WAANDISHI wa habari waula baada ya kuchaguliwa kwenye uchaguzi wa Chama Cha Soka Wilaya ya Kibaha (KIBAFA) ambapo Hassan Mtengefu amechaguliwa kuwa meneja wa habari wa chama hicho.
Chama hicho kimewateua waandishi hao ikiwa ni sehemu ya uundaji wa kamati mara baada ya uchaguzi mkuu wa chama hicho uliofanyika jana Mjini Kibaha.
Waandishi hao wameteuliwa kwenye kamati mbili ikiwemo ya nidhamu na maadili na kamati ya habari uhamasishaji na zawadi.
Ukiachilia mbali Mtengefu wengine ni Gustaph Haule aliyeteuliwa kwenye kamati ya nidhamu na maadili.
Wengine ni Mariam Songoro ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya habari uhamasishaji na zawadi huku wengine wakiwa ni Margareth Malisa, Ben Komba na John Gagarini ambao ni wajumbe.
No comments:
Post a Comment