Monday, July 31, 2023

MAKONGAMANO YA NANE NANE KUWA NA TIJA


Na Manase Madelemu, Dodoma 

MKUU wa mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamle amesema kuwa tofauti na maonesha ya miaka iliyopita ya nane nane mwaka huu 2023 yatahusisha matukio muhimu na makongamano yanayoongeza wigo wa uzalishaji bora.

Senyamule amesema hayo leo julai 31,2023 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Maadhimisho ya nane nane mwaka kikanda.

Amesema kutakuwa na makongamano ya tasnia ya alizeti,kongamano la zao la mtama ambapo mikoa ya Dodoma na singida ilikabidhiwa jukumu la kuzalisha alizeti Kwa wingi ili kupunguza nakisi ya mafuta ya kula nchini na hivyo kuokoa fedha za kigeni.

Aidha ameongeza kuwa kutakuwepo na siku maalumu ya uhamasishaji uzalishaji kuku wa kienyeji hasa katika mkoa wa Singida unafahamika katika mikoa mbalimbali hapa nchini hadi kufikia watu kuwaita kuku wa Singida 

Pia Senyamule amesema kuwa Katika maonesho ya mwaka huu kutakuwa na huduma za Afya na matibabu ya kibingwa zitakazotolewa na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa na huduma hizi zitatolewa bure.

Kauli mbiu ya maonesha na sherehe za nane nane kitaifa Kwa mwaka 2023 ni Vijana na wanawake ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu ya Chakula"na kauli mbiu kikanda Kilimo ni Biashara, Biashara ni Uwekezaji.

Saturday, July 29, 2023

PINDA KUZINDUA MAONYESHO NANE NANE KANDA YA MASHARIKI

 

WAZIRI Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya wakulima nane nane Kanda ya Mashariki Mkoani Morogoro Agosti Mosi mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maonyesho hayo yanashirikisha mikoa minne ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga na Morogoro.

Kunenge amesema kuwa hadi sasa tayari washiriki 589 wamejiandikisha kushiriki maonyesho hayo ambapo ni ongezeko la asilimia 22 ikilinganishwa na mwaka jana ambapo washiriki walikuwa 476.

Amesema kuwa maonyesho hayo ni ya 30 tangu kufanyika kwa kanda hiyo ya Mashariki ambapo kauli mbiu inasema Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula.

Aidha amesema kuwa wakulima na wananchi wanakaribishwa kujitokeza kwa wingi ili kujifunza teknolojia za kisasa kwenye sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi.

Friday, July 28, 2023

WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA MGENI RASMI NANE NANE KANDA YA MASHARIKI

WAZIRI Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye maonyesho ya wakulima nane nane Kanda ya Mashariki Mkoani Morogoro Agosti Mosi mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mjini Kibaha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema kuwa maonyesho hayo yanashirikisha mikoa minne ya Pwani, Dar es Salaam, Tanga na Morogoro.

Kunenge amesema kuwa hadi sasa tayari washiriki 589 wamejiandikisha kushiriki maonyesho hayo ambapo ni ongezeko la asilimia 22 ikilinganishwa na mwaka jana ambapo washiriki walikuwa 476.

Amesema kuwa maonyesho hayo ni ya 30 tangu kufanyika kwa kanda hiyo ya Mashariki ambapo kauli mbiu inasema Vijana na Wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula.

Aidha amesema kuwa wakulima na wananchi wanakaribishwa kujitokeza kwa wingi ili kujifunza teknolojia za kisasa kwenye sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi.

TASAC KUNUNUA BOTI ZA UOKOZI ZIWA VICTORIA

SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limesema limejipanga kununua boti tatu za uokozi katika Ziwa Victoria ambazo zitakwenda kusaidia kutatua changamoto ambazo zimekuwa zikijitokeza pindi ajali zinapotokea

Hayo yamesemwa jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Bw.Kaimu Abdi Mkenyenge wakati  akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa majukumu ya mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa mwaka wa fedha 2023/2024 .

Amesema  katika boti hizo tatu zitakazonunuliwa mbili zitakuwa ni za mwendonkasi kwaajili ya ukokozi na Moja itakuwa kwaajili ya kubebea majeruhi na wagonjwa (Ambulance) .

“Boti hizi tatu zitatumika kufanya uokozi katika ajali ambazo zimekuwa zikitokea katika Ziwa Victoria ambapo mbili zitakuwa ni za meendo kasi na Moja itatumika kama ambulance kwa ajili ya majeruhi”amesema

Aidha amesema TASAC  imeendelea kuimarisha udhibiti huduma za usafiri majini, na kuhakikisha kuna ushindani sawia miongoni mwa watoa huduma.

Amesema kuwa linafanya ufuatiliaji, tathmini na kutoa maelekezo kuhusu utekelezaji wa vigezo na viwango vya ubora wa huduma (performance standards and Benchmarks) kwa watoa huduma za bandari na usafiri majini.

“Tunaendelea kuratibu maombi ya tozo za usafiri wa meli katika Maziwa (Victoria na Nyasa) na kuhakikisha viwango vya tozo vinavyotumika haviathiri ushindani wa kibiashara;

“Lakini pia zoezi la urasimishaji wa bandari bubu Tanzania bara ambapo bandari bubu kumi na tatu (13) zilizowasilishwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) kwa ajili ya urasimishaji zilikaguliwa na kufanyiwa tathmini ya kina kwa kushirikiana na TPA, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Baraza la Usimamizi wa Mazingira (NEMC)”amesema Mkeyenge

Kadhalika amesema  bandari bubu kumi zilionekana kukidhi vigezo hivyo na kupendekezwa kwa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Uchukuzi) (WUU-U) kwa ajili ya kurasimishwa kwa mujibu wa sheria

“waendeshaji wa zilizokuwa bandari bubu binafsi tano (05) za Mwanza ambazo ni miongoni mwa zilizokuwa bandari bubu ishirini (20) zilizorasimishwa kupitia Tangazo la Serikali (GN) namba 293/2022 wamepewa leseni za uendeshaji huku TPA wakielekezwa kusimamia kwa karibu bandari kumi na tano (15) zilizobakia.

Akizungumzia kuhusu Kuboresha usalama, ulinzi kwa usafiri majini na kudhibiti uchafuzi wa mazingira baharini utokanao na meli amesema Shirika limetimiza lengo hilo la kimkakati kwa  kuendelea kusimamia usalama wa vyombo vya usafiri majini kwa kufanya ukaguzi wa meli kubwa na vyombo vidogo vya majini.

“Shirika lilifanya kaguzi za usalama kwa meli kubwa zibebazo tani 50 au zaidi ili kuhakikisha kuwa ni salama na zinaendeshwa na mabaharia wenye sifa katika mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara, Tanga, Mwanza, Kagera, Kigoma na Mbeya ambapo katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Juni, 2023, Shirika lilifanya jumla ya kaguzi za meli kubwa 288 ambapo kaguzi 165 zilikuwa za meli za kigeni na kaguzi 123 zilikuwa meli za ndani.”amesema

Kuhusu uratibu Shughuli za Utafutaji na Uokoaji Majini amesema Kituo cha Utafutaji na Uokoaji Majini kilichopo Dar es Salaam kinachoratibiwa na TASAC kiliendelea kufanya shughuli zake  katika kipindi cha Julai, 2022 hadi Juni, 2023 ambapo kituo kilipokea taarifa 4 za ajali zilizohusisha vyombo vya majini ambazo zilitokea katika eneo la maji ya Tanzania.

Katika ajali hizo  jumla ya watu 61 walihusika ambapo watu 58 sawa na 95% waliokolewa na watu 3 sawa na 5% walipoteza maisha.

Naye  Mkurugenzi wa Idara ya Habari -Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa amesema Serikali inataka kushirikiana na sekta binafsi kuendesha Bandari, mikataba nwatakaoendesha bado haijasainiwa.

“Sasa hivi ndio wataalamu wako mezani kuzungumza kuhusu mikataba, muda na gharama lakini hakuna bandari iliyouzwa, wataalamu watakapokamilisha majadiliano tutaangalia maslahi yetu yako wapi na maoni yanayotolewa na Watanzania yatazingatia Serikali iko macho wakati wote kuhakikisha maslahi ya Watanzania yanalindwa”amesema Msigwa.

Thursday, July 27, 2023

MRADI MKUBWA WA KILIMO CHA VANNILA WAZINDULIWA DODOMA UNAKWENDA KUGHARIMU ZAIDI YA BIL 30 ZA KITANZANIA.

 


KAMPUNI ya Vanilla international Limited imezindua Mradi wa kilimo cha Vanilla Mkoani Dodoma Vanilla village Dodoma katika Kitongoji cha Zamahero Kata ya Mayamaya Wilaya ya Bahi.

Uzinduzi huo umeambatana na utoaji Elimu kwa wananchi wa eneo hilo kuhusu kilimo cha Vanilla ambao umefanyika Julai 22 2023 katika shamba la kitalu (green House)kubwa ya kilimo hicho inayotumia njia za kisasa.

Mkurugenzi Mtendaji na muasisi wa makampuni ya Vanilla international Limited ,Simon Mkondya amesema shamba kitalu lipo kilomita 40 kutoka katikati  ya JIJI la Dodoma barabara kuu ya kwenda Arusha lenye ukubwa wa hekta 125.

Mkondya amesema uwekezaji huo unakuja baada ya mafanikio makubwa yaliyopatikana kupitia kilimo hicho katika kisiwa cha Zanzibar.

JWT YAVUTIWA UTALII UWEKEZAJI YAWATAKA WAFANYABIASHARA WAKAWEKEZE

 

KATIKA kuunga mkono jitihihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kutangaza utalii Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Pwani imetembelea vivutio vya utalii na kutambua fursa za uwekezaji zilizopo Wilayani Bagamoyo.

Akizungumza mara baada ya kutembelea vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji mwenyekiti wa Jwt Abdala Ndauka alisema kuwa baada ya ziara hiyo wameweza kutambua fursa mbalimbali kupitia utalii.

Ndauka alisema kuwa fursa kwa wafanyabiashara ni nyingi sana kwenye utalii pamoja na fursa nyingine kwenye sekta mbalimbali zikiwemo za utoaji huduma.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Majid Mhina alisema kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni maeneo mengi yanamilikiwa na watu binafsi.

Naye ofisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Magdalena Kitilla alisema kuwa kuhusu uwekezaji wametenga eneo lenye ukubwa wa hekta 9,800 ambalo linahitaji wawekezaji.

Kitilla alisema kuwa sekta ya utalii ina fursa nyingi ambapo kwenye sekta ya uvuvi kupitia uchumi wa buluu bado haujatumika ipasavyo ambapo kuna ufugaji wa vizimba baharini kunakofanyika ufugaji wa majongoo bahari ambapo ni mwekezaji ni mmoja tu.

Moja ya wafanyabiashara Fihiri Msangi alisema kuwa ziara hiyo wamejifunza mambo mengi ambayo watayafanyia kazi ili waangalie namna ya kuweza kuwekeza.

Msangi alisema kuwa fursa hizo watazitumia vizuri ili kuinua uchumi wa Mkoa huo ambao unategemea uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali na pia unauwekezaji mkubwa wa viwanda.

JWT WAVUTIWA NA VIVUTIO VYA UTALII NA UWEKEZAJI BAGAMOYO

KATIKA kuunga mkono jitihihada za Rais Dk Samia Suluhu Hassan kutangaza utalii Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Pwani imetembelea vivutio vya utalii na kutambua fursa za uwekezaji zilizopo Wilayani Bagamoyo.

Akizungumza mara baada ya kutembelea vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji mwenyekiti wa Jwt Abdala Ndauka alisema kuwa baada ya ziara hiyo wameweza kutambua fursa mbalimbali kupitia utalii.

Ndauka alisema kuwa fursa kwa wafanyabiashara ni nyingi sana kwenye utalii pamoja na fursa nyingine kwenye sekta mbalimbali zikiwemo za utoaji huduma.

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Majid Mhina alisema kuwa changamoto kubwa waliyonayo ni maeneo mengi yanamilikiwa na watu binafsi.

Naye ofisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo Magdalena Kitilla alisema kuwa kuhusu uwekezaji wametenga eneo lenye ukubwa wa hekta 9,800 ambalo linahitaji wawekezaji.

Kitilla alisema kuwa sekta ya utalii ina fursa nyingi ambapo kwenye sekta ya uvuvi kupitia uchumi wa buluu bado haujatumika ipasavyo ambapo kuna ufugaji wa vizimba baharini kunakofanyika ufugaji wa majongoo bahari ambapo ni mwekezaji ni mmoja tu.

Moja ya wafanyabiashara Fihiri Msangi alisema kuwa ziara hiyo wamejifunza mambo mengi ambayo watayafanyia kazi ili waangalie namna ya kuweza kuwekeza.

Msangi alisema kuwa fursa hizo watazitumia vizuri ili kuinua uchumi wa Mkoa huo ambao unategemea uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali na pia unauwekezaji mkubwa wa viwanda.

Wednesday, July 26, 2023


KATIKA kuhakikisha wafanyabiashara wanaondokana na changamoto mbalimbali Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) imejipanga kuhakikisha inakabili kero na kuzifikisha sehemu husika.

Hayo yamesemwa na  Mwenyekiti wa Jumuiya ya  Wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe wakati wa mkutano wa wafanyabiashara mkoani Tanga.

Amewataka wafanyabiashara hao kuungana na kuwa na sauti ya pamoja katika kuhakikisha wanajenga jumuiya yao kwa kutetea masilahi ya biashara zao.

Livembe amesema kuwa umoja wa wafanyabiashara unasaidia katika kutatua kero na kuisaidia serikali katika kutatua changamoto za wafanyabiashara pamoja na kuundwa kwa sera bora ya biashara.

"Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ipo katika kusaidia na kutatua kero za wafanyabiashara kwa makundi siyo kwa mtu mmoja mmoja ndiyo maana waliunda kamati maalum ambayo lengo lake lilikuwa ni kukusanya na kuchakata na kuwasilisha kwa serikali," amesema Livembe.

Awali katibu wa JWT Mkoa wa Tanga Ismail Masod amesema kuwa hadi sasa bei ya vitenge imeshuka ambapo awali ilikuwa kati ya shilling milioni 200 na milioni 300 lakini kwa sasa ni shilingi milioni 60 kwa kontena ambayo hiyo ni kazi ya kamati iliyoundwa.

Masod amewataka wafanyabiashara wa Tanga watumie fursa ambazo serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeziweka kwa kuagiza mizigo China kutokana na mfumo mzuri ambao serikali wameutengeneza.

Naye Mwenyekiti wa Kariakoo Martin Mbwana amesema kuwa serikali ipo pamoja na Jumuiya hiyo hivyo ametoa wito kwa wafanyabiashara watambue fursa na thamani ambayo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ambayo ameitoa kwa wafanyabiashara hao.

WATAKIWA KUINGIA MIKATABA NA WAWEKEZAJI KWENYE ARDHI BADALA YA KUIUZA

NAIBU Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Omar Kipanga amewataka wananchi wa Mafia wanaomiliki mashamba na viwanja vilivyopo karibu na ufukwe wa bahari kutokuyauza maeneo yao badala yake waingie ubia.

Akizungumza wakati wa ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo kwenye Kata ya kirongwe Vijiji vya Banja na Jojo.

Kipanga alisema kuwa baadhi ya wananchi wa Mafia wamekuwa wakiuza maeneo yao kwa wanaowaita  wawekezaji ambao wanavutiwa na maeneo hayo.

"Wananchi wanapaswa kuyakodisha maeneo hayo au wangie mikataba kwa kugawana asilimia angalau nusu kwa nusu ili kupata faida zaidi kuliko kuyauza,"alisema Kipanga.

Alisema kuwa mashamba/viwanja ni vyao lakini kwa Sasa utaratibu mzuri wa kupata maendeleo ya ardhi yako sio kuuza bali ni kuingia ubia na wawekezaji.

"Acheni kabisa tabia hii siyo nzuri itafika hatua ardhi yote ya maeneo ya Pwani ya Mafia itakuwa inamilikiwa na wageni na wenyeji watakua hawana ardhi wakati ni sasa kila mmoja apate faida ya ardhi katika uwekezaji,"alisema Kipanga.

Aidha alisema kuwa Serikali ya Rais Samia na Chama Cha Mapinduzi (CCM) inaboresha barabara za Mafia ni wazi maeneo hayo yanaenda kupanda thamani hivyo ni muhimu kuwawekea na kizazi cha baadae kupitia makubaliano kwenye ardhi.

JUMUIYA YA WAFANYABIASHARA TANZANIA (JWT) KUPAZA SAUTI

 

JUMUIYA ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT) imejipanga kuhakikisha inakabili kero za wafanyabiashara na kupokea maoni na mapendekezo ya wafanyabiashara wote nchini na kuzifikisha sehemu husika.

Hayo yameyasema na Mwenyekiti wa wafanyabiashara Tanzania Hamis Livembe wakati wa mkutano wa wafanyabiashara mkoani Tanga.

Amewataka wafanyabiashara hao kuungana na kuwa na sauti ya pamoja katika kuhakikisha wanajenga jumuiya yao kwa kutetea masilahi ya biashara zao.

Livembe amesema kuwa umoja wa wafanyabiashara unasaidia katika kutatua kero na kuisaidia serikali katika kutatua changamoto za wafanyabiashara pamoja na kuundwa kwa sera bora ya biashara.

"Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ipo katika kusaidia na kutatua kero za wafanyabiashara kwa makundi siyo kwa mtu mmoja mmoja ndiyo maana waliunda kamati maalum ambayo lengo lake lilikuwa ni kukusanya na kuchakata na kuwasilisha kwa serikali," amesema Livembe.

Awali katibu wa JWT Mkoa wa Tanga Ismail Masod amesema kuwa hadi sasa bei ya vitenge imeshuka ambapo awali ilikuwa kati ya shilling milioni 200 na milioni 300 lakini kwa sasa ni shilingi milioni 60 kwa kontena ambayo hiyo ni kazi ya kamati iliyoundwa.

Masod amewataka wafanyabiashara wa Tanga watumie fursa ambazo serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania imeziweka kwa kuagiza mizigo China kutokana na mfumo mzuri ambao serikali wameutengeneza.

Naye Mwenyekiti wa Kariakoo Martin Mbwana amesema kuwa serikali ipo pamoja na Jumuiya hiyo hivyo ametoa wito kwa wafanyabiashara watambue fursa na thamani ambayo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ambayo ameitoa kwa wafanyabiashara hao.

Monday, July 24, 2023

URAIA WETU YAZINDULIWA

SHIRIKA la Maendeleo ya Vijana (YPC) la Kibaha Mkoani Pwani limeingia mkataba wa miaka mitatu na Shirika la The Civil Society (FCS) chini ya udhamini wa Jumuiya ya Ulaya (EU) wa kutoa elimu Utawala wa Kidemokrasia kupitia mradi wa Uraia Wetu.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha Mkurugenzi wa YPC Israel Ilunde amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kwenye mikoa minne ya Kanda ya Mashariki.

Ilunde amesema kuwa mradi huo una lengo la kuendeleza mazingira wezeshi kwa ajili ya utawala wa kidemokrasia nchini ambapo kwa kanda ya mashariki ni mikoa ya Pwani, Dar es Salaam, Lindi na Morogoro.

Amesema kuwa mradi utawezesha majadiliano kati ya serikali na azaki kwa ajili ya uchechemuzi (ushawishi na utetezi) wa masuala wa kidemokrasia, maendeleo na kuboresha mahusiano na ushirikiano wa kikazi.

Aidha amesema kuwa mradi utatoa fursa wa azaki kujengewa uwezo kujiendesha kupitia shughuli zao ili kuwanufaisha wananchi wa kanda hiyo na Watanzania kwa ujumla.


Sunday, July 23, 2023

RC ATAKA WALIOCHOMA MOTO BONDE MZAKWE WASAKWE


MKUU wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama Mkoani Dodoma kuhakikisha vinawasaka na kuwabaini wote waliohusika na uchomaji moto katika Bonde la Mzakwe.

Senyamule ametoa agizo hilo leo Julai 21, 2023 mara baada ya kufika katika eneo hilo kujionea athari za uharibifu zilizosababishwa na moto ulioanza majira ya saa saba mchana.

Amesema asilimia 70 ya maji katika Jiji la Dodoma yanatoka katika bonde la Mzakwe na ni eneo la hifadhi hivyo ni muhumimu kukakikisha linalindwa na kuhifadhiwa kwa ustawi wa afya na mazingira ya watu wote.

Aidha, amewapongeza vijana wa JKT Makutupora walioshiriki katika zoezi la kuzima moto uliotokea hii leo tarehe katika Bonde la Mzakwe Jijini Dodoma. Senyamule amewapongeza kwa uzalendo walionyesha wa kudhibiti moto huo na kuzuia usilete madhara makubwa, amesema wameonyesha uzalendo mkubwa, uhodari na ushupavu.

 "Tumesikitishwa sana na moto huu kwa kuwa si kwamba umeathiri ikolojia ya eneo hili lakini pia umeharibu miundombinu ya Tanesco ikiwa ni pamoja na nguzo, hivyo kwanza nawapongeza vijana wetu kwa jitihada za kufanikisha kuzima moto huu na pili vyombo vyote vinavyohusika na uchunguzi vifanye kazi yake ili kubaini chanzo” Senyamule amesisitiza.

Amemuagiza Meneja wa Bonde la Wami Ruvu kuhakikisha kuwa wanachonga barabara maalum kwa lengo la kukinga moto katika bonde hilo ili athari za moto zisiwe kubwa pindi moto utokeapo.

Awali Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Dodoma Julishaeli Mfinanga amesema kuwa walipata taarifa kwa njia ya simu kupitia namba za dharura 114 na kuwahi eneo la tukio kwa haraka. Amesema moto umedhibitiwa na hakuna madhara makubwa na wanaendelea na doria kuhakikisha usalama katika eneo hilo.

Saturday, July 22, 2023

*UJUMBE KUTOKA KENYA WAJIFUNZA USIMAMIZI SEKTA YA MADINI*

Ujumbe kutoka Kenya ukiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Madini wa nchi hiyo Elijah Mwangi umefika nchini kujifunza kuhusu namna bora ya usimamizi wa Sekta ya Madini ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Madini Kheri Mahimbali ameupokea ujumbe huo.

Akizungumza katika kikao na ujumbe huo, Mahimbali amesema Tanzania ni sehemu salama ya uwekezaji kutokana na uongozi bora wa Serikali unaosimamiwa na Rais Samia Suluhu Hassan ambapo umepelekea kuifanya sekta hiyo kupata mafanikio makubwa.

Mahimbali amesema Wizara ya Madini ina Taasisi tano ambazo ni Tume ya Madini, Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Taasisi ya Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) pamoja na Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) ambazo hutekeleza majukumu yake kwa ushirikiano.

Naye, Katibu Mkuu Wizara ya Madini kutoka Kenya Elijah Mwangi ameipongeza Wizara ya Madini kwa usimamizi bora wa sekta hiyo na kumuomba Mahimbali kuendelea kushirikiana katika nyanja mbalimbali ikiwemo tafiti na usimamizi wa biashara ya madini.

Katika kikao hicho mada mbalimbali zimewasilishwa ambapo Mtendaji Mkuu wa  GST Dkt. Mussa Budeba amewasilisha mada juu ya madini yapatikanayo Tanzania na aina za tafiti zilizokwisha fanyika. 

Dkt. Budeba amesema kwa sasa GST imejikita zaidi kwenye tafiti za madini ya kimkakati ambapo mpaka sasa Tanzania imefanyiwa tafiti za Kijiolojia kwa asilimia 96.

Kwa upande wake, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Mhandisi Ally Maganga amewasilisha mada juu ya shughuli za Tume ya Madini ikiwemo uwepo wa Masomo na Vituo vya Ununuzi wa Madini, Mfumo wa Leseni pamoja na shughuli za wachimbaji wadogo.

Mhandisi Maganga amesema   uwepo wa masoko na vituo vya kuuzia madini umesaidia kuongeza mapato ya Sekta ya Madini ambapo mchango wa sekta hiyo kwenye Pato la Taifa umeendelea kuimarika mwaka hadi mwaka ambapo kwa sasa umefikia asilimia 9.7 ikiwa lengo ni kufikia mchango wa asilimia 10 ifikapo mwaka 2025.

Friday, July 21, 2023

MKE WA MBUNGE AWAPIGA TAFU WASANII.

 


KATIKA kuhakikisha sanaa inakuwa Wilayani Kibaha mke wa Mbunge wa Kibaha Mjini Selina Koka ametoa kiasi cha shilingi milioni 1.2 ili kuendeleza sanaa hiyo kupitia Chama Cha Waigizaji Wilayani Kibaha humo.


Mke huyo wa Mbunge huyo alitoa fedha hizo wakati wa uzinduzi wa chama hicho uliofanyika Visiga Madafu wilayani humo.


Akikabidhi cheki ya fedha hizo aliwataka waigizaji hao kuzitumia fedha hizo kwa ajili ya kujiletea maendeleo yao na kukuza tasnia hiyo ya sanaa ambayo imekuwa na kuwa na maslahi mazuri.


Awali Rais wa chama hicho Dk Cynthia Henjewele alisema kuwa wasanii wanapaswa kuungana na kutumia fursa za mikopo kupitia mfuko wa utamaduni ambayo inatolewa kwa wasanii ambazo hazina riba.

MKE WA MBUNGE ACHANGIA MAMILIONI CHAMA CHA WAIGIZAJI KIBAHA

MKE wa Mbunge wa Kibaha Mjini Selina Koka ametoa kiasi cha shilingi milioni 1.2 kwa Chama Cha Waigizaji Wilayani Kibaha kwa ajili ya kuendeshea shughuli zao.

Koka alitoa fedha hizo wakati wa uzinduzi wa chama hicho uliofanyika Visiga Madafu wilayani humo.

Akikabidhi cheki ya fedha hizo aliwataka waigizaji hao kuzitumia fedha hizo kwa ajili ya kujiletea maendeleo yao na kukuza tasnia hiyo ya sanaa ambayo imekuwa na kuwa na maslahi mazuri.

"Tumieni sanaa kwa ajili ya kuelimisha jamii, kuburudisha na kufundisha ili muwe sehemu ya maendeleo ya nchi na kujinufaisha wenyewe kwa wenyewe,"alisema Koka.

Awali Rais Sanaa za Maonyesho Tanzania Dk Cynthia Henjewele alisema kuwa wasanii wanapaswa kuungana na kutumia fursa za mikopo kupitia mfuko wa utamaduni ambayo inatolewa kwa wasanii ambazo hazina riba.

Henjewele alisema kuwa ili wasanii waweze kutambulika wanapaswa kujisajili ili watambulike kisheria ambapo wakijirasimisha watapata fursa mbalimbali.

Naye Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya ya Kibaha Mjini Jumanne Kambi alimshukuru mke wa Mbunge kwa mchango wake wa kukuza sanaa kwenye Wilaya hiyo.

Kambi alisema kuwa kwa kuwa sasa wana ofisi na tayari wana wanachama 700 watahakikisha wanachama wao wanaingia mikataba yenye manufaa kwa wasanii tofauti na kipindi cha nyuma ambapo walikuwa wanadhulumiwa haki zao.



WANANCHI WATAKIWA KULIPA ANKARA ZA MAJI NA KULINDA MAZINGIRA


Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya maji Safi na usafi wa Mazingira Bunda BUWSSA Bi Ester Gilyoma ametoa wito kwa wananchi wa Halmashauri ya Bunda iliopo Mkoani Mara kwa wale wanaotumia maji ya BUWSSA kuacha tabia ya wizi wa maji na badala yake wahakikishe wanalipa Ankara za maji, sambamba na utunzaji wa vyanzo na miundombinu ya maji katika Halmashauri hiyo.

Bi Ester ametoa wito huo  Jijini Dodoma katika mkutano wake na Wana habari wakati akielezea utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa mwaka wa fedha 2023/2024.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji huyo amesema kuwa hapo awali kulikuwa na changamoto kwa wakazi wa Bunda kwa kupata maji yasiyo Safi na salama ambapo kwasasa ndani ya uongozi wa Raisi wa awamu ya sita ya Dkt Samia Suluhu Hassan Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya maji ikiwemo chujuo la kuchuja na kutibu maji hivyo maji machafu Bunda Sasa basi.

Pia amesema wanaendelea na jitihada za kupunguza au kuondoka kabisa changamoto za upotevu wa maji ikiwa ni pamoja kuwepo kwa Mpango wa kubadili mita goigoi kwani kwa mwaka wa Jana upotevu ulikuwa asiliamia 45,lakini mpaka Sasa upotevu umeendelea kupungua mpaka asiliamia 36.

WANANCHI WATAKIWA KUJITOKEZA MAADHIMISHO YA MASHUJAA JULAI 25

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule ametoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Dodoma na Mikoa jirani kushiriki hafla ya Maadhimisho ya kumbukizi ya siku ya Mashujaa itakayofanyika Julai 25 mwaka huu katika eneo la kudumu la mashujaa lililopo Mji wa Serikali Mtumba ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Wito huo umetolewa leo tarehe 20/07/2023 alipofanya Mkutano na waandishi wa Habari katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Jengo la Mkapa kwa dhumuni la kuukaribisha Umma wa Watanzania kushiriki kuwaenzi mashujaa waliolipigania Taifa la Tanzania.

"Julai 25 ya kila mwaka Tanzania huwa inaadhimisha kumbukumbu ya siku ya Mashujaa waliopoteza maisha yao wakiutetea, kuupigania na kuulinda Uhuru wa Nchi yetu.  Siku hii ni muhimu kwa sababu inatukumbusha kuhusu wajibu wetu wa kutunza historia ya Mashujaa waliopigania, kutetea na kulinda Uhuru wa Nchi ya Tanzania ili kurithisha vizazi vijavyo umuhimu wa kutumia historia hii kukuza na kuendeleza amani na mshikamano wa kitaifa bila kujali tofauti mbalimbali, ikiwemo za kikabila, kidini na  itikadi za kisiasa.

"Ninapenda kuwajulisha kuwa tofauti na ilivyozoeleka katika miaka ya nyuma, ambapo Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa katika Mkoa wa Dodoma yalikuwa yanafanyika katika Viwanja vya Jamatin vilivyopo katikati ya Mji wa Dodoma, mwaka huu (2023) Kilele cha Maadhimisho haya kitafanyika katika Uwanja mpya wa kudumu wa Mashujaa uliopo katika eneo la Mji wa Serikali Mtumba, Dodoma.  Mgeni Rasmi katika Maadhimisho hayo atakuwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama", Mhe. Senyamule

Aidha, shughuli za Mashujaa zitatanguliwa na uwashaji wa Mwenge wa Mashujaa saa 6:00 Usiku wa tarehe 24 Julai, 2023 kuamkia tarehe 25 Julai 202 ambapo Mhe.Senyamule amepewa heshima ya kuuwasha Mwenge huo wa Mashujaa kwa niaba ya Wanadodoma na Mwenge huo utazimwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma Mhe. Prof. Davis Mwamfupe tarehe 25 Julai 2023 saa 6:00 Usiku.

Tumebakiza takribani siku nne tuadhimishe Siku ya Mashujaa Maandalizi ya Maadhimisho yamekamilika kwa 100% kwaiyo nichukue fursa hii kuwakaribisha Viongozi na Wananchi wote wa Mkoa wa Dodoma na kutoka nje ya Mkoa wa Dodoma, ikiwemo Mikoa jirani ya Singida, Manyara, Iringa na Morogoro kujitokeza kwa wingi kuja kuungana na Wanadodoma katika kuadhimisha siku hii muhimu, ambayo inafanyika kwa mara ya kwanza katika kiwanja kipya kilichopo eneo la Mtumba".

Hatahivyo Mhe.Senyamule ametumia fursa hiyo kuzishukuru Taasisi zote, ambazo kwa namna moja au nyingine zimeshiriki katika ujenzi wa Mnara Mpya wa Mashujaa katika Mji wa Serikali – Mtumba

Thursday, July 20, 2023

*MBOYA MBUZI SODO CUP YAFANA*




KIBAFA INATISHA...ikiwa ni wiki mbili baada ya uongozi mpya wa chama cha soka wilaya ya Kibaha kuingia madarakani imeshuhudiwa viongozi wa chama hicho wakihudhuria mashindano ya soka la ufukweni maarufu kama "Beach soka"

Mashindano hayo yamefanyika Mlandizi yakiwa ni ya Mboya mbuzi SODO cup...

Katika mashindano hayo imeshudiwa viongozi kadhaa wapya wa KIBAFA wakihudhuria ambapo wameongozwa na mwenyekiti wa KIBAFA comrade Robert Munisi...makamu mwenyekiti bwana David Mramba...

Pia alikuwepo katibu msaidizi wa KIBAFA bwana Omary Abdul pamoja na wajumbe  wa kamati tendaji ya KIBAFA bila kusahau mwenyekiti wa kamati ya Beach soka bwana Nassoro Shomvi

Katika hali ya kuonesha KIBAFA wapo kazini pia mbunge wa jimbo la Kibaha vijiijini mheshimiwa Michael Mwakamo alihudhuria mashindano hayo hali iliyoibua shangwe na vibe la aina yake kwa wakazi na mashabiki wa Beach soka waliojitokeza kutoka Mlandizi na Kibaha kwa ujumla...

Katika mashindano hayo timu ya Kilangalanga umeibuka mshindi wa fainali hiyo baada ya kuibamiza timu ya Msalabani goli 4-1 na kuifanya timu ya Kilangalanga kupata zawadi ya mbuzi mnyama huku mshindi wa pili na washiriki wengine nao wakijizolea zawadi lukuki....ambapo mshindi wa pili ambaye ni timu ya Msalabani wamepata zawadi ya kuku ndege....mfungaji bora akipata pesa taslimu elfu30,mchezaji bora wa mshindano sambamba na golikipa bora wakipata mche wa sabuni kila mmoja.

Katika nyakati mbalimbali mwenyekiti wa KIBAFA comrade Robert Munisi amekuwa akisikika akisema KIBAFA ya sasa ni kwa ajili ya kuhakikisha soka linachezwa Kibaha na kuhakikisha Kibaha inakuwa wilaya ya mfano kwa Tanzania nzima

Wednesday, July 19, 2023

*WIZARA YA MADINI YADHAMIRIA KUONDOA CHANGAMOTO KWA WACHIMBAJI WA MADINI WAKUBWA NA WA KATI*

*Dkt. Biteko asikiliza mafanikio na kero za wachimbaji wa madini wakubwa na wa kati*

WIZARA ya Madini imedhamiria kuweka mipango thabiti kuhakikisha changamoto zilizopo kwenye Sekta ya Madini zinatatuliwa kwa lengo la kuongeza tija kwenye uzalishaji wa madini nchini.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Madini Dkt. Doto Biteko wakati akifungua kikao cha kujadili maendeleo, changamoto na kero zinazozikabili Kampuni kubwa na za kati zinazojishughulisha na uchimbaji wa madini nchini.

"Leo ni siku ya kuwasikiliza wachimbaji wakubwa wa madini na wa kati kama tunavyo wasikiza Wachimbaji Wadogo kama wanachangamoto gani ili tuweze kuzifanyia kazi lakini pia tunajiandaa na Mkutano wa Mkuu wa Kisekta wa Mwaka unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu," amesema Dkt. Biteko.

Pamoja na mambo mengine, Dkt. Biteko amesema tayari serikali imerahisisha mazingira ya kikodi kwa wachimbaji wa madini ili kuondokana na changamoto mbalimbali zinazoweza kujitokaza katika kutimiza wajibu yao.

Kwa upande wake, Waziri wa Madini Maji, Nishati na Madini kutoka Zanzibar Staibu Hassan ameipongeza Wizara ya Madini kwa hatua kubwa ambapo amesema wizara hiyo imekuwa mwalimu wa mataifa mengi kujifunza usimamizi bora wa shughuli za biashara na uchimbaji madini.

Naye, Mwenyekiti wa Chemba ya Migodi, Mhandisi Philibart Rweyemamu amesema Chama anachokiongoza kipo tayari kushirikiana na serikali ili kuondoa changamoto na kutoa suluhisho la kudumu katika sekta hiyo ili hatimaye kufikia lengo la kuchangia asilimia 10 kwenye Pato la Taifa ifikapo 2025.

"Kikao cha namna hii kitakuwa kinafanyika kila robo mwaka ili kutoa taarifa kwa serikali juu ya maendeleo ya shughuli zetu, kuueleza umma nini kinachofanyika pamoja na kuishauri serikali kitu gani tunafikiri kifanyike ili kurahisisha utendaji wa Sekta ya Madini," amesema Mhandisi Rweyemamu.

Katika kikao hicho Kampuni tano za uchimbaji mkubwa wa madini zimetoa taarifa za utekelezaji wa miradi inayotekelezwa ikiwemo Kampuni ya Nyati Corporation, Sotta Mining, Tembo Nickel Corporation, Twiga Minerals na Faru Graphite Limited.

WATAKIWA WASIDANGANYE MAKAZI

MKUU wa Mkoa wa Dodoma,Mhe.Rosemary Senyamule amewaasa wananchi na wakazi wa Dodoma kuacha kudanganya maeneo ya makazi ili kuepusha migogoro ya ardhi.

Mhe.Senyamule ameyasema hayo wakati akizindua mpango mkakati kwa ajili ya kushughulikia na kutatua migogoro ya ardhi kwa jiji la Dodoma.

Aidha amesema kuwa jiji la Dodoma limekuwa na ongezeko la wananchi hivyo kufuatia ongezeko hilo limepelekea matumizi ya ardhi kuwa ni mengi na mengine kuwa ya kiholela bila mpangilio ambapo kwa kutatua changamoto hii mkoa wa Dodoma kupitia Mkuu wa mkoa wa Dodoma imeandaa timu kwa ajili ya kutatua na kumaliza migogoro.

"Kuna changamoto mbalimbali zinazochangia migogoro hii kushindwa kuisha kutokana na uchache wa vifaa vya tehama, ukosefu wa huduma bora kwa wananchi,eneo la jiji kuwa dogo, lugha mbaya kwa wananchi zinazotolewa na watumishi wa jiji,kipandikizi yaani kupandikiza zaidi ya kiwanja kimoja kupewa watu tofauti pamoja na wananchi kupuuza jumbe za simu" Amesisitiza Senyamule.

Aidha ameongeza kuwa jambo hili litafanyika ndani ya miezi 6 yaani Julai hadi Disemba ambapo kutafanyika uhakiki wa maeneo ambayo yanamalalamiko ambapo wahusika wanavamia maeneo ambayo sio ya kwao pamoja na kurekebisha mifumo kwa kushirikiana na ofisi ya Rais tamisemi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Dodoma,Mhe. Jabir Shekimweri amesema kuwa mpango huo utaweza kuwasaidia kutambua mapungufu gani ya ndani na madhaifu gani ya nje ili ili kuishi matarajio ya kiongozi wa kitaifa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuhakikisha jiji la Dodoma linapagwa vizuri ili kuendana na hadhi ya makao makuu ya nchi.

Amesema ni matumaini yake kwamba elimu ya kutosha itatolewa kwa kamati ili kuhakikisha wanakuwa na uelewa huku akisisitiza maeneo ya wazi kupewa watu sahihi ili kuhakikisha wanajenga vitu vyenye manufaa kwa wananchi.

Aidha ametoa rai kwa watumishi wa ardhi kuhudumia wateja vizuri kwa kutoa kauli nzuri kwa wateja pamoja na kuheshimu watu.

TCRA KUENDELEA KUSIMAMIA SEKTA YA MAWASILIANO

MAMLAKA ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema inaendelea kusimamia Sekta ya Mawasiliano kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika ngazi ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa ili kuhakikisha Sekta ya Mawasiliano inatoa mchango katika maendeleo ya nchi na kuwa kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa kidijiti na uchumi wa buluu.

Hayo ameyasema Mkurugezi Mtendaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Dkt. Jabiri Bakari wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini dodoma kuhusu taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya TCRA 2022/23 na Mpango kazi 2023/24.

Dkt,Jabiri amesema Takwimu zinaonesha kuwa wastani wa bei ya dakika ndani ya Mitandao bila kifurushi zinaendelea kushuka na  Mwenendo wa gharama za upigaji wa simu nje ya kifurushi zimeendelea kushuka hivyo kwa gharama za mwingiliano kumepelekea kuwa na tofauti ndogo sana ya gharama za kupiga simu ndani na nje ya mtandao.

Aidha, Dkt Jabiri ametoa rai kwa Vyombo vya utangazaji kuendelea kuzingatia sheria, kanuni na weledi katika kutoa maudhui, vilevile kwa wananchi kutosambaza maudhui ambayo yanakiuka misingi ya sheria, mila na desturi za Taifa la Tanzania. 

TCRA ilianzishwa chini ya Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Namba 12 ya mwaka 2003 baada ya kuunganishwa kwa iliyokuwa Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC) na Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC). TCRA ilianza kutekeleza majukumu yake tarehe 1 Novemba 2003.

WAZALISHAJI CHUMVI WATAKIWA KUONGEZA UZALISHAJI





WAZIRI wa Madini Dk Dotto Biteko amewatakaka wazalishaji wa chumvi nchini kuongeza uzalishaji chumvi ili kukidhi soko la ndani na la nje kutoka tani 273,000 kwa mwaka hadi tani 303,000.

Aliyasema hayo alipofanya ziara ya siku moja kutembelea kuona uzalishaji wa chumvi kwenye kampuni za Sea Salt na Stanley and Sons Ltd zilizopo Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani.

Dk Biteko alisema kuwa uzalishaji wa chumvi utakapo ongezeka utasaidia kuongeza mapato na kutoa ajira kwa wananchi ambapo asilimia 15 ya chumvi ndiyo inayopelekwa soko la nje.

"Chumvi hiyo inatumika kwa ajili ya chakula, viwandani na kuuzwa soko la nje ambapo chumvi kutoka nje ya nchi inauzwa kwa gharama ndogo ikilinganishwa na inayozalishwa ndani kutokana na gharama za uendeshaji,"alisema Dk Biteko.

Alisema kuwa ili kuongeza uzalishaji na kupunguza gharama mamlaka za serikali za mitaa zinapaswa kufanya marejeo ya sheria zake ndogo ili zilingane ambapo kwa sasa kila Halmashauri inatoza gharama zake.

"Serikali baada ya kuona malalamiko ya wazalishaji walifuta kodi 17 na mrabaha kutoka asilimia tatu hadi asilimia moja lengo likiwa ni kupunguza gharama za uzalishaji ili bei iwe ndogo,"alisema Dk Biteko.

Aidha alisema kuwa makampuni hayo pia yawasaidie wazalishaji wadogo kwa kununua chumvi yao ili kuongeza uzalishaji na kuwataka wazalushaji hao kutokuwa watu wa kulalamika sana juu ya tozo na kodi kwani fedha hizo zinatumika kwa ajili ya kutoa huduma za maendeleo.

"Tanzania ina Pwani kubwa lakini uzalishaji wa chumvi ni mdogo licha ya kuzuia chumvi za nje ili kukuza soko la chumvi inayozalishwa hapa nchini lakini pia wazalishaji wazingatie ubora,"alisema Dk Biteko.

Naye Ofisa Madini Mkoa wa Pwani Mhandisi Ally Maganga alisema kuwa Wilaya ya Bagamoyo inazalisha chumvi tani 90,000 hadi 100,000 kwa mwaka na kuingiza kati ya shilingi milioni 300 hadi miluoni 350.

Maganga alisema kuwa kuna leseni 48 za uchimbaji chumvi huku ndogo zikiwa 46 ambapo ni 15 tu ndizo zinafanya kazi huku nyingine zikiwa hazifanyi kazi kutokana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na mitaji, soko na mazingira.

Awali Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Muharami Mkenge pia kupunguzwa gharama kwa magari yanayochukua chumvi kutozwa fedha nyingi na Hifadhi za Taifa (Tanapa) ambapo makampuni hayo kutumia barabara za hifadhi ya Saadani.

Mkenge alisema kuwa endapo baadhi ya changamoto zikiondolewa Bagamoyo inaweza kulisha chumvi nchi nzima kwani wanauwezo huo wa uzalishaji.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kampuni ya H J Stanley and Sons Richard Stanley alisema kuwa baadhi ya changamoto ni kukosekana kwa umeme, maji na ubovu wa barabara.

Stanley alisema kuwa changamoto nyingine ni uingizwaji wa chumvi toka nchi nyingine ambapo miundombinu ikiwa mizuri gharama za chumvi zitapungua na bei itashuka.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo Shauri Selenda alisema kuwa kilio cha wawekezaji hao kinafanyiwa kazi kwa kuboresha miundombinu na upatikanaji wa maji na umeme na barabara.

Selenda alisema tayari miundombinu hiyo imewekwa kwenye bajeti kwa ajili ya kuanza utekelezaji kwa mwaka huu wa fedha ili kuwaondolea kero wawekezaji hao.

Mwisho.

Monday, July 17, 2023

MAMLAKA YA UDHIBITI MBOLEA NCHINI TFRA YAHIMIZA UWEKEZAJI VIWANDA VYA MBOLEA NCHINI

MAMLAKA ya udhibiti wa mbole nchini (TFRA) inaendelea kudhibiti ubora wa mbolea kuhamasisha uwekezaji wa ujenzi wa viwanda vya kuzalisha mbolea na kuimarisha utoaji huduma bora kwa wakulima.

Aidha itahakikisha Tanzania kuwa kitovu cha uzalishaji wa mbolea kwa nchi za afrika mashariki na nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
 
Hayo  ameyasema Leo july 17, 2023  Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya udhibiti wa mbolea Tanzania(TFRA) Dkt. Stephan Ngailo wakati akieleza utekelezaji wa majukumu ya mamlaka hiyo na mwelekeo wa utekelezaji wa mwaka wa fedha 2023/24 

Dkt Ngailo amesema  Kilimo ni biashara ambapo amebainisha kuwa Mamlaka hiyo itahakikisha ajenda na maono hayo yanafikiwa kwa kuimarisha upatikanaji na usambazaji wa mbolea bora kwa wakati na kwa bei himilivu.

Alisema lengo la sera ni kuendeleza sekta ya kilimo yenye ufanisi, ushindani na faida Hivyo kuboresha maisha ya Watanzania na kufikia ukuaji mpana wa uchumi na kupunguza
umaskini

Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) ni taasisi iliyo chini ya Wizara ya Kilimo, Sheria ya Mbolea Namba 9 ya Mwaka 2009 (Fertilizer Act, 2009) na kanuni zake za Mwaka 2011,TFRA ilianza kutekeleza majukumu yake mnamo Agosti 2012.

PPRA YAWATAKA WADAU WAKE KUZINGATIA MAADILI

MAMLAKA ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imewataka wanaojihusisha na Ununuzi wa Umma ikiwemo watumishi wa Umma na wazabuni kuzingatia maadili katika utendaji wao.

Aidha Mamlaka haitasita kuwachukulia hatua kwa mujibu wa Sheria wale wote watakaokiuka taratibu au watakajihusisha na kuisababi utakaoisababishia hasara serikali.

Hayo ameyasema Leo July 17 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma Eliakim Maswi wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini dodoma kuhusu utekelezaji wa Majukumu ya PPRA na mwelekeo wa utekelezaji wa Mwaka wa fedha 2023/24.
      
Maswi amesema Ununuzi wa Umma unakabiliwa na hatari kubwa ya rushwa ambapo watendaji na maafisa serikalini wamekuwa wakilalamikiwa na kuhisiwa kuwa wanajihusishwa na vitendo vya rushwa kwa kutoa mikataba na kuwapa faida zisizo halali wazabuni wasiyo na sifa.

Amesema serikali inaendelea kudhibiti matumizi ya fedha za umma kwa kutumia njia mbalimbali ikiwemo mifumo ya kielektroniki Ili kuleta tija na ufanisi unaostahili katika utekelezaji wa bajeti husika.         

Katika Mwaka wa fedha 2023/24 Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma  imetenga shillingi billion 40.4 kwa ajili ya utekelezaji wa Majukumu yake ambapo kiasi cha shilling billion 20 ni kwa ajili ya uendeshaji na ukaguzi wa taasisi  nunuzi pamoja na ujengwaji wa uwezo wa watumishi.

Sunday, July 16, 2023

MWENYEKITI WA UWT TAIFA CHATANDA AIELEKEZA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUTATUA CHANGAMOTO ZA NDOVU LINDI

 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa CC Mary Chatanda ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha inashughulikia changamoto za ndovu waliovamia makazi ya watu Mkoani Lindi. 

Ameyasema hayo leo katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Naipingo Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi. 

Amefafanua kuwa ndovu hao wamevamia makazi ya watu kutokana na wananchi kuingia katika maeneo ya Hifadhi.

"Wizara ya Maliasili Utalii shirikianeni na Wizara ya Mifugo muwatoe wafugaji walioingia kwenye maeneo ambayo ndovu wanakaa" Chatanda amesisitiza 

Ameelekeza hatua za haraka zichukuliwe kuwatoa wananchi katika hifadhi ili kunusuru mazao ya wananchi yanayoliwa na ndovu pamoja na vifo vya wananchi. 

Kufuatia hoja hiyo, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii  Mhe. Mary Masanja ameahidi  Wizara ya Maliasili na Utalii kupeleka helikopta ya kufukuza ndovu ambayo  itaweka kambi katika maeneo husika.

"Tutahakikisha tunaleta helikopta ambayo itakaa kuondoa ndovu hawa  ili wananchi waishi bila taharuki" Mhe. Masanja amesisitiza.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan inajua Changamoto zinazowakabili wananchi hivyo imepanga  kuongeza idadi ya askari na kujenga vituo vya askari ili kuondokana na tatizo la ndovu.

Kuhusu malipo ya kifuta jasho/machozi, Mhe. Masanja amesema Serikali imetenga fedha  kiasi cha shilingi milioni 612 kwa Wilaya ya Nachingwea mwaka ili kukabiliana na changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu hususan ndovu.

Pia amesema Serikali itachukua vijana kwenye maeneo yenye changamoto za ndovu na kuwapatia mafunzo ya kukabiliana na wanyamapori hao.

Thursday, July 13, 2023

TASAF YABADILISHA MAISHA YA AKINAMAMA WAJENGA NYUMBA ZA KISASA



MFUKO wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) umeleta mabadiliko makubwa kwa walengwa wake ambapo Zubeda Juma miaka (70) mkazi wa Kijiji cha Kisanga kata ya Masaki Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani amefanikiwa kujenga nyumba ya tofali kutoka nyumba ya udongo aliyokuwa anaishi awali.


Aidha Halima Salehe naye amefanikiwa kujenga nyumba ya tofali kutokana na fedha za mfuko huo ambao umekuwa mkombozi kupitia mpango wa kunusuru kaya masikini.

Juma akitoa ushuhuda mbele ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete alipotembelea Kijiji hicho kuzungumza na walengwa na wananchi.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete alimchangia na wadau wengine walimchangia huku Halmashauri ya Kisarawe ikiahidi kuhakikisha inakamilisha sehemu itakayobakia.

Alisema kuwa nyumba yake ambayo ni ya kisasa imekamilika ambapo anaishi ila amebakiza kuweka milango na madirisha ambayo ameyaziba kwa kutumia mabati.

Naye Salehe alisema kuwa nyumba yake imefikia hatua ya boma ili kukamilika na kumshukuru Rais Dk Samii Suluhu Hassan kwa kuendeleza mpango huo kutoka kwa mtangulizi wake na kuwafanikisha kubadilisha maisha yao.

Naibu Waziri Ridhiwani alisema mpango huo una lengo la kuwaondoa wananchi kwenye lindi la umasikini ambapo watu milioni 1.3 wananufaika na mpango huo wa kunusuru kaya maskini na kuondoka kwenye umaskini na utegemezi.

Wednesday, July 12, 2023

WATUMISHI WAFANYE KAZI KIMKAKATI

WATUMISHI wa Umma wametakiwa kufanya kazi kimkakati kwa kuwatumikia wananchi na kwa kuwa na wivu wa maendeleo sehemu wanazozifanyia kazi kwa kuacha alama.

Hayo yalisemwa na NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete alipokuwa akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kwenye ofisi za Halmashauri hiyo zilizopo Mlandizi.

Alisema kuwa serikali inafanya shughuli zake kimkakati hivyo lazima nao wafanye kazi kwa kuzingatia mikakati hiyo ya serikali ili mipango ya maendeleo kwa wananchi ifikiwe.

"Serikali ina mikakati yake hivyo lazima kila mtumishi wa umma ahakikishe anazingatia mikakati iliyopo ili kufanikisha malengo ya maendeleo kwa wananchi ambapo wanawategemea watumishi kuwaonyesha njia,"alisema Kikwete.

Alisema asingependa kuona watumishi hawawajibiki kwenye maeneo yao ya kazi na kusababisha malengo ya kuwaletea maendeleo wananchi yasifanikiwe hivyo wasije wakajikuta wanaondolewa au kufukuzwa kazi.

"Kutokana na changamoto zilizopo hapa ofisa utumishi Edward Mahona nakutaka ushughulikie chanfamoto za watumishi siyo lazima kuleta kwetu kwani baadhi ya mambo mnaweza kuyatatua wenyewe hivyo tatua mara moja,"alisema Riziwani.

Aidha alisema kuwa ofisa huyo anatakiwa kukaa na watumishi na kuongea nao kujua changamoto zao kwani malalamiko yaliyotolewa yanapaswa kufanyiwa kazi ili wafanye kazi kwa moyo kwani shida zao zinatatuliwa.

Moja ya watumishi Winifrida Toegale ambaye ni ofisa mtendaji wa kijiji alisema kuwa wanatumia fedha zao binafsi kwani hakuna fedha wanazopewa kwa ajili ya kuendeshea ofisi.

Toegale alisema kuwa licha ya kutumia fedha zao za mishahara lakini kwa upande wao walioajiriwa mwaka 2012 hawakupandishwa vyeo hadi mwaka 2020 jambo ambalo limekuwa changamoto kubwa na inawavunja moyo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha Butamo Ndalahwa alisema kuwa wanakabiliwa na uhaba wa watumishi 441 ambapo waliopo ni 1,571 na mahitaji ni 2,012 na wameweka bajeti ya kuajiri watumishi 211 kwenye kada mbalimbali.

Ndalahwa alisema kuwa madai ya watumishi 342 ni milioni 756 ambapo madai yaliyolipwa ni 251 ya shilingi milioni 455 bado madai 91 yenye thamani ya shilingi milioni 329 kwa upande wa watumishi 70 waliogushi vyeti 56 walijaza fomu huku 12 bado taratibu zinaendelea.

Tuesday, July 11, 2023

VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI VYA TASAF VIKOPESHWE ASILIMIA 10 ZA HALMASHAURI



NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejmenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete ameshauri Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha kuvipatia fedha za mikopo za asilimia 10 vikundi vya ujasiriamali vilivyopo kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) 

Kikwete ameyasema hayo kwenye Kitongoji cha Mwembebaraza kata ya Janga Mlandizi Wilayani Kibaha alipotembelea vikundi vya wajasiriamali wanaotokana na fedha za kuweka akiba na kukuza uchumi wa kaya (LE) kupitia Tasaf.

Amesema kuwa wajasiriamali watokanao na vikundi hivyo wanafanya shughuli ambazo zinaonekana na ni watunzaji wazuri wa fedha ambapo wanakopeshana wenyewe kwa wenyewe japo ni kidogo lakini manufaa yanaonekana.

"Nafikiri mkurugenzi katika zile asilimia 10 vikopesheni vikundi hivi kwani wanauaminifu mkubwa na wanatumia fedha kwa malengo ambayo yanaonekana kupitia miradi hii kuanzia ile ya uhawilishaji wa fedha, miradi ya ajira za muda na miradi ya ujenzi wa miundombinu,"alisema Kikwete.

Aidha amesema kuwa endapo fedha zitatolewa kwa vikundi hivyo fedha za serikali hazitapotea ambapo vikundi vinavyolengwa vimekuwa havirudishi fedha wanazokopeshwa lakini vikundi vya Tasaf ni waaminifu sana.

"Tasaf imekuwa mkombozi kwani imeweza kubadili maisha ya kaya lengwa kutoka chini na kuinuka kiuchumi na kuondoka kwenye hali ya chini na kuboresha maisha kama malengo ya serikali yalivyowekwa kwani mpango umetafsiriwa kwa vitendo,"alisema Kikwete.

Kwa upande wake mratibu wa Tasaf Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha akisoma taarifa ya mpango huo wa kunusuru kaya masikini Sijaona Muhunzi alisema kuwa kaya lengwa zimenufaika kupitia vikundi na mtu mmoja mmoja.

Muhunzi alisema kuwa baadhi ya walengwa wameweza kujenga nyumba, kufanya ufugaji, kilimo cha mboga mboga, kusomesha watoto na kuongeza maudhurio shuleni na kliniki ambapo ni moja ya masharti kwa familia lengwa watoto kwenda shule na kliniki kwa asilimia 100.

Naye Dalia Hassan amesema kupitia mpango huo amemsomesha mwanae ambaye kwa sasa yuko chuo kikuu anasema alianza kupewa ruzuku ya shilingi 40,000 mwaka 2012 ambapo aliingiza kwenye biashara ya karanga.

Hassan amesema kuwa fedha hizo zilimwezesha kuanza kilimo cha mpunga na pilipili vimemsaidia kumsomesha mwanae huyo na kuwataka walengwa wenzake kuwa na malengo makubwa ya kujiletea maendeleo.

MHE.MASANJA : FILAMU YA "THE ROYAL TOUR" IMEFANIKIWA KWA KIWANGO KIKUBWA SANA

 



NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amesema filamu ya “The Royal Tour” iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kwa kiwango kikubwa na kwamba kwa sasa watalii wameongezeka.

Mhe. Masanja ameyasema hayo leo Julai 11,2023 alipotembelea Maonesho ya 47 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam maarufu kama Sabasaba yanayoendelea Jijini humo.

“Tunatambua kwamba ni nadra sana kumpata Kiongozi anayeamua kuongoza kwa vitendo  kama alivyofanya  Rais Samia, ametangaza kwa vitendo vivutio vyetu hivyo tunatakiwa kuvitembelea vivutio hivyo  ili kumuunga mkono” Mhe. Masanja amesisitiza.

Mhe. Masanja ametumia nafasi hiyo kuwahimiza Watanzania kutembelea vivutio vya utalii vilivyoko nchini akitolea mfano wa maeneo ya Malikale, Misitu ya Asili, tamaduni za Kitanzania, historia za Tanzania za Waasisi wa Taifa na maeneo mengine ya utalii.

“Tutembelee vivutio vyetu, ukishakitembelea kile kivutio unakuwa umechangia pato la Taifa lakini hata wewe mwenyewe utakuwa umejifunza historia ya nchi ilivyo lakini pia utapunguza hata msongo wa mawazo” Mhe. Masanja amefafanua.