Thursday, July 27, 2023

JWT YAVUTIWA UTALII UWEKEZAJI YAWATAKA WAFANYABIASHARA WAKAWEKEZE

 

KATIKA kuunga mkono jitihihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kutangaza utalii Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Pwani imetembelea vivutio vya utalii na kutambua fursa za uwekezaji zilizopo Wilayani Bagamoyo.

Akizungumza mara baada ya kutembelea vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji mwenyekiti wa Jwt Abdala Ndauka alisema kuwa baada ya ziara hiyo wameweza kutambua fursa mbalimbali kupitia utalii.

Ndauka alisema kuwa fursa kwa wafanyabiashara ni nyingi sana kwenye utalii pamoja na fursa nyingine kwenye sekta mbalimbali zikiwemo za utoaji huduma.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Majid Mhina alisema kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni maeneo mengi yanamilikiwa na watu binafsi.

Naye ofisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Magdalena Kitilla alisema kuwa kuhusu uwekezaji wametenga eneo lenye ukubwa wa hekta 9,800 ambalo linahitaji wawekezaji.

Kitilla alisema kuwa sekta ya utalii ina fursa nyingi ambapo kwenye sekta ya uvuvi kupitia uchumi wa buluu bado haujatumika ipasavyo ambapo kuna ufugaji wa vizimba baharini kunakofanyika ufugaji wa majongoo bahari ambapo ni mwekezaji ni mmoja tu.

Moja ya wafanyabiashara Fihiri Msangi alisema kuwa ziara hiyo wamejifunza mambo mengi ambayo watayafanyia kazi ili waangalie namna ya kuweza kuwekeza.

Msangi alisema kuwa fursa hizo watazitumia vizuri ili kuinua uchumi wa Mkoa huo ambao unategemea uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali na pia unauwekezaji mkubwa wa viwanda.

No comments:

Post a Comment