Wednesday, August 9, 2023

MAOFISA UGANI WATAKIWA KWENDA VIJIJINI

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bahi na Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa Mhe. Donard Megitii amewataka maafisa ugani kwenda vijijini kutoa elimu juu ya ufugaji bora na wenye tija kwa ajili ya manufaa ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Megitii ametoa rai hiyo Jijini Dodoma katika ufunguzi wa kongamano la kuku Katika viwanja vya maonesho ya nanenane Nzuguni Jijini Dodoma.

Amesema vijijini bado kuna shida ya wataalam na maafisa hao hawatembelei Wafugaji hivyo kama Mkoa jambo hilo walipe uzito wasiishie kwenye kongamano kwamba watu wameonesha nia njema na ndio maana wanakuja wapate elimu, ujuzi na kuwaunganisha na maafisa ugani kwa maana ya Mifugo, Kilimo kwenda vijijini kuwatembelea Wafugaji na kuwapa elimu.

“Wafugaji wa kuku wanapaswa kuongeza uzalishaji wenye tija Dodoma ili kujivunia uwepo wa makao makuu na nawaomba wataalam nendeni mkawape elimu bora ya kufuga washiriki waliofika na kwamaana wana nia njema ya kutaka kutambua mbinu za ufugaji bora ili waweze kupata tija nakuongeza mitaji pamoja na uchumi wao,”amesema.

Aidha, amewataka wafugaji kuzingatia ulishaji na utunzaji wa chakula cha mifugo pamoja na kuzingatia kanuni za magonjwa.

“Tunashindwa kufuga kwa tija kwasababu hatuzingatii kanuni za kiafya kwa maana ya ufugaji bora kwahiyo tukizingatia kuchanja kuku yaani kuwapatia kinga ili wasipate maradhi ya kuambukiza halafu ukawapa maji ya kutosha nina uhakika tutabadilisha maisha na kuuza kuku kila siku.” amesema.

Akifanya majumuisho baada ya kuzunguka katika baadhi ya mabanda amesema amefurahi kuona kikundi cha vijana wanufaika wa Mikoa ya vijana ya 4% ilivyoweza kubadilisha maisha ya vijana watano na kuajiri vijana wengine watano.

“Hii inaonesha kuwa mafanikio kwa vijana ni makubwa na utayari wa vijana kujifunza ni mkubwa hivyo kinachobaki kwetu Viongozi ni kuhamasisha wananchi kukubali na kuanza kutumi bidhaa zetu,”amesema.

No comments:

Post a Comment