Na John Gagarini, Bagamoyo
KAYA 1,138 katika vijiji vitano kwenye kata ya Miono wilayani
Bagamoyo mkoani Pwani vinakabiliwa na baa la njaa na kuhitaji msaada wa
chakula.
Kwa mujibu wa Diwani
wa kata hiyo Sangali Kiselu alisema kuwa kaya hizo zinahitaji msaada ili
kukabiliana na njaa hiyo.
Kiselu alisema kuwa kutokana na tatizo hilo uongozi wa kata
ya Miono umeiomba serikali Mkoani Pwani kuharakisha kuwapatia msaada wa chakula kaya
hizo ili kukabiliana na tatizo hilo.
“Hali kwa sasa inazidi kuwa mbaya katika kaya hizo ikiwa ni
kati ya kaya 4,271 zenye watu zaidi ya 20,000 ambazo zimekumbwa na baa hilo la
njaa,” alisema Kiselu.
Alivitaja vijiji ambavyo vimepata athari hiyo kuwa ni
Kweikonje, Masimbani, Mihuga, Kikalo na Miono kwenye kata hiyo.
Kweikonje, Masimbani, Mihuga, Kikalo na Miono kwenye kata hiyo.
Kwa upande wake mtendaji wa kata hiyo Ramadhani Nguya alisema
kwa sasa wanahofia kutokana na hali kufikia pabaya hivyo haina budi kutoa kilio
hicho kwa niaba ya wananchi ili kunusuru maisha yao.
Naye Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Ahmed Kipozi amekiri kuwepo kwa
hali hiyo nakusema si kweli kuwa serikali inachelewesha kupeleka msaada wa
chakula katika maeneo hayo.
“Serikali imeshaidhinisha tani 400 ambazo zitasambazwa katika
maeneo mbalimbali yaliokumbwa na baa hilo wilayani humo, ikiwa ni pamoja na
kata ya Kibindu, Mbwewe, Kimange, Miono na Kiwangwa ambayo haijapata athari
sana.
Kipozi alisema kuwa janga la njaa limezikumba kata hizo
kutokana na mavuno hafifu kwa mwaka jana yaliyosababishwa na mvua iliyokuwa hairidhishi
hivyo kwa sasa amehimiza kilimo cha mhogo na mtama ambayo yanahimili ukame.
Mwisho
Mwisho
No comments:
Post a Comment