Monday, August 7, 2023

CWT KIBAHA WATAKA MABORESHO KIKOKOTOO

CHAMA Cha Walimu Tanzania (CWT) Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani kimeomba kanuni ya kikokotoo kuangaliwa upya au kirudishwe cha zamani ambacho kilikuwa ni asilimia 50 badala ya cha sasa ambacho ni asilimia 33.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa chama hicho Mwita Magige alipozungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake.

Magige amesema kuwa kanuni ya kugawa kikokotoo cha sasa iangaliwe upya ambapo mafao wanayoyapata baada ya kustaafu ni madogo tofauti na yale ya awali.

Amesema kuwa kanuni hiyo iangaliwe upya kwa kuboreshwa na ikiwezekana kirudishwe kikokotoo cha zamani ambacho ni kizuri kuliko cha sasa.

Aidha amesema kuwa kuboreshwa kikokotoo kutawafanya walimu wawe na morali ya kazi kwani watakuwa wanafuraha na malipo hayo mara baada ya kustaafu.


No comments:

Post a Comment