Monday, July 17, 2023

PPRA YAWATAKA WADAU WAKE KUZINGATIA MAADILI

MAMLAKA ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imewataka wanaojihusisha na Ununuzi wa Umma ikiwemo watumishi wa Umma na wazabuni kuzingatia maadili katika utendaji wao.

Aidha Mamlaka haitasita kuwachukulia hatua kwa mujibu wa Sheria wale wote watakaokiuka taratibu au watakajihusisha na kuisababi utakaoisababishia hasara serikali.

Hayo ameyasema Leo July 17 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma Eliakim Maswi wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini dodoma kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya PPRA na mwelekeo wa utekelezaji wa Mwaka wa fedha 2023/24.
      
Maswi amesema Ununuzi wa Umma unakabiliwa na hatari kubwa ya rushwa ambapo watendaji na maafisa serikalini wamekuwa wakilalamikiwa na kuhisiwa kuwa wanajihusishwa na vitendo vya rushwa kwa kutoa mikataba na kuwapa faida zisizo halali wazabuni wasiyo na sifa.

Amesema serikali inaendelea kudhibiti matumizi ya fedha za umma kwa kutumia njia mbalimbali ikiwemo mifumo ya kielektroniki Ili kuleta tija na ufanisi unaostahili katika utekelezaji wa bajeti husika.         

Katika Mwaka wa fedha 2023/24 Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma  imetenga shillingi billion 40.4 kwa ajili ya utekelezaji wa Majukumu yake ambapo kiasi cha shilling billion 20 ni kwa ajili ya uendeshaji na ukaguzi wa taasisi  nunuzi pamoja na ujengwaji wa uwezo wa watumishi.

No comments:

Post a Comment