Friday, July 21, 2023

MKE WA MBUNGE AWAPIGA TAFU WASANII.

 


KATIKA kuhakikisha sanaa inakuwa Wilayani Kibaha mke wa Mbunge wa Kibaha Mjini Selina Koka ametoa kiasi cha shilingi milioni 1.2 ili kuendeleza sanaa hiyo kupitia Chama Cha Waigizaji Wilayani Kibaha humo.


Mke huyo wa Mbunge huyo alitoa fedha hizo wakati wa uzinduzi wa chama hicho uliofanyika Visiga Madafu wilayani humo.


Akikabidhi cheki ya fedha hizo aliwataka waigizaji hao kuzitumia fedha hizo kwa ajili ya kujiletea maendeleo yao na kukuza tasnia hiyo ya sanaa ambayo imekuwa na kuwa na maslahi mazuri.


Awali Rais wa chama hicho Dk Cynthia Henjewele alisema kuwa wasanii wanapaswa kuungana na kutumia fursa za mikopo kupitia mfuko wa utamaduni ambayo inatolewa kwa wasanii ambazo hazina riba.

No comments:

Post a Comment