Monday, February 25, 2013

RAGE ACHANGIA TAWI LA SIMBA KIBAHA



Na John Gagarini, Kibaha
MWENYEKITI wa Klabu ya Simba Ismail Aden Rage ameendesha harambee kuchangia tawi la Simba Kwa Mfipa wilayani Kibaha mkoani Pwani kwa ajili ya shughuli mbalimbali ambapo alifanikisha kupatikana kwa kiasi cha shilingi 420,000.
Harambee hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki Kwa Mathias wilayani Kibaha kwenye ukumbi wa Back Yard ambapo mbali ya kuendesha harambee walijadili mambo mbali mbali ya kuisaidia klabu hiyo kufanikiwa kwenye mashindano mbalimbali.
Rage alitoa kiasi cha shilingi 100,000 ikiwa ishara ya kuanzisha harambee hiyo na kufuatiwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa NEC kutokea wilayani Kibaha Rugemalila Rutatina ambaye alitoa kiasi cha shilingi 100,000.
Kwa upande wake mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka yeye aliahidi kutoa kutoa kiasi cha shilingi 100,000 na wanachama, wapenzi na mashabiki wa timu hiyo nao walichangia fedha na kufikia kiasi hicho.
“Fedha hizi zilizochangwa zinapaswa kutumika kwa ajili ya malengo yaliyowekwa ikiwa ni pamoja na kufungua akaunti pamoja na mambo mbalimbali ya tawi,” alisema Rage.
Aliwataka wadau wa Simba kujitokeza kuisaidia timu yao ili kuhakikisha inafanikiwa kutetea ubingwa wake wa ligi kuu ya Voda Com ambao kwa sasa inaonekana kama imeuweka rehani baada ya kufungwa na Mtibwa Sugar ya Morogoro.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment