Saturday, July 1, 2023

MHE.MARY MASANJA ATEMBELEA OFISI ZA CCM MKOANI MWANZA

 


Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja leo ametembelea Ofisi za Chama cha Mapinduzi jijini Mwanza na kufanya mazungumzo na Katibu wa  CCM, Mkoa wa Mwanza Ndugu Omary Mtuwa.

Pia, alipata nafasi ya kuzungumza na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Ndugu Sixbert Reuben Jichabu.

Mhe. Masanja anatarajia kushiriki katika Harambee ya Kuchangia ujenzi wa Nyumba ya Ibada ya Kanisa la Pasiansi SDA jijini humo tarehe 1 Julai,2023.

No comments:

Post a Comment