Thursday, February 14, 2013

UBALOZI MISRI WATOA MSAADA HOSPITALI


Na John Gagarini, Bagamoyo

UBALOZI wa Misri nchini umetoa msaada ya vifaa mbalimbali vya kisasa katika hospitali ya wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani vyenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni moja.

Vifaa hivyo vilivyotolewa ni Madawa, Vitanda pamoja na vya wodi ya upasuaji kwa ajili ya kuboresha hudum za afya kwenye hospitali hiyo.  
 
Akikabidhi vifaa hivyo balozi wa Misri hapa nchini Bw Hossam Eldin Moharam alisema wananchi wa Misri wameamua kutoa msaada huo kwa  marafiki zao wa Bagamoyo ili kudumisha na kuenzi urafiki wa muda mrefu baina ya wananchi wa nchi hizo mbili.
 
Bw Moharam alisema kuwa hapendi kuita ni msaada wa vifaa walivyovitoa kutokana na ukaribu na urafiki  uliopo baina ya nchi hizo.
 
“Tunaomba vifaa hivi vilivyotolewa kwenye hospitali hii vilindwe kwani vinahitaji uangalizi mkubwa ili viweze kusadia kutoa huduma bora za afya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo Bw Shukuru Mbatto alisema msaada huo ni chachu kwa watumishi wa hospitali hiyo katika uboreshaji wa utoaji  huduma bora .
 

Naye mmoja wa wadau waliofanikisha upatikanaji wa msaada huo, Bw Yusuph Kikwete alisema akiwa ni kiongozi wa muungano wa marafiki wa Bagamoyo walizungumza na balozi huyo kuhusiana na ombi la msaada wa vifaa kwa ajili ya maabara mpya ya hospitali hiyo .
 
 Mwisho

No comments:

Post a Comment