Aidha itahakikisha Tanzania kuwa kitovu cha uzalishaji wa mbolea kwa nchi za afrika mashariki na nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
Hayo ameyasema Leo july 17, 2023 Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya udhibiti wa mbolea Tanzania(TFRA) Dkt. Stephan Ngailo wakati akieleza utekelezaji wa majukumu ya mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa mwaka wa fedha 2023/24
Dkt Ngailo amesema Kilimo ni biashara ambapo amebainisha kuwa Mamlaka hiyo itahakikisha ajenda na maono hayo yanafikiwa kwa kuimarisha upatikanaji na usambazaji wa mbolea bora kwa wakati na kwa bei himilivu.
Alisema lengo la sera ni kuendeleza sekta ya kilimo yenye ufanisi, ushindani na faida Hivyo kuboresha maisha ya Watanzania na kufikia ukuaji mpana wa uchumi na kupunguza
umaskini
Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) ni taasisi iliyo chini ya Wizara ya Kilimo, Sheria ya Mbolea Namba 9 ya Mwaka 2009 (Fertilizer Act, 2009) na kanuni zake za Mwaka 2011,TFRA ilianza kutekeleza majukumu yake mnamo Agosti 2012.
No comments:
Post a Comment