Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mwenyekiti wa chama hicho Mwita Magige alipozungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake.
Magige amesema kuwa kanuni ya kugawa kikokotoo cha sasa iangaliwe upya ambapo mafao wanayoyapata baada ya kustaafu ni madogo tofauti na yale ya awali.
Amesema kuwa kanuni hiyo iangaliwe upya kwa kuboreshwa na ikiwezekana kirudishwe kikokotoo cha zamani ambacho ni kizuri kuliko cha sasa.
Aidha amesema kuwa kuboreshwa kikokotoo kutawafanya walimu wawe na morali ya kazi kwani watakuwa wanafuraha na malipo hayo mara baada ya kustaafu.
No comments:
Post a Comment