Friday, June 30, 2023

KPC YATAKIWA KUPAMBANA NA VITENDO VYA UKATILI KWENYE JAMII



MJUMBE wa Kituo cha Msaada wa Kisheria Kibaha (KPC) Lydia Mgaya amekitaka kituo hicho kufuatilia baadhi ya matukio ya Ukatili kwa watoto na wanawake kwenye jamii ili wahusika wachukuliwe hatua.

Ameyasema hayo kwenye ofisi za KPC zilizopo Mjini Kibaha baada ya kuteuliwa kwenye nafasi hiyo ambapo amesema baadhi ya matukio yamekuwa yanashindwa kuendelea kutokana na kutokuwa na kutofuatiliwa.

Mgaya ambaye pia ni diwani wa viti maalumu amesema baadhi ya matukio likiwemo la binti mmoja ambaye ni mwanafunzi wa shule ya sekondari kubakwa na baba yake wa kambo tangu mwezi wa Aprili mwaka huu lakini haliendi kwa haraka hali inayoweza kusababisha kutofanikiwa.

"Nashukuru kwa kuniteua kwenye nafasi hii nawapongeza kwani kuna tukio nilileta kwenu sasa liko mahakamani nataka na hili lifuatiliwe ili liende kwenye utaratibu ili muhusika achukuliwe hatua na mtoto apate haki yake,"alisema Mgaya.

Alisema kuwa tukio lingine ni mtoto kupigwa na mjomba wake baba kampiga na kumjeruhi mwanae hivyo kituo hicho kina nafasi kubwa ya kuzifuatilia kesi hizo ili ziende kwa utaratibu mzuri kwani wanaofanyiwa hawana sauti.

Naye meneja wa kituo hicho Dismas Chihwalo amesema kuwa katika kuhakikisha vitendo vya ukatili vinapungua ndani ya jamii wanatoa elimu na msaada wa sheria kwa viongozi wa kata, mitaa, wanafunzi na wananchi.

Chihwalo amesema kwa sasa mwamko wa jamii kuripoti matukio umekuwa ni mkubwa tofauti na zamani baada ya kupatiwa elimu ya sheria na msaada wa sheria ambapo watu walikuwa hawatoi taarifa yanaporokea matukio ya ukatili kwenye jamii.

No comments:

Post a Comment