Friday, June 9, 2023

WADHAMINI WA MICHEZO WATAKIWA KUBORESHA ZAWADI ZA WASHINDI




WADHAMINI wa Michezo Mkoani Pwani wametakiwa kutoa zawadi ambazo zitakuwa kumbukumbu kwa washindi wa michezo mbalimbali ili kuleta hamasa kwa vijana kushiriki kwenye michezo.

Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na  mdhamini wa mashindano ya Umoja wa Michezo Sanaa kwa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) Mkoa wa Pwani Musa Mansour na kwa kuwa michezo ni ajira wadhamini waangalie kwa kuboresha upande wa zawadi ili ziwe kivutio.

Mansour alisema kuwa ili vijana wafikie malengo ya kuwa wachezaji bora na kufanikiwa lazima wawe na nidhamu ambapo kwa sasa michezo inawaletea maisha mazuri wachezaji na mamlaka husika ziboreshe viwanja na kuwapatia vifaa vya michezo na kuboresha maeneo ya wazi.

Naye ofisa michezo wa mkoa huo Grace Bureta alisema kuwa jumla ya wachezaji 120 wamechaguliwa kuunda timu ya  Mkoa ambayo itashiriki mashindano ya Taifa yatakayofanyika  mkoani Tabora ambapo timu hiyo imeiingia kambini kwenye shule ya sekondari Kibaha.





No comments:

Post a Comment