Na Mwandishi
Wetu, Kibaha
ASKARI wa
Jeshi la Polisi kituo kidogo Cha Kwa Mathiasi Wilyani Kibaha mkoani Pwani Pc
Ramadhan amelazwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kujeruhiwa na
wananchi waliovamia kituo hicho kutaka kuwatoa watu waliowatuhumu kuwa wameiba
simu.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani humo Ulrich
Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Februari 21 mwaka huu majira ya saa 1
usiku baada ya wananchi hao kutaka kuwatoa watu waliodai kuwa wameiba simu na
kutaka kuwaua.
Kamanda Matei
alisema kuwa chanzo cha tukio hilo kilianza kwenye uwanja wa mpira wa miguu
baina ya timu za Palasupalasu na Kigogo ya Jijini Dar es Salaam, ambapo mchezo
huo uliokuwa ukichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole kulivunjika kutokana na
vurugu zilizojitokeza.
“Baada ya
mchezo huo kuvunjika washabiki wa timu hizo walianza kushambuliana na ndipo
watu waliotuhumiwa ambao ni Michael Mathias (30) na Hashim Noah (19) ambaye ni
mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Mwanagati Jijini Dar es Salaam kukimbia kwa
kutumia pikipiki na walipoona wmezidiwa waliiacha pikipiki kisha kuingia kwenye
msikiti wa Tanita,” alisema Kamanda Matei.
Aidha alisema
kuwa baada ya kuingia ndani ya msikiti huo wananchi hao waliuzunguka msikiti
huo kisha kutaka kuwatoa watu hao ili wawaue ndipo polisi walipofika na
kuwatawanya wananchi hao lakini waligoma na kuanza kuwarushia mawe polisi ndipo
polisi walipopiga risasi kuwatawanya wananchi hao.
“Katika
vurugu hizo Maria Stamford alipigwa risasi ya ziwa na Idd Shukuru alipigwa mguu
wa kulia kisha waliwachukuwa watu hao na pikipiki yao ndipo wanannchi hao
walikwenda hadi kwenye kituo hicho wakidhani kuwa watu hao wako pale kwani
waliiona ile pikipiki nje ya kituo hicho,” alisema KamandaMatei.
Aliendelea
kusema kuwa walikivamia kituo hicho na kumpiga askari huyo ambaye alikuwa
amevaa sare na askari mwingine Bonventura kisha kuvunja mlango na kuwaangalia
watu wale lakini hawakuwakuta na kuharibu vitu mbalimbali.
“Uchunguzi
ulibaini kuwa watu wale hawakuwa wezi bali walikuwa ni mashabiki wa timu
mojawapo ambao walizushiwa kuwa wezi jambo ambalo si la kweli majeruhi
wanaendelea vyema na matibabu na kwa sasa tayari wameunda tume ndogo kufuatilia
tukio hilo na hakuna mtu aliyekamtwa kuhusiana na tukio hilo,” alisema Kamanda Matei
.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment