alitoa ahadi ya kutoa kiasi cha shilingi milioni nne kwa ajili ya kumalizia nyumba ya Mwalimu kwenye shule ya msingi Java na mifuko 50 ya saruji katika shule ya msingi Kwamakuru,Manda Mazingara ,Kata ya Mkange ili kukarabati madarasa matano ambayo yamebomoka.
Bwanamdogo alisema mbali ya mchango huo pia atatoa 200,000 za kununulia nyavu,400,000 ya umeme wa jua katika shule ya msingi Saadan, mabati 70 katika ujenzi wa soko la Saadan na mifuko 50 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya serikali ya kijiji cha Mkange.
Alisema ahadi hizo ni za awamu ya pili baada ya kukamilisha ahadi mbalimbali alizozitoa kipindi cha uchaguzi na kuzikamilisha kupitia fedha za mfuko wa jimbo fedha , wafadhili na binafsi.
"Lengo la kutoa vitu hivyo pamoja na fedha ni kuhakikisha fedha zilizotengwa kwa ajili ya kutatua kero za wananchi zinatumika ipasavyo ili kuondoa kero ambazo zinaweza kutatuliwa na viongozi waliochaguliwa na wananchi katika chaguzi mbalimbali," alisema Bwanamdogo
Aliwataka viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM na serikali wajenge ushirikiano katika kufanya maamuzi na majukumu mbalimbali ili kuleta maendeleo hatimaye kukuza uchumi wa jimbo hilo.
"Msiwe na tabia ya kusemana ndani ya jamii na badala yake watumie vikao halali vya chama katika kuwekana sawa kama endapo kuna kiongozi anamapungufu ili kuleta heshima ya chama," alisema Bwanamdogo.
Mbunge huyo wa jimbo la Chalinze hicho ni kikao chake cha kwanza kuzungumza tangu arejee nchini India kwa matibabu mara baada ya kuugua kwa takriban miezi Saba kuaznia July 2012 alipoanza kuugua ghafla kwenye bunge lililofanyika mwezi huo.
Picha zikimuonyesha Mbunge Said Bwanamdogo akizungumza juzi katika kikao cha kwanza cha Halmashauri ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kata ya Mkange Tarafa ya Miono picha na John Gagarini.
E89A9800.JPG 1645K View Share Download |
E89A9785.JPG 1792K View Share Download |
E89A9779.JPG 1581K View Share Download |
E89A9774.JPG 1431K View Share Download |
No comments:
Post a Comment