Monday, July 3, 2023

WAZIRI MKUU MAJALIWA ATAKA UFAFANUZI KWA MAKATIBU WAKUU UNUNUZI WA MARUMARU TOKA NJE


Na. Wellu Mtaki Dodoma.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kassim Majaliwa amewaagiza makatibu wakuu kukaa ili kuweze kujua sababu za tiles za ndani hazitumiki mpaka wakandarasi wanaosimamia ujenzi wa majengo ya wizara wanaziagiza kutoka nje ya nchi.

Waziri mkuu ametoa agizo hilo leo Julai 3,2023 Jijini Dodoma wakati akikagua mradi wa ujenzi wa majengo ya ofisi za wizara na taasisi katika mji wa serikali Mtumba.

Amesema vipo viwanda vingi vya utengenezaji wa vifaa hivyo nchni maeneo ya Mkulanga, Chalinze na Mbagara hivyo ni lazima wajitahidi kutumia bidhaa za ndani ili kuongeza mzunguko wa fedha, dola wanayo ipeleka nje iweze kubakia.

“Tulitarajia viwanda vya ndani ndivyo vinapata haya malipo, watu wa TBS wamekataa bidhaa zetu? Wakatudhibitishia hizo za Uturuki na Ujerumani kwanza tunapoteza muda mwingi kusubulia bidhaa kutoka nje ya nchi tulitegemea viwanda vya ndani ndo viwe vianapata haya malipo, ”amesema Majaliwa.

Majaliwa amesema kama wanaona bidhaa zinazo zalishwa hazina ubora wawaambie waongeze ubora kuliko kuwaacha wanazalisha lakini hazitumiki na haziuziki ndani ya nchi, maana ya uwekezaji ambao Rais anautaka na unaonekana pamoja na kuwatia matumani wakiwekeza faida itapatikana.

Akitoa tadhmini kuhusu ujenzi wa maradi Waziri Mkuu amesema kazi zinaendelea vizuri, hivyo hawana budi kufuta mbinu sahihi ya kukamilisha ujenzi wa majengo na moja kati ya mbinu rahisi ni kufanya kazi usiku na mchana, pamoja na kuongeza wafanyakazi na kupeana zamu za usimamizi.

“Wakandarasi ndiyo wenye majukumu ya kusimamia kazi kufanyika usiku na mchana, simamieni ujenzi wa majengo ili muhakakikishe unakamilika kwa kiwango bora zaidi kinachohtajika ili magorofa yasije kuporomoka,”amesema.

Naye, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Jenista Mhagama amesema mbali na mradi wa ujenzi wa majengo ya wizara pia mradi mwingine unaotekelezwa katika eneo hilo ni ujenzi wa uwanja wa Mashujaa ambao utakuwa na mnara utakaoongoza kwa urefu barani Afrika. Mnara huo utakuwa na urefu wa mita 110.

Awali, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Dkt. Jim Yonazi alisema watahakikisha wanasimamia kikamilifu ujenzi wa mradi huo ili ukamilike kwa wakati na kwa viwango vinavyostahili. “Ifikapo Septemba 30, 2023 mradi huo utakuwa umekamilika.”

No comments:

Post a Comment