Friday, February 1, 2013

KINYOZI ADAKWA KWA KUISHI NA MWANAFUNZI



Na Mwandishi Wetu, Kibaha

SAKATA la kutafuta wanafunzi watoro katika shule ya Sekondari ya Bundikani Kata ya Maili Moja wilayani Kibaha limeibua mapya baada ya mwanafunzi wa kidato cha pili kukutwa kwa kwa mwanaume ambaye ni kinyozi baada ya kushindwa kwenda shule kwa muda wa siku tatu.
Mwanafunzi huyo ambaye ni miongoni mwa wanafunzi waliofeli mtihani wa kidato cha pili mwaka jana na kutakiwa kurudia kidato cha pili mwaka huu, alikutwa kwa kijana huyo Martin Joseph (16) mkazi wa Maili Moja shuleni jirani na shule hiyo.
Tukio hilo lilitokea juzi baada ya kijana huyo kukamatwa na mgambo wa kata ambao wamepewa kazi ya kuwakamata wanafunzi watoro wa shule hiyo ambapo hivi karibuni baadhi ya wanafunzi walikamatwa porini huku wengine wakiwa na kondomu na kupewa adhabu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuchapwa viboko na wazazi wao kwenye baraza la kata hiyo.
Kijana huyo alifikishwa kwenye baraza la usuluhishi la kata ya Maili Moja  linaloongozwa na mwenyekiti Bw Amadeus Ngombale, aliskiri kukaa na mwanafunzi huyo kwa kipindi hicho licha ya kuwa mwanafunzi huyo kutokwenda shule tangu ilipofunguliwa mwanzoni mwa mwezi huu.
“Mimi sikujua kama ni mwanafunzi kwani hakuniambia anasoma shule na nilikaa naye kwa siku tatu ila nilishangaa kuona mgambo wamekuja ofini kwangu na kunikamata kwa madai kuwa ni kwanini nimekaa na mwanafunzi na kumsababisha asiende shule,” alisema Joseph.
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Flora Chibululu alisema kuwa mwanafunzi huyo ni moja kata ya wanafunzi wlaiofeli mwaka jana kidato cha pili na kutakiwa kurudia kidato hicho lakini walishangaa ni kwanini haendi shule.
“Huyu mwanafunzi ni miongoni mwa wale wanaorudia kidato cha pili mwaka huu na baada ya kukutwa kwa mwanaume tulimpa barua aje na mlezi wake ambaye ni bibi yake ambaye ndiye anayeishi naye,” alisema Chibululu.
Aidha alisema kuwa mwanafunzi huyo alisema kuwa anaishi na bibi yake kwa sababu baba yake hamtunzi kutokana na tabia zake ambazo zimekuwa ni kero.
Kijana huyo kutokana na kukubali tuhuma hizo alipelekwa polisi kwa ajili ya kufikishwa mahakamani kutokana na tukio hilo ambalo ni moja ya changamoto kubwa kwa wanafunzi wa kike kwenye wilaya ya Kibaha na mkoa wa Pwani
Mwisho.

 

No comments:

Post a Comment