Na Manase Madelemu, Dodoma
MKUU wa mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamle amesema kuwa tofauti na maonesha ya miaka iliyopita ya nane nane mwaka huu 2023 yatahusisha matukio muhimu na makongamano yanayoongeza wigo wa uzalishaji bora.
Senyamule amesema hayo leo julai 31,2023 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Maadhimisho ya nane nane mwaka kikanda.
Amesema kutakuwa na makongamano ya tasnia ya alizeti,kongamano la zao la mtama ambapo mikoa ya Dodoma na singida ilikabidhiwa jukumu la kuzalisha alizeti Kwa wingi ili kupunguza nakisi ya mafuta ya kula nchini na hivyo kuokoa fedha za kigeni.
Aidha ameongeza kuwa kutakuwepo na siku maalumu ya uhamasishaji uzalishaji kuku wa kienyeji hasa katika mkoa wa Singida unafahamika katika mikoa mbalimbali hapa nchini hadi kufikia watu kuwaita kuku wa Singida
Pia Senyamule amesema kuwa Katika maonesho ya mwaka huu kutakuwa na huduma za Afya na matibabu ya kibingwa zitakazotolewa na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa na huduma hizi zitatolewa bure.
Kauli mbiu ya maonesha na sherehe za nane nane kitaifa Kwa mwaka 2023 ni Vijana na wanawake ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu ya Chakula"na kauli mbiu kikanda Kilimo ni Biashara, Biashara ni Uwekezaji.
No comments:
Post a Comment