KIBAFA INATISHA...ikiwa ni wiki mbili baada ya uongozi mpya wa chama cha soka wilaya ya Kibaha kuingia madarakani imeshuhudiwa viongozi wa chama hicho wakihudhuria mashindano ya soka la ufukweni maarufu kama "Beach soka"
Mashindano hayo yamefanyika Mlandizi yakiwa ni ya Mboya mbuzi SODO cup...
Katika mashindano hayo imeshudiwa viongozi kadhaa wapya wa KIBAFA wakihudhuria ambapo wameongozwa na mwenyekiti wa KIBAFA comrade Robert Munisi...makamu mwenyekiti bwana David Mramba...
Pia alikuwepo katibu msaidizi wa KIBAFA bwana Omary Abdul pamoja na wajumbe wa kamati tendaji ya KIBAFA bila kusahau mwenyekiti wa kamati ya Beach soka bwana Nassoro Shomvi
Katika hali ya kuonesha KIBAFA wapo kazini pia mbunge wa jimbo la Kibaha vijiijini mheshimiwa Michael Mwakamo alihudhuria mashindano hayo hali iliyoibua shangwe na vibe la aina yake kwa wakazi na mashabiki wa Beach soka waliojitokeza kutoka Mlandizi na Kibaha kwa ujumla...
Katika mashindano hayo timu ya Kilangalanga umeibuka mshindi wa fainali hiyo baada ya kuibamiza timu ya Msalabani goli 4-1 na kuifanya timu ya Kilangalanga kupata zawadi ya mbuzi mnyama huku mshindi wa pili na washiriki wengine nao wakijizolea zawadi lukuki....ambapo mshindi wa pili ambaye ni timu ya Msalabani wamepata zawadi ya kuku ndege....mfungaji bora akipata pesa taslimu elfu30,mchezaji bora wa mshindano sambamba na golikipa bora wakipata mche wa sabuni kila mmoja.
Katika nyakati mbalimbali mwenyekiti wa KIBAFA comrade Robert Munisi amekuwa akisikika akisema KIBAFA ya sasa ni kwa ajili ya kuhakikisha soka linachezwa Kibaha na kuhakikisha Kibaha inakuwa wilaya ya mfano kwa Tanzania nzima
No comments:
Post a Comment