Halmashauri kuu ya ccm Taifa ( NEC) imepokea na kujadili kwa kina taarifa ya makubaliano ya Uwekezaji na uendeshaji wa bandari na kuazimia kwamba Uwekezaji na uendeshaji wa bandari hiyo ni kwa manufaa ya uchumi wa Nchi pamoja na utekelezaji wa vitendo vya Ilani ya CCM ya Mwaka 2020 - 2025.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma katibu wa Halmashauri kuu ya Ccm Itikadi na Uenezi Bi Sofia Mjema amesema halmashauri kuu ya Ccm imekutana Katika kikao Chake Cha kawaida chini ya mwenyekiti wa Ccm na RAIS wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hasani.
Mjema amesema kikao hicho kimeazimia kwamba serikali iongeze kasi ya kutoa Elimu kwa wananchi juu ya uhalisia uliomo Katika makubaliano ya Uwekezaji na uendeshaji wa bandari.
No comments:
Post a Comment