SHIRIKA la Maendeleo ya Vijana (YPC) la Kibaha Mkoani Pwani limeingia mkataba wa miaka mitatu na Shirika la The Civil Society (FCS) chini ya udhamini wa Jumuiya ya Ulaya (EU) wa kutoa elimu Utawala wa Kidemokrasia kupitia mradi wa Uraia Wetu.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha Mkurugenzi wa YPC Israel Ilunde amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kwenye mikoa minne ya Kanda ya Mashariki.
Ilunde amesema kuwa mradi huo una lengo la kuendeleza mazingira wezeshi kwa ajili ya utawala wa kidemokrasia nchini ambapo kwa kanda ya mashariki ni mikoa ya Pwani, Dar es Salaam, Lindi na Morogoro.
Amesema kuwa mradi utawezesha majadiliano kati ya serikali na azaki kwa ajili ya uchechemuzi (ushawishi na utetezi) wa masuala wa kidemokrasia, maendeleo na kuboresha mahusiano na ushirikiano wa kikazi.
Aidha amesema kuwa mradi utatoa fursa wa azaki kujengewa uwezo kujiendesha kupitia shughuli zao ili kuwanufaisha wananchi wa kanda hiyo na Watanzania kwa ujumla.
No comments:
Post a Comment