Wednesday, July 19, 2023

TCRA KUENDELEA KUSIMAMIA SEKTA YA MAWASILIANO

MAMLAKA ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema inaendelea kusimamia Sekta ya Mawasiliano kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika ngazi ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa ili kuhakikisha Sekta ya Mawasiliano inatoa mchango katika maendeleo ya nchi na kuwa kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa kidijiti na uchumi wa buluu.

Hayo ameyasema Mkurugezi Mtendaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Dkt. Jabiri Bakari wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini dodoma kuhusu taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya TCRA 2022/23 na Mpango kazi 2023/24.

Dkt,Jabiri amesema Takwimu zinaonesha kuwa wastani wa bei ya dakika ndani ya Mitandao bila kifurushi zinaendelea kushuka na  Mwenendo wa gharama za upigaji wa simu nje ya kifurushi zimeendelea kushuka hivyo kwa gharama za mwingiliano kumepelekea kuwa na tofauti ndogo sana ya gharama za kupiga simu ndani na nje ya mtandao.

Aidha, Dkt Jabiri ametoa rai kwa Vyombo vya utangazaji kuendelea kuzingatia sheria, kanuni na weledi katika kutoa maudhui, vilevile kwa wananchi kutosambaza maudhui ambayo yanakiuka misingi ya sheria, mila na desturi za Taifa la Tanzania. 

TCRA ilianzishwa chini ya Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Namba 12 ya mwaka 2003 baada ya kuunganishwa kwa iliyokuwa Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC) na Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC). TCRA ilianza kutekeleza majukumu yake tarehe 1 Novemba 2003.

No comments:

Post a Comment