Saturday, February 16, 2013

STORY PWANI



Na John Gagarini, Mkuranga
IMEELEZWA kuwa kuishi mbali na vituo vyao vya kazi kwa baadhi ya maofisa
ugani kwenye vijiji wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani kumechangia kudumaza
shughuli za kilimo wilayani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mafunzo kwenye kijiji cha
Msufini kata ya Mbezi, mratibu wa mradi wa Wajibu wa Jamii Katika Usimamizi
wa Rasilimali za Umma za Sekta ya Kilimo wilaya hiyo (POCUSO), Bw Said
Gwaja alisema kuwa maofisa hao wamekuwa hawafiki kwenye vijiji
walivyopangiwa.

Bw Gwaja alisema kuwa kutokana na kuishi mbali na vituo vyao vya kazi
wamekuwa wakiishia ofisini na kushindwa kwenda kwenye maoeneo waliyopangiwa
hasa yale ya vijijini.

“Ni vema wangekaa kwenye maeneo yao ya kazi ili iwe rahisi kwao kutoa
huduma kwa wakulima ambao wanakosa fursa nyingi kutokana na kutofahamishwa
namna ya kuweza kuzipata,” alisema Bw Gwaja.

Alisema kuwa fursa ambazo wakulima walipaswa kuzijua zinashindwa kuwafikia
kwani wanazipata wakati muda wa kilimo unakuwa umepita hivyo kushindwa kupata pembejeo za ruzuku kwa wakati muafaka.
Aidha alisema kuwa endapo wangekuwa wanafanya kazi kwenye maeneo waliyopangiwa hususani vijijini ingekuwa raisi kwao kujua chanagamoto zinazo wakabili wakulima hivyo ingekuwa rahisi kuwasaidia kuliko ilivyosasa.
Aliwataka wakulima kujitokeza kwenye mafunzo yanayoandaliwa na shirika lake ili waweze kujua namna ya kufuatilia matumizi ya rasilimali za wananchi zikiwemo zile za kilimo ambazo nyingine zinawalenga wao moja kwa moja.
Mwisho.

Na John Gagarini, Kibaha

WATANZANIA wametakiwa kuwekeza kwenye hisa za makampuni na taasisi za fedha nchini badala ya kuwaachia wageni pekee ili  nao wamiliki makampuni na taasisi hizo.
Hayo yamesemwa na mjumbe wa bodi ya soko la hisa Dar es Salaam  Bw Arphaxad Masambu  wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha.

Bw Masambu alisema Watanzania wengi hawana tabia ya kuwekeza katika hisa za makampuni mbalimbali na kusababisha makampuni mengi na taasisi nyingi nchini kumilikiwa na wageni kutoka katika mataifa ya nje na kuwaacha wazawa wakiwa masikini wa kipato.

“Faida ya kununua na kumiliki hisa kuwa si kwa mnunuzi wa hisa pekee bali ni pamoja na vizazi yaani watoto wajukuu, vitukuu kunufaika na hisa hizo,” alisema Bw Masambu.

Alisema kuwa uuzaji wa hisa za makampuni na taasisi ni kwaajili ya kuonfgeza nguvu ya pamoja katika kuendesha na kusimamia kampuni hizo na taasisi hizo ili kuzalisha na kutoa faida yenye tija kwa wengi zaidi.

Naye Mwenyekiti wa chemba ya wafanyabiashara (TCCIA) mkoa wa Pwani Bi Kasa Mlonja aliwataka wananchi, wakulima na wafanyabiashara kuwekeza katika hisa mbalimbali zinazouzwa katika taasisi za fedha na makampuni ilikuwa na madaraka kamili ya hizo kampuni na taasisi kwa lengo la kuendeleza nchi yetu.

Mwisho.   
Na John Gagarini, Kibaha
DIWANI wa kata ya Maili Moja Bw Andrew Lugano amesikitishwa na mamalaka ya maji safi na majitaka (DAWASCO) kushindwa kuwahudumia wananchi hali inayosababisha kukosa maji kwa zaidi ya mwezi sasa.
Akizungumza mara baad aya kufanya ziara kwenye kata hiyo kuangalia maeneo ambayo yamekuwa yakikosa maji kwa muda mrefu, huku akiwa ameambatana na meneja wa DAWASCO Bw Robert Mugabe alisema kuwa hakuna sababu ya wananchi kukosa maji kwa muda wote huo na uongozi upo.
Bw Lugano alisema kuwa amekuwa akipata kero hiyo ya maji toka kwa wananchi na jitihada zake za kufuatilia zimekuwa zikigonga mwamba hali iliyomlazimu kumtoa meneja huyo ofisini kwake Jumamosi na kumwonyesha jinsi gani wananchi wanavyotaabika kwa kukosa maji.
“Siwezi kukubali kuona wananchi wakihangaika kutafuta maji huku chanzo cha maji kikiwa jirani hivyo lazima kampuni hiyo ijali wananchi ili waondokane na kero hiyo,” alisema Bw Lugano.
Moja ya wakazi wa kata hiyo ambaye anakaa mtaa wa Mzimuni Bw Mohamed Atiki alisema kuwa wamekuwa wakipata tabu kubwa ya kupata maji hali inayowasababisha kununua maji kwa bei ya shilingi 500 kwa dumu la lita 20.
“Tumekuwa tukihangaika kwa kipindi kirefu licha ya kutoa taarifa ya ukosefu wa maji kwenye kampuni hii ya maji hivyo lazima wabadili utendaji kazi wao,” alisema Bw Atiki.
Kwa upande wake meneja wa DAWASCO Kibaha Bw Robert Mugabe alisema kuwa tatizo kubwa lililosababisha wananchi kukosa maji ni kutokana na ujenzi wa barabara katika kata hiyo.
“Mabomba mengi yamekatwa kutokana na ujenzi wa barabara lakini hata hivyo tayari tumewasiliana na mkandarasi ili kuangalia namana ya kuweza kurekebisha hali hiyo,” alisema Bw Mugabe.
Bw Mugabe alisema kuwa tayari wameshafanya tathmini ya uharibifu uliofanyika na wakati wowote wataanza kufunga mabomba yaliyokatwa ili wananchi hao waendelee kupata maji kama kawaida.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kisarawe
IMEELEZWA ukosefu wa vifaa kwa watoto wenye ulemavu 89 wilayani Kisarawe mkoani Pwani wameshindwa kuanza masomo kutokana na kukosa vifaa vya kusomea.
Hayo yalisemwa na katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wilayani Kisarawe Bw Ibrahim Tully alisema kuwa jumla ya watoto wenye ulemavu katika wilaya hiyo ni 218.
Bw Tully alisema alisema kuwa kati ya watoto hao ni 34 hivyo kuwafanya watoto hao kushindwa kuanza shule hadi kufikia umri wa miaka 12 na kuendelea.
“Tatizo hilo linasababishwa na uhaba wa fedha wa kununua vifaa hivyo kutoka kwa wazazi na kukosekana kwa wafadhili wa kudumu kusaidia hali hiyo,” alisema Bw Tully.
Aidha alisema mbali ya hayo ,tatizo jingine kubwa ni baadhi ya wazazi na walezi kuwanyanyapaa watoto wenye ulemavu wanaoishi nao kwa kuona aibu kuwaanzisha shule jambo linalowanyima haki yao msingi.   
“Tunakabiliana na hali hiyo kwa kutafuta wafadhili ili kusaidia upatikanaji wa baiskeli maalum kwa ajili ya watoto hao waweze kwenda shule,” alisema Bw Tully.
Bw Tully alisema katika jitihada hizo tayari wamepata baiskeli  50 za aina hiyo na kati ya hizo 10 wamezigawa kwa watoto wa Tarafa ya Chole na nyingine 40 zilizobaki watazigawa kwa watoto wenye ulemavu katika kata zilizopo wilayani kisarawe.
Pia wilaya hiyo ina changamoto ya ukosefu wa shule maalum ya watoto wenye ulemavu ikiwemo wenye ulemavu wa akili ambao  hawawezi kuchanganywa na watoto wengine kwasababu ya mahitaji yao kuhitajika kuwa rafiki zaidi.
Hata hivyo alisema kufuatia tatizo hilo jitihada za hali na mali zinafanyika kujenga shule hiyo mwaka huu ambapo wameshapata eneo lenye heka 100 katika kijiji cha Kidugalo  kata ya Mzenga na mchakato wa kupata hati unaendelea.
Mwisho                                                                                     
Na John Gagarini, Bagamoyo
VIONGOZI wa vikundi vya ujasiriamali kwenye kata ya Msata wilayani Bagamoyo wametakiwa kutumia fedha wanazopewa na sereikali na wafadhili mbalimbali kuzitumia kwa mipango waliojiwekea ili waweze kujikwamua na hali ngumu ya kiuchumi.
Hayo yalisemwa na Ofisa Mtendaji Kata ya Msata Bw Edgar Nazar wakati
akizungumza na kikundi cha Lulenga kinachojihusisha na ufugaji
nyuki na mazingira ambacho kimepatiwa zaidi ya sh. Mililioni nne  kwa ajili ya
utoaji wa elimu inayohusiana na sekta ya nyuki.

Bw Nazar alisema kuwa serikali na wadau mbalimbali wa maenedeleo wamekuwa wakitoa fedha nyingi kwa ajili ya kufadhili miradi ya maendeleo kupitia vikundi hivyo lazima zitumike kwa malengo husika.
“Serikali  imekuwa ikielekeza masuala mbalimbali yanayohusiana na ujasiliamali na
ushahidi huo ni huu wa Wizara ya Misitu kutoa kiasi hiki cha fedha kwa
ajili ya kuendeleza ufugaji nyuki na mazingira, niwaombe fedha hizi
zitumike kama zilivyolengwa,” alisema Bw Nazar.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kikundi hicho Bw Douglas Kilomo alisema kuwa kwa msimu wa mwaka uliopita kulikuwepo na mgongano kati yao na
wafugaji jamii ya wamasai hali iliyosababisha kusimama kwa shughuli
zetu kutokana na mgongano huo,” ilieleza sehemu ya taarifa.

Bw Kilomo alisema uwa zoezi la ufugaji nyuki linaendana na sanjali na utunzaji wa
mazingira hivyo amewaasa kuzingatia hayo ili kujiletea mafanikio katika zao la asali ambalo kwa sasa lina soko kubwa.

“Ufugaji nyuki ni sekta ambayo haihitaji mtaji mkubwa kama ilivyo
miradi mingine, unapokuwa na mzinga tu unasubiri mazao ambapo kwa
mwaka unavuna mara tatu sawa na sh. Laki 9 hivyo niwaombe muwe makini
kwa hilo,” alisema Bw Kilomo.

Naye mmoja wa wanakikundi Bw Mohamed Mrisho ameeleza kuwa mafunzo hayo anaimani yatawaongezea ufanisi wa shughuli zao na kujiongezea kipato chao.

MWISHO.

No comments:

Post a Comment