Friday, August 25, 2023

JWT LATOA SIKU 7 WENYE MAVAZI YA JESHI KUYASALIMISHA

Jeshi la Ulinzi la  Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetoa siku 7 za kusalimisha mavazi ya Jeshi kwa yeyote ambaye ana mavazi hayo iwe anavaa,kuuza au kwa wasanii kupanda nayo katika majukwaa ya utumbuizaji.

Hayo yametolewa na Luten Kanali Gaudentius Ilonda ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano makao makuu ya Jeshi (JWTZ) wakati akizungumza na wanahabari kuhusu katazo hilo na ukikwajji wa Sheria ya uvaaji wa mavazi hayo Jijini Dodoma

Aidha Luteni Kanali Ilonda amesema kuwa mavazi yanayokatazwa na Jeshi ni pamoja na kombati (vazi la mabaka), Makoti,Tisheti, Kofia,Viatu kwa mujibu wa sheria mbalimbali kama anavyoelezea.

Kwa upande wake msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa idara ya habari maelezo Bwana Gerson Msigwa amewaomba wazazi na walezi kuwakagua watoto wao ili kama Wana sale za Jeshi wazizuie na kusalimisha.

No comments:

Post a Comment