Na John
Gagarini, Kibaha
MFANYABIASHARA
wa Jijini Dar es Salaam Ambrose Mapunda mwenye umri kati ya 50 na 55 amekutwa
amekufa na mwili wake kuwekwa chini ya uvungu wa kitanda wa nyumba ya kulala
wageni ya Cham Cham Msata wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha kwa niaba ya kamanda wa
polisi mkoa wa Pwani ofisa upelelezi wa Jeshi la polisi Juma Yusuph alisema
kuwa mwili wa marehemu ulikutwa ukiwa uchi.
Kamanda Yusuph
alisema kuwa tukio hilo lilitokea kati ya Fabruari 22 na 24 mwaka huu kwenye
nyumba ya kulala wageni ya Cham Cham huku ukiwa na jeraha kubwa kichwani huku
shingo yake ikiwa imenyongwa.
“Marehemu alikutwa
akiwa chini ya uvungu huku mwili wake ukiwa hauna nguo na jeraha huku ukiwa
umenyongwa shingo ambapo mtu aliyehusika na tukio hilo hakuweza kufahamika mara
moja,” alisema kamanda Yusuph.
Alisema kuwa
marehemu hakukutwa na chochote licha ya kuwa alifika kwenye nyumba hiyo ya
kulala wageni akiwa na begi kwenye chumba namba mbili.
“Ujumbe
uliokutwa kwenye chumba hicho ulisema kuwa umenidhulumu tulikubaliana unilipe
kiasi cha shilingi 20,000 lakini hujanilipa, ujumbe huu umeandaikwa na mtu
asiyefahamika,” alisema Kamanda Yusuph.
Aidha alisema
kuwa mhuduma na mlinzi wa nyumba hiyo ya kulala wageni wanashikiliwa kwa
mahojiano zaidi kuhusu tukio hilo na polisi wanaendelea na uchunguzi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment