Friday, March 10, 2023

WEJISA WASHEREHEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI



WANAWAKE WA WEJISA WAJUMUIKA KUSHEHEREKEA SIKU YA WANAWAKE DAR

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Weka Jiji Safi (WEJISA Company Ltd) kupitia kwa Mkurugenzi Mkuu wake Bi.Nuru Hassan amepongeza juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Samia Suluhu Hassan katika kuweka mazingira mazuri ya kufanya kazi ikiwemo wafanyakazi wanawake jambo ambalo limeongeza uchapakazi kwa jinsia hiyo.

Nuru amesema hayo kwenye maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ambayo inafanyika Machi 8 ya Kila mwaka.

"Rais wetu Samia tunamuunga mkono kwa sababu nafasi aliyonayo amesaidia kuongeza mwamko kwa wanawake kufanya kazi na wale ambao walikuwa hawana kazi na kutafuta shughuli zozote ili waweze kujiondoa kwenye utegemezi," alisema Nuru.

Amesema kuwa kampuni ya WEJISA itaendelea kushirikiana na Serikali bega kwa bega na ndiyo maana leo tumekuja hapa kusheherekea pamoja na kujifunza mengi kwa wafanyakazi wetu wanawake,"alisema Nuru Hassan

Aidha amesema kuwa amepata faraja kujumuika na Wanawake hao kwani wamekuwa chachu ya Maendeleo ya Kampuni hiyo.

Wanawake hao wa WEJISA wanatoka vitengo mbalimbali ikiwemo wanaosafisha maeneo ya Jiji, ikiwemo ufagiaji, ukusanyaji wa taka na usafi wa mazingira.

Lengo la tukio hilo ni kupeana moyo kama Wanawake katika kuamua mambo na kufanikisha utendaji bora wa kazi.

Kwa upande wake Patricia Kimelemeta Mwandishi Kinara wa Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Mtoto Mkoa wa Dar es Salaam ambaye alitoa mada ya malezi na makuzi kwa watoto katika tukio hilo la kusheherekea siku ya Wanawake, ambapo alitoa rai Kwa wazazi kuendelea kutoa elimu kwa watoto wao ikiwemo kujenga ukaribu wa kuwachunguza ilikujua changamoto wanazokutana nazo.

Kwa upande wao baadhi ya Wanawake wafanyakazi wa WEJISA waliishukuru kampuni hiyo kwani imekuwa mkombozi kwao na wamekuwa wakifanya kazi moyo.

"Mimi nina familia, nikitoka nyumbani naandaa kabisa chakula kwa wanangu.

Aidha, amewataka Wanawake kuzingatia sheria za Usalama barabarani kwani wamekuwa wakishuhudia matukio mengi, ikiwemo wao kugongwa.' Alisema Bi. Asha Salum.

Kwa upande wake. Bi. Sharifa Magombeka amesema kuwa, anafanya kazi ya kuzoa taka ilikupata kipato chake halali,

"Mwanamke ni kujitambua, nafanya kazi yangu ya kuzoa taka hii kupata kipato kihalali, tunamshukuru Mhe Rais kuendelea kuweka mazingira ya ufanyaji kazi na tumejumuika hapa tumepata elimu, lakini pia tumefurahia pamoja" alisema Sharifa.


No comments:

Post a Comment