kwa ajili ya Hospitali na Vituo vya Afya.
Hayo yamesemwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Kusirye Ukio wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mchangiaji Damu wa Dunia kimkoa ambapo maadhimisho hayo yamefanyika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani Tumbi.
Kwa upande wake Msimamizi wa Huduma kwa Mteja na Wachangiaji Damu Salama Makao Makuu Kaito Tamba amesema kuwa kwa sasa mpango ni kukusanya chupa 600,000 kwa mwaka
Akisoma risala ya siku hiyo Mkuu wa Idara ya Maabara Hospitali ya Tumbi Simon Lupatu amesema kuwa kauli mbiu ya mwaka huu inasema "Changia Damu Okoa Maisha" ambapo wanahitaji mashine kwa ajili ya uzalishaji mazao ya damu.
Naye Mkuu wa Idara ya Kinamama na Uzazi wa Hospitali ya Tumbi Dk Alfonce Moyo amesema kuwa takwimu zinaonyesha vifo vilivyotokea kwa mwezi Januari hadi Juni mwaka huu asilimia 80 vilitokana na kupoteza damu nyingi.
Saturday, June 13, 2026
*SERIKALI YADHAMIRIA KUWAENDELEZA WACHIMBAJI WADOGO NCHINI*
▪️Taarifa ya mapendekezo ya kuwaendeleza Wachimbaji wadogo yawasilishwa
▪️Prof Mkumbo aeleza umuhimu wa sekta ya madini kufikia Dira 2050
Lengo ni Kuongeza Ajira, Kupunguza Umaskini na Kukuza Uchumi
▪️Mfuko wa Dhamana kutatua changamoto ya mitaji kwa wachimbaji
▪️Serikali yaanzisha mfuko wa Madini kwa ajili ya Utafiti wa Madini
📍 Dar Es Salaam
Serikali imesisitiza kufanyia kazi kwa haraka Mapendekezo yaliyotolewa na Timu ya Wataalamu iliyoundwa Kuishauri Wizara ya Madini kuhusu namna ya Kuwaendeleza Wachimbaji Wadogo Kiuchumi na kueleza kuwa, utatuzi wa changamoto za Mitaji, Teknolojia na upatikanaji wa taarifa sahihi za Kijiolojia kwa Wachimbaji Wadogo wa Madini ni hatua muhimu ya kuongeza ajira kwa watanzania, kupunguza umaskini na kukuza uchumi wa Taifa kuelekea Dira 2050.
Hayo yamebainishwa Juni 13, 2026 jijini Dar Es Salaam na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, wakati wa hafla ya Kupokea Mapendekezo ya Kuwaendeleza Wachimbaji Wadogo Nchini na kusisitiza kwamba, maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha mipango ya maendeleo inajibu changamoto tatu kuu za taifa ambazo ni kuongeza mitaji kwa wananchi, kuzalisha ajira na kupunguza umaskini.
Amesema kuwawezesha wachimbaji wadogo kupata mitaji na teknolojia, kunafungua fursa za kuongeza uzalishaji, ajira na kipato cha wananchi na kuongeza kuwa hiyo ndiyo njia mojawapo ya kupambana na umaskini.
‘’Kazi kubwa ya Waziri ni kutoa mwelekeo wa kisera wa taasisi au wizara anayoiongoza. Kwa muda niliokaa kwenye Wizara yangu, Mhe. Mavunde amekua akijua kipaumbele anachokitaka na jinsi ya kukipata,’’amesisitiza Prof. Mkumbo.
Ameongeza kwamba, hali ya umaskini nchini bado ipo kwa kiwango cha juu na kutolea mfano wa Mkoa wa Geita ambao unaoongoza kwa shughuli za uchimbaji madini ya dhahabu nchini ambapo hali ya umaskini inafikia asilimia 38 na kusisitiza kwamba, wachimbaji wadogo wanapowezeshwa wanasaida kutatua changamoto kama hizo na kuongeza kuwa, Sekta ya Madini imewekwa kama moja ya sekta muhimu za kimageuzi inayotarajiwa kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na ajira ambapo awali haikuwa ikibeba watu wengi.
Naye, Waziri wa Madini Anthony Mavunde akizungumza katika halfa hiyo, amesema Serikali iliamua kuunda kamati hiyo kutokana na mchango mkubwa unaotolewa na wachimbaji wadogo katika Sekta ya Madini, licha ya kukabiliwa na changamoto za mitaji, teknolojia na upatikanaji wa huduma za kifedha , hivi sasa wanachangia asilimia 40 ya makusnyo ya maduhuli ya Serikali.
Ameongeza kwamba, kuwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika Sekta ya Madini ndani ya miaka ya hivi karibuni yanaonyesha umuhimu wa kuwawezesha zaidi wachimbaji wadogo ili waongeze mchango wao katika uchumi wa taifa.
Kwa mujibu wa Waziri Mavunde, Mwaka wa Fedha 2015/16 Sekta ya Madini katika mwaka mmoja iliingiza shilingi bilioni 161 pekee katika Mfuko Mkuu wa Serikali.
Hata hivyo, kufuatia mageuzi mbalimbali yaliyofanyika ikiwemo mabadiliko ya sheria, kuanzishwa kwa masoko ya madini na udhibiti wa biashara haramu ya madini, makusanyo yameongezeka kwa kiwango kikubwa kufikia Shilingi trilioni 1.107 mwaka 204/25 na mpaka kufikia tarehe 13, Juni, tayari Serikali imekusanya shilingi trilioni 1.3.
Amesisitiza kuwa jukumu la Serikali yoyote duniani ni kuwawezesha wananchi wake kufanya shughuli za uzalishaji kwa tija zaidi sababu ambayo ilipelekea Serikali kuweka mkakati maalum wa kuwawezesha wachimbaji wadogo ili waweze kukua na kuwa wachimbaji wa kati na baadaye wakubwa.
Kuhusu changamoto ya mitaji, Waziri Mavunde amesema Serikali imeanza utekelezaji wa Kampuni ya dhamana ya mikopo (Credit Guarantee Corporation) itakayosaidia wachimbaji kupata mikopo kutoka taasisi za fedha mbalimbali.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Victor Tesha amesema suluhu ya changamoto hizo ni kujenga mfumo jumuishi wa kuwawezesha wachimbaji wadogo kupitia upatikanaji wa mitaji, teknolojia za kisasa, taarifa za kijiolojia na uratibu wa taasisi zinazohusika na sekta hiyo huku akipendekeza kuanzishwa kwa Mfuko wa Madini Tanzania utakaowezesha miradi yenye sifa kupata fedha za kuendeleza uzalishaji, kununua mitambo na kuboresha shughuli za uchimbaji, na kuongeza kwamba, mfuko huo utasaidia kugharamia tafiti na taarifa za kijiolojia kwa wachimbaji.
Ameongeza kuwa, baada ya mfuko huo kukua na kuimarika, hatua itakayofuata itakuwa ni kuanzisha Benki ya Wachimbaji itakayotoa huduma maalumu za kifedha kwa sekta ya madini kwa masharti yanayoendana na mazingira ya wachimbaji.
‘’Kamati pia imependekeza mikopo ielekezwe zaidi katika ununuzi wa mitambo na teknolojia badala ya fedha taslimu pekee, ili kuongeza tija, uzalishaji na usalama katika shughuli za uchimbaji,’’ amesema Tesha.
Naye, rais wa Shirikisho la Vyama Vya Wachimbaji Wadogo John Bina, ameipongeza Serikali kwa ripoti hiyo na kueleza imetokana na Serikali kusikiliza na kuyafanyia kazi maoni na changamoto za wachimbaji wadogo, pamoja na kuipongeza kwa kutenga asilimia 10 ya mapato yanayotokana na shughuli za madini kwa ajili ya utafiti.
Wednesday, June 10, 2026
HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIBAHA YATOA MIKOPO YA SHILINGI MILIONI 991.5 KWA VIKUNDI
HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha Mkoani Pwani imetoa mikopo ya jumla ya shilingi milioni 991.5 kwa vikundi 51 vya ujasiriamali.
Tuesday, June 9, 2026
LULU YA WAJANE KUANZISHA MRADI WA MINOFU YA KUKU
POLISI PWANI KUFANYA UCHUNGUZI KISAYANSI KUCHUNGUZA MADAI MZAZI KUBADILISHIWA MTOTO
Sunday, June 7, 2026
MAFANIKIO YA GLOBAL PARTNERSHIP FOR EDUCATION CHINI YA UENYEKITI WA DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE
Na Albert Kawogo
TANGU Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ateuliwe kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Global Partnership for Education mwezi Septemba 2021, taasisi hiyo imeendelea kuimarisha juhudi za kuboresha elimu katika nchi zinazoendelea duniani.
Dkt. Kikwete akiwa kiongozi wa kwanza kutoka Afrika kushika nafasi hiyo muhimu katika historia ya shirika hilo,chini ya uongozi wake, GPE imeongeza juhudi za kuhakikisha watoto wengi zaidi wanapata elimu bora, hususan wale wanaotoka katika mazingira magumu, maeneo yenye migogoro, wakimbizi na watoto wenye ulemavu.
Taasisi hiyo imeendelea kushirikiana na serikali mbalimbali duniani kuboresha mifumo ya elimu na kuongeza uwekezaji katika sekta hiyo ambapo ufanisi mkubwa umeonekana.
Moja ya mafanikio makubwa yaliyoshuhudiwa ni kuongezeka kwa ufadhili wa miradi ya elimu katika nchi wanachama. Katika kipindi cha mkakati wa GPE 2025, mamia ya mamilioni ya watoto wamefikiwa kupitia programu za kuboresha upatikanaji wa elimu, mafunzo kwa walimu, usambazaji wa vitabu na ujenzi wa miundombinu ya shule.
Kufikia mwaka 2024, GPE iliripoti kuwafikia watoto milioni 253, kutoa mafunzo kwa walimu milioni 1.9, kusambaza vitabu milioni 169 na kujenga au kukarabati zaidi ya madarasa 36,000.
Aidha, chini ya uenyekiti wa Dkt. Kikwete, GPE imepanua ushirikiano wake kwa kuongeza nchi wanachama na wadau wapya wa maendeleo.
Mwaka 2024, nchi za Jordan na Lebanon zilijiunga rasmi na ushirikiano huo, huku Saudi Arabia ikitangaza mchango mkubwa wa kifedha kwa ajili ya kuboresha elimu katika nchi zenye kipato cha chini.
Katika eneo la usawa wa kijinsia, GPE imeongeza juhudi za kuhakikisha wasichana wanapata fursa sawa za elimu ambapo pia shirika hilo limeimarisha programu za kuwajumuisha watoto wenye ulemavu, wakimbizi na makundi mengine yaliyokuwa yakibaki nyuma katika upatikanaji wa elimu.
Dkt. Kikwete ambaye ni Rais mstaafu wa Tanzania ameongoza juhudi za kuhamasisha ufadhili zaidi wa elimu duniani, akisisitiza kuwa elimu ni msingi wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii
Kupitia mikutano yake mbalimbali ya kimataifa, Dkt Kikwete amekuwa mstari wa mbele kwenye kutetea uwekezaji mkubwa katika elimu ili kukabiliana na changamoto zilizotokana na athari za COVID-19, migogoro ya kimataifa na mabadiliko ya tabianchi.
Kwa ujumla, kipindi cha uenyekiti wa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete GPE
imeonyesha mafanikio makubwa hasa katika kupanua fursa za elimu, kuimarisha ubora wa kujifunza, kuongeza ushirikiano wa kimataifa na kuhakikisha watoto walio katika mazingira magumu wanapata haki yao ya msingi ya elimu bora.
Wednesday, June 3, 2026
RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN AWEKA SHADA LA MAUA KABURI ASKARI ASIYEFAHAMIKA
Na Mwandishi Wetu, TBN, Moscow
KENGELE kubwa iliyogongwa mara tisa, bendi ya jeshi ikiongoza nyimbo za maombolezo Rais Dk Samia Suluhu Hasan majira ya saa tano na dakika 23 aliweka shada la maua kwa kaburi la askari asiyefahamika, mjini hapa.
Aidha Baada ya shughuli la uwekaji wa taji hilo katika eneo ambalo moto huwaka daima ikiwa ni kumbukumbu ya wapiganaji wa Urusi waliopoteza maisha katika vita kuu ya pili, gadi tatu zilipita kwa mwendo wa haraka na kutoa heshima kwa Rais Samia baada ya kupigwa kwa wimbo wa taifa la Tanzania.
Hali ya askari katika uwanja huo walioonesha nidhamu ya hali ya juu ya kusimama tisti katika maeneo yao bila kutikisika , ubadilishanaji wa gadi za ulinzi na pia mwendo wa pole ambao ulimsindikiza Rais Samia kwenda kwenye tukio la uwekeaji wa shahada. Vilikuwa vitu vinavyovutia kuangalia.
Rais Samia ambaye yupo katika ziara ya kiserikali nchini hapa baadaye alienda kukutana na mwenyeji wake Rais Vladmir Putin
Zaidi ya maofisa 300 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ wamepata nafasi ya masomo katika nchi ya Urusi kwa ajili ya shahada ya kwanza na ya pili.
Askari hao wameenda kujifunza masuala ya kupambana na ugaidi, sayansi na teknolojia,mafunzo ya kijeshi, ulinzi wa amani, ununuzi na uhifadhi wa silaha,namna ya kukabiliana na majanga.
Tanzania na Urusi zina ushirikiano wa kijeshi kwa kuzingatia makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi yaliyosainiwa mwaka 2016 na makubaliano ya mwaka 2018 ya ushirikiano wa kifundi wa kijeshi.
Tanzania yenye ukuaji wa uchumi wa asilimia 5.5 kwa mwaka 2024 na ikikadiriwa kufikia asilimia 6 mwaka huu na ikiwa na mkakati wa kuhakikisha kwamba Dira ya maendeleo ya mwaka2050 inatekelezwa ziara ya Rais Samia nchini Urusi inatarajiwa kuzaa matunda yanayotarajiwa ya kuinua sekta ya ajira kukuza biashara na kuimarisha uwekezaji.
DK SAMIA SULUHU HASSAN KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMIVU YA CHUO KIKUU CHA RUDIN URUSI
Na Mwandishi Wetu ,TBN, Moscow
Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye yupo hapa shirikisho la Urusi kwa ziara ya kitaifa anatarajiwa kutunukiwa shahada ya uzamivu na Chuo Kikuu cha Rudin nchini hapa.
Tuzo hiyo inatokana na kutambua kazi yake na mchango wake katika jami ya Tanzania na dunia katika masuala ya msingi yanayohusu Maisha ya binadamu.
Chuo cha RUDIN chenye wanafunzi wa kitanzania 570 kufikia mwaka 2025 katika miaka zaidi ya 65 ya RUDIN, watanzania 1,132 wamepitia chuo hicho.
RUDIN kimesomesha zaidi ya wataalamu 200,000 duniani na sasa ina watu 44,000 kutoka nchi 160 duniani.
Chuo hiki ni cha 367 kwa ubora duniani kwa mujibu wa QS World University Ranking ya mwaka 2025.
Rais Dkt Samia ambaye amepokelewa jana na Waziri wa maendeleo ya Uchumi wa Russia Maxim Reshetnikov anatarajiwa kukutana na mwenyeji wake Rais Vladimir Putin na kufanya mazungumzo ya ana kwa ana kwa ajili ya kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi.
Aidha akiwa nchini hapa, akiwa kiongozi wa pili wa Tanzania kutembelea Urusi, ziara ya kwanza ikiwa imefanywa na baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere, atashiriki Jukwaa la uchumi la St Petersburg ambapo tanzania itanadi fursa za uwekezaji, na diplomasia ya Uchumi kwa viongozi, wawekezaji na watunga sera wa kimataifa.
Katika kufanikisha dira ya Maendeleo 2050 ziara hii ni kikolezo cha utekelezaji kwa mafanikio ya dira hiyo ambayo inahitaji raslimali watu wenye utaalamu na upeo mkubwa kusimamia na kuendesha miradi ya kimkakati itakayopelekea ajira, viwanda na biashara zitakazoingiza dola trilioni moja na kuwa katika uchumi wa kati wa juu.
Katika WhatsApp yake Rais Samia amesema Ziara hiyo ni muhimu hasa taifa linapoelekea kuanza utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050 ambayo inataka ushiriki mkubwa wa sekta binafsi.
"Tutafanya mazungumzo na wenyeji wetu yanayolenga kuimarisha ushirikiano katika sekta za kimkakati zinazogusa maisha ya wananchi."
"Aidha, tutashiriki majukwaa ya biashara na uwekezaji na kutatangaza fursa zilizopo nchini, pamoja na kufungua zaidi fursa za masoko kwa bidhaa za Tanzania nchini Urusi."




















