Tuesday, February 26, 2013

AKUTWA AMEFIA GESTI

Na Mwandishi Wetu, Kibaha
MWILI wa mfanyabiashara wa Jijini Dar es Salaam Ambrose Mapunda anayekadiriwa kuwa na umri kati (50) na (55) umekutwa chini ya uvungu wa nyumba ya kualala wageni huku ukiwa mtupu bila ya nguo.
Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ofisa upelelezi wa mkoa wa Pwani wa jeshi la polisi Juma Yusuph alisema kuwa tukio hilo lilitokea kwenye nyumba ya kulala wageni kwenye nyumba ya kulala wageni ya Cham Cham iliyopo wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.
Alisema tukio hilo lilitokea kati ya Fabruari 22 na 24 kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni huku ukiwa na jeraha kubwa kichwani huku shingo yake ikiwa imenyongwa.
“Marehemu alikutwa akiwa chini ya uvungu huku mwili wake ukiwa hauna nguo na jeraha huku ukiwa umenyongwa shingo ambapo mtu aliyehusika na tukio hilo hakuweza kufahamika mara moja,” alisema kamanda Yusuph.
Alibainisha kuwa marehemu hakukutwa na kitu chochote licha ya kuwa alifika kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni akiwa na begi kwenye chumba namba mbili.
“Ujumbe uliokutwa kwenye chumba hicho ulisema kuwa umenidhulumu tulikubaliana unilipe kiasi cha shilingi 20,000 lakini hujanilipa, ujumbe huu umeandaikwa na mtu asiyefahamika,” alisema Kamanda Yusuph.
Aidha alisema kuwa mhuduma na mlinzi wa nyumba hiyo ya kulala wageni wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi kuhusu tukio hilo na polisi wanaendelea na uchunguzi.
Mwisho.  

No comments:

Post a Comment