Friday, February 1, 2013

MWANAFUNZI ATOWEKA NYUMBANI BAADA YA KUFELI KIDATO CHA PILI




Na John Gagarini, Kibaha
MWANAFUNZI ambaye ni miongoni mwa wanafunzi waliofeli kidato cha pili mwaka jana kwenye shule ya sekondari ya Tumbi wilayani Kibaha mkoani Pwani Shaban Kihemele (16) ametoroka nyumbani kwa madai kuwa wanafunzi wenzake kumzomea kuwa amerudia darasa.
Akizungumza na waandishi wa habari hizi mjini Kibaha mzazi wa mtoto huyo Bw Shaban Kihemele alisema kuwa mwanae huyo huyo alitoroka Januari 24 mwaka huu na hadi leo hajaonekana licha ya jitihada za kumtafuta kushindwa kufua dafu.
Bw Kihemele alisema kuwa mwanae aliondoka nyumbani majira ya saa 4 asubuhi huku akiwa amevalia kaptura nyeusi ya Jeans iliyokatwa tisheti ya rangi ya zambarau yenye ufito mweupe kifuani na ndala nyekundu.
“Chanzo cha yeye kutoroka siku ya Januari 23 alimwambia mama yake kuwa kutokana na kufeli mtihani wa kidato cha pili ni vema wamwamishe shule kuliko kuendelea kusoma hapo kwani wanafunzi wanaomfahamu wanamzomea lakini mama yake alimwambia asubiri mimi nirudi kwani sikuwepo nilikuwa Bagamoyo kikazi,” alisema bw Kihemele.
Alisema mama yake alimjibu kuwa asubiri hadi nirudi lakini kesho yake alirudi kutoka shuleni na kubadilisha nguo huku majirani wakimwuliza kuwa ni kwanini amewahi kurudi na anakwenda wapi akawaambia yuko hapa hapa pia baba yake hajalipa ada hivyo amerudishwa.
“Alichukua fedha kiasi cha shilingi 20,000 kati ya shilingi 50,000 zilizokuwepo kasha akachukua na shuka kisha kuondoka kusikojulikana na inawezekana aliotoroka kutokana na kuona kuwa ni fedheha kurudia darasa na madai kuwa wenzake wanamzomea jambo ambalo linatushangaza,” alisema Bw Kihemele.
Aidha alisema siku ya kwanza walimsubiri hakutokea na ilipofika usiku walikwenda kutoa taarifa kituo cha polisi cha Maili Moja KMM/RB/108/2013 juu ya kutoonekana mtoto wao, walikwenda nyumbani kwao Bagamoyo lakini hawajaweza kufanikiwa kumwona pia waliwasiliana na ndugu zao wote lakini imeshindikana.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment