Na John Gagarini, Kibaha
MWANAFUNZI ambaye ni miongoni mwa wanafunzi waliofeli
kidato cha pili mwaka jana kwenye shule ya sekondari ya Tumbi wilayani Kibaha
mkoani Pwani Shaban Kihemele (16) ametoroka nyumbani kwa madai kuwa wanafunzi
wenzake kumzomea kuwa amerudia darasa.
Akizungumza na waandishi wa habari hizi mjini Kibaha
mzazi wa mtoto huyo Bw Shaban Kihemele alisema kuwa mwanae huyo huyo alitoroka
Januari 24 mwaka huu na hadi leo hajaonekana licha ya jitihada za kumtafuta
kushindwa kufua dafu.
Bw Kihemele alisema kuwa mwanae aliondoka nyumbani
majira ya saa 4 asubuhi huku akiwa amevalia kaptura nyeusi ya Jeans iliyokatwa
tisheti ya rangi ya zambarau yenye ufito mweupe kifuani na ndala nyekundu.
“Chanzo cha yeye kutoroka siku ya Januari 23
alimwambia mama yake kuwa kutokana na kufeli mtihani wa kidato cha pili ni vema
wamwamishe shule kuliko kuendelea kusoma hapo kwani wanafunzi wanaomfahamu
wanamzomea lakini mama yake alimwambia asubiri mimi nirudi kwani sikuwepo
nilikuwa Bagamoyo kikazi,” alisema bw Kihemele.
Alisema mama yake alimjibu kuwa asubiri hadi nirudi
lakini kesho yake alirudi kutoka shuleni na kubadilisha nguo huku majirani
wakimwuliza kuwa ni kwanini amewahi kurudi na anakwenda wapi akawaambia yuko
hapa hapa pia baba yake hajalipa ada hivyo amerudishwa.
“Alichukua fedha kiasi cha shilingi 20,000 kati ya
shilingi 50,000 zilizokuwepo kasha akachukua na shuka kisha kuondoka
kusikojulikana na inawezekana aliotoroka kutokana na kuona kuwa ni fedheha
kurudia darasa na madai kuwa wenzake wanamzomea jambo ambalo linatushangaza,”
alisema Bw Kihemele.
Aidha alisema siku ya kwanza walimsubiri hakutokea na
ilipofika usiku walikwenda kutoa taarifa kituo cha polisi cha Maili Moja
KMM/RB/108/2013 juu ya kutoonekana mtoto wao, walikwenda nyumbani kwao Bagamoyo
lakini hawajaweza kufanikiwa kumwona pia waliwasiliana na ndugu zao wote lakini
imeshindikana.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment