Thursday, August 31, 2023

JAMII PWANI YATAKIWA KUWALINDA WATOTO ILI WAISHI KWENYE MAZINGIRA MAZURI

WADAU wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) Mkoani Pwani wameshauriwa jamii kuwalinda watoto ili kuepukana na vitendo vya ukatili.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa Anjita Child Development Foundation Janeth Malela wakati wa kikao cha maandalizi ya uzinduzi wa Programu hiyo kwa Mkoa wa Pwani.

Malela alisema kuwa programu hiyo itasaidia kuimarisha ukuaji na maendeleo ya mtoto kikamilifu kimwili, kiakili, kukuza lugha, mawasiliano kijamii na kihisia. 

"Programu inalenga kuimarisha utoaji huduma bora za Afya, Lishe, Malezi yenye Mwitikio, ujifunzaji wa Awali na Ulinzi na Usalama kwa watoto wa miaka 0 hadi 8 na kuimarisha ushirikiano wa wadau wa sekta mbalimbali katika huduma za MMMAM,"alisema Malela.

Aidha alisema kuwa lengo kuu ni kusaidia watoto kwenye masuala ya malezi,makuzi,ujifunzaji,ulinzi wa mtoto,afya ili wakue katika mazingira mazuri na kukua kutokana na sheria zilizopo.

Kwa upande wake ofisa maendeleo ya jamii mkoa wa Pwani Rachel Chuwa alisema kuwa moja ya changamoto wanazozipata watoto ni baadhi ya wazazi na walezi kutowahudumia watoto wao kwa wakati kutokana na kutafuta mahitaji ya nyumbani.

Chuwa alisema kuwa malezi na makuzi wazazi wanapaswa wawahudumie lakini kwa sasa wanalelewa na televisheni na mitandao na suala la lishe shuleni baadhi wanatoa chakuka lakini waengine hawatoi hivyo mpango huo utasaidia kuondoa changamoto zolizopo ili wapate huduma stahiki.

Naye mkurugenzi wa shirika la maendeleo kwa vijana (YPC) Israel Ilunde alisema kuwa mpango huo ni muhimu sana kwani vijana wanakumbana na changamoto za kimaadili kutokana na kutopata malezi bora kutokana na hali ya kimaisha.

Ilunde alisema kuwa mpango huo utasaidia sana katika kuwalea watoto na kuondoa vitendo viovu kutokana na malezi watakayoyapata hivyo rasilimali zitengwe ili kuwalea watoto katika misingi mizuri ya kimaadili.

Mikoa 10 ambayo imeshazindua programu hiyo ni Tabora, Arusha, Morogoro, Rukwa, Manyara, Mbeya, Dodoma, Dar es Salaam, Kagera na Lindi.

JAMII PWANI YATAKIWA KUWALINDA WATOTO ILI WAISHI KWENYE MAZINGIRA MAZURI





WADAU wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) Mkoani Pwani wameshauriwa jamii kuwalinda watoto ili kuepukana na vitendo vya ukatili.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa Anjita Child Development Foundation Janeth Malela wakati wa kikao cha maandalizi ya uzinduzi wa Programu hiyo kwa Mkoa wa Pwani.

Malela alisema kuwa programu hiyo itasaidia kuimarisha ukuaji na maendeleo ya mtoto kikamilifu kimwili, kiakili, kukuza lugha, mawasiliano kijamii na kihisia. 

"Programu inalenga kuimarisha utoaji huduma bora za Afya, Lishe, Malezi yenye Mwitikio, ujifunzaji wa Awali na Ulinzi na Usalama kwa watoto wa miaka 0 hadi 8 na kuimarisha ushirikiano wa wadau wa sekta mbalimbali katika huduma za MMMAM,"alisema Malela.

Aidha alisema kuwa lengo kuu ni kusaidia watoto kwenye masuala ya malezi,makuzi,ujifunzaji,ulinzi wa mtoto,afya ili wakue katika mazingira mazuri na kukua kutokana na sheria zilizopo.

Kwa upande wake ofisa maendeleo ya jamii mkoa wa Pwani Rachel Chuwa alisema kuwa moja ya changamoto wanazozipata watoto ni baadhi ya wazazi na walezi kutowahudumia watoto wao kwa wakati kutokana na kutafuta mahitaji ya nyumbani.

Chuwa alisema kuwa malezi na makuzi wazazi wanapaswa wawahudumie lakini kwa sasa wanalelewa na televisheni na mitandao na suala la lishe shuleni baadhi wanatoa chakuka lakini waengine hawatoi hivyo mpango huo utasaidia kuondoa changamoto zolizopo ili wapate huduma stahiki.

Naye mkurugenzi wa shirika la maendeleo kwa vijana (YPC) Israel Ilunde alisema kuwa mpango huo ni muhimu sana kwani vijana wanakumbana na changamoto za kimaadili kutokana na kutopata malezi bora kutokana na hali ya kimaisha.

Ilunde alisema kuwa mpango huo utasaidia sana katika kuwalea watoto na kuondoa vitendo viovu kutokana na malezi watakayoyapata hivyo rasilimali zitengwe ili kuwalea watoto katika misingi mizuri ya kimaadili.

Mikoa 10 ambayo imeshazindua programu hiyo ni Tabora, Arusha, Morogoro, Rukwa, Manyara, Mbeya, Dodoma, Dar es Salaam, Kagera na Lindi.

CORECU LTD YASAIDIA CHANGAMOTO SHULE YA MSINGI MWENDAPOLE

 




CHAMA Cha Ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) LTD kitagharamia gharama za huduma ya maji kwenye Shule ya Msingi Mwendapole ili kukabiliana na changamoto ya maji shuleni hapo.

Aidha chama hicho pia kitagharamia utengenezaji wa mashine ya kudurusu na kuchapishia na kompyuta mpakato ili kurahisisha kazi za uchapaji na kudurusu zifanyikie shuleni hapo badala ya kuzipeleka sehemu nyingine ambapo inaondoa usiri wa kazi za shule ikiwemo mitihani.

Hayo yamesemwa na Meneja wa CORECU LTD Mantawela Hamis wakati wa mahafali ya darasa la saba ya Shule ya Msingi Mwendapole yaliyofanyika leo shuleni hapo Wilayani Kibaha.

Pia amewataka wazazi kuwalea wanafunzi hao kwenye maadili mema mara wamalizapo elimu yao ya msingi ili wajiandae kuendelea na masomo ya elimu ya sekondari.

Awali mwalimu mkuu wa shule hiyo Rajabu Chalamila amesema kuwa mbali ya changamoto ya vifaa vya stationari na maji pia wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa uzio.

Chalamila amesema kutokana na shule hiyo kutokuwa na uzio wanafunzi wamekuwa wakitoroka na kufanyiwa vitendo vya kikatili.


DIWANI KUIPSTIA SHULE PHOTOCOPY MASHINE

DIWANI wa Kata ya Kibaha Goodluck Manyama amejitolea kuipatia Shule ya Msingi Jitegemee mashine ya kudurufu karatasi ili kuipunguzia mzigo shule hiyo gharama za uchapishaji mitihani.

Aidha katika kukabili changamoto ya maji kwenye shule hiyo Halmashauri itapeleka mradi wa kisima cha maji.

Akizungumza shuleni hapo wakati wa mahafali ya darasa la saba alisema kuwa atawanunulia mashine hiyo baada ya shule hiyo kutoa ombi hilo kwake.

Manyama alisema kuwa hiyo ni moja ya changamoto kubwa zinayoikabili shule hiyo hivyo ameona awapunguzie mzigo huo ili kupunguza gharama za kudurusu mitihani na kazi nyingine za shule.

"Nimeona nitoe msaada huu ili iwe chachu na kwa wadau wengine wajitokeze kusaidia changamoto za shule ili wanafunzi waweze kusoma katika mazingira mazuri,"alisema Manyama.

Alisema kuwa atashirikiana na wadau wengine pamoja na wanajamii kuhakikisha wanatatua changamoto za shule hiyo ili itoe elimu bora kwa wanafunzi.

"Tumepata wadau watatuchimbia kisima ili maji yawe ya uhakika na tayari mipango imekamilika na kisima kitachimbwa hivyo tuvute subira baada ya muda mfupi maji yatapatikana,"alisema Manyama.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo Stori Samatta alisema kuwa katika kuhakikisha wanakabili changamoto amekuwa akishirikisha wadau kuchangia elimu shuleni hapo.

Samatta alisema kuwa licha ya kuwa na changamoto kwani baadhi ya wanajamii kutokuwa na moyo wa kuchangia lakini anawapa elimu ya kuwa na moyo wa kuchangia ili iwe faida kwa watoto wao.

Naye mwanafunzi Eveline Samweli alisema kuwa wanakabiliwa na baadhi ya changamoto ikiwa ni pamoja na upungufu wa maji, matundu ya vyoo, kutokuwa na uzio na chumba cha kompyuta na kompyuta.

Samweli alisema kuwa changamoto nyingine ni shule kutokuwa na jengo la utawala ambapo jumla ya wahitimu kwa mwaka huu ni 126 ambapo shule hiyo ina wanafunzi 912 na ilianzishwa mwaka 2004 na ina walimu 24.

JAMII PWANI YATAKIWA KUWALINDA WATOTO ILI WAISHI KWENYE MAZINGIRA MAZURI




WADAU wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) Mkoani Pwani wameshauriwa jamii kuwalinda watoto ili kuepukana na vitendo vya ukatili.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Mkurugenzi wa Anjita Child Development Foundation Janeth Malela wakati wa kikao cha maandalizi ya uzinduzi wa Programu hiyo kwa Mkoa wa Pwani.

Malela alisema kuwa programu hiyo itasaidia kuimarisha ukuaji na maendeleo ya mtoto kikamilifu kimwili, kiakili, kukuza lugha, mawasiliano kijamii na kihisia. 

"Programu hii ni kutoa huduma za Afya, Lishe, Malezi yenye Mwitikio, ujifunzaji wa Awali na Ulinzi na Usalama kwa watoto wa miaka 0 hadi 8 na kuimarisha ushirikiano wa wadau wa sekta mbalimbali katika huduma za MMMAM,"alisema Malela.

Aidha alisema kuwa lengo kuu ni kusaidia watoto kwenye masuala ya malezi,makuzi,ujifunzaji,ulinzi wa mtoto,afya ili wakue katika mazingira mazuri na kukua kutokana na sheria zilizopo.

Kwa upande wake ofisa maendeleo ya jamii mkoa wa Pwani Rachel Chuwa alisema kuwa moja ya changamoto wanazozipata watoto ni baadhi ya wazazi na walezi kutowahudumia watoto wao kwa wakati kutokana na kutafuta mahitaji ya nyumbani.

Chuwa alisema kuwa malezi na makuzi wazazi wanapaswa wawahudumie lakini kwa sasa wanalelewa na televisheni na mitandao na suala la lishe shuleni baadhi wanatoa chakuka lakini waengine hawatoi hivyo mpango huo utasaidia kuondoa changamoto zolizopo ili wapate huduma stahiki.

Naye mkurugenzi wa shirika la maendeleo kwa vijana (YPC) Israel Ilunde alisema kuwa mpango huo ni muhimu sana kwani vijana wanakumbana na changamoto za kimaadili kutokana na kutopata malezi bora kutokana na hali ya kimaisha.

Ilunde alisema kuwa mpango huo utasaidia sana katika kuwalea watoto na kuondoa vitendo viovu kutokana na malezi watakayoyapata hivyo rasilimali zitengwe ili kuwalea watoto katika misingi mizuri ya kimaadili.

Mikoa 10 ambayo imeshazindua programu hiyo ni Tabora, Arusha, Morogoro, Rukwa, Manyara, Mbeya, Dodoma, Dar es Salaam, Kagera na Lindi.

Wednesday, August 30, 2023

TUME YASAJILI WATAALAMU 1,600

 

Mkurugenzi wa Tume ya TEHAMA Dkt. Nkundwe Mwasaga amesema hadi kufikia Juni 31 , 2023  imesajili wataalam wa TEHAMA 1,600 wanaohudumia nchi nzima na bado zoezi la usajili linaendelea.

Dkt.Mwasaga ameyasema hayo leo Jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa shughuli mbalimbali za TUME hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka wa fedha wa 2023/2024.

Akitaja Mafanikio kwa mwaka wa fedha 2023/24 amesema Tume imefanikiwa Kuanzishwa kwa mradi wa kujengwa kituo kikubwa cha Taifa cha Ubunifu Dar Es Salaam kwa ajili ya kutoa huduma kwa wataalam, watafiti, na wabunifu wa TEHAMA. 

"Tunatengeneza mfumo jumuishi utakaounganisha usajili na uendelezaji wa wataalam na wabunifu TEHAMA nchini (ICT human capital development system): lengo la mfumo huu ni kutambua bunifu na kupanua wigo wa ukuzaji wa wabunifu na bidhaa na huduma za TEHAMA zinazozalishwa Tanzania na hivyo kukuza pato la Taifa na kuongeza fursa za ajira kupitia TEHAMA na maendeleo ya kidijitali duniani"Amesema Dkt.Mwasaga.

Aidha ameongeza kuwa wanaandaa mkutano wa mwaka wa TEHAMA (TAIC) na Tuzo ya TEHAMA Tanzania (Tanzania ICT Award)

"Hili lilikuwa kongamano kubwa la mwaka la TEHAMA lililofanyika Zanzibar mwezi Oktoba, 2022 na kuwashirikisha wawekezaji na wadau mbalimbali wa TEHAMA kutoka ndani na nje ya nchi wapatao 1,200"

Sanjari na hayo vipaumbele vya tume kwa mwaka 2023/24 ni pamoja na kuendelea na ukamilishwaji wa vituo vya ubunifu TEHAMA (Soft centers) katika Kanda 5 pamoja na kuanzisha kituo kimoja Zanzibar,kuanzisha kituo cha kutengeneza na kuboresha vifaa vya TEHAMA (ICT Refurbishment and Assembly centre),kuwezesha uanzishaji wa vituo vya majaribio vya ubunifu TEHAMA (District ICT Startups Innovation hubs) katika Wilaya 10,

Aidha vipaumbele vingine ni kufanya tafiti za maendeleo ya TEHAMA nchini na kufanya tathmini ya kitaifa ya hatua za utekelezaji wa mikakati mbalimbali ya TEHAMA,kuratibu na kuandaa matukio ya kuvutia uwekezaji na kutangaza masoko ya bidhaa za TEHAMA ndani na nje ya nchi,kushirikiana na washirika wa maendeleo na kampuni za kimataifa katika kuendeleza bunifu za TEHAMA ikiwemo kuwezesha utengenezaji wa bidhaa za TEHAMA hapa nchini pamoja na kujenga kituo cha Artificial Intelligence kwa ajili ya kuendeleza wataalam wa TEHAMA.

Kwa upande wake Msemaji Mkuu wa Serikali Ndugu Gerson Msigwa amesema Serikali imeamua kuwekeza kwa nguvu kwenye Tanzania ya Kidigitali chini ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambapo usimamizi m kuu unafanywa na Tume ya TEHAMA.

Ameongeza kuwa hili ni jambo kubwa kwani fedha nyingi imewekezwa kwa ajili ya kuboresha TEHAMA nchini kwani shughuli mbalimbali kwa sasa duniani zinafanyika kwa njia ya kidijitali ikiwemo huduma za malipo mabalimbali, huduma za afya za matibabu, uzalishaji, kilimo, uchimbaji wa madini.

Tuesday, August 29, 2023

PWANI YASHEREHEKEA USHINDI WA KWANZA NCHINI MKATABA WA LISHE

 


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mh. Angela Kairuki, akikabidhi Ngao ya Ushindi wa Kwanza kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mh. Abubakar Kunenge (katikati pichani) leo Agosti 29, 2023 kwa Mkoa wa Pwani kuibuka mshindi katika utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa mwaka 2022/23. Mwingine ni Katibu Tawala Mkoa huo na Skauti Mkuu wa Tanzania Rashid Mchata.

*Mkoa wa Pwani waongoza utekelezaji Mkataba wa Lishe kitaifa*

Mkoa wa Pwani umeongoza kwa kushika nafasi ya kwanza kwa tathmini ya Saba (7) ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa Mwaka 2022/2023.

Taarifa zilizotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa - (OR - TAMISEMI) zimeeleza kuwa Mkoa huo umefuatiwa na Lindi katika nafasi ya pili huku nafasi ya tatu ikienda kwa mkoa wa Iringa.

Kwa upande wa nafasi za Halmashauri, Mkoa wa Pwani umefanikiwa kuingiza halmashauri za Kibaha TC na Kibaha DC katika nafasi kumi za mwanzo.

Kibaha TC imekuwa ya na Kibaha DC ikiwa ni ya 10 huku hamashauri zingine za mkoa huo zikiwa zimeshika nafasi juu ya 100 za mwanzo.

Halamshauri hizo na nafasi zao kitaifa kwenye mabano ni Kisarawe (17), Rufiji (25), Bagamoyo (26) na Kibiti (54).

Zingine ni Chalinze (59), Mafia (91) na Mkuranga (93).

HIFADHI YA TAIFA KITULO KUTANGAZWA KITAIFA NA KIMATAIFA ILI KUVUTIA WATALII NA WAWEKEZAJI

 

Serikali imeendelea kujizatiti kwa  kuitangaza  Hifadhi ya Taifa ya Kitulo  ndani na nje ya nchi lengo likiwa ni kuwavutia watalii na wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali Duniani kupitia maonesho, matamasha na kwa  njia ya kidijitali.

Kauli hiyo imesemwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Makete, Mhe. Festo Sanga aliyetaka kujua mkakati wa Serikali wa kuitangaza Hifadhi ya Taifa ya Kitulo.

Amefafanua kuwa hifadhi hiyo imekuwa ikitangazwa katika matamasha mbalimbali ya Karibu Kusini, Kilifair na Maonesho ya Kimataifa ya Sabasaba na Nanenane na kwa njia ya kidigitali, mitandao ya kijamii, majarida na Safari Channel.

Kufuatia hatua hiyo Serikali imeanza kuboresha  miundombinu ndani ya hifadhi hiyo ikiwemo kufanya ujenzi wa nyumba tatu za malazi ya watalii na pia inatarajia  na kujenga nyumba mbili  na kambi moja  ya kuweka hema katika mwaka huu wa fedha 2023/2024, pamoja na  kukarabati miundombinu ya barabara.

Kuhusu utatuzi wa migogoro ya mipaka kati ya hifadhi hiyo na wananchi, Mhe. Masanja amesema tathmini ilishafanyika na kulielekeza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kuweka vigingi katika maeneo ambayo yameshaainishwa.

Saturday, August 26, 2023

WANANCHI TUMIENI VITUO VYA MSAADA WA SHERIA KUSULUHISHA KESI ZA MADAI KUPITIA VITUO VYA MSAADA WA SHERIA-KPC

WANANCHI Wilayani Kibaha Mkoani Pwani wametakiwa kutumia vituo vya msaada wa sheria kusuluhisha kesi za madai nje ya mahakama ili kuokoa muda na kuipunguzia mahakama mzigo wa mashauri.
Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na mkurugenzi wa Kituo cha Msaada wa Sheria Kibaha (KPC) Catherine Mlenga alipozungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake.

Mlenga alisema kuwa baada ya bunge kufanya marekebisho sheria inaruhusu wadai kukubaliana nje ya mahakama kwa maridhiano ya pande mbili na kumaliza shauri kisha kufutwa na mahakama.

"Tunawashauri wananchi watumie vituo hivi ili kutatua mashauri ya madai nje ya mahakama endapo watakubaliana na makubaliano hayo yatasajiliwa na mahakama na kuimaliza kesi hiyo,"alisema Mlenga.

Alisema kuwa faida ya kumaliza mashauri ya madai nje ya mahakama ni kuokoa muda na hakutakuwa na uadui baina ya pande hizo mbili tofauti na kuendesha kesi mahakamani.

"Njia hii ya usuluhishi na upatanishi ni nzuri kwani ni rafiki na haina uhasama ambapo kesi inapofanywa mahakamani kunakuwa na uhasama sana hivyo wananchi watumie fursa hii,"alisema Mlenga.

Aidha aliwataka wananchi kutumia zaidi maridhiano katika changamoto za mashauri ya madai ambapo itaipunguzia mahakama mlundikano wa kesi hivyo kutotumia muda mrefu.

Kwa upande wake meneja wa KPC Dismas Chihwalo alisema kuwa kituo chao kinatoa huduma bure kwa watu wenye mashauri mbalimbali ya kisheria.

Chihwalo alisema kuwa wameweza kutatua changamoto nyingi za kisheria na kufanikisha wananchi kupata haki zao kwa njia usuluhishi kwenye mashauri mbalimbali.


TUME YA TAIFA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA YAFADHILI MRADI UTAFITI CHANGAMOTO YA SOMO LA HISABATI

TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia imesema kuonekana na kuwepo kwa changamoto ya matokeo mabaya ya somo la hisabati katika matokeo ya Darasa la saba na kidato cha nne tume hiyo imefadhili mradi wa utafiti ili kugundua sababu ya tatizo hilo.

Hayo yameelezwa jijini hapa leo ,Agosti 25,2023 na Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo Dkt.Amos Nungu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa shughuli na mafanikio ya tume hiyo.

Vilevile Dkt.Nungu ametaja baadhi ya shughuli zilizotekelezwa na Tume hiyo kuwa ni pamoja na kuibua na kufadhili miradi ya kimkakati ambayo tayari michakato yake imefanyika na sasa ipo katika hatua ya mikataba ambapo Serikali kupitia COSTECH imeidhinisha jumla ya miradi saba kwa thamani ya shilingi milioni 150 kila mradi.

Amesema Miradi hiyo itafanyika ndani ya miaka miwili na inahusisha watafiti na wabunifu kutoka sekta zote za umma na binafsi.

Aidha amesema kuwa Serikali kupitia COSTECH, imeidhinisha miradi miwili kwa thamani ya shilingi milioni 120 kila mradi ambapo utekelezaji wake pia unahusisha watafiti kutoka vyuo mbalimbali hapa nchini na itafanyika ndani ya miaka miwili, sasa ipo hatua ya kusaini mikataba.

Akizungumzia majukumu na vipaumbele vya tume hiyo kwa mwaka wa fedha 2023/24, Dkt.Nungu amesema kuwa Tume hiyo imeendelea kusimamia miradi inayoendelea ukiwemo wa Kigoda cha Utafiti katika SUA na NM-AIST ambao ni mradi wa miaka mitano, wenye thamani ya takribani shilingi bilioni 5 pamoja na kushirikiana na Mabaraza ya Kikanda na Kimataifa kuhakikisha tunashiriki kutafuta fursa ambazo zitaendelea kuleta fedha za utafiti kupitia COSTECH au kuhamasisha Taasisi za ndani kuomba hizo fursa.

Kukamilisha zoezi la ufadhili wa pamoja miradi ya utafiti wa Mabaraza ya Utafiti duniani ikiwa ni njia mojawapo ya kuongeza kuonekana kwa watafiti wetu na kuitangaza nchi yetu katika nyanja hii ya utafiti pamoja na kukamilisha mchakato na kutoa fedha kwa maandiko mawili kwa kutoa mrejesho kwa walioshiriki lakini wakakosa, na kuwatembelea walioshinda.

Vilevile, kupitia mradi wa HEET, tunaboresha mifumo mbalimbali ili kuongeza ufanisi zaidi katika suala la uratibu wa ume. Ikumbukwe kuwa mradi huu ni mahususi kwa Taasisi za Elimu ya Juu hivyo, inabidi tuwe tayari kuwahudumia baada ya kukamilisha mabadiliko wanayofanya kupitia mradi huo.

MAOFISA MANUNUZI WATAKIWA KUZINGATIA UKOMO MATUMIZI YA KEMIKALI

Serikali imewataka maafisa ununuzi na ugavi kuzingatia ukomo wa matumizi ya kemikali na vifaa vyenye kemikali ambazo zinamong’onyoa tabaka la ozoni au kuwa na athari kwa afya ya binadamu na mazingira.

Hayo yamebainishwa leo Ijumaa Agosti 25, 2023 Jijini Dodoma na Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Switbert Mkama wakati akifungua warsha ya mafunzo kwa Maafisa ununuzi na ugavi kuhusu utekelezaji wa Itifaki ya Montreal inayohusu kemikali zinazomong’onyoa tabaka la ozoni.

Dkt. Mkama amesema mwanzoni mwa miaka ya 1970, wanasayansi walibaini baadhi ya kemikali zinazotengenezwa na binadamu ikiwemo majokofu, viyoyozi, vifaa vya kuzimia moto na utengenezaji wa magodoro vimejipenyeza angani na kumong'onyoa tabaka la hewa ya Ozoni na kusababisha madhara kwa afya ya binadamu na mazingira.

“Matokeo ya kumong’onyoka kwa Tabaka la Ozoni ni kuruhusu mionzi zaidi ya urujuani kufikia uso wa dunia ambayo husababisha madhara mbalimbali kwa afya ya binadamu na mazingira. Madhara hayo ni kama vile saratani ya ngozi, uharibifu wa macho unaosababisha upofu na athari kwa kwa ukuaji wa mimea na viumbe hai wengine” amesema Dkt. Mkama

Aidha Dkt. Mkama amesema matokeo ya uvumbuzi huo yalisababisha Shirika la Kimataifa linaloshughulikia Mazingira (UN Environment) kufanya tathmini ya kisayansi na kuamua kuchukua hatua madhubuti kulinda tabaka la Ozoni kwa kuanzisha Itifaki ya Montreal kuhusu udhibiti wa kemikali zinazomong'onyoa Tabaka la Ozoni iliyopitishwa mwaka 1987.

Akifafanua zaidi Dkt. Mkama amesema katika kutekeleza Itifaki hiyo, Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuandaa na kutekeleza Mpango wa Kuondosha Kemikali Zinazomong’onyoa Tabaka la Ozoni Jamii ya Hydrochlorofluorocarbons (HCFCs) ifikapo mwaka 2030 pamoja na Mpango wa utekelezaji wa Marekebisho ya Kigali ya kupunguza matumizi ya kemikali jamii ya hidrofluorokaboni.

“Chini ya Mipango hii mojawapo ya shughuli zinazotelekezwa na zinazopaswa kutekelezwa ni pamoja na kutoa mafunzo kwa maafisa ununuzi na ugavi kutoka katika Taasisi mbalimbali kukusu utekelezaji wa Itifaki husika ikiwemo utekelezaji wa Kanuni za Usimamizi wa Mazingira (Udhibiti wa Kemikali Zinazomong’onyoa Tabaka la Ozoni) za mwaka 2022” amesema Dkt. Mkama.

Dkt. Mkama amesema maafisa ununuzi na ugavi ni wahusika wakuu katika mchakato wa wa kushugulikia manunuzi ya vifaa mbalimbali katika ofisi za umma, hivyo wana wajibu mkubwa wa kutoa elimu ya Ozoni kwa wengine ili kuongeza juhudi za kuhifadhi Tabaka la Ozoni na kuokoa Maisha ya binadamu na viumbe hai.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Kemilembe Mutasa amesema katika kutekeleza Itifaki hiyo, Ofisi hiyo imeendelea kutoa mafunzo wa wadau mbalimbali wakiwemo maafisa ununuzi na ugavi kutoka katika Wizara mbalimbali kwa lengo la kuwajengea uelewa kuhusu matakwa ya Itifaki ya Montreal.

“Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania, Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Shirika la Viwango Tanzania na Vyuo mbalimbali vya Mafunzo ya Ufundi tumeendelea kutoa mafunzo kwa maafisa mbalimbali kuhusu usimamizi na udhibiti wa kemikali na vifaa vyenye kemikali zinazodhibitiwa chini ya Itifaki hii” amesema Kemilembe.

Friday, August 25, 2023

𝗖𝗕𝗪𝗦𝗢𝘀 𝗦𝗔𝗦𝗔 𝗞𝗨𝗧𝗨𝗠𝗜𝗔 𝗠𝗙𝗨𝗠𝗢 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗜𝗜𝗦

Vyombo vya Watumia Maji vya jamii (CBWSOs) vinavyosimamiwa na Wakala ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), vimetakiwa kutumia Mfumo wa pamoja wa Ankara za Maji (MAJIIS), ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma ya maji kwa wananchi.

Agizo hilo limetolewa hivi karibuni na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mhe. Kisare Makori, wakati akifunga mafunzo ya siku saba kwa Maafisa wa CBWSOs wa mkoa wa Kilimanjaro yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo cha USHIRIKA mjini Moshi .

Alisema, Serikali imedhamiria kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika taasisi za umma ili  kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi kwa urahisi, haraka na kwa gharama nafuu mahali walipo.

“Serikali ya awamu ya sita inachukua jitihada mbalimbali katika kuhakikisha TEHAMA inarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi, ambapo kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kwa kushirikiana na Wizara ya Maji, imetengeneza mfumo wa MAJIIS ili kutatua changamoto mbalimbali zilizokua zinaikabili Sekta ya Maji”, alisema.

Alifafanua kuwa, Serikali imewekeza katika mfumo huo hivyo ni jukumu la watumishi wa sekta ya Maji kufanya kazi ili kuhakikisha mfumo huo unakua mkombozi kwa wananchi.

Kwa upande wake mtaalamu wa TEHAMA kutoka Wizara ya Maji Mha. Masoud Almas alisema, mfumo wa MAJIIS umeboreshwa ili uweze kutumiwa na Vyombo vya Watumia Maji vya jamii (CBWSOs) vinavyotoa huduma vijijini ili kuhakikisha TEHAMA inarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi mahali walipo.

“Mkoa wa Kilimanjaro umekuwa ni mkoa wa kwanza kuanza kutumia mfumo huu wa MAJIIS kwa CBSWOs na Wizara itaendelea kuhakikisha CBSWOs zote katika mikoa mingine zinatumia mfumo huu ili kurahisisha utendaji kazi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi waishio vijijini” alisema.

Aliongeza kuwa, hadi sasa mfumo huo umeleta mafanikio makubwa kwa Wizara ya Maji ikiwa ni pamoja na kuongeza ukusanyaji wa mapato na kurahisiha upatikanaji wa taarifa za Mamlaka zote za Maji nchini.

“Hadi sasa, Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingiara za miji mikuu ya mikoa, miradi ya kitaifa, miji ya Wilaya na miji Midogo 87 Tanzania Bara na Zanzibar pamoja na Bodi za Maji za Mabonde 9 zinatumia Mfumo huu wa Pamoja”, alifafanua Almas.

Aidha, alibainisha kuwa ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi, mfumo wa MAJIIS umeunganishwa na mifumo mingine ya Serikali ikiwa ni pamoja na mfumo wa GePG, Mfumo wa Barua Pepe Serikalini (GMS), Mfumo wa Ujumbe Mfupi wa Simu za mkononi ambao hutumika kutoa taarifa za huduma kwa Wateja ikiwemo kutuma bili, mfumo wa NIDA na mfumo wa BRELA.

Jumla ya washiriki 72 kutoka Vyombo vya Watumia Maji vya jamii (CBWSOs) 39 vya mkoa wa Kilimanjaro walihudhuria mafunzo hayo.

JWT LATOA SIKU 7 WENYE MAVAZI YA JESHI KUYASALIMISHA

Jeshi la Ulinzi la  Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetoa siku 7 za kusalimisha mavazi ya Jeshi kwa yeyote ambaye ana mavazi hayo iwe anavaa,kuuza au kwa wasanii kupanda nayo katika majukwaa ya utumbuizaji.

Hayo yametolewa na Luten Kanali Gaudentius Ilonda ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano makao makuu ya Jeshi (JWTZ) wakati akizungumza na wanahabari kuhusu katazo hilo na ukikwajji wa Sheria ya uvaaji wa mavazi hayo Jijini Dodoma

Aidha Luteni Kanali Ilonda amesema kuwa mavazi yanayokatazwa na Jeshi ni pamoja na kombati (vazi la mabaka), Makoti,Tisheti, Kofia,Viatu kwa mujibu wa sheria mbalimbali kama anavyoelezea.

Kwa upande wake msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa idara ya habari maelezo Bwana Gerson Msigwa amewaomba wazazi na walezi kuwakagua watoto wao ili kama Wana sale za Jeshi wazizuie na kusalimisha.

BILIONI 858.5 ZAIDHINISHWA BARABARA ZA WILAYA NCHINI

Katika mwaka wa fedha 2023/24, jumla ya barabara zenye urefu wa km 21,057.06 zitafanyiwa matengenezo, km 427 zitajengwa kwa kiwango cha lami, km 8,775.62 zitajengwa kwa kiwango cha changarawe, madaraja na makalavati 855 yatajengwa pamoja na mifereji ya mvua km 70.

Aidha, Jumla ya Shilingi Bilioni 858.517 zimeidhinishwa kwa ajili ya ujenzi, ukarabati na matengenezo ya miundombinu ya barabara za Wilaya.

Taarifa hiyo imetolewa leo 24.8.2023 Jijini Dodoma na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seif wakati akizungumza ba waandishi wa Habari kuhusu utekelezaji wa Majukumu na mwelekeo wake katika mwaka wa fedha 2023/24.

Mhandisi Victor,amesema Kati ya fedha hizo, shilingi Bilioni 710.31 ni fedha za ndani na shilingi Bilioni 148.207 ni fedha za nje kupitia miradi ya RISE, TACTIC, Bonde la mto Msimbazi na Mradi wa Agri connect.

Pia amebainisha Madaraja hayo yamejengwa katika mikoa ya Kigoma 92, Singida 24, Tabora 5, Kilimanjaro 10, Mbeya 2, Arusha 6, Morogoro 2, Rukwa 3, Pwani 1, Ruvuma 3 na Iringa 15.

Kwa Upande wake  Msemaji Mkuu wa Serikali,  Gerson Msigwa amesema TARURA imeanzishwa mwaka 2017 lengo likiwa ni kupanua mawanda ya namna ambavyo tutawahudumia Watanzania kwa kuwaboreshea barabara.

KPC YAWAASA WANAFUNZI KIBAHA KUZINGATIA MAADILI



WANAFUNZI Wilayani Kibaha Mkoani Pwani wametakiwa kuzingatia maadili wanayofundishwa shuleni na kutojiingiza kwenye vitendo viovu vya utovu wa nidhamu.

Hayo yamesemwa na msaidizi wa sheria kutoka Kituo cha Msaada wa Sheria Kibaha (KPC) Dominika Ndumbaro alipokuwa akifundisha somo la sheria ya mtoto kwenye shule ya sekondari ya Mwambisi.

Ndumbaro amesema kuwa ili kuepukana na vitendo vya ukatili ambavyo wanafanyiwa wanafunzi wanapaswa kutojiingiza kwenye vitendo viovu vinavyosababisha ukatili.

Amesema baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakishiriki vitendo vya matumizi ya dawa za kulevya kama uvutaji bhangi, unywaji wa pombe, kwenda disko au sehemu za starehe.

Aidha alisema kuwa huko wanakutana na watu waliowazidi umri hivyo kuwafanyia vitendo vikiwemo vya ubakaji, ulawiti na hata vipigo endapo hawata sikiliza matakwa yao.

Aliongeza kuwa wanafunzi wanapojiingiza kwenye hali hiyo hushindwa kusoma na kujikuta wakiwa watoto wa mitaani na kujifunza wizi na kujiuza hivyo kutomaliza masomo yao.

Aliitaka jamii kwa kushirikiana na walimu na viongozi kukabili vitendo viovu kwa kuwahimiza wanafunzi kuwa na maadili mema na kumtanguliza Mungu ili kuepukana na vitendo hivyo.

Kituo cha Msaada wa Sheria kinanajihusisha na utoaji wa elimu ya sheria kwa masuala yote ya kisheria pia kinatoa msaada wa sheria kwa watu wenye changamoto za kisheria. 

Thursday, August 24, 2023

TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS NYERERE YATOA MSAADA WA WHEEL CHAIRS NA VITI.






TAASISI ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mkoa wa Pwani imetoa viti mwendo kwa wanafunzi wawili wenye ulemavu wanaosoma Shule ya Msingi Muungano iliyopo Wilayani Kibaha.

Aidha imetoa viti vitatu vya ofisini kwa ajili ya walimu wa shule hiyo ili kuwaondolea kero ya upungufu wa viti vya walimu kwenye shule hiyo.

Akikabidhi vifaa hivyo wakati wa mahafali ya 6 ya shule hiyo ya darasa la saba mratibu wa idara ya afya na mahitaji maalumu kutoka Taasisi hiyo Wilson Fungameza alisema kuwa wametoa viti mwendo hivyo baada ya kuona changamoto za wanafunzi hao wanazozipata wakati wa kwenda shule na kurudi nyumbani.

Fungameza ambaye ni muuguzi namba moja Tanzania na namba tano duniani alisema kuwa wamewapatia wanafunzi hao ili kiwarahisishia wazazi kwani walikuwa wakiwabeba kuwapeleka shuleni na kuwarudisha.

"Baada ya mwalimu mkuu kutoa ombi kwetu tuliona kuna umuhimu wa kuwasaidia watoto hao na wazazi kwani ilikuwa ni changamoto kubwa kwao hivyo kuwa na mazingira magumu ya kupata elimu,"alisema Fungameza.

Kwa upande wake katibu wa Taasisi hiyo Omary Punzi alisema kuwa jamii inapaswa kusaidia wanafunzi na watu wenye uhitaji ili waweze kufikia malengo yao kwa kuwapatia vifaa saidizi.

Punzi alisema kuwa kwakuwa taasisi yao inasaidia jitihada za serikali kwenye sekta mbalimbali ikiwemo ya elimu ili kuhakisha wanafunzi wanapata elimu bora.

Naye Mwalimu mkuu wa shule hiyo Faith Tawe alisema kuwa wanaishukuru taasisi hiyo kwa msaada walioutoa kwani utawapungizia mzigo wanafunzi na wazazi hao na pia viti vitasaidia walimu wakiwa ofisini.

Tawe aliomba wadau wengine wajitokeze kuwasaidia wanafunzi wanaotoka mazingira magumu pia shule ambayo nayo ina changamoto nyingi ikiwemo upungufu wa majengo.

Akisoma risala ya wahitimu wa shule hiyo Johnson Ernest alisema kuwa wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa madawati ambapo yaliyopo ni 188 kati ya madawati 588 yanayotakiwa.

Ernest alisema kuwa kutokana na changamoto hiyo wanafunzi wengi wanakaa chini ambapo shule hiyo ina wanafunzi 1,175 na ilianzishwa mwaka 2021 na ina walimu 22.

WAENEZI WATAKIWA KUSEMEA MIRADI UTEKELEZAJI ILANI YA CCM

WAENEZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya za Mkoa wa Pwani wametakiwa kuisemea miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya chama.

Hayo yalisemwa Wilayani Bagamoyo na Katibu wa Siasa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Pwani David Mramba alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa semina elekezi kwa waenezi wa wilaya za mkoa huo.

Mramba alisema kuwa semina hiyo ililenga waenezi hao kujua majukumu yao kwa wanachama na kwa wananchi ambapo wanapaswa kuielezea miradi ya maendeleo ambayo imetekelezwa kupitia ilani ya chama ya miaka mitano.

"Waenezi wanapaswa kusemea shughuli mbalimbali za chama pamoja na utekelezaji wa ilani kupitia miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ambayo inaongozwa na CCM,"alisema Mramba.

Alisema kuwa kuelezea miradi inayotekelezwa kwanza ni kumsaidia Rais Dk Samia Suluhu Hassan kumsemea jitihada anazozifanya kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo.

"Mambo mengi yanafanywa na serikali ya awamu ya sita lakini baadhi hayasemwi lakini mafunzo haya yawe sehemu ya kukitangaza chama na uzuri wa sera zake ili kuwavutia watu kujiunga nacho,"alisema Mramba.

Aidha alisema kuwa waenezi hao kupitia mafunzo hayo kubadilika na kwenda kisasa na kuacha kufanya kazi kwa mazoea kwani nyakati za sasa zimebadilika lazima wajitume.

Kwa upande wake Mwenezi wa Kibaha Mjini Clemence Kagaruki alisema kuwa mafunzo jayo watayashusha ngazi ya kata na matawi ili kuboresha utendaji kazi.

Kagaruki alisema kuwa pia yamewajengea uwezo wa kujiandaa kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji utakaofanyika mwakani na uchaguzi mkuu wa 2025.

Naye Mwenezi wa Wilaya ya Kibiti Juakali Kuanya alisema kuwa atakuwa kiungo muhimu katika kutoa taarifa mbalimbali kwa wananchi na umma kwa ujumla.

Kuanya alisema kuwa atatumia mafunzo hayo kuleta mabadiliko ambayo yataleta maendeleo kwa wananchi kupitia sera za chama na mipango mbalimbali ya kiwilaya na kitaifa.

Moja ya wakufunzi wa mafunzo hayo Khadija Juma alisema somo alilofundisha ni kuhusu uzalendo ambalo ni muhimu kwa kila Mtanzania kulijua ili kuitetea nchi yake.

Juma alisema kuwa ili watu waweze kutekeleza majukumu yao lazima wawe wazalendo kama ilivyokuwa kwa waasisi wa nchi ambao walitanguliza uzalendo kwanza.

Wednesday, August 23, 2023

KPC WAJADILI MAREKEBISHO YA BAADHI YA SHERIA

KITUO cha Msaada wa Sheria Kibaha (KPC) kimefurahishwa na marekebisho ya baadhi ya sheria yaliyofanyika kati ya mwaka 2019-2023 ikiwemo ya uendeshaji wa mirathi ambapo imeongeza adhabu kwa msimamizi wa mirathi anaposhindwa kutimiza wajibu wake kutoka shilingi 2,000 hadi milioni 2.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa kituo hicho Catherine Mlenga mara baada ya kufanya kikao kupitia marekebisho hayo yaliyofanyika kupitia bunge kwa mujibu wa sheria.

Mlenga alisema kuwa kwa mujibu wa sheria kifungu cha 107 (3) cha sheria ya usimamizi wa mirathi sura 352 ni kuwa msimamizi wa mirathi endapo atashindwa kupeleka taarifa za ukusanywaji na ugawaji wa mali ndani ya muda uliopangwa anaweza kuondolewa na kushtakiwa.

"Kabla ya mabadiliko adhabu ilikuwa ni kulipa shilingi 2,000 au kifungo cha miezi sita ambapo sheria hiyo imefanyiwa marekebisho ambapo faini isiyopungua milioni mbili au kifungo kisichopungua miaka miwili,"alisema Mlenga.

Tuesday, August 22, 2023

MAKAM WA RAIS DK MPANGO ATAKA WAKUU WA MIKOA KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI





MAKAMU wa Rais wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Philip Mpango ameitaka mikoa nchini kushirikiana na sekta binafsi ikiwemo mabaraza ya biashara ya mikoa na kutowatumia wakati wa kuomba michango ya shughuli za maendeleo.

Dk Mpango aliyasema hayo jana Mjini Kibaha kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere wakati akifungua mafunzo ya uongozi kwa wakuu wa mikoa na makatibu Tawala wa mikoa Tanzania Bara.

Alisema kuwa baadhi ya sekta hiyo imeikitumika na kuwa nao karibu wanapokuwa wanahitaji michango kutoka kwao ikiwemo ya mbio za mwenge, ugeni na maadhimisho mbalimbali.

"Mnapaswa kuwa karibu na sekta binafsi na mabaraza ya biashara ya mikoa yenu kwani ni wadau muhimu wa maendeleo na wakifanya vizuri watatoa ajira kwa watu wengi hivyo lazima muwashirikishe na kuwa karibu nao kwenye mipango mbalimbali ya maendeleo,"alisema Dk Mpango.

Alisema kuwa baadhi ya wakuu wa mikoa wamekuwa na mahusiano mabaya na waliochini yao na wengine hujihusisha unyanyasaji wa kijinsia, kuwa wababe na upendeleo kwenye upandishwaji vyeo.

Kwa upande wake Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Angellah Kairuki alisema kuwa mafunzo hayo ni maelekezo ya Rais kutaka viongozi wapewe mafunzo mbalimbali ya kuwajengea uwezo ili kuboresha utendaji kazi wao.

Kairuki alisema kuwa mafunzo hayo ni kama waliofanyiwa wakuu wa Wilaya 139 huko Dodoma Machi mwaka huu, mafunzo kwa maofisa tarafa na watendaji wa kata 356 kwenye mikoa ya Songwe, Njombe, Katavi na Rukwa na yatafanywa ya wakurugenzi Septemba mwaka huu.

Naye Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete aliyemwakilisha waziri George Simbachawene alisema kuwa kundi hilo ni muhimu sana kwani asilimia 70 ya viongozi hao ndiyo wanaosimamia masuala mazima ya maendeleo.

Kikwete alisema kuwa viongozi hao wanaliwakilusha Taifa kwenye sera zote za serikali kupitia mamlaka za mikoa na serikali za mitaa hivyo watahakikisha kunakuwa na tija kwenye ofisi za umma kuwa na utawala bora na maadili kwa utumishi wa umma.


Sunday, August 20, 2023

NYERERE SUPER CUP KUANZA KUTIMUA VUMBI TAREHE 23.9.2023

 


Katika kundeleza FIKRA za mwasisi wetu wa Taifa Mwalimu  Nyerere Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ikiongozwa na Katibu wa Taasisi hiyo Ndugu Omary Punzi Tarehe 20.8.2023 imefanya Hitimisho la kikao Cha maandalizi ya Mashindano ya NYERERE SUPER CUP yatakaotimua vumbi Tarehe 23.9.2023 na kutamatika 12.10.2023.Mashindano hayo yatashirikisha Wilaya Mbili wilaya ya KIBITI na RUFIJI Kwa Timu 12 Timu sita kutoka kundi A (KIBITI)Timu shiriki Bungu,Jaribu,Mtawanya, Kibiti,Mchukwi,Dimani,na  upande wa kundi B Rufiji timu zinazoshiriki Ngorongo,Utete,.Mgomba, Muhoro,Umwe na Mkongo vikao hivyo vyote viwili Cha Tarehe 19.8.2023 na 20.8.2023 vilikuwa na agenda ya Kuandaa kanuni na ratiba ya kuanza Usajili wa wachezaji,wajumbe wote walikubaliana Dirisha la Usajili lifunguliwe tarehe 23.8.2023 na kuisha 13.8.2023  inatoa shukrani Kwa NSSF na Chuo Cha Afya St David college Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na wilaya ya Kibiti na Rufiji,Ofisi ya Mbunge Kibiti na Rufiji,Chama Cha Mpira KIBITI na RUFIJI

TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE YATOA SHUKRANI KWA WADAU MAANDALIZI NYERERE SUPER CUP

Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani inatoa shukrani Kwa Viongozi wote mliofanikisha safari yetu ya maandalizi ya NYERERE SUPER CUP Taasisi inashukuru 1.Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani 2.ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kibiti na Rufiji 3.Ofisi ya Mbunge Kibiti na Rufiji 4.Chama Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani COREFA 5.Chama cha Mpira wilaya Kibiti na Rufiji 6.Mdhamini Nssf na St David college Chuo Cha Afya kimara temboni,Madiwani wa Kibiti na Rufiji kuruhusu Viongozi wao kuhudhuria kikao na washiriki waliohudhuria UZALENDO NI KULIPENDA TAIFA LAKO MITANO TENA

*LYIDENGE ATAKA WAFANYAKAZI WA MIRADI KUWA NA NIDHAMU*

MKUU wa Polisi Wilaya ya Chalinze, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Sophia Lyidenge amewataka wafanyakazi wa mradi wa umeme wa serikali kuwa na nidhamu na kutokujihusisha na vitendo vya kihalifu.

Amebainisha hayo leo Agosti  20 alipotembela mradi huo wakati  akizungumza na wafanyakazi hao kuona kama wana changamoto zozote za kiusalama.

SSP Lyidenge aliwaeleza wafanyakazi hao kuwa wameaminiwa na serikali kufanya kazi hivyo wanatakiwa kuwa waadilifu na wasijihusishe na vitendo vya kihalifu ikiwemo wizi wa vitendea kazi na kuwataka wawe walinzi wa kwanza wa vifaa hivyo.

Sambamba na hayo SSP Lyidenge aliwasihi viongozi wa mradi huo kuwa na mahusiano mazuri na wafanyakazi ikiwemo lugha nzuri yenye staha ili kuongeza hamasa ya utendaji na kufikia malengo ya mradi kwa wakati uliokusudiwa.

"Niwaombe viongozi kuwatia moyo na kuwa na lugha shawishi kwa mnao wasimamia ili mradi huu uweze kukamilika kwa wakati, lugha zisizo na staha huwavunja moyo watendaji na kujikuta ikiwapunguzia morali ya kujituma". 

Sote tunatambua umuhimu wa mradi huu utakavyochochea maendeleo ya kiuchumi kwa kwa wakazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani na taifa kwa ujumla” alisema Lyidenge

CCM WAASWA KUFUATA UTARATIBU

 

WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani wanaotoa misaada na kufanya shughuli za maendeleo wametakiwa kufuata utaratibu ili kuepusha mkanganyiko na viongozi waliochaguliwa na wananchi.

Hayo yalisemwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa Hamoud Jumaa wakati wa mkutano wa tathmini baada ya ziara ya CCM Kibaha Mjini.

Jumaa alisema kuwa kukisaidia chama siyo tatizo lakini kinachotakiwa ni utaratibu kufuatwa ili kusitokee tofauti baina ya wale wanaosaidia na wale waliochaguliwa.

"Tunajua kwa sasa ni kipindi cha kuelekea uchaguzi mwakani ni wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa na 2025 ni uchaguzi mkuu hivyo wanaotoa misaada ndani ya chama wafuate taratibu lakini siyo kosa kukisaidia chama,"alisema Jumaa.

Alisema chama kinasaidiwa na wanachama na wadau mbalimbali wana haki ya kufanya hivyo ili mradi wazingatie utaratibu uliowekwa na chama wa namna ya kuchangia.

"Chama kinajengwa na wanachama na wanaokichangia siyo tatizo hata mimi kwenye eneo langu nachangia lakini kwa kufuata utaratibu hivyo na wengine wafuate utaratibu wa chama,"alisema Jumaa.

Kwa upande wake mwentekiti wa CCM Kibaha Mjini Mwajuma Nyamka alisema kuwa utekelezaji wa ilani umefanyika kwa asilimia zaidi ya asilimia 90 ndani ya kipindi cha miaka miwili tu.

Nyamka alisema kuwa wanamshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Kibaha fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo ambapo miradi mingi inaendelea na mingine imekamilika.

Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa kwa kushirikiana na serikali na wananchi wameendelea kukabili changamoto kwenye jimbo hilo.

Koka alisema utekelezaji wa ilani unaendelea vizuri na hakuna kilichokwama kila kitu kinakwenda vizuri lengo likiwa ni kuwaondolea changamoto wananchi na kutimiza malengo ya Rais.

Naye mwenekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Focus Bundala alisema kuwa wanaishukuru serikali kutoa kwa kuipatia Halmashauri kiasi cha shilingi bilioni 8.

Bundala alisema kuwa baadhi ya fedha zimetumika kwenye ujenzi wa shule sita za sekondari na shule tisa za msingi na miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na barabara, maji na afya.

COREFA YAZINDUA KITUO CHA SOKA KWA VIJANA KIBAHA


CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimezindua kituo cha michezo kwa vijana chini ya miaka 17 kikiwa na lengo la kuibua na kukuza vipaji vya vijana ndani ya mkoa huo.

Akizindua kituo hicho kwa Kanda ya Kaskazini kaimu mkuu wa wilaya ya Kibaha Moses Magogwa ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema kuwa uwekezaji kwa vijana kutasaidia kuwa na timu bora za baadaye.

Magogwa ambaye ni katibu tawala wa wilaya (DAS) na mwenyekiti wa kamati ya michezo wa wilaya alisema kuwa serikali inaunga mkono suala la michezo kwani ni sehemu ya kutoa ajira kwa vijana.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha soka mkoa wa Pwani Robert Munisi alisema kuwa malengo ya kuanzisha kituo hicho na vingine kwenye kila wilaya itakuwa na vituo vitatu ambapo kutakuwa na vituo 21 kwa mkoa mzima ni kuibua vipaji na kuviendeleza.

Naye mratibu wa kituo hicho Abdulakarimu Alawi alisema kuwa jumla ya vijana 500 wa shule za msingi na sekondari ambapo vijana wanacheza kutegemeana na umri wao.

JAMII IMETAKIWA KUPANDA MITI KWENYE MIRADI ILI KUHIFADHI MAZINGIRA

 

Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Switbert Mkama ameitaka jamii kupanda miti kuzunguka maeneo yenye miradi ili kuhifadhi mazingira na kuifanya kuwa endelevu.

Amesema hayo alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa Mradi ya Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa Kutumia Mfumo Mfumo Ikolojia Vijijini (EBARR) katika Wilaya ya Kaskazini ‘A‘ Mkoa wa Kaskazini, Unguja - Zanzibar.

Akikagua visima, ujenzi wa majengo ya vituo vya wajasiriamali wa ufugaji, ushonaji, utengenezaji wa sabuni pamoja na vitalu nyumba katika Shehia za Jugakuu, Mbuyutende na Kijini, Dkt. Mkama amesema ameridhishwa hatua iliyofikiwa.

Aidha, aliwahimiza viongozi wakiwemo masheha wa shehia hizo ambazo zimefaidika na miradi ya visima kuwasimamia wananchi kupanda miti na kuimwagilia.

“Binafsi nimeridhishwa na namna mnavyosimamia miradi hii na nawapongeza masheha kwa kuisimamia na wananchi kwa kuipokea na kushiriki kikamilkfu katika kuitekeleza, niwaombe mhakikishe inaendelea kuwa na ubora ule ule,“ amesisitiza.

Kwa vile ujenzi wa majengo ya wajasiriamali wa ushonaji na uzalishaji wa sabuni utahusisha mashine na vifaa, Dkt. Mkama alisema ni muhimu kuwepo na mpango mkakati ili mradi uwe endelevu hata pale utakapokwisha muda wake.

Alisema vyerehani vitakavyotolewa pamoja na vifaa vingine vikiwemo taa na mabomba ya maji vitahitaji matengenezo madogo madogo na kulipiwa umeme hivyo wanajamii waangalie namna ya kuuhudumia bila kusubiri serikali.

Saturday, August 19, 2023

NYERERE SUPER CUP KUFANYIKA KIBITI NA RUFIJI KUANZA SEPT 23 MWAKA HUU

Katika kuelekea kumbukizi ya Miaka 23 ya kifo Cha Mwalimu Julius kambarage Nyerere na kuenzi FIKRA zake kwa vitendo Taasisi ya kumbukumbu ya mwalimu Julius Kambarage Nyerere Tarehe 19.8.2023 imefanya kikao cha maandalizi ya NYERERE SUPER CUP.

Wilaya ya Kibiti itashirikisha timu 6 Bungu Jaribu, Mtawanya, Kibiti, Mchukwi, na Dimani na Wilaya ya Rufiji timu 6 Ngorongo, Utete, Mgomba, Muhoro, Umwe na Mkongo.

Mashindano hayo yanatarajiwa kunaza Tarehe 23.9.2023 na kwisha 12.10.2023 tunashukuru 1.Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani 2.Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kibiti 3.Ofisi ya Mkuu wa Mkuu wa wilaya ya Rufiji 4.Ofisi ya Mbunge wa Kibiti na Rufiji 6.Madiwani wa Rufiji na Kibiti 7.Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani COREFA 8.Chama Cha Mpira wa Miguu Kibiti na Rufiji 9.Chuo Cha Afya St David college kimara 10. Mfuko wa NSSF Temboni na wadau wote kufanikisha Safari hii UZALENDO NI KULIPENDA TAIFA LAKO MITANO TENA

MNEC HAMOUD JUMAA ATAKA SUALA LA BANDARI RAIS ASISEMWE VIBAYA





MJUMBE wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) Hamoud Jumaa amevitaka baadhi ya vyama vya upinzani nchi kuacha kumsema vibaya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuhusu suala la mkataba wa Bandari badala yake watoe ushauri.

Jumaa aliyasema hayo Kata ya Mtambani Mlandizi Kibaha alipokuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa operesheni ya kuanza maandalizi ya uchaguzi ngazi ya serikali za vijini yenye kauli mbiu ya Simika Bendera.

Alisema kuwa anawashangaa wapinzani kutoa maneno mabaya kwa Rais kuhusu mkataba wa Bandari ambapo walipaswa kutoa ushauri na si kumsema vibaya.

"Suala la mkataba wa bandari ni jambo la msingi na Rais yuko makini na mkataba huo ili kuongeza mapato ya nchi na kama wao wanaona kuna jambo basi washauri na siyo kutoa maneno yasiyofaa,"alisema Jumaa.

Aidha alisema kuwa wanamshukuru Rais kwani ameonyesha uvumilivu mkubwa licha ya kusakamwa kuhusu suala la bandari ambalo mchakato wake bado unaendelea.

"Tumechoka kusikia Rais anasemwa vibaya yule ni kiongozi hivyo lazima aheshimiwe ila tunampongeza kwa ustaamilivu anaouonyesha kwani hawajibu licha ya kusemwa vibaya,"alisema Jumaa.

Aliwataka viongozi kuwajali viongozi wa ngazi za chini hususani mabalozi na viongozi wa mashina kwani wao ndiyo wako karibu na wanachama kwani ili kushinda uchaguzi kwani ndiyo malengo ya chama chochote.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Said Kanusu alisema kuwa anashangazwa na watu kutoa maneno kuwa eti bandari imeuzwa wapinzani wameishiwa hoja.

Kanusu alisema kuwa wananchi wawe na imani na wasikatishwe tamaa na wanaoleta hoja zisizo na msingi ajenda ya nchi ni kuleta maendeleo na miradi.

Naye Diwani wa Kata ya Mtambani Godfrey Mwafulilwa alisema kuwa kauli mbiu hiyo ni kuimarisha ngazi ya chini ya mabalozi kuwapa nguvu kwani wanakazi kubwa kukiimairisha chama.

Mwafulilwa alisema kuwa ngazi ya msingi sana ni balozi ambapo chama kinarudi chini ambako huko ndiko kwenye wanachama na hoja za wanachama na wananchi.

Alisema kuwa Rais ni mvumilivu na hawavutiwi na tabia inayofanywa na watu wanamchafua wao wanapaswa kuja na hoja na ushauri ila siyo kumchafua.