Friday, June 2, 2023

AHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA KWA KUUA WATOTO WAKE WATATU KWA KUWANYWESHA SUMU

MKULIMA na mkazi wa Ditere Wilaya ya Kipolisi Chalinze Mkoani Pwani Salehe Masokola amehukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kuwaua watoto wake watatu kwa kuwanywesha sumu.

Watoto hao watatu waliouwawa kwa kunyweshwa sumu ni Sheila Masokola (8), Nurdin Masokola (6) na Sabrati Masokola miezi (6).

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani (ACP) Muhudhwari Msuya alisema kuwa mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo Novemba 26 mwaka 2018 baada ya kutoelewana na mke wake.

Msuya alisema kuwa baada ya kutengana mkewe aliondoka na watoto ambapo aliwafuata watoto wake kwa mama yao na kurudi nao nyumbani kwake ambapo alitekeleza mauaji hayo baada ya mkewe kugoma kurudi nyumbani ili waendelee kuishi.

Alisema kuwa baada ya kutekeleza mauaji hayo alikamatwa na kesi kufunguliwa kwenye kituo cha polisi Chalinze ambapo upelelezi ulifanyika na kupatikana na hatia na kuhukumiwa hadi kufa hukumu na Jaji wa Mahakama Kuu Elizabeth Mkwizu.

No comments:

Post a Comment