Na John
Gagarini, Mkuranga
IMEELEZWA
kuwa kuishi mbali na vituo vyao vya kazi kwa baadhi ya maofisa
ugani kwenye vijiji wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani kumechangia kudumaza
shughuli za kilimo wilayani humo.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mafunzo kwenye kijiji cha
Msufini kata ya Mbezi, mratibu wa mradi wa Wajibu wa Jamii Katika Usimamizi
wa Rasilimali za Umma za Sekta ya Kilimo wilaya hiyo (POCUSO), Bw Said
Gwaja alisema kuwa maofisa hao wamekuwa hawafiki kwenye vijiji
walivyopangiwa.
Bw Gwaja alisema kuwa kutokana na kuishi mbali na vituo vyao vya kazi
wamekuwa wakiishia ofisini na kushindwa kwenda kwenye maoeneo waliyopangiwa
hasa yale ya vijijini.
“Ni vema wangekaa kwenye maeneo yao ya kazi ili iwe rahisi kwao kutoa
huduma kwa wakulima ambao wanakosa fursa nyingi kutokana na kutofahamishwa
namna ya kuweza kuzipata,” alisema Bw Gwaja.
Alisema kuwa fursa ambazo wakulima walipaswa kuzijua zinashindwa kuwafikia
kwani wanazipata wakati muda wa kilimo unakuwa umepita hivyo kushindwa kupata pembejeo za ruzuku kwa wakati muafaka.
ugani kwenye vijiji wilayani Mkuranga mkoa wa Pwani kumechangia kudumaza
shughuli za kilimo wilayani humo.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mafunzo kwenye kijiji cha
Msufini kata ya Mbezi, mratibu wa mradi wa Wajibu wa Jamii Katika Usimamizi
wa Rasilimali za Umma za Sekta ya Kilimo wilaya hiyo (POCUSO), Bw Said
Gwaja alisema kuwa maofisa hao wamekuwa hawafiki kwenye vijiji
walivyopangiwa.
Bw Gwaja alisema kuwa kutokana na kuishi mbali na vituo vyao vya kazi
wamekuwa wakiishia ofisini na kushindwa kwenda kwenye maoeneo waliyopangiwa
hasa yale ya vijijini.
“Ni vema wangekaa kwenye maeneo yao ya kazi ili iwe rahisi kwao kutoa
huduma kwa wakulima ambao wanakosa fursa nyingi kutokana na kutofahamishwa
namna ya kuweza kuzipata,” alisema Bw Gwaja.
Alisema kuwa fursa ambazo wakulima walipaswa kuzijua zinashindwa kuwafikia
kwani wanazipata wakati muda wa kilimo unakuwa umepita hivyo kushindwa kupata pembejeo za ruzuku kwa wakati muafaka.
Aidha
alisema kuwa endapo wangekuwa wanafanya kazi kwenye maeneo waliyopangiwa
hususani vijijini ingekuwa raisi kwao kujua chanagamoto zinazo wakabili
wakulima hivyo ingekuwa rahisi kuwasaidia kuliko ilivyosasa.
Aliwataka
wakulima kujitokeza kwenye mafunzo yanayoandaliwa na shirika lake ili waweze
kujua namna ya kufuatilia matumizi ya rasilimali za wananchi zikiwemo zile za
kilimo ambazo nyingine zinawalenga wao moja kwa moja.
Mwisho.
Na
John Gagarini, Kibaha
WATANZANIA
wametakiwa kuwekeza kwenye hisa za makampuni na taasisi za fedha nchini badala
ya kuwaachia wageni pekee ili nao
wamiliki makampuni na taasisi hizo.
Hayo yamesemwa
na mjumbe wa bodi ya soko la hisa Dar es Salaam
Bw Arphaxad Masambu wakati
akizungumza na waandishi wa habari mjini Kibaha.
Bw Masambu
alisema Watanzania wengi hawana tabia ya kuwekeza katika hisa za makampuni
mbalimbali na kusababisha makampuni mengi na taasisi nyingi nchini kumilikiwa
na wageni kutoka katika mataifa ya nje na kuwaacha wazawa wakiwa masikini wa
kipato.
“Faida ya
kununua na kumiliki hisa kuwa si kwa mnunuzi wa hisa pekee bali ni pamoja na
vizazi yaani watoto wajukuu, vitukuu kunufaika na hisa hizo,” alisema Bw
Masambu.
Alisema kuwa
uuzaji wa hisa za makampuni na taasisi ni kwaajili ya kuonfgeza nguvu ya pamoja
katika kuendesha na kusimamia kampuni hizo na taasisi hizo ili kuzalisha na
kutoa faida yenye tija kwa wengi zaidi.
Naye Mwenyekiti
wa chemba ya wafanyabiashara (TCCIA) mkoa wa Pwani Bi Kasa Mlonja aliwataka
wananchi, wakulima na wafanyabiashara kuwekeza katika hisa mbalimbali
zinazouzwa katika taasisi za fedha na makampuni ilikuwa na madaraka kamili ya
hizo kampuni na taasisi kwa lengo la kuendeleza nchi yetu.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
DIWANI wa kata ya Maili Moja Bw Andrew Lugano
amesikitishwa na mamalaka ya maji safi na majitaka (DAWASCO) kushindwa
kuwahudumia wananchi hali inayosababisha kukosa maji kwa zaidi ya mwezi sasa.
Akizungumza mara baad aya kufanya ziara kwenye kata
hiyo kuangalia maeneo ambayo yamekuwa yakikosa maji kwa muda mrefu, huku akiwa
ameambatana na meneja wa DAWASCO Bw Robert Mugabe alisema kuwa hakuna sababu ya
wananchi kukosa maji kwa muda wote huo na uongozi upo.
Bw Lugano alisema kuwa amekuwa akipata kero hiyo ya
maji toka kwa wananchi na jitihada zake za kufuatilia zimekuwa zikigonga mwamba
hali iliyomlazimu kumtoa meneja huyo ofisini kwake Jumamosi na kumwonyesha
jinsi gani wananchi wanavyotaabika kwa kukosa maji.
“Siwezi kukubali kuona wananchi wakihangaika kutafuta
maji huku chanzo cha maji kikiwa jirani hivyo lazima kampuni hiyo ijali
wananchi ili waondokane na kero hiyo,” alisema Bw Lugano.
Moja ya wakazi wa kata hiyo ambaye anakaa mtaa wa
Mzimuni Bw Mohamed Atiki alisema kuwa wamekuwa wakipata tabu kubwa ya kupata
maji hali inayowasababisha kununua maji kwa bei ya shilingi 500 kwa dumu la
lita 20.
“Tumekuwa tukihangaika kwa kipindi kirefu licha ya
kutoa taarifa ya ukosefu wa maji kwenye kampuni hii ya maji hivyo lazima
wabadili utendaji kazi wao,” alisema Bw Atiki.
Kwa upande wake meneja wa DAWASCO Kibaha Bw Robert
Mugabe alisema kuwa tatizo kubwa lililosababisha wananchi kukosa maji ni kutokana
na ujenzi wa barabara katika kata hiyo.
“Mabomba mengi yamekatwa kutokana na ujenzi wa
barabara lakini hata hivyo tayari tumewasiliana na mkandarasi ili kuangalia
namana ya kuweza kurekebisha hali hiyo,” alisema Bw Mugabe.
Bw Mugabe alisema kuwa tayari wameshafanya tathmini ya
uharibifu uliofanyika na wakati wowote wataanza kufunga mabomba yaliyokatwa ili
wananchi hao waendelee kupata maji kama kawaida.
Mwisho.
Na John
Gagarini, Kisarawe
IMEELEZWA
ukosefu wa vifaa kwa watoto wenye ulemavu 89 wilayani Kisarawe mkoani Pwani
wameshindwa kuanza masomo kutokana na kukosa vifaa vya kusomea.
Hayo
yalisemwa na katibu wa chama cha watu wenye ulemavu wilayani Kisarawe Bw
Ibrahim Tully alisema kuwa jumla ya watoto wenye ulemavu katika wilaya hiyo ni
218.
Bw Tully alisema
alisema kuwa kati ya watoto hao ni 34 hivyo kuwafanya watoto hao kushindwa
kuanza shule hadi kufikia umri wa miaka 12 na kuendelea.
“Tatizo hilo
linasababishwa na uhaba wa fedha wa kununua vifaa hivyo kutoka kwa wazazi na
kukosekana kwa wafadhili wa kudumu kusaidia hali hiyo,” alisema Bw Tully.
Aidha alisema
mbali ya hayo ,tatizo jingine kubwa ni baadhi ya wazazi na walezi kuwanyanyapaa
watoto wenye ulemavu wanaoishi nao kwa kuona aibu kuwaanzisha shule jambo
linalowanyima haki yao msingi.
“Tunakabiliana
na hali hiyo kwa kutafuta wafadhili ili kusaidia upatikanaji wa baiskeli maalum
kwa ajili ya watoto hao waweze kwenda shule,” alisema Bw Tully.
Bw Tully
alisema katika jitihada hizo tayari wamepata baiskeli 50 za aina hiyo na
kati ya hizo 10 wamezigawa kwa watoto wa Tarafa ya Chole na nyingine 40
zilizobaki watazigawa kwa watoto wenye ulemavu katika kata zilizopo wilayani
kisarawe.
Pia wilaya
hiyo ina changamoto ya ukosefu wa shule maalum ya watoto wenye ulemavu ikiwemo
wenye ulemavu wa akili ambao hawawezi kuchanganywa na watoto wengine
kwasababu ya mahitaji yao kuhitajika kuwa rafiki zaidi.
Hata hivyo
alisema kufuatia tatizo hilo jitihada za hali na mali zinafanyika kujenga shule
hiyo mwaka huu ambapo wameshapata eneo lenye heka 100 katika kijiji cha
Kidugalo kata ya Mzenga na mchakato wa
kupata hati unaendelea.
Mwisho
Na John
Gagarini, Bagamoyo
VIONGOZI wa
vikundi vya ujasiriamali kwenye kata ya Msata wilayani Bagamoyo wametakiwa
kutumia fedha wanazopewa na sereikali na wafadhili mbalimbali kuzitumia kwa
mipango waliojiwekea ili waweze kujikwamua na hali ngumu ya kiuchumi.
Hayo yalisemwa
na Ofisa Mtendaji Kata ya Msata Bw Edgar Nazar wakati
akizungumza na kikundi cha Lulenga kinachojihusisha na ufugaji
nyuki na mazingira ambacho kimepatiwa zaidi ya sh. Mililioni nne kwa ajili ya
utoaji wa elimu inayohusiana na sekta ya nyuki.
akizungumza na kikundi cha Lulenga kinachojihusisha na ufugaji
nyuki na mazingira ambacho kimepatiwa zaidi ya sh. Mililioni nne kwa ajili ya
utoaji wa elimu inayohusiana na sekta ya nyuki.
Bw Nazar alisema
kuwa serikali na wadau mbalimbali wa maenedeleo wamekuwa wakitoa fedha nyingi
kwa ajili ya kufadhili miradi ya maendeleo kupitia vikundi hivyo lazima zitumike
kwa malengo husika.
“Serikali imekuwa ikielekeza masuala mbalimbali
yanayohusiana na ujasiliamali na
ushahidi huo ni huu wa Wizara ya Misitu kutoa kiasi hiki cha fedha kwa
ajili ya kuendeleza ufugaji nyuki na mazingira, niwaombe fedha hizi
zitumike kama zilivyolengwa,” alisema Bw Nazar.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kikundi hicho Bw Douglas Kilomo alisema kuwa kwa msimu wa mwaka uliopita kulikuwepo na mgongano kati yao na
wafugaji jamii ya wamasai hali iliyosababisha kusimama kwa shughuli
zetu kutokana na mgongano huo,” ilieleza sehemu ya taarifa.
Bw Kilomo alisema uwa zoezi la ufugaji nyuki linaendana na sanjali na utunzaji wa
mazingira hivyo amewaasa kuzingatia hayo ili kujiletea mafanikio katika zao la asali ambalo kwa sasa lina soko kubwa.
“Ufugaji nyuki ni sekta ambayo haihitaji mtaji mkubwa kama ilivyo
miradi mingine, unapokuwa na mzinga tu unasubiri mazao ambapo kwa
mwaka unavuna mara tatu sawa na sh. Laki 9 hivyo niwaombe muwe makini
kwa hilo,” alisema Bw Kilomo.
Naye mmoja wa wanakikundi Bw Mohamed Mrisho ameeleza kuwa mafunzo hayo anaimani yatawaongezea ufanisi wa shughuli zao na kujiongezea kipato chao.
MWISHO.
ushahidi huo ni huu wa Wizara ya Misitu kutoa kiasi hiki cha fedha kwa
ajili ya kuendeleza ufugaji nyuki na mazingira, niwaombe fedha hizi
zitumike kama zilivyolengwa,” alisema Bw Nazar.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa kikundi hicho Bw Douglas Kilomo alisema kuwa kwa msimu wa mwaka uliopita kulikuwepo na mgongano kati yao na
wafugaji jamii ya wamasai hali iliyosababisha kusimama kwa shughuli
zetu kutokana na mgongano huo,” ilieleza sehemu ya taarifa.
Bw Kilomo alisema uwa zoezi la ufugaji nyuki linaendana na sanjali na utunzaji wa
mazingira hivyo amewaasa kuzingatia hayo ili kujiletea mafanikio katika zao la asali ambalo kwa sasa lina soko kubwa.
“Ufugaji nyuki ni sekta ambayo haihitaji mtaji mkubwa kama ilivyo
miradi mingine, unapokuwa na mzinga tu unasubiri mazao ambapo kwa
mwaka unavuna mara tatu sawa na sh. Laki 9 hivyo niwaombe muwe makini
kwa hilo,” alisema Bw Kilomo.
Naye mmoja wa wanakikundi Bw Mohamed Mrisho ameeleza kuwa mafunzo hayo anaimani yatawaongezea ufanisi wa shughuli zao na kujiongezea kipato chao.
MWISHO.
No comments:
Post a Comment