Katika mchezo huo ambao ulipigwa kwenye uwanja wa Mwendapole hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimefungana magoli hayo.
Wapolo ndiyo waliokuwa wakwanza kuandika bao dakika ya 2 kupitia kwa Adolf Mpangule huku Umwelani wakisawazisha kupitia kwa Baraka Jafary dakika ya 26.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi huku kukiwa na kosa kosa za hapa na pale lakini hadi dakika 90 hakuna mbabe aliyepatikana na kuingia hatua ya matuta.
Ambapo washindi walipata penati 3 huku Wapolo wakikosa penati zote na kupata 1 hivyo kutawazwa mabingwa na kujinyakulia kiasi cha shilingi milioni 2 taslimu.
Wapolo walijinyakulia seti mbili za jezi na mpira mmoja ambapo washindi walikabidhiwa zawadi na katibu tawala wa wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ambaye alimwakilisha mkuu wa wilaya ya Kibaha Nickson John.
Magogwa amesema kuwa serikali itashirikiana na wadau wa michezo ili kuendeleza michezo kwenye wilaya hiyo.
Naye mwenyekiti wa chama cha soka wilaya ya Kibaha (KIBAFA) Robert Munis alisema kuwa mashindano hayo yamehamasisha mpira kwenye wilaya hiyo.
Kwa upande wake mratibu wa mashindano hayo Othaman Shija amesema kuwa changamoto kubwa ni kukosa wadhamini wa mashindano hayo na kuomba wadau kujitokeza kudhamini michuano hiyo inayofanyika kila mwaka ikiwa ni mwaka wake wa pili.
No comments:
Post a Comment