MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge leo Juni 15, 2023 amezindua Mpango wa Usafiri wa Dharura kwa Mama Wajawazito, Wanawake waliojifungua na Watoto Wachanga ujulikanao kama M-Mama.
Akizindua Mpango huo katika Ukumbi wa Baraza la wakunga na uuguzi Kibaha, Hafla iliyohudhuriwa na Viongozi wote wa Mkoa huo Kunenge amesema:- M -Mama ni Mpango ambao Mhe Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameanzisha ili kuokoa maisha ya Mama na Mtoto. Hivyo amewataka Viongozi wote wa Mkoa Kuweka kipaumbele na kuhakisha inafanikiwa.
Ameeleza mpango huo unaendea sambamba na lishe, Kuhudhuria kliniki na wakati wa kujifungua kuwahi kituo cha afya kwa wamama Wajawazito na Watoto."Mpango huo ni mnyororo wa thamani wa uzazi" Ameeleza Kunenge.
Amewataka Viongozi wote wa Mkoa wa kuhakikisha M Mama inafanikiwa. "Suala hili liingizwe kwenye viashiria vya upimaji utendaji kazi wa Watumishi kila mmoja kwenye eneo lake ambapo kila mtu atapimwa navyo" amesema Kunenge.
No comments:
Post a Comment