Na John Gagarini, Kibaha
SEIKALI imeshauriwa kubadili mfumo wa upatikanaji wa majaji
kwa kufanyiwa usaili badala ya kuteuliwa ili kuleta utawala bora wa kisheria.
Hayo yalisemwa jana mjini Kibaha na mwakilishi wa mawakili mkoani
Pwani, Saiwelo Kumwenda, wakati wa maadhimisho ya siku ya sheria nchini kwenye
mkoa huo zilizofanyika kwenye viwanja vya mahakama.
Alisema kuwa ili kuimarisha utawala wa sheria ni vema
waajiriwe kwa kwa kufanyiwa usaili rasmi na chombo kisicho na mfungamano wa
kiutawala na serikali.
“Ni vema majaji wakaomba kazi na kufanyiwa usaili na wale
watakaofuzu vigezo vinavyotakiwa ndiyo watakaopata nafasi hiyo tofauti na sasa
ambapo huteuliwa na Raisi,” alisema Bw Kumwenda.
Alisema kuwa mfumo wa kuteua si mzuri katika mfumo wa kutaka
kuimarisha utawala wa sheria ili kuepuka malalamiko na manunguniko.
Aidha alitaka viongozi wan chi kusaidia kulinda uhuru wa
mahakama ili nchi iendelee kufuata utawala wa sheria na mfumo mzima wa
demokrasia.
Pia kuchukua hatua ya kinidhamu kwa watumishi wale ambao
wanaonekana au watathibitika kuwa kazi zao za kutafsiri sheria, kusikiliza
mashauri na kuyatolea maamuzi hawaijui vizuri wala hawazielewi.
Kwa upande wake hakimu mkazi mfawidhi wilaya ya Kibaha mkoani
Pwani Bi Bahati Ndesarua alisema kuwa utawala wa sheria una umuhimu kwa kugawa
madaraka kwa kuzingatia taratibu.
Bi Ndesarua alisema kuwa utawala wa sheria unasaidia kukua
kwa uchumi na watu kupata haki zao bila ya kumwonea mtu kutokana na uwezo wake.
Aliwataka wananchi kushiriki katiba zoezi la uboreshaji wa
katiba mpya ili kutoa mchango wao wa mawazo na kuifanya iweze kuwa na manufaa
kwa kila mtu.
Naye mgeni rasmi kamanda wa polisi mkoani Pwani Bw Ulrich
Matei alisema kuwa wananchi waachane na tabia ya kuvunja sheria kwa kuwapiga na
kuwaua watuhumiwa.
Bw Matei alsiema kuwa ni vema wananchi hao wakawapeleka
kwenye vyombo vya sheria ili haki iweze kutendeka na si kutumia mabavu kwa
kuwaua.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment