Tuesday, June 27, 2023

JAMII YAASWA KUWEKEZA UJUZI KWA WATOTO



Jamii imeaswa kuwekeza zaidi kwenye  kuongeza ujuzi wa malezi makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto ili kuwa na Taifa lenye raia wenye misingi imara katika nyanja zote.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mwanaid Ali Khamis wakati akifungua Mafunzo  ya kitaifa ya Sayansi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto kwa Wadau kutoka mikoa 16 Nchini pamoja na Wizaraa za kisekta ,Mkoani Dodoma, Juni 26, 2023.

“Mafunzo haya yasiishie tu maofisini bali yafike hadi ngazi za Vijiji kwani huko watu huchelewa kupata taarifa za mambo ya msingi. Mnatakiwa mshuke kwa wananchi wa ngazi za chini kwani  Malezi ya awali ni ya muhimu sana katika makuzi ya mtoto”Alisema Mwanaidi.

Akielezea lengo la Mafunzo hayo Naibu katibu Mkuu  kutoka  Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Wakili Amon Mpanju amesema  mafunzo hayo ni muhimukwaajili  yakuwaongezea ujuzi Wataalam husika ili waweze kutekeleza Majukumu yao kama inavyostahili

“Lengo la mafunzo haya ni kuwajengea uwezo bobezi ili waweze kutekeleza inavyostahili,  kwani mafunzo haya yanatolewa na chuo cha Aga khan ambacho kina Mamlaka ya kutoa mafunzo hisika" amefafanua Mpanju

Akiongea wakati wa Mafunzo hayo Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mtoto kutoka Wizra ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Waanwake na Makundi Maalum, Sebastian Kitiku,  amesema Wizara itaendelea kushirikiana  kwa karibu na wadau wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Mtoto ili kuhakikisha kuna mazingira salama ya ustawi na Maendeleo ya Watoto Nchini.

Naye mshiriki Tedson Ngwale ambaye ni Afisa Maendeleo kutokea Shinyanga ameishukuru Serikali kwa jitihada hizo za kuhakikisha inaanda mazingira salama kwa watoto kwa kutoa mafunzo hayo kwa maafisa maaendeleo na Ustawi wa Jamii.

“Tuna ahidi kuitendea haki Serikai kupitia Mafunzo haya  kwa kutekeleza kama tulivyoelekezwa na kama ilivyokusudiwa kwa kuwafikia Wananchi wa ngazi zote hasa vijijini ambako kuna changamoto zaidi”.

No comments:

Post a Comment