Friday, July 21, 2023

WANANCHI WATAKIWA KULIPA ANKARA ZA MAJI NA KULINDA MAZINGIRA


Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya maji Safi na usafi wa Mazingira Bunda BUWSSA Bi Ester Gilyoma ametoa wito kwa wananchi wa Halmashauri ya Bunda iliopo Mkoani Mara kwa wale wanaotumia maji ya BUWSSA kuacha tabia ya wizi wa maji na badala yake wahakikishe wanalipa Ankara za maji, sambamba na utunzaji wa vyanzo na miundombinu ya maji katika Halmashauri hiyo.

Bi Ester ametoa wito huo  Jijini Dodoma katika mkutano wake na Wana habari wakati akielezea utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa mwaka wa fedha 2023/2024.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema kuwa hapo awali kulikuwa na changamoto kwa wakazi wa Bunda kwa kupata maji yasiyo Safi na salama ambapo kwasasa ndani ya uongozi wa Raisi wa awamu ya sita ya Dkt Samia Suluhu Hassan Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya maji ikiwemo chujuo la kuchuja na kutibu maji hivyo maji machafu Bunda Sasa basi.

Pia amesema wanaendelea na jitihada za kupunguza au kuondoka kabisa changamoto za upotevu wa maji ikiwa ni pamoja kuwepo kwa Mpango wa kubadili mita goigoi kwani kwa mwaka wa Jana upotevu ulikuwa asiliamia 45,lakini mpaka Sasa upotevu umeendelea kupungua mpaka asiliamia 36.

No comments:

Post a Comment