Saturday, July 29, 2023

PINDA KUZINDUA MAONYESHO NANE NANE KANDA YA MASHARIKI

 

WAZIRI Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya wakulima nane nane Kanda ya Mashariki Mkoani Morogoro Agosti Mosi mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maonyesho hayo yanashirikisha mikoa minne ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga na Morogoro.

Kunenge amesema kuwa hadi sasa tayari washiriki 589 wamejiandikisha kushiriki maonyesho hayo ambapo ni ongezeko la asilimia 22 ikilinganishwa na mwaka jana ambapo washiriki walikuwa 476.

Amesema kuwa maonyesho hayo ni ya 30 tangu kufanyika kwa kanda hiyo ya Mashariki ambapo kauli mbiu inasema Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula.

Aidha amesema kuwa wakulima na wananchi wanakaribishwa kujitokeza kwa wingi ili kujifunza teknolojia za kisasa kwenye sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi.

No comments:

Post a Comment