WADAU wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) Mkoani Pwani wameshauriwa jamii kuwalinda watoto ili kuepukana na vitendo vya ukatili.
Thursday, August 31, 2023
JAMII PWANI YATAKIWA KUWALINDA WATOTO ILI WAISHI KWENYE MAZINGIRA MAZURI
JAMII PWANI YATAKIWA KUWALINDA WATOTO ILI WAISHI KWENYE MAZINGIRA MAZURI
WADAU wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) Mkoani Pwani wameshauriwa jamii kuwalinda watoto ili kuepukana na vitendo vya ukatili.
CORECU LTD YASAIDIA CHANGAMOTO SHULE YA MSINGI MWENDAPOLE
CHAMA Cha Ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) LTD kitagharamia gharama za huduma ya maji kwenye Shule ya Msingi Mwendapole ili kukabiliana na changamoto ya maji shuleni hapo.
DIWANI KUIPSTIA SHULE PHOTOCOPY MASHINE
JAMII PWANI YATAKIWA KUWALINDA WATOTO ILI WAISHI KWENYE MAZINGIRA MAZURI
WADAU wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) Mkoani Pwani wameshauriwa jamii kuwalinda watoto ili kuepukana na vitendo vya ukatili.
Wednesday, August 30, 2023
TUME YASAJILI WATAALAMU 1,600
Mkurugenzi wa Tume ya TEHAMA Dkt. Nkundwe Mwasaga amesema hadi kufikia Juni 31 , 2023 imesajili wataalam wa TEHAMA 1,600 wanaohudumia nchi nzima na bado zoezi la usajili linaendelea.
Dkt.Mwasaga ameyasema hayo leo Jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa shughuli mbalimbali za TUME hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka wa fedha wa 2023/2024.
Akitaja Mafanikio kwa mwaka wa fedha 2023/24 amesema Tume imefanikiwa Kuanzishwa kwa mradi wa kujengwa kituo kikubwa cha Taifa cha Ubunifu Dar Es Salaam kwa ajili ya kutoa huduma kwa wataalam, watafiti, na wabunifu wa TEHAMA.
"Tunatengeneza mfumo jumuishi utakaounganisha usajili na uendelezaji wa wataalam na wabunifu TEHAMA nchini (ICT human capital development system): lengo la mfumo huu ni kutambua bunifu na kupanua wigo wa ukuzaji wa wabunifu na bidhaa na huduma za TEHAMA zinazozalishwa Tanzania na hivyo kukuza pato la Taifa na kuongeza fursa za ajira kupitia TEHAMA na maendeleo ya kidijitali duniani"Amesema Dkt.Mwasaga.
Aidha ameongeza kuwa wanaandaa mkutano wa mwaka wa TEHAMA (TAIC) na Tuzo ya TEHAMA Tanzania (Tanzania ICT Award)
"Hili lilikuwa kongamano kubwa la mwaka la TEHAMA lililofanyika Zanzibar mwezi Oktoba, 2022 na kuwashirikisha wawekezaji na wadau mbalimbali wa TEHAMA kutoka ndani na nje ya nchi wapatao 1,200"
Sanjari na hayo vipaumbele vya tume kwa mwaka 2023/24 ni pamoja na kuendelea na ukamilishwaji wa vituo vya ubunifu TEHAMA (Soft centers) katika Kanda 5 pamoja na kuanzisha kituo kimoja Zanzibar,kuanzisha kituo cha kutengeneza na kuboresha vifaa vya TEHAMA (ICT Refurbishment and Assembly centre),kuwezesha uanzishaji wa vituo vya majaribio vya ubunifu TEHAMA (District ICT Startups Innovation hubs) katika Wilaya 10,
Aidha vipaumbele vingine ni kufanya tafiti za maendeleo ya TEHAMA nchini na kufanya tathmini ya kitaifa ya hatua za utekelezaji wa mikakati mbalimbali ya TEHAMA,kuratibu na kuandaa matukio ya kuvutia uwekezaji na kutangaza masoko ya bidhaa za TEHAMA ndani na nje ya nchi,kushirikiana na washirika wa maendeleo na kampuni za kimataifa katika kuendeleza bunifu za TEHAMA ikiwemo kuwezesha utengenezaji wa bidhaa za TEHAMA hapa nchini pamoja na kujenga kituo cha Artificial Intelligence kwa ajili ya kuendeleza wataalam wa TEHAMA.
Kwa upande wake Msemaji Mkuu wa Serikali Ndugu Gerson Msigwa amesema Serikali imeamua kuwekeza kwa nguvu kwenye Tanzania ya Kidigitali chini ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambapo usimamizi m kuu unafanywa na Tume ya TEHAMA.
Ameongeza kuwa hili ni jambo kubwa kwani fedha nyingi imewekezwa kwa ajili ya kuboresha TEHAMA nchini kwani shughuli mbalimbali kwa sasa duniani zinafanyika kwa njia ya kidijitali ikiwemo huduma za malipo mabalimbali, huduma za afya za matibabu, uzalishaji, kilimo, uchimbaji wa madini.
Tuesday, August 29, 2023
PWANI YASHEREHEKEA USHINDI WA KWANZA NCHINI MKATABA WA LISHE
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI Mh. Angela Kairuki, akikabidhi Ngao ya Ushindi wa Kwanza kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mh. Abubakar Kunenge (katikati pichani) leo Agosti 29, 2023 kwa Mkoa wa Pwani kuibuka mshindi katika utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa mwaka 2022/23. Mwingine ni Katibu Tawala Mkoa huo na Skauti Mkuu wa Tanzania Rashid Mchata.
*Mkoa wa Pwani waongoza utekelezaji Mkataba wa Lishe kitaifa*
Mkoa wa Pwani umeongoza kwa kushika nafasi ya kwanza kwa tathmini ya Saba (7) ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa Mwaka 2022/2023.
Taarifa zilizotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa - (OR - TAMISEMI) zimeeleza kuwa Mkoa huo umefuatiwa na Lindi katika nafasi ya pili huku nafasi ya tatu ikienda kwa mkoa wa Iringa.
Kwa upande wa nafasi za Halmashauri, Mkoa wa Pwani umefanikiwa kuingiza halmashauri za Kibaha TC na Kibaha DC katika nafasi kumi za mwanzo.
Kibaha TC imekuwa ya na Kibaha DC ikiwa ni ya 10 huku hamashauri zingine za mkoa huo zikiwa zimeshika nafasi juu ya 100 za mwanzo.
Halamshauri hizo na nafasi zao kitaifa kwenye mabano ni Kisarawe (17), Rufiji (25), Bagamoyo (26) na Kibiti (54).
Zingine ni Chalinze (59), Mafia (91) na Mkuranga (93).
HIFADHI YA TAIFA KITULO KUTANGAZWA KITAIFA NA KIMATAIFA ILI KUVUTIA WATALII NA WAWEKEZAJI
Serikali imeendelea kujizatiti kwa kuitangaza Hifadhi ya Taifa ya Kitulo ndani na nje ya nchi lengo likiwa ni kuwavutia watalii na wawekezaji kutoka sehemu mbalimbali Duniani kupitia maonesho, matamasha na kwa njia ya kidijitali.
Kauli hiyo imesemwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Makete, Mhe. Festo Sanga aliyetaka kujua mkakati wa Serikali wa kuitangaza Hifadhi ya Taifa ya Kitulo.
Amefafanua kuwa hifadhi hiyo imekuwa ikitangazwa katika matamasha mbalimbali ya Karibu Kusini, Kilifair na Maonesho ya Kimataifa ya Sabasaba na Nanenane na kwa njia ya kidigitali, mitandao ya kijamii, majarida na Safari Channel.
Kufuatia hatua hiyo Serikali imeanza kuboresha miundombinu ndani ya hifadhi hiyo ikiwemo kufanya ujenzi wa nyumba tatu za malazi ya watalii na pia inatarajia na kujenga nyumba mbili na kambi moja ya kuweka hema katika mwaka huu wa fedha 2023/2024, pamoja na kukarabati miundombinu ya barabara.
Kuhusu utatuzi wa migogoro ya mipaka kati ya hifadhi hiyo na wananchi, Mhe. Masanja amesema tathmini ilishafanyika na kulielekeza Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kuweka vigingi katika maeneo ambayo yameshaainishwa.
Saturday, August 26, 2023
WANANCHI TUMIENI VITUO VYA MSAADA WA SHERIA KUSULUHISHA KESI ZA MADAI KUPITIA VITUO VYA MSAADA WA SHERIA-KPC
TUME YA TAIFA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA YAFADHILI MRADI UTAFITI CHANGAMOTO YA SOMO LA HISABATI
TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia imesema kuonekana na kuwepo kwa changamoto ya matokeo mabaya ya somo la hisabati katika matokeo ya Darasa la saba na kidato cha nne tume hiyo imefadhili mradi wa utafiti ili kugundua sababu ya tatizo hilo.
Hayo yameelezwa jijini hapa leo ,Agosti 25,2023 na Mkurugenzi Mkuu wa Tume hiyo Dkt.Amos Nungu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa shughuli na mafanikio ya tume hiyo.
Vilevile Dkt.Nungu ametaja baadhi ya shughuli zilizotekelezwa na Tume hiyo kuwa ni pamoja na kuibua na kufadhili miradi ya kimkakati ambayo tayari michakato yake imefanyika na sasa ipo katika hatua ya mikataba ambapo Serikali kupitia COSTECH imeidhinisha jumla ya miradi saba kwa thamani ya shilingi milioni 150 kila mradi.
Amesema Miradi hiyo itafanyika ndani ya miaka miwili na inahusisha watafiti na wabunifu kutoka sekta zote za umma na binafsi.
Aidha amesema kuwa Serikali kupitia COSTECH, imeidhinisha miradi miwili kwa thamani ya shilingi milioni 120 kila mradi ambapo utekelezaji wake pia unahusisha watafiti kutoka vyuo mbalimbali hapa nchini na itafanyika ndani ya miaka miwili, sasa ipo hatua ya kusaini mikataba.
Akizungumzia majukumu na vipaumbele vya tume hiyo kwa mwaka wa fedha 2023/24, Dkt.Nungu amesema kuwa Tume hiyo imeendelea kusimamia miradi inayoendelea ukiwemo wa Kigoda cha Utafiti katika SUA na NM-AIST ambao ni mradi wa miaka mitano, wenye thamani ya takribani shilingi bilioni 5 pamoja na kushirikiana na Mabaraza ya Kikanda na Kimataifa kuhakikisha tunashiriki kutafuta fursa ambazo zitaendelea kuleta fedha za utafiti kupitia COSTECH au kuhamasisha Taasisi za ndani kuomba hizo fursa.
Kukamilisha zoezi la ufadhili wa pamoja miradi ya utafiti wa Mabaraza ya Utafiti duniani ikiwa ni njia mojawapo ya kuongeza kuonekana kwa watafiti wetu na kuitangaza nchi yetu katika nyanja hii ya utafiti pamoja na kukamilisha mchakato na kutoa fedha kwa maandiko mawili kwa kutoa mrejesho kwa walioshiriki lakini wakakosa, na kuwatembelea walioshinda.
Vilevile, kupitia mradi wa HEET, tunaboresha mifumo mbalimbali ili kuongeza ufanisi zaidi katika suala la uratibu wa ume. Ikumbukwe kuwa mradi huu ni mahususi kwa Taasisi za Elimu ya Juu hivyo, inabidi tuwe tayari kuwahudumia baada ya kukamilisha mabadiliko wanayofanya kupitia mradi huo.
MAOFISA MANUNUZI WATAKIWA KUZINGATIA UKOMO MATUMIZI YA KEMIKALI
Serikali imewataka maafisa ununuzi na ugavi kuzingatia ukomo wa matumizi ya kemikali na vifaa vyenye kemikali ambazo zinamong’onyoa tabaka la ozoni au kuwa na athari kwa afya ya binadamu na mazingira.
Hayo yamebainishwa leo Ijumaa Agosti 25, 2023 Jijini Dodoma na Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Dkt. Switbert Mkama wakati akifungua warsha ya mafunzo kwa Maafisa ununuzi na ugavi kuhusu utekelezaji wa Itifaki ya Montreal inayohusu kemikali zinazomong’onyoa tabaka la ozoni.
Dkt. Mkama amesema mwanzoni mwa miaka ya 1970, wanasayansi walibaini baadhi ya kemikali zinazotengenezwa na binadamu ikiwemo majokofu, viyoyozi, vifaa vya kuzimia moto na utengenezaji wa magodoro vimejipenyeza angani na kumong'onyoa tabaka la hewa ya Ozoni na kusababisha madhara kwa afya ya binadamu na mazingira.
“Matokeo ya kumong’onyoka kwa Tabaka la Ozoni ni kuruhusu mionzi zaidi ya urujuani kufikia uso wa dunia ambayo husababisha madhara mbalimbali kwa afya ya binadamu na mazingira. Madhara hayo ni kama vile saratani ya ngozi, uharibifu wa macho unaosababisha upofu na athari kwa kwa ukuaji wa mimea na viumbe hai wengine” amesema Dkt. Mkama
Aidha Dkt. Mkama amesema matokeo ya uvumbuzi huo yalisababisha Shirika la Kimataifa linaloshughulikia Mazingira (UN Environment) kufanya tathmini ya kisayansi na kuamua kuchukua hatua madhubuti kulinda tabaka la Ozoni kwa kuanzisha Itifaki ya Montreal kuhusu udhibiti wa kemikali zinazomong'onyoa Tabaka la Ozoni iliyopitishwa mwaka 1987.
Akifafanua zaidi Dkt. Mkama amesema katika kutekeleza Itifaki hiyo, Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuandaa na kutekeleza Mpango wa Kuondosha Kemikali Zinazomong’onyoa Tabaka la Ozoni Jamii ya Hydrochlorofluorocarbons (HCFCs) ifikapo mwaka 2030 pamoja na Mpango wa utekelezaji wa Marekebisho ya Kigali ya kupunguza matumizi ya kemikali jamii ya hidrofluorokaboni.
“Chini ya Mipango hii mojawapo ya shughuli zinazotelekezwa na zinazopaswa kutekelezwa ni pamoja na kutoa mafunzo kwa maafisa ununuzi na ugavi kutoka katika Taasisi mbalimbali kukusu utekelezaji wa Itifaki husika ikiwemo utekelezaji wa Kanuni za Usimamizi wa Mazingira (Udhibiti wa Kemikali Zinazomong’onyoa Tabaka la Ozoni) za mwaka 2022” amesema Dkt. Mkama.
Dkt. Mkama amesema maafisa ununuzi na ugavi ni wahusika wakuu katika mchakato wa wa kushugulikia manunuzi ya vifaa mbalimbali katika ofisi za umma, hivyo wana wajibu mkubwa wa kutoa elimu ya Ozoni kwa wengine ili kuongeza juhudi za kuhifadhi Tabaka la Ozoni na kuokoa Maisha ya binadamu na viumbe hai.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Kemilembe Mutasa amesema katika kutekeleza Itifaki hiyo, Ofisi hiyo imeendelea kutoa mafunzo wa wadau mbalimbali wakiwemo maafisa ununuzi na ugavi kutoka katika Wizara mbalimbali kwa lengo la kuwajengea uelewa kuhusu matakwa ya Itifaki ya Montreal.
“Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania, Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Shirika la Viwango Tanzania na Vyuo mbalimbali vya Mafunzo ya Ufundi tumeendelea kutoa mafunzo kwa maafisa mbalimbali kuhusu usimamizi na udhibiti wa kemikali na vifaa vyenye kemikali zinazodhibitiwa chini ya Itifaki hii” amesema Kemilembe.
Friday, August 25, 2023
𝗖𝗕𝗪𝗦𝗢𝘀 𝗦𝗔𝗦𝗔 𝗞𝗨𝗧𝗨𝗠𝗜𝗔 𝗠𝗙𝗨𝗠𝗢 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗝𝗜𝗜𝗦
Vyombo vya Watumia Maji vya jamii (CBWSOs) vinavyosimamiwa na Wakala ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), vimetakiwa kutumia Mfumo wa pamoja wa Ankara za Maji (MAJIIS), ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi pamoja na kuimarisha utoaji wa huduma ya maji kwa wananchi.
Agizo hilo limetolewa hivi karibuni na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mhe. Kisare Makori, wakati akifunga mafunzo ya siku saba kwa Maafisa wa CBWSOs wa mkoa wa Kilimanjaro yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo cha USHIRIKA mjini Moshi .
Alisema, Serikali imedhamiria kuimarisha matumizi ya TEHAMA katika taasisi za umma ili kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi kwa urahisi, haraka na kwa gharama nafuu mahali walipo.
“Serikali ya awamu ya sita inachukua jitihada mbalimbali katika kuhakikisha TEHAMA inarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi, ambapo kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) kwa kushirikiana na Wizara ya Maji, imetengeneza mfumo wa MAJIIS ili kutatua changamoto mbalimbali zilizokua zinaikabili Sekta ya Maji”, alisema.
Alifafanua kuwa, Serikali imewekeza katika mfumo huo hivyo ni jukumu la watumishi wa sekta ya Maji kufanya kazi ili kuhakikisha mfumo huo unakua mkombozi kwa wananchi.
Kwa upande wake mtaalamu wa TEHAMA kutoka Wizara ya Maji Mha. Masoud Almas alisema, mfumo wa MAJIIS umeboreshwa ili uweze kutumiwa na Vyombo vya Watumia Maji vya jamii (CBWSOs) vinavyotoa huduma vijijini ili kuhakikisha TEHAMA inarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi mahali walipo.
“Mkoa wa Kilimanjaro umekuwa ni mkoa wa kwanza kuanza kutumia mfumo huu wa MAJIIS kwa CBSWOs na Wizara itaendelea kuhakikisha CBSWOs zote katika mikoa mingine zinatumia mfumo huu ili kurahisisha utendaji kazi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi waishio vijijini” alisema.
Aliongeza kuwa, hadi sasa mfumo huo umeleta mafanikio makubwa kwa Wizara ya Maji ikiwa ni pamoja na kuongeza ukusanyaji wa mapato na kurahisiha upatikanaji wa taarifa za Mamlaka zote za Maji nchini.
“Hadi sasa, Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingiara za miji mikuu ya mikoa, miradi ya kitaifa, miji ya Wilaya na miji Midogo 87 Tanzania Bara na Zanzibar pamoja na Bodi za Maji za Mabonde 9 zinatumia Mfumo huu wa Pamoja”, alifafanua Almas.
Aidha, alibainisha kuwa ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi, mfumo wa MAJIIS umeunganishwa na mifumo mingine ya Serikali ikiwa ni pamoja na mfumo wa GePG, Mfumo wa Barua Pepe Serikalini (GMS), Mfumo wa Ujumbe Mfupi wa Simu za mkononi ambao hutumika kutoa taarifa za huduma kwa Wateja ikiwemo kutuma bili, mfumo wa NIDA na mfumo wa BRELA.
Jumla ya washiriki 72 kutoka Vyombo vya Watumia Maji vya jamii (CBWSOs) 39 vya mkoa wa Kilimanjaro walihudhuria mafunzo hayo.
JWT LATOA SIKU 7 WENYE MAVAZI YA JESHI KUYASALIMISHA
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetoa siku 7 za kusalimisha mavazi ya Jeshi kwa yeyote ambaye ana mavazi hayo iwe anavaa,kuuza au kwa wasanii kupanda nayo katika majukwaa ya utumbuizaji.
Hayo yametolewa na Luten Kanali Gaudentius Ilonda ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano makao makuu ya Jeshi (JWTZ) wakati akizungumza na wanahabari kuhusu katazo hilo na ukikwajji wa Sheria ya uvaaji wa mavazi hayo Jijini Dodoma
Aidha Luteni Kanali Ilonda amesema kuwa mavazi yanayokatazwa na Jeshi ni pamoja na kombati (vazi la mabaka), Makoti,Tisheti, Kofia,Viatu kwa mujibu wa sheria mbalimbali kama anavyoelezea.
Kwa upande wake msemaji Mkuu wa Serikali na Mkurugenzi wa idara ya habari maelezo Bwana Gerson Msigwa amewaomba wazazi na walezi kuwakagua watoto wao ili kama Wana sale za Jeshi wazizuie na kusalimisha.
BILIONI 858.5 ZAIDHINISHWA BARABARA ZA WILAYA NCHINI
Katika mwaka wa fedha 2023/24, jumla ya barabara zenye urefu wa km 21,057.06 zitafanyiwa matengenezo, km 427 zitajengwa kwa kiwango cha lami, km 8,775.62 zitajengwa kwa kiwango cha changarawe, madaraja na makalavati 855 yatajengwa pamoja na mifereji ya mvua km 70.
Aidha, Jumla ya Shilingi Bilioni 858.517 zimeidhinishwa kwa ajili ya ujenzi, ukarabati na matengenezo ya miundombinu ya barabara za Wilaya.
Taarifa hiyo imetolewa leo 24.8.2023 Jijini Dodoma na Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seif wakati akizungumza ba waandishi wa Habari kuhusu utekelezaji wa Majukumu na mwelekeo wake katika mwaka wa fedha 2023/24.
Mhandisi Victor,amesema Kati ya fedha hizo, shilingi Bilioni 710.31 ni fedha za ndani na shilingi Bilioni 148.207 ni fedha za nje kupitia miradi ya RISE, TACTIC, Bonde la mto Msimbazi na Mradi wa Agri connect.
Pia amebainisha Madaraja hayo yamejengwa katika mikoa ya Kigoma 92, Singida 24, Tabora 5, Kilimanjaro 10, Mbeya 2, Arusha 6, Morogoro 2, Rukwa 3, Pwani 1, Ruvuma 3 na Iringa 15.
Kwa Upande wake Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema TARURA imeanzishwa mwaka 2017 lengo likiwa ni kupanua mawanda ya namna ambavyo tutawahudumia Watanzania kwa kuwaboreshea barabara.
KPC YAWAASA WANAFUNZI KIBAHA KUZINGATIA MAADILI
WANAFUNZI Wilayani Kibaha Mkoani Pwani wametakiwa kuzingatia maadili wanayofundishwa shuleni na kutojiingiza kwenye vitendo viovu vya utovu wa nidhamu.
Thursday, August 24, 2023
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS NYERERE YATOA MSAADA WA WHEEL CHAIRS NA VITI.
TAASISI ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mkoa wa Pwani imetoa viti mwendo kwa wanafunzi wawili wenye ulemavu wanaosoma Shule ya Msingi Muungano iliyopo Wilayani Kibaha.
WAENEZI WATAKIWA KUSEMEA MIRADI UTEKELEZAJI ILANI YA CCM
WAENEZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya za Mkoa wa Pwani wametakiwa kuisemea miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya chama.
Wednesday, August 23, 2023
KPC WAJADILI MAREKEBISHO YA BAADHI YA SHERIA
KITUO cha Msaada wa Sheria Kibaha (KPC) kimefurahishwa na marekebisho ya baadhi ya sheria yaliyofanyika kati ya mwaka 2019-2023 ikiwemo ya uendeshaji wa mirathi ambapo imeongeza adhabu kwa msimamizi wa mirathi anaposhindwa kutimiza wajibu wake kutoka shilingi 2,000 hadi milioni 2.
Tuesday, August 22, 2023
MAKAM WA RAIS DK MPANGO ATAKA WAKUU WA MIKOA KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI
MAKAMU wa Rais wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Philip Mpango ameitaka mikoa nchini kushirikiana na sekta binafsi ikiwemo mabaraza ya biashara ya mikoa na kutowatumia wakati wa kuomba michango ya shughuli za maendeleo.
Sunday, August 20, 2023
NYERERE SUPER CUP KUANZA KUTIMUA VUMBI TAREHE 23.9.2023
Katika kundeleza FIKRA za mwasisi wetu wa Taifa Mwalimu Nyerere Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ikiongozwa na Katibu wa Taasisi hiyo Ndugu Omary Punzi Tarehe 20.8.2023 imefanya Hitimisho la kikao Cha maandalizi ya Mashindano ya NYERERE SUPER CUP yatakaotimua vumbi Tarehe 23.9.2023 na kutamatika 12.10.2023.Mashindano hayo yatashirikisha Wilaya Mbili wilaya ya KIBITI na RUFIJI Kwa Timu 12 Timu sita kutoka kundi A (KIBITI)Timu shiriki Bungu,Jaribu,Mtawanya, Kibiti,Mchukwi,Dimani,na upande wa kundi B Rufiji timu zinazoshiriki Ngorongo,Utete,.Mgomba, Muhoro,Umwe na Mkongo vikao hivyo vyote viwili Cha Tarehe 19.8.2023 na 20.8.2023 vilikuwa na agenda ya Kuandaa kanuni na ratiba ya kuanza Usajili wa wachezaji,wajumbe wote walikubaliana Dirisha la Usajili lifunguliwe tarehe 23.8.2023 na kuisha 13.8.2023 inatoa shukrani Kwa NSSF na Chuo Cha Afya St David college Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na wilaya ya Kibiti na Rufiji,Ofisi ya Mbunge Kibiti na Rufiji,Chama Cha Mpira KIBITI na RUFIJI
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE YATOA SHUKRANI KWA WADAU MAANDALIZI NYERERE SUPER CUP
Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani inatoa shukrani Kwa Viongozi wote mliofanikisha safari yetu ya maandalizi ya NYERERE SUPER CUP Taasisi inashukuru 1.Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani 2.ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kibiti na Rufiji 3.Ofisi ya Mbunge Kibiti na Rufiji 4.Chama Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani COREFA 5.Chama cha Mpira wilaya Kibiti na Rufiji 6.Mdhamini Nssf na St David college Chuo Cha Afya kimara temboni,Madiwani wa Kibiti na Rufiji kuruhusu Viongozi wao kuhudhuria kikao na washiriki waliohudhuria UZALENDO NI KULIPENDA TAIFA LAKO MITANO TENA
*LYIDENGE ATAKA WAFANYAKAZI WA MIRADI KUWA NA NIDHAMU*
Amebainisha hayo leo Agosti 20 alipotembela mradi huo wakati akizungumza na wafanyakazi hao kuona kama wana changamoto zozote za kiusalama.
SSP Lyidenge aliwaeleza wafanyakazi hao kuwa wameaminiwa na serikali kufanya kazi hivyo wanatakiwa kuwa waadilifu na wasijihusishe na vitendo vya kihalifu ikiwemo wizi wa vitendea kazi na kuwataka wawe walinzi wa kwanza wa vifaa hivyo.
Sambamba na hayo SSP Lyidenge aliwasihi viongozi wa mradi huo kuwa na mahusiano mazuri na wafanyakazi ikiwemo lugha nzuri yenye staha ili kuongeza hamasa ya utendaji na kufikia malengo ya mradi kwa wakati uliokusudiwa.
"Niwaombe viongozi kuwatia moyo na kuwa na lugha shawishi kwa mnao wasimamia ili mradi huu uweze kukamilika kwa wakati, lugha zisizo na staha huwavunja moyo watendaji na kujikuta ikiwapunguzia morali ya kujituma".
Sote tunatambua umuhimu wa mradi huu utakavyochochea maendeleo ya kiuchumi kwa kwa wakazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani na taifa kwa ujumla” alisema Lyidenge
CCM WAASWA KUFUATA UTARATIBU
WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani wanaotoa misaada na kufanya shughuli za maendeleo wametakiwa kufuata utaratibu ili kuepusha mkanganyiko na viongozi waliochaguliwa na wananchi.
COREFA YAZINDUA KITUO CHA SOKA KWA VIJANA KIBAHA
JAMII IMETAKIWA KUPANDA MITI KWENYE MIRADI ILI KUHIFADHI MAZINGIRA
Naibu Katibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Switbert Mkama ameitaka jamii kupanda miti kuzunguka maeneo yenye miradi ili kuhifadhi mazingira na kuifanya kuwa endelevu.
Amesema hayo alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji wa Mradi ya Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa Kutumia Mfumo Mfumo Ikolojia Vijijini (EBARR) katika Wilaya ya Kaskazini ‘A‘ Mkoa wa Kaskazini, Unguja - Zanzibar.
Akikagua visima, ujenzi wa majengo ya vituo vya wajasiriamali wa ufugaji, ushonaji, utengenezaji wa sabuni pamoja na vitalu nyumba katika Shehia za Jugakuu, Mbuyutende na Kijini, Dkt. Mkama amesema ameridhishwa hatua iliyofikiwa.
Aidha, aliwahimiza viongozi wakiwemo masheha wa shehia hizo ambazo zimefaidika na miradi ya visima kuwasimamia wananchi kupanda miti na kuimwagilia.
“Binafsi nimeridhishwa na namna mnavyosimamia miradi hii na nawapongeza masheha kwa kuisimamia na wananchi kwa kuipokea na kushiriki kikamilkfu katika kuitekeleza, niwaombe mhakikishe inaendelea kuwa na ubora ule ule,“ amesisitiza.
Kwa vile ujenzi wa majengo ya wajasiriamali wa ushonaji na uzalishaji wa sabuni utahusisha mashine na vifaa, Dkt. Mkama alisema ni muhimu kuwepo na mpango mkakati ili mradi uwe endelevu hata pale utakapokwisha muda wake.
Alisema vyerehani vitakavyotolewa pamoja na vifaa vingine vikiwemo taa na mabomba ya maji vitahitaji matengenezo madogo madogo na kulipiwa umeme hivyo wanajamii waangalie namna ya kuuhudumia bila kusubiri serikali.
Saturday, August 19, 2023
NYERERE SUPER CUP KUFANYIKA KIBITI NA RUFIJI KUANZA SEPT 23 MWAKA HUU
Katika kuelekea kumbukizi ya Miaka 23 ya kifo Cha Mwalimu Julius kambarage Nyerere na kuenzi FIKRA zake kwa vitendo Taasisi ya kumbukumbu ya mwalimu Julius Kambarage Nyerere Tarehe 19.8.2023 imefanya kikao cha maandalizi ya NYERERE SUPER CUP.
Wilaya ya Kibiti itashirikisha timu 6 Bungu Jaribu, Mtawanya, Kibiti, Mchukwi, na Dimani na Wilaya ya Rufiji timu 6 Ngorongo, Utete, Mgomba, Muhoro, Umwe na Mkongo.
Mashindano hayo yanatarajiwa kunaza Tarehe 23.9.2023 na kwisha 12.10.2023 tunashukuru 1.Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani 2.Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kibiti 3.Ofisi ya Mkuu wa Mkuu wa wilaya ya Rufiji 4.Ofisi ya Mbunge wa Kibiti na Rufiji 6.Madiwani wa Rufiji na Kibiti 7.Chama Cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani COREFA 8.Chama Cha Mpira wa Miguu Kibiti na Rufiji 9.Chuo Cha Afya St David college kimara 10. Mfuko wa NSSF Temboni na wadau wote kufanikisha Safari hii UZALENDO NI KULIPENDA TAIFA LAKO MITANO TENA
MNEC HAMOUD JUMAA ATAKA SUALA LA BANDARI RAIS ASISEMWE VIBAYA
MJUMBE wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) Hamoud Jumaa amevitaka baadhi ya vyama vya upinzani nchi kuacha kumsema vibaya Rais Dk Samia Suluhu Hassan kuhusu suala la mkataba wa Bandari badala yake watoe ushauri.